Skip to main content

Posts

Showing posts from February 5, 2023

KASORO ZA KISHERIA ZAWAWEKA NJIA PANDA WATU WENYE ULEMAVU MAHKAMANI

    NA HAJI NASSOR, PEMBA: “KESI ya mtoto wangu mwenye ulemavu wa matamshi, ilifutwa mwaka 2021 mahakamani, kwa sababu ya siuntafahamu ya eneo alilobakwa ni tofauti na walilolitaja mashahidi,’’anasema mama wa mtoto huyo.   Mama huyo mkaazi wa Pujini Dodo wilaya ya Mkoani, anasema tokea asili mtoto wake anaulemavu wa akili na matamshi, sasa kasoro ya kumbu kumbu yake ndio chanzo cha kukosa haki zake.   Anasema bado watu wenye ulemavu, mara baada ya kubakwa imekuwa ni shida mpya kuvifikia vyombo vya sheria, kutokana na ulemavu wao wakati mwengine sheria kuwa na kasoro kwao.   Baada ya mtoto wake kubakwa na mtuhumiwa Abdalla Khatib Abdalla miaka 25, mwanzoni mwa mwaka 2018, kesi hiyo ilichukua tena miezi minane, hadi kufika mahakamani.   “Nilipofika kituo cha Polisi Chake chake, kwanza sikupata ushirikiano, na walionipokea wakaniambia kesi yangu inaweza kuwa ngumu mahakani, kwa sababu hakuna mkalimani,’’anasimulia.   Anasema ingawa askari hao wenyewe kwa wenyewe, wal

TAMWA, INTERNEWS NGUVU MOJA KUTAKA SHERIA MPYA YA HABARI ZANZIBAR

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::: ‘’BILA ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi’’. ‘’Tena pia mtu huyo ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati, na rai anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio ya nchini na duniani kote, ambayo ni muhumi kwa maisha yake’’. Ndivyo Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, inavyoelekeza kifungu cha 18 juu ya upatikanaji na utoaji wa habari kwa raia, tena bila ya kujali mipaka ya nchi. Mwanasheria wa kujitegemea Khalfan Amour Mohamed, anasema suala la kupata habari, au kutoa ni haki ya kikatiba, ambayo inatofautiana na haki nyingine. ‘’Ukitaka kuzigawa haki hizi, basi zipo haki za kikatiba na haki nyingine zilizotengenezewa sheria yake mbali mbali, mfano haki ya elimu,’’anafafanua. Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuwajali wananchi wake, haikuishia tu ndani ya Katiba kifungu cha 18 ya up

VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA WAENDELEA KUHUBIRI AMANI KWA WANAFUNZI WA VYUO VIKUU

Na Nusra Shaaban, Unguja;              Viongozi hao   kutoka   vyama   vinne vya siasa Zanzibar   kama vile Chama cha mapinduzi CCM, Chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA, ACT Wazalendo pamoja na Chama cha wananchi CUF    wamejumuika kwa pamoja huko katika chuo cha utawala wa umma (IPA) kilichopo Tunguu Wilaya ya kati Unguja. Awali   Ikumbukwe kwamba   mwaka   wa 2022    viongozi hao walipatiwa mafunzo   na   Jumuiya ya   Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA) kwa kushirikiana na Konrad Adenauer Stiftung   (KAS)   katika utekelezaji wa mradi wa “amani yetu mshikamano wetu” unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU). Lengo   la kujumuika kwa viongozi   hao   ni   kuendelea kuhubiri   amani   ya nchi   kwa kutoa mafunzo ya kudumisha amani kwa wanafunzi hao hasa ikizingatiwa kwamba wao ndio viongozi wa kesho. Akizungumza wakati akitoa   mafunzo hayo Mjumbe kikosi kazi cha ng’ome ya wanawake Taifa ACT Wazalendo bi Halima Ibrahim alisema wanafunzi hao ndio viongozi watarajiwa hivyo w

CHAPO; WASAIDIZI WA SHERIA CHAPUWENI WIGO WA WANANCHI KUFUATA SHERIA

NA JUMA SEIF, PEMBA; Wazaidiz wa sheria wametakiwa kuhakikisha wanaisaidia na kuilekeza  jamii katika kutekeleza sheria za nchi. Akizungumza katika mkutano wa jumuiya ya Wasaaidizi wa sheria ya Wilaya ya Chake chake CHAPO uliofanyika Febuari 4, 2023 mjumbe wa bodi wa jumuiya hiyo Kassim Ali Omar amesema wasaidizi wa sheria wanawajibu wa kuiyelekeza jamii katika kuzifahamu na kujuwa namna bora ya kuzitekeleza. Amesema sheria inagusa kila pahala katika maisha ya watu kwani sheria hizo zina lengo la kuleta ustawi na usawa katika maisha ya watu. Mjumbe huyo amesema wasaidizi washeria wanawajibu mkubwa wa kuisadia jamii hasa wakati anapokuwa na tatizo kwqni ndani ya jamii kuna watu wengi wanapokumbwa na tatizo hajui wapi namna ya kuzipata haki zake. "Ni lazima sisi wasaisizi wa sheria tuwape wananchi njia ya kujua haki zao kipinsi wanapokuwa na tatizo, kwani mtu hadi anagika mahakamani anakuwa hajui chochote kuhusu sheria ya kosa lake". Pia Adam Abdalla Fakih ambaye ni mjumbe wa C

WAANDISHI KUWENI WAKALI HADI SHERIA MPYA YA HABARI IPATIKANE ZANZIBAR

  NA HAJI NASSOR, UNGUJA WAAANDISHI wa habari wameshauriwa kutoa maoni yao katika kupata sheria mpya ya habari,. ambayo itapelekea kufanya kazi zao kwa ufanisi bila kukandamiza uhuru wao. Mjumbe wa Bodi ya Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA), Shifaa Said Hassan, alieleza hayo Febuari 8, 2023 wakati akifungua mkutano wa majadiliano kuhusu sheria zinazokandamiza uhuru wa habari Zanzibar kwa vyombo vya habari uliofanyika katika ukumbi wa Mfuko wa Hifadhi wa Jamii Zanzibar ZSSF Kariakoo mjini Unguja. Alisema kupatikana kwa uhuru wa vyombo vya habari nchini ni fursa ya kuwa na sheria na muundo huo utakaoendana na wakati uliopo. Alibainisha kuwa tasnia ya bahari ni muhimu katika nchi kwani inachochea maendeleo ya mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla kiuchumi, kisiasa na kijamii. Aidha alisema wanabari ndio wanaojua changamoto wanazokabiliana nazo katika utelelezaji wa majukumu yao ikiwemo kukosa taarifa katika wizara na tasisi za serikali hali ambayo inakandamiza