Skip to main content

Posts

Showing posts from August 25, 2024

FAWE Zanzibar, UN Women zinavyowezesha Wanawake kufikia kizazi chenye Haki na Usawa Kiuchumi

KATIKA jitihada za kuhakikisha Tanzania inafanikisha utekelezaji wa malengo manne ya kizazi chenye, Jukwaa la Wanawake Wanaelimu wa Afrika, Zanzibar (FAWE Zanzibar) inawezesha wanawake Zanzibar kukabiliana na vikwazo kiuchumi. Kwa kushirikiana na UN Women Tanzania, FAWE Zanzibar inachangia ufikiaji wa malengo hayo kupitia utekelezaji wa  Mpango wa Pamoja wa Umoja wa Mataifa wa Kuharakisha Maendeleo ya Kiuchumi kwa Wanawake Vijijini (JPRWEE) unaolenga kuhakikisha ustawi wa wanawake vijijini na haki zao. Utekelezaji wa mpango huo unaenda sambamba na utoaji wa mafunzo kwa wanawake ili kuwasaidia  kupata ujuzi wa biashara, elimu ya kifedha, pamoja na fursa za kupata mikopo ili kuanzisha na kukuza biashara zao. Miongoni mwa mafanikio yaliyoelezwa na wanufaika wa mradi huo ambao unatekelezwa Mkoa wa Kusini Unguja ni kuongezeka kwa ajira, hali iliyoboresha kipato cha kaya na kupunguza utegemezi kwa waume.  Walisema mradi huo umewawezesha wanawake wengi kuanzisha biashara ndogo ndogo, kama vil

‘CHAPO’ YAPATA MKURUGENZI MPYA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ALIYEKUWA Mratibu wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba, ‘CHAPO’ Mohamed Hassan Abdalla, amechaguliwa kwa kura za ndio, kushika nafasi ya Mkurugenzi wa Jumuiya hiyo, iliyokuwa wazi. Mahamed Hassan, ambae hakuwa na mpinzani katika uchaguzi huo mdogo na wa dharura, alijizolea kura 15 kati ya kura zote 17 zizopigwa na wanachama wa CHAPO. Akitoa matokeo hayo leo Augost 31, 2024, Makamu Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi ya 'CHAPO' Hafidh Abdi Said, alisema wapiga kura wote, walitarajiwa wewe 23, ingawa hadi muda wa kupiga kura unafika kulikuwa na wajumbe 17 pekee. Alieleza kuwa, kwa mujibu wa katiba ya CHAPO, imeanisha idadi ya wajumbe wote, ni kufikia nusu, ili kufanya uamuzi iwe wa uchaguzi ama kupitisha ajenda. ‘’Idadi ya wanachama hai 17, kati ya 23 haijakikua katiba ya 'CHAPO' na ndio maana, tumefanya zoezi la uchaguzi na mshindi ambae ni Mohamed Hassan Aballa, kwa nafasi ya Mkurugenzi ameshinda,’’alifafanua.

'MAYELE' WA ZANZIBAR AFUNGWA MIAKA 14 KWA ULAWITI

  NA MARYAM NASSOR, ZANZIBAR MAHKAMA maalum ya kupinga makosa ya udhalilishaji mkoa wa Mahonda Unguja, imemuhukumu kijana Sharif Juma Hamad (33) maarufu  ‘MAYELE’wa Mzambarau mbata Unguja, kutumikia kifungo cha  miaka 14, kwa kukutwa na hatia ya makosa mawili ya udhalilishaji. Akisomewa hukumu hiyo, Hakimu Luciano Makoe Nyengo, alisema kuwa mshitakiwa huyo amekutwa na hatia hiyo, baada ya mahakama kujiridhisha  na ushahidi uliyoletwa na upande wa Mashtaka, ulioongozwa na Mwendesha Mashtaka Hariri Yeshau Ali, na vielelezo vilivyowasilishwa. Hakimu Luciano, alisema kuwa Mshitakiwa huyo anatiwa hatiani kwa makosa mawili aliyoshitakiwa  likiwmo la kulawiti mtoto wa kiume mwenye miaka 12, kwa kosa hilo atatumikia kifungo cha maiaka 14 chuo cha mafunzo. Kosa la pili, ni kutorosha mtoto wa kiume alie chini wa uwangalizi wa wazazi wake, ambapo ni kinyume na kifungu cha 113 (1) (b) cha sheria nambari 6 ya mwaka 2018, sheria ya Zanzibar na kosa hilo atatumikia kifungo cha miaka 10. Aidha, Hakimu

EU YAJA NA MRADI WA KIJANI PEMBA KUIMARISHA HUDUMA KWA WANANCHI

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA WAZIRI wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar Shamata Shaame Khamis amesema, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar itahakikisha inasimamia vyema utekelezaji wa mradi wa Kijani (SASA) Pemba utakaoimarisha ustahamilivu wa mazingira, ambao unalenga kuleta mageuzi ya upatikanaji wa huduma bora nchini. Alisema kuwa, mradi huo utasaidia upatikanaji wa maji safi na salama, kufanya ukarabati wa maskuli 19 na ukarabati wa vituo vya afya kumi (10), kuwawezesha wajasiriamali wadogo wadogo kwa kuwapatia mafunzo na mikopo nafuu, kuwasaidia akinamama wanaolima mwani pamoja na usimamizi wa usafi wa mazingira katika miji. Akizindua mradi huo katika Uwanja wa michezo Madungu Chake Chake Waziri huyo alisema kuwa, ni vyema mradi wa Kijani (Green and Smart Cities Programe) utekelezwe kwa haraka, ili wananchi wanufaike kwani ni muhimu sana kwao. ‘’Tuhakikishe mradi huu tunautekeleza kwa malengo tuliyoyakusudia na Serikali inaendelea kuthamini michango ya wa

KAMPUNI YA ‘FOREVER LIVING PRODUCTS INTERNATIONAL’ YATUA PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI kisiwani Pemba, wameshauriwa kutumia virutubisho lishe, vinywaji na bidhaa kadhaa zinazozalishwa kwa mti wa Mshubiri, ili kuboresha afya zao, ikiwemo kupunguza takamwili zilizozidi. Ushauri huo umetolewa na Msambazaji huru wa kampuni ya Forever Living Products International, Imani Lushino, wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi, juu uwepo wa wasambazaji huru wa bidhaa hizo kisiwani Pemba. Alisema, kwa zaidi ya miaka  2000 mmea wa mshubiri umekua na manufaa mengi ndani na nje ya mwili wa binadamu na kuwa bidhaa kama mafuta na virutubisho lishe zinazolishwa kupitia mti huo zina msaada mkubwa kuboresha afya. Alisema, kwa miaka hii na kwa aina ya vyakula watu wanavyokula bila ya kuzingatia lishe bora, kumesababisha kiwango cha magonjwa hasa yasiyoambukizwa kuzidi kuongezeka kutokana na Kinga ya mwili kupungua inapokosa lishe bora iliyosheheni virutubisho vyote vinavyohitajika na mwili, Alieleza kuwa, tayari kampuni hi

TIGO-ZANTEL WAUMIMINIA MILION 350 MFUKO WA WANAOANGUKA MIKARAFUU

    HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MTANDAO wa simu za mkononi wa Tigo-Zantel, umechangia shilingia milion 350, kwenye mfuko wa fidia kwa ajili ya wananchi wanaopatwa na hasara ya kuanguka mkarafuu, wakati wanapoliokoa zao hilo. Hafla ya kukabidhi fedha hizo, kupitia mfano wa hundi, lilifanyika leo Augost 27, 2024 ukumbi wa Kiwanda cha Makonyo Wawi Chake chake Pemba, kwenye hafla pia ya kuwakabidhi zawadi wakulima bora wa karafuu, waliokubali fedha zao za malipo kupitia Tigo pesa. Akizungumza mara baada ya kukabidhi mfano huo wa hundi, Mkurugenzi wa mtandao wa simu wa Tigo- Zantel Aziz Said Ali, alisema huo ni mwanzo kwa Tigo-Zantel, kuwachangia wanoanguka mikarafuu. Alieleza kuwa, mtandao wa simu, kila siku umekuwa ukijali mno ubinaadamu na maendeleo yao, na ndio maana, wamevutika mno kutoa shilingi milioni 350, kwa ajili ya kuutunisha mfuko huo. Aidha, mtandao huo wa simu katika hafla hiyo, iliwakabidhi wakulima 25 zawadi za simu, baiskeli na piki piki, kwa baadhi yao waliopokele

'ZAPCO' YAIBUKA NA MIKAKATI MIPYA KWA ZAO LA KARAFUU

NA ASHA ABDALLA, PEMBA@@@@  KATIBU Mtendaji wa Jumuiya ya wazalishaji karafuu Zanzibar, 'ZACPO' Abuubakar Mohamed Ali, amewataka wakulima wa zao la mikarafuu, kuungana kwa pamoja katika jumuiya hiyo, ili kulitanua zao kuu la karafuu. Aliyasema hayo Augost 25 ,2024 wakati alipokua na wakulima na wanachama wao, wa mikoa miwili ya Pemba, katika ukumbi wa kiwanda cha Makonyo Wawi, wilaya ya Chake chake, Pemba, kwenye mkutano wa kukumbushana majukumu. Alieleza kua, wakulima wote kisiwani Pemba ni vyema katika kushirikiana na ZACPO, ili kua kitu kimoja na kuweza kutengeza sauti ya pamoja, amabayo itaweza kusikika kwa kila upande, ili wananchi wahamasike zaidi katika upandaji wa mikarafu na kuiepusha kutoweka.  Aidha Katibu huyo Mtendaji, alisema jumuiya hiyo imeundwa kwa lengo ni kuanzisha mfuko, ambao utaweza kuwasaidia wale wote wanaoshughulika na ukulima wa zao la karafuu, wakiwemo wanaolima, wakodishwaji, wakodishaji pamoja na wale ambao wanasaidia kwanamna moja ama nyingine,  Ha

UKUZAJI VIPAJI VYA WANAFUNZI WA KIKE SKULI YA UWELEWENI, WAELEWA NA CHUNGU YA CHANGAMOTO

  NA HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@ MPIRA wa kikapu ‘basketball’ ni aina ya mchezo unaochezwa sehemu nyingi   duniani. Kwani kama ilivyo michezo mingine, nao huimarisha afya, huleta ajira, huondosha ubaguzi, na kuunganisha watu wa aina mbalimbali. Mchezo huu ni wa pili kwa umaarufu, baada ya mpira wa miguu kwa kupendwa na mashabiki wa michezo nchini, ambao wengi walicheza skulini na kupata wafuasi wengi. Kwa mujibu wa umoja wa Mataifa, mchezo huu ulianzishwa na Mwalimu James Naismith, kwenye chuo cha Springfield College huko, Massachusetts mwaka 1891. Alibuni mchezo huu kwa ajili ya wanafunzi wake, ili wapate mazoezi wakati wa kipupwe waliposhindwa kucheza nje, ambapo kwa mara ya kwanza, ulichezwa Disemba 21 mwaka huo huo 1891 nchini Berlin. Mpira wa kikapu, ulienea haraka ndani na nje ya vyuo vya Marekani, katika karne ya 20, ambapo mwaka 1936 mchezo huu ulikubaliwa kwenye michezo ya Olimpiki. Shirikisho la mpira wa kikapu duniani ‘FIBA’ na chombo cha usimamizi wa mpira huo du

MAKAMU WA PILI AIPA KAZI WIZARA, KUENDELEZA, KUKUZA, KULINDA UTAMADUNI

 NA KHAULAT SULEIMAN, SUZA@@@@ MAKAMU wa Pili wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla, amesema kua Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale, inajukumu la kuhakikisha wanalinda mila, silka na asili ya Zanzibar, kwa kuona kua ni fursa kwa wananchi na serikali kwa ujumla.  Ameeleza hayo kwenye Tamasha la Utamaduni wa mswahili wa kipemba, jana August 25, 2024 lililofanyika ukumbi wa zamani wa Baraza la Wawakilishi Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba. Alisema wakati umefika sasa kwa Wizara hiyo, kwa kuweka taratibu mbali mbali ambazo zitaihamasisha jamii, kuendeleza kulinda na kuuenzi utamaduni wa Zanzibar.  "Wizara  mnatakiwa kua wabunifu, ili kuendelea kuongeza watalii na pato katika nchi, mnatakiwa kutoa elimu katika jamii, kwamba utalii sio wa kutembea uchi, kwani ni fursa ambayo inasaidia kuleta maendeleo yenye kulinda heshima na utamaduni,''alisema. Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Mudrik Ramadhani Soraga, amempongeza Afisa Mdhamin Zuhura Mgeni Othman kwa kuona ipo haja ya kuandaa