Skip to main content

Posts

Showing posts from December 14, 2025

UIMARISHAJI MASLAHI NI HATUA YA KUMUANDAA MSTAAFU MTARAJIWA "GORA"

    NA  MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ NAIBU Katibu Mkuu wa Utumishi na Utawala bora Zanzibar Omar Haji Gora, amesema kupandishwa kwa mshahara   kwa   watumishi wa   Umma katika serikali ya awamu ya nane ni miongoni mwa juhudi za serikali za kuwaandalia mustakbali mzuri wa maisha watumishi baada ya kustaafu. Alisema hayo katika ufunguzi wa mafunzo ya maandalizi ya kustaafu kwa wastaafu watarajiwa watakaolipwa   mafao yao ya kustaafu kazi na mfuko wa hifadhi ya jamii Zanzibar ZSSF, yaliofanyika katika ukumbi wa Kiwanja cha kufurahishia watoto Tibirinzi Chake chake Pemba. Alisema katika kuhakikisha watumishi wa umma wanakua na mustakbali nzuri wa maisha yao baada ya kustaafu serikali imechukua juhudi kadhaa ikiwa ni pamoja na kuongeza mishahara kwa wafanyakazi wa serikali, kupandisha pensheni, pamoja na kutoa mafunzo ya maandalizi kwa wastaafu ili kuweza kupata uelewa   wa namna bora ya kujiandalia mazingira ya kuyakabili maisha baada ya kustaafu. ...

JAMII YATAKIWA KUCHUKUA TAHADHARI KUKABILIANA NA HAKI YA TABIA ZA NCHI

  NA SALMA OMAR, PEMBA @@@ ANGOZA kwa kushirikiana na Mashirika ya kiraia pamoja na serikali, zimeiasa   jamii kushirikiana kwa pamoja katika kukabiliana na changamoto za haki ya tabia ya nchi. Hayo yamesemwa katika mkutano wa mafunzo na majadiliano yaliyoshirikisha jamii na taasisi mbalimbali zikiwemo asasi za kiraia, pamoja na wawakilishi kutoka serikalini katika ukumbi wa Samail Gombani Chake chake Pemba. Mwenyekiti wa ANGOZA Hassan Khamis Juma, amesisitiza jamii kushirikiana kwa pamoja katika kukabiliana na haki za tabia ya nchi, ikiwemo kujiepusha na uharibifu na uchafuzi wa mazingira. Alieleza kua kwani, kufanya hivyo kunaweza   kupelekea athari kubwa katika jamii na kusababisha maafa baadae, na jamii kuishi katika mazingira magumu. ‘’Niwaombe sana wanajamii, kwanza waziunge mkono asasi kama ANGOZA, maana zinakuwa na wajibu wa kuhakikisha wanawakinga wananchi na majanga kadhaa, yakiwemo ya athari za mazingira,’’alisema. Kwa upande wake, mwakilishi kuto...

WAZIRI PEMBE ATOA MWEZI MMOJA NA NUSU UJENZI VYOO UWANJA WA TENIS CHAKE CHAKE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WAZIRI wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Zanzibar, Riziki Pembe Juma, ametoa mwezi mmoja na nusu, kuanza ujenzi wa vyoo vya wanawake na wanaume, katika uwanja wa mpira wa kikapu Tenis Chake chake. Alisema, haiwezekani kama wafadhili wamesaidia kujengja uwanja huo, kisha kuwasubiria kujenga na vyoo, hivyo ni vyema, jambo hilo likaratibiwa na wizara husika kwa haraka. Waziri Pemba, alitoa agizo hilo jana, wakati alipofika uwanjani hapo, kukagua uwanja huo, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku tatu kisiwani Pemba, tokea alipochaguliwa. Alisema, anataka kuona ndani ya mwezi mmoja na nusu, iwe harakati na maandalizi ya vyoo hivyo umeshaanza kwa kasi, ili kuona wapi wamekwama na kusaidia. Alieleza kuwa, kama taasisi ya kimataifa ya ‘GIZ’ imeshasaidia kujenga viwanja vya aina hiyo Unguja na Pemba, na kama hawakufanikiwa kujenga vyoo, wizara hiyo ifanye. Waziri Pemba, alifafanua kuwa mwezi mmoja na nusu unatosha kwa wizara ya Habari, Sanaa, U...

WIZARA YA HABARI, MKANDARASI WALIFELISHA ENEO KISHINDENI UJENZI UWANJA WA SOKA PEMBA

                                                NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@@ WIZARA ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Zanzibar, imeshauriana na kukubaliana na kampuni ya Reform spots, kwamba sasa uwanja wa mpira wa mkoa wa kaskazini Pemba, uhamishiwe eneo la Kinyikani, badala ya Kishindeni . Hayo yalifahiamika jana, kwenye ziara ya Waziri wa huyo, Riziki Pembe Juma na Katib Mkuu wake Mattar Zahor Massoud, baada ya kutembelea ujenzi unaozorota wa uwanja wa mkoa huo, eneo la Kishindeni. Akiwa eneo hilo, Waziri huyo na ujumbe wake, walieleza kushangaazwa kwao, na kuzorota kwa ujenzi wa uwanja huo. Waziri Pembe, alisema haiwezekani uwanja huo kuwenda mwendo wa kusuasua ujenzi wake, ingawa baada ya kuelezwa sababu, alishauri kuhamishiwa ujenzi wake. Alisema, kama inawezekana, kusiwe na gharama za nyongeza kwa ujenzi wa eneo la Kishindeni, kutokana na uwepo wa h...

KAMATI YA DINI MBALI MBALI PEMBA YAKOSHWA NA UTULIVU ULIOPO ZANZIBAR

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ Viongozi wa kamati ya dini mbali mbali kisiwani Pemba (Pemba Interfaith Committee), wameipongeza jamii ya   wazanzibari kwa kuendelea kuishi kwa umoja na mshikamano, jambo lililoifanya Zanzibar kua mfano bora wa ustaarabu na utulivu. Tamko hilo lilitolewa na   Mwenyekiti wa kamati hiyo kwa upande wa wanawake Amina Salim Ahmed   katika ukumbi wa mikutano wa Samail uliopo Gombani Chake chake   Pemba,   katika   kikao cha tathmini ya juhudi zilizofanywa na kamati katika kushajihisha amani   kabla, wakati na baadhi ya uchaguzi mkuu uliofanyika   Oktaba 29 mwaka huu. Alieleza tamko hili ni mwendelezo wa wito wa kila mara unaosisitiza kwamba amani tulionayo ni tunu na kila mmoja anapaswa kuithamini na kuilinda kwa matendo ya kheri na kauli zenye hekima. Alisema kuimarika kwa amani kabla, wakati na baada ya uchaguzi   kulitokana na juhudi kubwa zinazofanywa na viongozi wa dini, Serikali, na wananchi katika k...

WAZIRI PEMBE" SIJARIDHISHWA UJENZI UWANJA WA SOKA KANGANI

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WAZIRI wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Zanzibar Riziki Pembe Juma, amesema hajaridhishwa na kasi ya ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu uliopo Kangani wilaya ya Mkoani Pemba. Alisema, sababu ambazo zilizotolewa za kuzorotesha ujenzi wa uwanja huo, hazijamridhisha na kuwataka wajenzi wa uwanja huo, kuzidisha kasi ya ujenzi. Waziri Pembe, aliyasema hayo jana uwanjani hapo, kwenye ziara ya siku tatu, aliyoambatana na Katibu Mkuu wake, Mattar Zahor Massoud, ya kuvitembelea viwanja kadhaa kisiwani humo. Alieleza kuwa, sababu ya uhaba wa tendaji, kuadimika kwa saruji na kuchelewa kuvipokea baadhi ya vifaa vya ujenzi huo, wala sio sababu za msingi. Alieleza kuwa, viwanja hivyo vinasubiri kwa hamu na wananchi na wanamichezo ili wavitumie, hivyo lazima kampuni ya Reform Sports kutoka Uturuki, inayojenga viwanja hvyo kuzidisha kasi. Alieleza kuwa, serikali imeamua kutoa fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya viwanja hivyo, ni...