MRADI WA ‘PAMOJA’ WABISHA HODI PEMBA, WAANZIA WILAYA YA CHAKECHAKE KWA MAJARIBIO, WANANCHI WAUFURAHIA
NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ TAKWIMU kutoka Mtakwimu Mkuu wa serikali Zanzibar, zinaendelea kutishia usalama wa wanawake na watoto wa Unguja na Pemba. Maana, kwa miaka mkitatu iliyopita, imekusanya matukio 4,991 ya ukatili na udhalilishaji, ambao wengi wa waathirika ni wanawake na watoto. Ijapokuwa, namba inaonesha kupungua kila mwaka kwa miaka hiyo, lakini kwa juhudi za serikali, washirika wake wa maendeleo, taasisi binafsi na mtu mmoja mmoja, bado maumivu yapo. Maana mwaka 2023, ilikusanya matukio 1,954 ingawa mwaka uliofuata, yalishuka na kuripotiwa matukio1,8 09, na mwaka jana, yakashuka tena na kuripotiwa matukio 1,228. Utaona kuwa, mwaka 2023, matukio 1,954, yalioripotiwa, ingawa mwaka 2024 kulikuwa na mapungufu ya matukio 145, maana yalikuwa 1,809 na mwaka 2025, kukiripotiwa pungufu ya 581 kati ya yale yaliokusanywa 1,228. Hapo sasa, ndio maana kwa Zanzibar nzima, ukiyakusanya matukio hayo kwa kipindi kuanzia mwezi Januari 2023 hadi Disemba 2025, utabaini matukio ...