Skip to main content

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE




NA WAANDISHI WETU, PEMBA:::


DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani.

Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani.

Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu.

Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo.

"Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje daktari fulani, kwa hiyo kesho (siku ya pili yake), atakuja kunichukua ili ukanipe dawa nyingine", alisema mtoto.

Alisema kuwa, siku ya pili wakati yupo skuli, daktari huyo alimpigia simu na kumeleza kuwa, akirudi skuli amsubiri kwa rafiki yake, mpaka atakapotoka kazini daktari huyo, ili akamchukue kwa ajili ya kumpatia dawa nyingine,

‘’Alikuja kunichukua nikijua naenda kupewa dawa nyingine, kumbe alinipeleka hadi nyumbani kwake Kangangani, ingawa nilipomuuliza, alijibu hana mke,’’alisimulia mtoto huyo.

Mtoto huyo alieleza kuwa, walipofika kwenye nyumba hiyo, waliwakuta vijana wawili, na kumtambulisha kuwa ni ndugu zake, na kisha kabla ya kumbaka alimfanyia uchunguuzi wa virusi vya Ukiwmi.

‘’Usiwe na wasi wasi wowote wewe uko salama na mimi niko salama, hatuna maambukizi ya Virusi vya Ukimwi, na kisha aliniletea futari na kuanza kupiga,’’alifafanua.

Alifahamisha kuwa, aliishi hapo kwa muda wa siku tano huku akiwa anafanyiwa kitendo cha ubakaji na mtuhumiwa huyo.

"Aliniambia simu niizime, lakini siku ya tano baada ya kuwasha simu alinipigia shoga yangu na kuniambia kwamba wazazi wangu wananitafuta, ndipo nilipompigia simu Is-hak (mtuhumiwa) na kumweleleza", alisema.

Aidha mtoto huyo alieleza kuwa, daktari huyo (mtuhumiwa) anapokwenda kazini, alikuwa anamfungia mlango, ingawa kwa siku ya tano alimtoa na kuandoka eneo hilo.

Mama mzazi wa mtoto huyo alieleza kuwa, mwanawe aliondoka kwenda skuli, ingawa alikuja kupata wasiwasi kuona ilipofika saa 9:00 jioni, kuwa hajarudi na kuanza kupiga simu kwa ndugu na jamaa wa karibu.

Alisema kuwa, aliporudi mumewe (baba mzazi) akamwambia kwamba mtoto wao hajarudi na ndipo walipochukua uamuzi wa kwenda kituo cha Polisi Chake Chake kutoa taarifa.

"Ilipofika siku ya tano nilimpigia simu nikampata, nikamnasihi arudi nyumbani, aliporudi kabla ya chochote tulirudi tena kituo cha Polisi Chake chake, ambapo awali walipeleka malalamiko,’’alieleza mama huyo.

Alisema kuwa, wakati anamuhoji mwanawe alimwelezea kuwa amechukuliwa na kijana na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi katika shehia ya Kangagani na kusema kuwa tayari ameshamuharibu.

Mratibu wa wanawake na watoto shehia hiyo Awena Salim Kombo, alisema kuwa amepokea taarifa ya tukio hilo na kusema kwamba tayari askari wameshakwenda kufanya uchunguzi wa tukio hilo.

"Nilipomuuliza mtoto aliniambia kuwa, daktari huyo alikwenda kumchukua kwa rafiki yake, kwa lengo la kuja kumpa dawa, lakini alipofika ndio alimuweka ndani", alisema.




Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba Juma Sadi Khamis, alithibitisha kupokea kwa taarifa hizo, na kusema kwamba upelelezi utakapokamilika atatoa taarifa rasmi.

‘’Mtuhumiwa tuna echini ya ulinzi, ambapo tulimpokea akitokea Mkoa wa kusini Pemba, na anaendelea kuhojiwa, baadae taarifa rasmi zitatolewa kwa kina,’’alisema Kamanda.

Tukio linalofafana hili, liliwahi kutokea Novemba 21, mwaka 2019, katika hospitali ya Chake chake, baada ya daktari wa kitengo cha Atrasaund, kudaiwa kuomba rushwa ya ngono kwa mjamzito, kama sharti la kumpa huduma.

Aidha Disemba 18, mwaka mwaka 2019, TBC 1, iliripoti Afisa Muuguzi msaidizi wa kituo cha Afya Mamba mkoani Katavi kushikiliwa na Jeshi la Polisi, kwa tuhuma za kumbaka mjamzito, wakati alipokuwa akimsaidia kujifungua.

Mwisho

Comments

Post a Comment

BLOG'S VISITORS

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch