Skip to main content

Posts

Showing posts from July 17, 2022

JAJI MKUU AWAKOLEZA 'SPEED' MAHAKIMU KESI ZA UDHALILISHAJI PEMBA

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA JAJI Mkuu wa Zanzibar Khamis Ramadhan Abdalla amewataka mahakimu kuendelea na kasi ya kusikiliza kesi za udhalilishaji kwa haraka, ili ziweze kupata hatia kwa muda mfupi. Akiwasilisha ripoti ya ziara ya Jaji huyo iliyofanyika kuanzia Julai 18 mwaka huuu, Kaimu Mrajis Mahakama Kuu Zanzibar Salum Hassan Bakar alisema, takwimu zinaonesha kupungua kwa kiasi kikubwa mrundikano wa mashauri hayo mahakamani. Alisema kuwa, katika ripoti hiyo Jaji Mkuu aleleza kuwa, pamoja na kuridhika kwa kasi ya uendeshaji wa mashauri hayo kwa mahakama za udhalilishji Mkoa wa Kaskazini na Kusini Pemba, lakini bado mahakimu wana jukumu la kuziendesha kesi hizo kwa haraka zaidi. ‘’Vile vile aliridhishwa na ujaji wa mashahidi mahakamani na kuwaasa wale wachache ambao wanakaidi, wajitokeze kufika mahakamani ili kuyamaliza kabisa mashauri hayo’’, alisema Kaimu huyo. Aidha aliwaagiza mahakimu na makadhi kuyafanyia kazi mashauri yaliyofikishwa mahakamani kuanzia mwaka 2020 kuja chini

WAANDISHI PEMBA 'ANDIKENI HABARI ZITAKAZOWAAMSHA WANAWAKE KUDAI HAKI ZAO'

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:: email: pembatoday@gmail.com:: MRATIBU wa Chama cha waandishi wa habari Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba Fat-hya Mussa Said, amewataka waandishi wa habari kisiwani humo, kuandika habari za uchambuzi wa kitakwimu zinazolenga kuwahamasisha wanawake kudai haki zao za kisiasa, demokrasia na uongozi. Alisema, vyombo vya habari vinamchango mkubwa wa kuibadilishaji jamii, juu ya mitazamo hasi ya wanawake kuwa viongozi, hivyo uandishi wao wenye uchambuzi wa takwimu utasaidia kwa wanawake hao. Akizungumza kwenye ufungaji wa mafunzo ya siku tatu yaliyofanyika ofisi ya TAMWA-Pemba, alisema wanawake wana haki kama wanaume kupata fursa za kuongoza kuanzia ngazi ya jamii hadi taifa, na hilo litawezekana ikiwa vyombo vya habari, vitafanya ushawishi na utetezi wenye uchambuzi. ''Kayafanyieni kazi mafunzo haya, kupitia mradi huu wa kuwawezesha wanawake kudai haki zao za uongozi, demokrasi na siasa 'SWIL' , maana wanawake wana haki sawa kwenye fursa kama wa

DAKTARI MWENGINE PEMBA ALIYEDAIWA KUMBAKA MGONJWA WAKE, ACHIWA HURU

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MAHAKAMA ya mkoa Chake chake, imemuachia huru daktari Hassan Said Mohamed miaka (38) wa kituo cha hospitali   ya Chake chake Pemba, baada ya mtoto wa aliyedai kubakwa mara tatu kumkana daktari huyo mahakamani. Mahakama hiyo maalum ya makosa ya udhalilishaji, chini ya hakimu Muumini Khamis Juma, ililazimika kumuachia huru daktari huyo, kwa vile muathirika (mtoot) amesema hajawahi kukutana kimapenzi na mtuhumiwa huyo. Akiwa mahakamani hapo tokea Juni 29, mwaka huu akisubiri hukumu baada ya upande wa mashtaka kufunga ushahidi wao, daktari huyo hakuamini macho yake, baada ya hakimu Muumini alipomtamkia kumuachia huru. ‘’Licha ya ushahidi uliotolewa na mashahidi watatu mahakamani hapa, lakini kutokana na maelezo ya mtoto wa miaka 17, ambae anadaiwa ulimbaka mara tatu, na yeye kushindwa kukutambua, sasa uko huru,’’alisema Hakimu huyo. Hakimu huyo alisema, ushahidi ambao ungepaswa kuzingatiwa zaidi ni wa mtoto mwenyewe, anayedai kubakwa, ingawa kila anapohoji

TAMWA-ZANZIBAR WAANDISHI ONGEZENI NGUVU KUWAAMSHA WANAWAKE KUDAI HAKI ZAO

NA HABIBA ZARALI, PEMBA WAANDISHI wa habari wametakiwa  kuongeza nguvu katika kuandika habari zinazowajengea uwezo wanawake kutambua sera mbalimbali zinazozungumzia haki zao, ili iwe rahisi kujua namna ya kushiriki na kudai haki zao za uongozi. Kauli hiyo   imetolewa na Mkurugenzi wa Chama Cha waandishi wa habari  TAMWA Zanzibar Dk. Mzuri Issa Ali wakati akifunguwa mafunzo ya kuwajengea uwezo  waandishi wa kuandika habari za uchambuzi kuhusu ushiriki wa wanawake katika masuala ya uongozi. Alisema ni wajibu wa waandishi kuendelea kuelimisha jamii kuondokana na mitazamo hasi  inayorudisha nyuma jitihada za wanawake kuweza kushika nafasi za uongozi. Alifahamisha kuwa  ni vyema kwa waandishi hao kuelimisha jamii kuhusu itikadi mbovu zinazowavunja moyo wanawake na watoto wa kike na badala yake ziweze kuwajengea uwezo kuhusu kuwania nafasi za uongozi. "Tunataka nafasi za uongozi kwa sasa ziangalie uwiano wa kijinsia kwa wanaume na wanawake wakati tukijiandaa kwa safari ya 2025", al

WATOTO WATANO WASALIMIKA KUPOTEZA UHAI PEMBA NYUMBA YAO IKITEKETEA KWA MOTO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA::: WATOTO watano  wa  familia  moja  wakaazi wa kijiji cha Mtega Wawi Wilaya  ya  Chake chake  Pemba, wamesalimika  kufa baada ya  nyumba  waliokuwa wakiishi kuteketea  kwa moto na kuunguza  vitu  vyote  vilivyo kuwemo ndani. Mashuhuda  wa tukio  hilo  wamesema  kuwa , wameona  moshi mkubwa  ukitokea kwenye  mapaaa ya nyumba  hiyo huku  watoto hao  , wakiwa  nje  ya  nyumba  yao  wakipga  kelele  kuashiria kuomba  msaada. Mmoja kati ya mashuhuda  hao Ibrahim Mohamed  Ali , amesema  kuwa  baada  ya  kusikia kelele hizo,  alifika  kwenye  nyumba  hiyo, na kuwakuta  baadhi  ya  watu wengine wakianza  kuokoa  vitu  vilivyokuwa  ukumbini . Alieleza  kuwa wakati huo baadhi yao wameshapiga  simu Kikosi  cha  zima  moto na uokozi na  baada ya dakika  10 kilifika  na kuanza kuuzima moto huo ingawa nyumba yote  iliteketea kwa moto.  “ Moto  ulikuwa  mkubwa  sana na  vyumbani kulizidiwa  na   moshi  mkubwa  mweusi  ambao  ulituzuia kuweza  kuingia  kwa  ajili  ya kuokoa  v

TAMWA-ZANZIBAR YAGUNDUA SHERIA YA MAGAZETI SI RAFIKI KWA UHURU WA HABARI ZANZIBAR

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA   Sheria nambari 5 ya Wakala wa Habari, Magazeti na Vitabu ya mwaka 1988 ambayo imefanyiwa marekebisho mwaka 1997, bado baadhi ya vifungu vyake vinaminya uhuru wa habari nchini.   Kifungu cha 27 (1) ni miongoni mwa vifungu kinachompa Mamlaka Ofisa yeyote wa Polisi kukamata gazeti lolote, popote litakapoonekana limechapwa au kuchapishwa au ambalo kwa maoni yake atalituhumu kwamba limechapwa au kuchapishwa kinyume na sheria.   Ambapo kifungu cha 27 (3) pia kinampa Mamlaka hakimu kumuamuru Ofisa yeyote wa cheo cha mkaguzi au zaidi ikiwa ana sababu ya maana ya kuamini kwamba atachelewa kupata hati ya upekuzi anaweza kutekeleza uwezo alio nao kwa mujibu wa sheria.   Vifungu hivi kwa nyakati za sasa havipaswi kuwepo katika sheria hiyo kutokana na kuwa sio rafiki kwa uhuru wa vyombo vya habari nchini.   Wadau mbali mbali wamekaa pamoja kuvifanyia uchechemuzi baadhi ya vifungu vinavyokandamiza uhuru wa vyombo vya habari tangu mwaka 2010 ingawa bado vinaendelea kutumika,

KATIBU MKUU KILANGI: KIPAUMBELE CHAKE NI UWAJIBIKAJI KWANZA

  Na Salma Lusangi KATIBU Mkuu wizara ya Maji, Nishati na Madini Joseph Kilangi, amewataka watendaji wote wa wizara hiyo kuwajibika katika kuwahudumia wananchi huduma ya maji, Nishati na Madini ili kuwaondolea kero inayowakabili katika kupata huduma hizo. Aliyasema hayo katika ukumbi wa ZURA wakati akizungumza na watendaji hao kwa ajili ya kuboresha utendaji kazi wa wizara anayoisimamia, ili kupunguza malalamiko ya huduma ya maji safi na salama kwa wananchi wa Zanzibar. Alisema Maji yanaweza kupatikana kila kona ya Zanzibar lakini anashangazwa kwanini watu hawapati maji huenda kuna watu wanafunga maji kwa makusudi ili watumia magari kwa ajili ya kufanya biashara ya maji huku wananchi wakiteseka, jambo ambalo sio sahihi hata kwa Mwenyezi Mungu. “Kila mfanyakazi ndani ya wizara hii akiulizwa nafasi yake ya kazi aseme mimi nawatumikia wananchi kupata huduma ya maji kwa hiyo mfanyakazi yeyote atakayemuona mtu anafunga koki ya maji basi atowe taarifa kwa kiongozi wake haiwezikani watu wakos

WATAALAMU 'ECD' PEMBA: WATOA RAI KWA WAZAZI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA WAZAZI na walezi kisiwani Pemba, wametakiwa kuwasiliana kwa ishara, maneno na kuwafanyia uchangamshi wa michezo kadhaa watoto wao wachanga, kwani kufanya hivyo ni njia rahisi ya kugundua, ikiwa wamezaliwa na ulemavu ama laa. Aidha wazazi hao wameelezwa kuwa, kufanya njia hizo zitakuza kwa haraka ufahamu wa wazazi kwa watoto wao, ikiwa wamezaliwa na ulemavu ama laa. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, wataalamu wa malezi na makuzi ya awali ya kisayansi ya mtoto ‘SECD’ kisiwani Pemba, walisema wapo watoto wamekuwa wakizaliwa na ulemavu, ingawa kisha huishi nao kwa wazazi kukosa kuwafuatilia. Mmoja kati ya wataalamu hao, Rashid Said Nassor alisema, ni rahisi kwa wazazi na walezi, kutambua ulemavu wa awali wa watoto wao, ikiwa wataanza utamaduni wa kuwasiliana nao mapema. Alisema, mtoto baada ya kuzaliwa ubongo wake uko tayari kupokea jambo lolote, hivyo ni wakati mwafaka kwa wazazi na walezi, kuanza nao mawasiliano na uchangamshi ili kujua, ikiwa wa