Skip to main content

Posts

Showing posts from March 2, 2025

RC SALAMA: ASEMA JAMBO KUHUSU ZSSF, MASHEHA KASKAZINI PEMBA

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@@ MKUU wa mkoa wa kaskazini Pemba, Salama Mbarouk Khatib amesema vikao kazi kwa masheha na watendaji wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar ‘ZSSF’ vinasaidia kuongeza ushirikiano na ufanisi wa kazi. Alisema, unapokuwa karibu na ofisi ya tawala za Mikoa ndio umeifikia jamii kwa urahisi, na kiyume chake ni kudhoofisha utendaji kazi ofisi isiyotaka ushirikiano na masheha. Hayo yameelezwa leo Machi 7, 2025 na Mkuu wa wilaya ya Wete Abdalla Rashid Ali, kupitia hutuba ya Mkuu huyo mkoa, wakati wa ufunguzi wa kikao kazi, cha masheha na watendaji wa ZSSF, kilichofanyika ukumbi wa mikutano Jamhuri Wete. Alisema, ushirikiano huo ambao ‘ZSSF’ wameuomba ni eneo zuri la utendaji kazi, kwani chanzo cha jamii na kuifikia kwa haraka na wepesi ni uwepo wa masheha. Alieleza kuwa, kilichofanywa na ‘ZSSF’ kinaashiria umoja na mshikamo katika kufanikisha majukumu ya kila siku, yanayosimamiwa na viongozi wakuu wa nchi. Alifahamisha kuwa, ndani ya wilaya na mkoa, wamekuwa...

ZSSF: 'MASHEHA WARIPOTINI WANACHAMA WETU WANAOFARIKI KUONDOA UDANGANYIFU'

    N A FATMA HAMAD , PEMBA@@@@ MASHEHA wa mkoani wa kusini Pemba, wametakiwa kutoa taarifa kwa  Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) ,  endapo kutatokea  kifo cha mwanachama wa mfuko huo katika shehia zao, ili kupunguza udanganyifu hasa katika malipo ya fedha za s erikali. Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mafao kutoka Mfuko huo Zanzibar, Mussa Yussuf wakati akiwasilisha mada ya dhima ya m asheha ,  katika utoaji wa huduma za ZSSF ,  k wenye kikao kazi kilichofanyika leo Machi 6, 2025 Tibirinzi Chakechake Pemba. Alisema kumekuwepo na baadhi ya watu wamekua wakipeleka taairifa za vifo vya jamaa zao  katika mfuko huo ,  ambazo si o  za ukweli, hivyo endapo watapeleka taarifa wataepusha kutokea kwa udanganyifu  huo . ‘’Wamekua wakitujia watu na taarifa za jamaa zao kufariki na kudai mafao yao, lakini tukifanya uchunguzi tunagundua kwamba sio ukweli ni uzushi  mtupu, hivyo mtusaidie ,’’alisema. Ali fafanua  kuwa ,  endapo M...

WASTAAFU WATARAJIWA PEMBA WANOLEWA KUYAKABILI MAISHA YA URAIANI

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ WATUMISHI wa umma wanaotarajiwa kustaafu wametakiwa kuwa makini wanapopokea ushauri wa watu mbali mbali, ili waepuke kupoteza fedha nyingi bila ya mafanikio. Akifungua mafunzo kwa wastaafu hao watarajiwa, leo Machi 5, mwaka 2025 Afisa Mdhamin Ofisi ya Rais Katiba, Sheria Utumishi na Utawala Bora Pemba Halima Khamis Ali alisema, kuna watu wengi watajitokeza kuwapa ushauri wa mambo mbali mbali, hivyo wawe makini katika kuupokea na kuutekeleza. Alisema kuwa, wastaafu bado wana mchango mkubwa kwa taifa, hivyo kuna haja ya kujipanga mapema katika kujitafutia miradi ambayo itaendeleza maisha yao baada ya kustaafu. "Kila mtu atakujia kukushauri kufanya biashara na wingine watakushauri kufanya vitu vyingine, lakini muwe makini ili fedha zenu za kiinua mgongo, zitumike kuwakomboa kimaisha na sio kuwasababishia matatizo," alisema Mdhamini huyo. Aliwataka watumishi hao wayafanyie kazi mafunzo waliyopatiwa, kwani wanakwenda kulitumikia taifa kwa upande mwingin...

VIJANA WENYE ULEMAVU WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA ZA KIUCHUMI

IMEANDIKWA NA KHAULAT SULEIMAN, PEMBA@@@ MKAGUZI wa shehia ya Pandani Wilaya ya Wete Pemba, Inspekta wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba Khalfan Ali Ussi amewataka vijana kufanya kazi za kuwapatia kipato ili kuepukana na vitendo viovu, ambavyo ni hatarishi na vinaweza kuharibu malengo yao. Ameyasema hayo mara baada ya kukabidhi viatu Sultan Hamad Issa ambaye ni mjasirimali mwenye mlemavu wa ngozi mkaazi wa shehia ya Pandani wilaya ya Wete mkoa wa Kaskazini Pemba. Alisema, kuna baadhi ya vijana wenye ulemavu wanashindwa kujishughulisha na badala yake kutegemea wazee, jambo ambalo linaongeza mzigo katika familia, kwani ulemavu mwengine unamuwezesha kijana kufanya kazi na kuweza kujikwamua kiuchumi. ‘’Nampongeza kijana huyu kwa kushirikiana na wenzake na kujiajiri kwa kuanzisha kikundi cha mifugo, ili kuweza kupata za mkopo, mafunzo na kitendea kazi ambavyo vinaweza kuboresha mradi wao,’’ alisema Mkaguzi huyo. Aidha, alimpongeza kijana huyo kwa kuamua kushirikiana na wenzake katika...

ZULEKHA’S JOURNEY: FROM STRUGGLES TO LEADERSHIP IN CLIMATE-RESILIENT AGROFORESTRY

  BY KHELEF NASSOR, ZANZIBAR@@@ Zulekha Ali Mohammed, a 26-year-old woman from Hindi village in Kambini Shehia, Wete District, Pemba, has emerged as a beacon of hope for many women in her community. Born in Wingwi village, Micheweni District, she grew up in a rural setting where access to higher education was a challenge for many girls. After completing her secondary education at Wingwi Secondary School in 2013, she remained at home, assisting her parents in farming. In 2015, Zulekha was forced into marriage, and over the years, she became a mother to five children—two boys and three girls. Like many rural women, she found herself in an extended family setup, struggling to meet household expenses. Determined to support her husband and ensure food security for her children, she joined him in farming. However, the journey was far from easy. “We spent many hours working on our farm, but because we lacked modern agricultural skills and relied on traditional farming methods, our har...

WAMBAA, CHUMBAGENI KUFANYA MASHINDANI YA QUR-AN MWISHONI MWA MWEZI HUU

   NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ JUMUIYA ya kuhifadhisha kur-an ya kanda ya Wambaa na Chumbageni wilaya ya Mkoani Pemba, inakushudia kuendesha mashindako ya kanda, mwishoni mwa mwezi huu, na kuwaomba waumini wenye uwezo, kuiunga mkono jumuiya hiyo, kwa ajili ya zawadi za washindi. Hayo yameelezwa jana na Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo ustadhi Hassan Othman Khamis, kwenye mfululizo wa vikao vya maadalizi, vilichofanyika Chumbageni chini ya msaidizi mlezi wao, Abrhaman Mohamed Khamis. Alisema, tayari Jumuiya hiyo imeshafanya mashindano ya mchujo uliofanyika Machi 1, mwaka huu, hivyo sasa inatoa nafasi kwa kuandaa mashindano makubwa, mwishoni mwa mwezi huu. Alieleza kuwa, ni nafasi kwa wenye uwezo kushirikiana na Jumuia hiyo, kwa ajili ya kukitangaaza kitabu cha Allah (S.W) kupitia mfumo wa mashindanI kwa wanafunzi. Mwenyekiti huyo, aliwakumbusha wale wenye nia ya kuungana nao, kuwa mwenye kuchangia jambo jema hasa katika mwezi huu mtukufu wa ramadhan, Muumba ameshahidi malipo makubwa kw...