NA MARYAM NASSOR, UNGUJA@@@ @ SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar, imesema mageuzi ya sera na sheria za habari nchini yaendane sambamba na kanuni na maadili ya vyombo vya habari. Akizungumza katika kongamano la madhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari, Katibu mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Fatma Hamad Rajab, akimuakilisha waziri wa wizara hiyo alisema hilo litafanikiwa. Alisema, Serikali ya awamu ya nane, inafanya juhudi kubwa ya kuweka mazingira rafiki kwa uhuru wa vyombo vya habari nchini, bila ya kuathiri uhuru wa mtu mwingine. Alieleza kuwa, hivyo wandishi wa habari wanatakiwa kufanya kazi zao kwa kuzingatia sheria, weledi na maadili, ili kunufaika na sekta hiyo. Nae Afisa sheria kutoka Tume ya Utangazaji Zanzibar Khadija Mabrouk Hassan, alisema rasimu ya sheria ya habari tayari inafanyiwa kazi kwa sasa na iko katika hatua za mwisho katika afisi ya Mwanasheria mkuu kwa hatua zaidi. Alisema, sheria zilizofanyiwa k
NA NIHIFADHI ISSA, ZANZIBAR.@@@@ WAANDISHI wa habari wanajukumu la kuendelea kufanya uchechemuzi wa mabadiliko ya sheria zenye mapungufu na ambazo sio rafiki kwa tasnia ya habari ili kutoa fursa ya upatikanaji wa sheria zilizo bora. Yamebainishwa hayo na Mkurugenzi wa Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA Zanzibar Dkt. Mzuri Issa nakusema kuwa Sheria nambari 5 ya Wakala wa Habari, Magazeti na Vitabu ya mwaka 1988, ambayo imefanyiwa marekebisho sheria namba 8 mwaka 1997 sheria hii licha yakuwa ni kongwe imekuwa na mapungufu mengi yanayokwamisha haki na uhuru wa vyombo vya habari Zanzibar. Akizungumza katika kikao cha kujadili mapungufu ya sheria zinazokwamisha uhuru wa habari huko katika ukumbi wa TAMWA Tunguu amesema Demokrasia sahihi hutegemea uhuru wa vyombo vya habari unavyoweza kusimamia maslahi ya jamii, ikiwemo uhuru wa kutoa maoni na kujieleza bila ya kuingiliwa pamoja kusambaza taarifa na mawazo ya aina mbalimbali kwa kufuata