Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

KITUO CHA ELIMU MBADALA WINGWI CHEMCHEM YA AJIRA KWA VIJANA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@ WIZARA ya Elim una Mafunzo ya Amali Zanzibar, ni moja ya wizara tegemezi hapa Zanzibar, katika kufanikisha maendeleo ya kila siku. Wizara hii, awali ilikuwa na mfumo wa elimu ya msingi, sekondari na chuo kikuu pekee, kwa miaka kadhaa. Kisha, wizara hiyo ikaanzisha mfumo wa Mafunzo ya Amali, ambao mfumo huu uliwahusu zaidi wale, walioshindwa kuendelea na elimu ya sekondari. Na kwa wakati huo, elimu ya lazima kwa Zanzibar, iliishia darasa la kumi (F11), ingawa miaka 1980, elimi ya lazima iliishia darasa la kumi na moja (F111). Haja ya kuongeza kiwango cha elimu Zanzibar, haikuja bure bali, ilitokana na maendeleo ya kielimu ya kidunia, nah apo sasa elimu ya lazima hadi sasa kwa Zanzibar inaishia kidato cga nne. JE WALIOSHINDWA KUMALIZA ELIMU YA LAZIMA WAFANYE NINI Wizara kwa muda mrefu sasa na kama alivyowahi kusema Katibu mkuu wa wizara hiyo Khamis Abdalla Said, kuwa hakuna mtoto wa kizanzibari ambae hatopata elimu. Hapa, akaenda mbali zaidi, ...
Recent posts

WANANCHI PEMBA, WAMPA TANO DK. MWINYI KWA HUTUBA YA UJENZI WA AMANI

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI wa mkoa wa kusini Pemba, wameipongeza hutuba ya uzinduzi wa mwenge wa uhuru kitaifa kwa mwaka 2026, iliyotolewa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi. Walisema, hutuba hiyo ilitoa mwelekeo wa umoja, mshikamano, upendo miongoni mwa wananchi wa Tanzania, jambo linalofaa kuungwa mkono. Wakizungumza mara baada ya kumalizika kwa hafla ya uzinduzi wa mwenge huo, jana uwanja wa michezo Gombani, walisema hutuba imewakumbusha watanzania wajibu wao, kwa maslahi mapana ya taifa. Mmoja kati ya wananchi hao Ali Ameir Haji wa Mchangamdogo, alisema hutuba hiyo kama wananchi waliifuatilia kwa makini, basi ni darasa tosha wa ujenzi wa amani. Alieleza kuwa, hutuba nyingi anazozitoa Dk. Mwinyi kwenye hafla kadhaa za kitaifa, huwa na mwelekeo mpana, ingawa hiyo ya kwenye uzinduzi wa mwenge wa uhuru, imeongezeka mara dufu. ‘’Kwa hakika hutuba hiyo, ilijaa kila kitu mfano, imehamasisha upendo, nidhamu, umo...

ANGALIA HAFLA YA UZINDUZI WA MWENGE WA UHURU KITAIFA MKOA WA KUSINI PEMBA MWAKA 2026

 

DK. MWINYI KUZINDUA MWENGE WA UHURU ASUBUHI HII UWANJA WA GOMBANI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, asubuhi ya leo April 2, 2026, anatarajiwa kuwa mgeni, rasmi katika uzinduzi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa, utakaofanyika, uwanja wa michezo Gombani Chake Chake Pemba. Taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa kusini Pemba, Rashid Hadid Rashid, kwa vyombo vya habari, ilieleza kuwa, tayari maandalizi yote yameshakamilika kwa shughuli hiyo ya kitaifa. Taarifa hiyo ilieleza kuwa, Dk. Mwinyi ataingia kwenye kitabu cha kumbukumbu kwa zoezi hilo, ambapo kwa mara ya kwanza, lilifanyika zaidi ya miaka 10 iliyopita kisiwani humo. Mkuu huyo wa mkoa katika taarifa yake, ilifafanua kuwa, Dk. Mwinyi atawahutubia wananchi watakaohudhuria, pamoja na kuzindua rasmi mbio za mwenge wa uhuru kitaifa, kwa mwaka 2026. Alieleza kuwa, wananchi watakaohudhuria kwenye zoezi hilo la kitaifa, kabla ya Dk. Mwinyi kufanya uzinduzi huo, watashuhudia burudani kadhaa uwanjani hapo. Alisema, m...

UNAIFAHAMU KAULIMBIU YA MWENGE WA UHURU WA MWAKA HUU?

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ……..MWENGE wa uhuru ni chombo cha kitaifa. Baada ya taifa la Tanzania kupata huru, kilianzisha chombo hicho, kikiwa na malengo kadhaa ndani yake. Kwa wakati huo, taarifa zinaeleza ni hayati Rais wa kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ndie aliyeuasisi. Kumbe unaweza kuthibitisha kuwa, chimbo la mwenge huo wa uhuru, ni maono ya Baba wa taifa, hasa pale alipousimamisha juu ya mlima Kilimanjaro. Akatamka kuwa, ‘ lengo ni kuleta matumaini pale pasipo na matumaini, upendo pale penye chuki na heshima pale palipojaa dharau’ . Mwenge huo, kwa mara ya kwanza, uliwashwa mwaka 1961, baada ya Mwalimu Nyerere kumteua Luteni Alexander Gwebe Nyirenda kutekeleza azma hiyo iliyoitwa “Operesheni Mwangaza”. Kwa mwaka jana, aliyekua Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Philipi Isdori Mpango, wakati akiwahutubia wananchi wa Mkoa wa Pwani, kwenye uzinduzi, alisema mwenge ni kielelezo cha umoja na mshikamano. Akafafanua kuwa, tangu ...

CFP YAANZA KUMALIZA KIU YA UKOSEFU WA MAJI KWA WAKULIMA KILIMO MSITU PEMBA, FATMA BAKAR AANZA KUUAGA UMASKINI

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@ ….nilianza na shamba moja la ekari moja, na sasa nimeongeza mawaili yenye ukubwa na nusu nusu eka kila moja, ndio maneno ya mkulima kilimo msitu Fatma Bakari wa Chato. Chato hiyo, sio ile ya Mkoani Dodoma Tanzania bara, hapana ipo kijiji cha Gombeume, shehia ya Mchanga mdogo wilaya ya Wete Pemba. Hapo ndio anapoishi mkulima huyo, ambae kwa sasa anajiita mtaalamu wa kilimo msitu, ama kilimo mchanganyiko wa miti ya biashara na chakula. ALIANZAJE KILIMO MSITU Alianza kuwataja Jumuiya ya Uhifadhi yaw a Misutu Pemba ‘CFP’ na Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar, kwamba ndio waliomzua yeye na sasa kuwa mkulima mtaalam wa kilimo msitu. Alijifunza nini maana ya kilimo hicho, kinalimwaje na faida zake za muda mfupi na mrefu, katika maisha ya kila siku. Baada ya mafunzo, huku na muume, akiwa ameshafariki, ndipo mwaka 2024 mwezi wa August, alipoanza kilimo hicho ndani ya shamba la urithi la aliyekuwa muume wake. Hapo akiwa na utaalamu, ...