NA ZUHURA JABIR, ZANZIBAR @@@ Wanawake ni nguzo muhimu katika maendeleo ya familia, jamii na taifa. Kwa miaka mingi, juhudi mbalimbali zimefanywa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na taasisi za kiraia ili kuhakikisha wanawake wanapata haki sawa za kushiriki katika uongozi na maamuzi ya maendeleo. Pamoja na hatua hizo, bado wanawake wengi hukutana na changamoto zinazowazuia kufikia nafasi za uongozi kutokana na mila na desturi, mitazamo hasi ya kijamii, ukosefu wa fursa za elimu na uwezeshaji wa kiuchumi. Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, pamoja na marekebisho yake, na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 zinatambua usawa wa watu wote mbele ya sheria bila ubaguzi wa kijinsia. Aidha, Tanzania imeridhia mikataba mbalimbali ya kimataifa inayolinda haki za wanawake, ikiwemo Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Kutokomeza Aina Zote za Ubaguzi dhidi ya Wanawake (CEDAW), Itifaki ya Maput...
NA HABIBA ZARALI PEMBA@@@@ KILA siku wanawake vijana wenye ulemavu, huamka wakiwa na ndoto kama vijana wengine kupata elimu, kujiajiri, kushika nafasi za uongozi na kushiriki katika maamuzi, yanayogusa maisha yao. Mara nyingi ndoto hizo, hukwama si kwa sababu ya ukosefu wa uwezo, bali ni vikwazo, vinavyotokana na mitazamo hasi ya jamii, unyanyapaa na kukosekana kwa mifumo jumuishi. Katika kipindi ambacho dunia inaendelea kusisitiza usawa wa kijinsia, haki za binadamu na maendeleo jumuishi, wanawake vijana wenye ulemavu, bado ni miongoni mwa makundi yanayokabiliwa na changamoto kubwa za kutoshirikishwa. Licha ya kuwa na uwezo, elimu na vipaji, wengi wao hukosa nafasi, kutokana na mazingira yasiyowawezesha kushiriki kwa usawa. Awena Khamis Rashid, mwenye ulemavu wa ngozi (albino), kutoka mkoa wa kaskazini Pemba, anasema wao mara nyingi, hushirikishwa kwa jina tu, lakini si kwa vitendo. Maana hupewa ...