NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MKUU wa mkoa wa kusini Pemba Rashid Hadid Rashid, amesema jumuiya ya kitaifa ya wafanyabiashara Zanzibar ‘ZNCC’ imekuwa chanzo kikuu cha kuwaonesha njia za kujiajiri vijana, kutokana na juhudi zake mbalimbali. Mkuu huyo wa mkoa, aliyasema hayo leo Julai 11, 2026 ukumbi wa Kiwanja cha kufurahishia watoto Tibirinzi Chake chake, kwenye hafla ya kukabidhi ruzuku kwa wajasiriamali, kupitia mradi wa ‘ Inclucities’ , unoaendeshwa kwa pamoja na jumuiya hiyo na Trias na Enabel kama mtekelezaji mkuu. Alisema ZNCC, imekuwa ikihangaika huku na kule, ili kuhakikisha wajasiriamali, wanaendelea kujiajiri wakiwa na uhakika wa uwezeshaji, kama mfano wa ruzuku kama hizo zilizotolewa. Alifahamisha kuwa, kwa ZNCC kufanya hivyo, ndio maono ya serikali iliyomadarakani, kuhakikisha wajasiriamali wanawezeshwa kwa njia tofauti. ‘’Kwanza niwapongeze sana wenzetu wa ZNCC kwa kushirikiana na Trias na Enabel, ambapo leo tunashuhudia utoaji wa ruzuku, kwa wajasiriamali wetu,...
NA MWANDISHI MAALUM, ZANZIBAR@@@@ AFISA Uchunguzi kutoka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) Ofisi ya Zanzibar, Abdul-latif Ali Sheha amewasihi wazazi na walezi wa Shehiya ya Kinuni, kujenga utamaduni wa kuzilinda na kuziishi haki za watoto kwa vitendo. Abdullatif alitoa nasaha hizo kwa wazazi na walezi 637 katika Madrasatul Thamaraatul Jannah iliyopo Shehia ya Kinuni, Mkoa wa Mjini Magharibi wakati akiwapa hao elimu ya haki za watoto na wajibu wa jamii katika kuzuia vitendo vya ukatili wa watoto na uvunjwaji wa haki za binadamu ikiwa ni mwendelezo wa kutoa elimu na msaada wa sheria wakati wa mwendelezo wa zoezi la Kampeni ya Msaada wa Kisheria wa Mama Samia Awamu ya Pili (MSLAC II) unaoendelea katika Wilaya tatu za Mkoa wa Mjini Magharibi. “Mtoto ana haki ya kuishi katika mazingira salama, kupatiwa elimu na kulindwa dhidi ya aina zote za unyanyasaji" Alisisitiza bw. Abdullatif. Pia aliwaeleza wazazi hao kuwa jamii inapaswa kuachana na tabia ya kuoneana muhali ...