NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ TAIFA la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, sasa limo kwenye shamra shamra ya kusherehekea siku yake za kuzaliwa ‘birthday ’. Taifa hili ambalo liliasisiwa mapema Aprili 26, mwaka 1964, kwa wasisi, kuchanganya udogo kama ishara ya kuunganisha nchi mbili na kuwa na taifa moja. Maana kabla ya Muungano huo, tusema chini ya mwaka 1963, Zanzibar ikijulikana kama Jamhuri ya watu wa Zanzibar, ambapo baada ya Muungano huo, taifa jipya sasa limezaliwa, nalo ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Yapo malengo mablimbali yaliosababisha hata waasisi wetu, Julias Kambarage Nyerere kwa Tanzania bara na Sheikh Abeid Amani Karume kwa Zanzibar, yaliowasukuma kuungana. Moja wapo ni kuimarisha uhusiano wa umoja wa kitaifa, sambamba na kutanua fursa za uongozi, kwa nchi mbili hizi, ikiwa ni pamoja na kitaaluma, uongozi na biashara. Na ndio maana katika safu ya uongozi, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekuwa ikitanua wigo wa uongozi kwa wazanzibari, amb...
NA HAJI NASSOR, PEMBA@ WIZARA ya Elim una Mafunzo ya Amali Zanzibar, ni moja ya wizara tegemezi hapa Zanzibar, katika kufanikisha maendeleo ya kila siku. Wizara hii, awali ilikuwa na mfumo wa elimu ya msingi, sekondari na chuo kikuu pekee, kwa miaka kadhaa. Kisha, wizara hiyo ikaanzisha mfumo wa Mafunzo ya Amali, ambao mfumo huu uliwahusu zaidi wale, walioshindwa kuendelea na elimu ya sekondari. Na kwa wakati huo, elimu ya lazima kwa Zanzibar, iliishia darasa la kumi (F11), ingawa miaka 1980, elimi ya lazima iliishia darasa la kumi na moja (F111). Haja ya kuongeza kiwango cha elimu Zanzibar, haikuja bure bali, ilitokana na maendeleo ya kielimu ya kidunia, nah apo sasa elimu ya lazima hadi sasa kwa Zanzibar inaishia kidato cga nne. JE WALIOSHINDWA KUMALIZA ELIMU YA LAZIMA WAFANYE NINI Wizara kwa muda mrefu sasa na kama alivyowahi kusema Katibu mkuu wa wizara hiyo Khamis Abdalla Said, kuwa hakuna mtoto wa kizanzibari ambae hatopata elimu. Hapa, akaenda mbali zaidi, ...