NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI wa mkoa wa kusini Pemba, wameipongeza hutuba ya uzinduzi wa mwenge wa uhuru kitaifa kwa mwaka 2026, iliyotolewa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi. Walisema, hutuba hiyo ilitoa mwelekeo wa umoja, mshikamano, upendo miongoni mwa wananchi wa Tanzania, jambo linalofaa kuungwa mkono. Wakizungumza mara baada ya kumalizika kwa hafla ya uzinduzi wa mwenge huo, jana uwanja wa michezo Gombani, walisema hutuba imewakumbusha watanzania wajibu wao, kwa maslahi mapana ya taifa. Mmoja kati ya wananchi hao Ali Ameir Haji wa Mchangamdogo, alisema hutuba hiyo kama wananchi waliifuatilia kwa makini, basi ni darasa tosha wa ujenzi wa amani. Alieleza kuwa, hutuba nyingi anazozitoa Dk. Mwinyi kwenye hafla kadhaa za kitaifa, huwa na mwelekeo mpana, ingawa hiyo ya kwenye uzinduzi wa mwenge wa uhuru, imeongezeka mara dufu. ‘’Kwa hakika hutuba hiyo, ilijaa kila kitu mfano, imehamasisha upendo, nidhamu, umo...