NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI 710, wakiwemo wanafunzi wa kike 663, sambamba na wasikilizaji 4,800 wa redio mbalimbali, wamefikiwa na elimu ya kisheria, haki za binaadamu, kupitia mradi uliokuwa ukiendeshwa na Jumuiya ya wasaidizi wa sheria Wete ‘WEPO’ hivi karibuni. Hayo yalibainishwa na Mratibu wa Uwezeshaji wa upatikanaji wa haki, kutoka ‘WEPO’ Rashid Hassan Mshamata leo Mei 10, 2026 skuli ya sekondari ya Utaani Wete, wakati wa mjadala wa wazi. Alisema, wapo waalimu na wazazi, wakimwemo wanawake 27 na wanaume 19, walifikia wakati wa utekelezaji wa mradi huo. Alieleza kuwa, kwa sasa matumaini yao, ni kuona jamii, imebadilika na waliokalia haki za wingine, sasa wanapata haki zao, kama sheria zilivyo. Alifafanua kuwa, kwa mfano waligundua ipo familia, ambayo, haijarithi kwa miaka 30 sasa, ambapo wanaume, wamekalia mirathi, jambo ambalo linaendelea kuwanyima haki wingine. ‘’Mradi huu, tulifanya shughuli kadhaa, lakini mafanikio yapo, maana hata wakati wa urushaji ...
NA MWANDISHI MAALUM, ZANZIBAR Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto leo Mai 07 imekaa kikao kazi na Benki ya Dunia kwa ajili ya kupitia mipango ya utekeleza ya Mradi wa Kukuza Usawa wa Kijinsia Tanzania- PAMOJA, unaotekelezwa na Wizara hiyo kwa Kushirikiana na Wakala wa Uwezeshaji KIuchumi (ZEEA). Akizungumza katika kikao kilichofanyika katika Ukumbi wa Mradi wa PAMOJA Kinazini, Unguja. Mkurugenzi Idara ya Mipango, Sera na Utafiti, Wizara ya Maendeleo, Jinsia, Wazee na Watoto Ndugu Daima Mohammed Mkalimoto amesema kilao hicho kimeleta tija kutokana na michango ya wadau iliyotolewa ili kuhakikisha utekelezaja wa Mradi unawanufaisha walengwa walikusudiwa wakiwemo wanawake na watoto. Ameeleza kwamba Mradi wa PAMOJA unalengo la kuwainua wanawake kiuchumi kupitia ZEEA, pia luwalinda na kuwahifadhi wahanga wa matukio hayo, hivyo Benki ya Dunia wametoa maelekezo kwaajili ya kuleta ufani. Naye Mratibu wa Mradi wa PAMOJA Ndugu Aisha Abbas Seif amesema k...