Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

SIKU YA WANAWAKE DUNIANI, KILIO, KIGUGUMIZI KWA WANAWAKE WENYE ULEMAVU NA UONGOZI, KATIJA AELEZEA MAGUMU

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WIKI iliyopita, ilikuwa ni siku ya wanawake duani kote.   Kwao na jamii, siku ya kimataifa, yenye lengo la kuchanbua matamu na mchungu wanayoyapitia katika maisha yao.   Wanawake, ni jamii na jamii ni wanawake, hivyo kila nyanja na ukumbi nao wapo, maana ni binaadamu.   Iwenye kwenye uongozi, uchumi, ajira, siasa, uongozi, utamaduni na udumishaji amani na utulivu.   Hapa ni Kiuyu Wete, mbele yangu namuoba mjasiriamali, kwa aina ya mwendo wake ambao sio wa kawaida, bila shaka ni mtu mwenye ulemavu wa viungo.   Niliharakia, kutaka kumjua ni nani, nilipomkaribia ana nadisha haya…kangaa…kangaaa…na wale wa wapenzi wa madira na vipodozi nipo njooo ujichagulie.   Kauli hizo, zilinifanya nisimame pembeni kidogo, mwa nyumba ya Asha Haji Makame, nae mjasiriamali huyo, aligeuka nyuma ghafla, kwa kule kutafuta wateja na alinifuata.   …..assalama alyekum, baada ya kuitikia mjasiriamali huyo, alimuuliz...
Recent posts

‘ZIC’ YAGAWA CHAKULA MAANDALIZI YA SIKUKUU KWA MAYATIMA, WAFUTARI NAO PAMOJA MTAMBWE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MKUU wa wilaya ya Wete Rashid Abdalla Rashid, amesema jambo la kugawa chakula kwa mayatima, lililofanywa na Shirika la Bima Zanzibar ‘ZIC’ ni la kiutu na linafaa kuigwa na mashirika mingine. Mkuu huyo wa wilaya, aliyasema hayo jana, kwenye kijiji cha kulelea mayatima, Bwagayamoyo Mtambwe Wete, mara baada ya kumaliza hafla ya ugawaji wa chakula kwa ajili ya sikukuu, iliyoandaliwa na ‘ZIC’. Alisema, ‘ZIC’ imefikiria jambo jema kwa watoto hao, kwani wameondokewa na baba zao, hivyo wanapopata mashirika kama hayo, hurejesha matumaini na furaha. Alieleza kuwa, ijapokuwa kuondokewa na jambo kubwa na linalochelewa kusahaualika, lakini ugawaji huo wa chakula hicho, na kwa uhakika, inawapunguzia machungu watoto hao. ‘’Kwanza niwapongeza sana wenzetu wa ‘ZIC’ kwa uamuzi wao, kwanza kuwagawiya futari mayatima tena hawa, waliopo hapa Mtambwe,’’alisema. Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa wilaya ya Wete, aliwataka wazazi na walezi wanaowalea watoto hao m...

MKURUGENZI BARAZA LA MJI MKOANI MGENI RASMI MASHINDANI YA QUR-AN WAMBAA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MKURUGENZI wa Baraza la Mjia Mkoani Muumini Abeid Salum, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi, katika mashindani ya sita ya tahafidhil-quran, ya kanda ya Wambaa wilayani humo asubuhi ya kesho Machi 14, 2026. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Katibu wa Jumuiya ya tahafidhil qur-an kanda ya Wambaa, Mwalimu Abdalla Haji Ali, alisema tayari maandalizi ya shughuli hiyo, yameshakamilika. Alisema, Mkurugenzi huyo, atawashuhudia wanafunzi wakishindana kwa juzuu ya kwanza, pili, tatu, tano, saba, 10 na 20, wakiwemo wanafunzi wa kike na kiume. Alieleza kuwa, mashindani hayo ya aina yake kwa mwaka huu, yanatarajiwa kufanyika msikiti wa Ijumaa Wambaa wilayani humo. Alisema, baada ya majaji kukamilisha kazi yao hiyo na kutoa matokeo, mgeni rasmi huyo atatoa zawadi ikiwemo fedha taslimu, kwa washindi na washiriki wote 45. ‘’Ni kweli asubuhi hii, Mkurugenzi wetu wa Baraza la mji la Mkoani, atayashuhudia mashindani ya sita ya tahafidhi qur-an, yanayoandaliwa ...