NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ SERIKALI ya Canada, imesema itaendelea kushirikiana na serikali za Tanzania, katika maeneo mbalimbali, ikiwemo kwenye uchumi wa buluu, ili walengwa wakuze pato lao na taifa. Hayo yameleezwa leo Juni 23, 2026 na Balozi wa taifa hilo, nchini Tanzania Emily Burns, kwenye hafla ya ugawaji wa vitendea kazi kwa vikundi vya wajasiriamali, waliokeza kwenye bahari, na ufunguzi wa kituo cha mafunzo eneo la Chamanangwe wilaya ya Wete Pemba. Alisema, ushirikiano huo, anaamini utawasaidia wajasriamali waliokeza kwenye eneo hilo, hasa wanawake na vijana, ambao kwa muda mrefu walikuwa hawakuhusishwa moja kwa moja. Alieleza kuwa, kwa eneo la Zanzibar na baadhi ya mikoa ya Tanzania bara, ilivyozungurukwa na bahari, wakati umefika manufaa yake, yawanufaishe makundi yote. ‘’Serikali ya Canada, inaziahidi serikali zote mbili kwamba, ushirikiano huu kwenye sekta ya uchumi wa buluu, utakuwa endelevu pamoja na maeneo mingine,’’alifafanua. Katika hatua nyingine, B...
NA MOZA SHABAN, PEMBA@@@@ SERIKALI ya awamu ya nane, imekuwa ikigeuza sekta ya elimu kwa vitendo, ikiwemo ujenzi wa dahalia. Maana lengo hasa ni kuwapunguzia umbali wa kutembea masafa marefu wanafunzi, pale wanapokwenda na kurudi skuli. Dahalia hizo, zimekuwa zikiwasaidia wanafunzi hao, katika kuongeza ufaulu na maarifa ya kujifunza, masomo yao na kupata utulivu, wa kujiepusha na vitisho vya udhalilishaji. Maana alishasema mara kadhaa, Ofisa Mdhamini wa wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba, Mohamed Nassor Salum kuwa, wamekuwa wakipokea kesi za vitisho vya ubakaji kwa wanafunzi. Anasema, wapo wanafunzi hasa kuanzia kidato cha nne, wamekuwa wakiviziwa vichakani, iwe wanapokwenda ama wanaporudi masomoni. ‘’Mazingira haya ya ujenzi wa dakhalia, ni kuwahakikishia ulinzi wao, maana mingi yapo karibu mno na skuli, wanazosoma,’’anasema. Anakiri kuwa, wahalifu wa ubakaji, walishazoea kutumia vichaka, ili kuwadhalilisha wanafunzi. ‘’Sasa wanafunzi wetu hasa wa...