Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

CFP YAANZA KUMALIZA KIU YA UKOSEFU WA MAJI KWA WAKULIMA KILIMO MSITU PEMBA, FATMA BAKAR AANZA KUUAGA UMASKINI

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@ ….nilianza na shamba moja la ekari moja, na sasa nimeongeza mawaili yenye ukubwa na nusu nusu eka kila moja, ndio maneno ya mkulima kilimo msitu Fatma Bakari wa Chato. Chato hiyo, sio ile ya Mkoani Dodoma Tanzania bara, hapana ipo kijiji cha Gombeume, shehia ya Mchanga mdogo wilaya ya Wete Pemba. Hapo ndio anapoishi mkulima huyo, ambae kwa sasa anajiita mtaalamu wa kilimo msitu, ama kilimo mchanganyiko wa miti ya biashara na chakula. ALIANZAJE KILIMO MSITU Alianza kuwataja Jumuiya ya Uhifadhi yaw a Misutu Pemba ‘CFP’ na Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar, kwamba ndio waliomzua yeye na sasa kuwa mkulima mtaalam wa kilimo msitu. Alijifunza nini maana ya kilimo hicho, kinalimwaje na faida zake za muda mfupi na mrefu, katika maisha ya kila siku. Baada ya mafunzo, huku na muume, akiwa ameshafariki, ndipo mwaka 2024 mwezi wa August, alipoanza kilimo hicho ndani ya shamba la urithi la aliyekuwa muume wake. Hapo akiwa na utaalamu, ...
Recent posts

UZINDUZI MBIO ZA MWENGE WA UHURU KITAIFA 2026, NI ZAMU YA MKOA WA KUSINI PEMBA

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ CHIMBO la mwenge wa Uhuru, ni nia ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, kuweka mwenge juu ya kilele cha mlima Kilimanjaro. Lengo ni kuleta matumaini pale pasipo na matumaini, upendo pale penye chuki na heshima pale palipojaa dharau. Ambapo nia hiyo, aliitoa kwa mara ya kwanza mwaka 1959 huko New York, alipohutubia Baraza la Udhamini la Umoja wa Mataifa. Kwa wakatu huo, alimteua Luteni Alexander Gwebe Nyirenda kutekeleza azma hiyo iliyoitwa “Operesheni Mwangaza”, ambapo yeye na wenzake, walianza maandalizi mwezi Novemba 1961. Kabla ya Tanganyika kupata uhuru, ambapo hatimaye usiku wa mkesha wa sherehe za uhuru tarehe 9 Desemba 1961, Luteni Nyirenda na wenzake, waliwasha na kusimika mwenge wa uhuru na Bendera ya Tanganyika kwenye kilele cha mlima Kilimanjaro. Hiyo ilikuwa kama ishara ya kuwa huru, kwa kupandisha mwenge kileleni ilikuwa kwanza, ni kuonesha kazi ngumu iliyoko mbele ya kulijenga taifa changa la Tanganyika. Pili, ilikuwa ni ku...

DK. MWINYI KUINGIA KWENYE HISTORIA UZINDUZI MWENGE WA UHURU PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa, utakaofanyika Aprili 2 mwka huu katika Uwanja wa  michezo Gombani Chake Chake Pemba. Taarifa hiyo imetolewa na Mkuu wa  Mkoa wa Kusini Pemba, Rashid Hadid Rashid, wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya uzinduzi wa mbio za mwenge wa uhuru kwa mwaka 2026 ofisini kwake  Chake Chake Pemba. Alisema kuwa, katika uzinduzi huo Dk. Mwinyi atahutubia wananchi pamoja na kuzindua rasmi mbio za mwenge wa uhuru na kuendelezwa kwa ufunguzi wa miradi mbali mbali ya maendeleo katika wilaya nne kisiwani Pemba. Alisema, mwenge wa uhuru hukimbizwa nchi nzima ikiwa ni sehemu ya kuenzi uhuru wa taifa, kuenzi maendeleo ya nchi sambamba na kudumisha Amani, mshikamano na maelewano ya wananchi katika shughuli mbali mbali za maendeleo ya taifa. "Mwenge wa uhuru mwaka huu 2026 unatarajiwa kuzinduliwa P...

SIKU YA WANAWAKE DUNIANI, KILIO, KIGUGUMIZI KWA WANAWAKE WENYE ULEMAVU NA UONGOZI, KATIJA AELEZEA MAGUMU

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WIKI iliyopita, ilikuwa ni siku ya wanawake duani kote.   Kwao na jamii, siku ya kimataifa, yenye lengo la kuchanbua matamu na mchungu wanayoyapitia katika maisha yao.   Wanawake, ni jamii na jamii ni wanawake, hivyo kila nyanja na ukumbi nao wapo, maana ni binaadamu.   Iwenye kwenye uongozi, uchumi, ajira, siasa, uongozi, utamaduni na udumishaji amani na utulivu.   Hapa ni Kiuyu Wete, mbele yangu namuoba mjasiriamali, kwa aina ya mwendo wake ambao sio wa kawaida, bila shaka ni mtu mwenye ulemavu wa viungo.   Niliharakia, kutaka kumjua ni nani, nilipomkaribia ana nadisha haya…kangaa…kangaaa…na wale wa wapenzi wa madira na vipodozi nipo njooo ujichagulie.   Kauli hizo, zilinifanya nisimame pembeni kidogo, mwa nyumba ya Asha Haji Makame, nae mjasiriamali huyo, aligeuka nyuma ghafla, kwa kule kutafuta wateja na alinifuata.   …..assalama alyekum, baada ya kuitikia mjasiriamali huyo, alimuuliz...