NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ RIPOTI ya Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto ‘UNICEF’, lile la masuala ya wanawake, UN-Women na shirika la Plan International, inaonesha idadi ya wasichana wanaoandikishwa skuli, kwa sasa ni kubwa kuliko wakati wowote. Ripoti hiyo iliotolewa mwaka 2020, inaeleza idadi ya wasichana watoro skulini tangu mwaka 1995 imepungua na sasa wasichana wana fursa ya kusoma skuli za sekondari, kuliko wavulana. HALI ILIVYO NCHINI Mitandao inaripoti, kiwango cha wanafunzi wanaojiunga na elimu ya sekondari nchini Tanzania ina uwiano nzuri, ambapo wasichana hufikia karibu nusu ya wanafunzi wanaosajiliwa. Hata hivyo, kutoka elimu ya msingi hadi sekondari kwa ujumla asilimia 56 ni ya wasichana, huku asilimia 34 pekee ndio wanaomaliza elimu ya sekondari. Huku mitandao ikiripoti, hata Zanzibar kunauwiano mzuri wa wasichana wanao jiunga na masomo ya sekondari, kati yao na wavulana. Idadi ya wanaomaliza na kufaulu ni pungufu ikilinganishwa na wavulan...
NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ WANAWAKE wanaofanya biashara katika masoko ya Mjini Wete na Kifumbikai Wilaya ya Wete Kaskazini Pemba, wameshauriwa kuripoti vitendo vya ukatili na udhalilishaji kwa viongozi wao wa masoko, ili kuchukua hatua zaidi katika kukabiliana navyo. Ushauri huo umetolewa na Msimamizi wa masoko na mazingira Wilaya ya Wete Sadri Mussa Said, wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake Wete Kaskazini Pemba. Alise katika masoko yote kuna viongozi waliochaguliwa kwa ajili ya kusimamia wafanyabiashara na kuwatatulia changamoto zao mbali mbali za kimazingira na kinidhamu, hivyo ni vizuri kuwatumia ili kupata msaada wa changamoto hizo wanapokua katika shughuli zao za kibiashara. "Masoko yote kuna viongozi waliochaguliwa kwa ajili ya kusimamia wafanyabiashara na kuwatatulia changamoto zao mbali mbali za kimazingira na kinidhamu, hivyo tunawashauri wanawake kuwatumia kuripoti matukio ya udhalilishaji yanapotokezea, ili kupata m...