Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

MABWENI KWA WANAFUNZI YAPUNGUZA VITISHO VYA UBAKAJI, YAWAPA UHAKIKA WA MAKAAZI

    NA MOZA SHABAN, PEMBA@@@@ SERIKALI ya awamu ya nane, imekuwa ikigeuza sekta ya elimu kwa vitendo, ikiwemo ujenzi wa dahalia. Maana lengo hasa ni kuwapunguzia umbali wa kutembea masafa marefu wanafunzi, pale wanapokwenda na kurudi skuli. Dahalia hizo, zimekuwa zikiwasaidia wanafunzi hao, katika kuongeza ufaulu na maarifa ya kujifunza, masomo yao na kupata utulivu, wa kujiepusha na vitisho vya udhalilishaji. Maana alishasema mara kadhaa, Ofisa Mdhamini wa wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba, Mohamed Nassor Salum kuwa, wamekuwa wakipokea kesi za vitisho vya ubakaji kwa wanafunzi. Anasema, wapo wanafunzi hasa kuanzia kidato cha nne, wamekuwa wakiviziwa vichakani, iwe wanapokwenda ama wanaporudi masomoni. ‘’Mazingira haya ya ujenzi wa dakhalia, ni kuwahakikishia ulinzi wao, maana mingi yapo karibu mno na skuli, wanazosoma,’’anasema. Anakiri kuwa, wahalifu wa ubakaji, walishazoea kutumia vichaka, ili kuwadhalilisha wanafunzi. ‘’Sasa wanafunzi wetu hasa wa...
Recent posts

WASICHANA NA ELIMU YA JUU, VIGINGI NA MASHIMO YA KUWAKATISHA TAMAA YAZIDI

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ RIPOTI ya Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto ‘UNICEF’, lile la masuala ya wanawake, UN-Women na shirika la Plan International, inaonesha idadi ya wasichana wanaoandikishwa skuli, kwa sasa ni kubwa kuliko wakati wowote. Ripoti hiyo iliotolewa mwaka 2020, inaeleza idadi ya wasichana watoro skulini tangu mwaka 1995 imepungua na sasa wasichana wana fursa ya kusoma skuli za sekondari, kuliko wavulana. HALI ILIVYO NCHINI Mitandao inaripoti, kiwango cha wanafunzi wanaojiunga na elimu ya sekondari nchini Tanzania ina uwiano nzuri, ambapo wasichana hufikia karibu nusu ya wanafunzi wanaosajiliwa. Hata hivyo, kutoka elimu ya msingi hadi sekondari kwa ujumla asilimia 56 ni ya wasichana, huku asilimia 34 pekee ndio wanaomaliza elimu ya sekondari. Huku mitandao ikiripoti, hata Zanzibar kunauwiano mzuri wa wasichana wanao jiunga na masomo ya sekondari, kati yao na wavulana. Idadi ya wanaomaliza na kufaulu ni pungufu ikilinganishwa na wavulan...

WAFANYABIASHARA WANAWAKE MASOKONI WATAKIWA KUTOVUMILIA VITENDO VYA UDHALILISHAJI

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ WANAWAKE wanaofanya biashara katika masoko ya Mjini Wete na Kifumbikai Wilaya ya Wete Kaskazini Pemba, wameshauriwa kuripoti   vitendo vya ukatili na udhalilishaji kwa viongozi wao wa masoko, ili kuchukua hatua zaidi katika kukabiliana navyo. Ushauri huo umetolewa na Msimamizi wa masoko na mazingira Wilaya ya Wete Sadri Mussa Said,   wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake Wete Kaskazini Pemba. Alise katika masoko yote kuna viongozi waliochaguliwa kwa ajili ya kusimamia wafanyabiashara na kuwatatulia changamoto zao mbali mbali za kimazingira na kinidhamu, hivyo ni vizuri kuwatumia ili kupata msaada wa changamoto hizo wanapokua katika shughuli zao za kibiashara. "Masoko yote kuna viongozi waliochaguliwa kwa ajili ya kusimamia wafanyabiashara na kuwatatulia changamoto zao mbali mbali za kimazingira na kinidhamu, hivyo   tunawashauri wanawake kuwatumia kuripoti matukio ya udhalilishaji yanapotokezea, ili kupata m...

NAIBU WAZIRI AELEZA HATUA ZA SERIKALI KUIMARISHA USTAWI WA MTOTO

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ S ERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ime sema inae ndelea kuchukua hatua mbalimbali za kuimarisha ustawi na ulinzi wa watoto nchini. Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa wizara hiyo Zawadi Amour Nassor, wakati akifungua kongamano la maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika,  leo  tarehe 16 Juni 2026 katika ukumbi wa ZSSF Tibirinzi Chake chake Pemba. Alisema hatua hizo ni pamoja na kuimarisha mifumo ya ulinzi wa mtoto ,  kuendeleza kampeni za kupinga ukatili dhidi ya watoto, kuimarisha huduma za afya na lishe, kuhamasisha malezi chanya pamoja na kuendeleza ushiriki wa watoto katika masuala yanayowahusu. " Serikali inae ndelea kuchukua hatua mbali m bali za kuimarisha ustawi na ulinzi wa watoto , ikiwa ni pamoja na kuimarisha mifumo ya ulinzi wa mtoto , kuendeleza kampeni za kupinga ukatili dhidi ya watoto, kuimarisha huduma za afya na kuhamasisha malezi chanya " alisema. A...

MRADI WA ‘PAMOJA’ WABISHA HODI PEMBA, WAANZIA WILAYA YA CHAKECHAKE KWA MAJARIBIO, WANANCHI WAUFURAHIA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ TAKWIMU kutoka Mtakwimu Mkuu wa serikali Zanzibar, zinaendelea kutishia usalama wa wanawake na watoto wa Unguja na Pemba. Maana, kwa miaka mkitatu iliyopita, imekusanya matukio 4,991 ya ukatili na udhalilishaji, ambao wengi wa waathirika ni wanawake na watoto. Ijapokuwa, namba inaonesha kupungua kila mwaka kwa miaka hiyo, lakini kwa juhudi za serikali, washirika wake wa maendeleo, taasisi binafsi na mtu mmoja mmoja, bado maumivu yapo. Maana mwaka 2023, ilikusanya matukio 1,954 ingawa mwaka uliofuata, yalishuka na kuripotiwa matukio1,8 09, na mwaka jana, yakashuka tena na kuripotiwa matukio 1,228. Utaona kuwa, mwaka 2023, matukio 1,954, yalioripotiwa, ingawa mwaka 2024 kulikuwa na mapungufu ya matukio 145, maana yalikuwa 1,809 na mwaka 2025, kukiripotiwa pungufu ya 581 kati ya yale yaliokusanywa 1,228. Hapo sasa, ndio maana kwa Zanzibar nzima, ukiyakusanya matukio hayo kwa kipindi kuanzia mwezi Januari 2023 hadi Disemba 2025, utabaini matukio ...