IMEANDIKWA NA TATU MAKAME MAHUJAJI watarajiwa wameaswa kuacha kushughulikia simu wanapokuwa katika ibada ya Hijja, ili waweze kuitekeleza kwa utulivu, unyenyekevu na kupata radhi za Mwenyezi Mungu. Wito huo umetolewa na Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Ali Abdulghulam Hussein, wakati akifunga mafunzo kwa Mahujaji watarajiwa iliyofanyika katika Ukumbi wa Shantimba, Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja yaliandaliwa na Taasisi ya Khairat Hajj and Umra Travel. Alisema, ni muhimu kwa mahujaji kufuata miongozo wanayopewa na viongozi wa Hijja na kuepuka vitendo vinavyoweza kuharibu ibada hiyo, ikiwemo kutumia simu bila ulazima au kujihusisha na mambo yasiyo na tija. “Niwaase mahujaji watarajiwa msijishughulishe na mambo yasiyo na faida kama kuangalia michezo wakati wa ibada, hilo linaweza kuharibu utekelezaji wa nguzo ya tano ya Uislamu,” alisema Abdulghulam. Aidha, aliwataka kuwa wavumilivu katika kipindi chote cha ibada hiyo ili waweze kuitekeleza kikamilifu na...
NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ‘…….SEA Cucumbers’ ama matango bahari…... Na wingine huliita jongoo la pwani, ama kiazi bahari. Ni aina ya wanyama ama kiumbe, kinachoendesha maisha yake baharini. Kitango bahari, kina ngozi ngumu kiasi na mwili mrefu ambapo muonekano na maumbile yake ni sawa na kitango kinacholiwa nchi kavu. Kitango bahari, kinaendelea kufafanuliwa kwenye vitabu na mitandao kuwa, kina mwili mrefu wenye via vya uzazi, moja iliyo na matawi. Wanyama hawa, wanapatikana kwenye sakafu za bahari duniani kote, wakiwa wamegawanyika kwenye spishi zaidi ya 1,717. Ingawa nyingi zao, zinapatikana eneo la Asia-Pasifiki, ambapo kwa Zanzibar utafiti umeonesha zipo zaidi ya aina 35. Vitango bahari, huishi kwa kutambaa kwenye sakafu ya bahari, na kuweka hifadhi na kujisitiri kwenye matumbawe. Maisha ya viumbve hawa, waliokua hawakuwa na thamani kwa zaidi ya karne moja Zanzibar, maisha yao yana mchango mkubwa katika ikolojia ya bahari, hasa katika kuisafisha. ...