Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

MSITU WA NGEZI PEMBA NA SAFARI YA UHIFADHI, WATIMIZA MIAKA 67, ILIANZA NA WAKOLONI

  NA ASHA SALIM- WKUMM, PEMBA@@@@ SEKTA ya kilimo Zanzibar, inaendelea kutumia nyezo muhimu na mipango thabiti, katika kunyanyua wakulima waweze kujikimu na kunufaika kupitia shuhuli za kilimo. Katika kuhakikisha hilo, ushirikiano wa karibu kupitia washirika mbalimbali wa maendeleo na miradi inayosainiwa na serikali ya Mapinduzi Zanzibar, kusaidia utekelezaji wa sekta hiyo zinaonekana. Juhudi hizo, zinaendelea kwa ushirikiano wa karibu, kupitia idara zake, zinazotekeleza majukumu yake chini ya wizara hiyo, na sasa serikali kujivunia kufikia mafanikio makubwa ya kiuchumi. Eeneo ambalo, serikali imekuwa na mfano mzuri wa utendaji kazi, ni kushughulikia kwa karibu msitu wa hifadhi ya Ngezi Micheweni. KWANI MSITU WA NGEZI ULIANZIA WAPI Taarifa zilizopo kwenye tovuti ya ‘ Ngezi Vumawimbi Heritage Organization , zinaeleza kuwa, m aeneo yanayozunguka msitu wa Ngezi, kumbe yamekaliwa kwa muda mrefu sana na Waarabu au Waajemi waliowahi kuishi. Infaghamika kuwa, kupitia tovuti...
Recent posts

CFP, CFI, ‘GLOBAL AFFAIRS CANADA WAWATANGAAZIA NEEMA WANAOLIMA KILIMO MSITU

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@   ….kilimo ni maji, na maji ni kilimo… Maji ndio mama wa taifa wa kilimo, bila ya maji hakuna kilimo.   Ni maneno ya mtafiti wa kilimo kutoka Afrika Kusini, Mr. Rugeng Mjinja Zuma, wakati akiwasilisha utafiti wa kilimo mwaka 1999, chuo cha kilimo, nchini humo.   Akasema, kama mataifa yana baba wa taifa, basi kwenye kilimo, baba wa taifa ni maji.   Kelvin John Musetepe wa Burundi mtaalamu wa kilimo cha umwagiliaji, mwaka 2000, alimwambia Waziri wa kilimo nchini humo, kama hakuna maji, basi hakuna kilimo.   Waziri huyo, alikuwa ameshaondolewa kwenye nafasi ya uwaziri wa maji, miezi mitatu iliyopita, jambo lililomkasirisha.   Rais wa awamu ya nane ya Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, wakati akilihutubia Baraza la Wawakilishi, aliiagiza wizara husika, kuhakikisha huduma ya maji, iko vizuri.   ‘’Sasa huduma ya maji sio tu kwa ajili ya matumizi ya ndani, kama kupikia na kunywa, sasa ni kwa ajili ya ku...

LEO NI SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI, HAYA UNAYAJUA?

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ KILA ifikapo Juni 5 ya kila mwaka, Zanzibar huungana na nchi nyingine, kuadhimisha siku ya mazingira duniani.   Siku hii kwa mujibu wa mitandao ya kijamii, ilianzishwa mwaka wa1972, ambapo ni miaka 54, sasa imeshapita.   Iliasisiwa wakati wa mkutano wa Stockholm wa Umoja wa Mataifa, tena kuhusu mazingira ya binadamu nchini Sweden.   Inafafanuliwa kuwa, pia mkutano huo, ulipitisha azimio la kuunda  United Nations Environment Programme (UNEP),  ili kuongeza juhudi za kimataifa za kupamba na uhifadhi wa mazingira.   Aidha mtandao wa dcc.go.tz unaripoti kuwa, sherehe rasmi ya kwanza, ilifanyika mwaka wa 1973 chini ya kaulimbiu “Dunia Moja Pekee ”.   Tena tarehe hii, imekuwa jukwaa la kimataifa la kuhamasisha jamii, kuchukua hatua za kulinda , kuhifadhi mazingira na kuendeleza uendelevu wa rasilimali za asili.   UNEP, inahimiza jamii kuchukua hatua kali dhidi ya wale wachafuzi, wah...