NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAKIKUNDI cha ufugaji wa majongoo bahari, ‘ tumuombe mola’ cha Makangaale wilaya ya Micheweni Pemba, wanatarajia kujipatia shilingi milioni 20 mwishoni mwa mwaka huu, ikiwa watafanikiwa kuuza bidhaa hiyo, baada ya kuekeza vifaranga vyenye thamani ya shilingi million 1.6 mwaka jana. Fedha hizo, ni uwekezaji wa vifaranga 3,300 vya majongoo habari, walivyovinunua kwa shilingi 1,650,000 wastani wa shilingi 500 kila kifaranga kimoja, chenye urefu kati ya nchi nne hadi tano. Wanakikundi hao cha ‘ tumuombe mola ’ wamesema kati ya vifaranga hivyo, wanatarajia kuvuna majongoo yaliokwisha pevuka 2,500 na kisha kila moja kuliuza kwa bei ya shilingi 8,000 na kujipatia shilingi milioni 20. Mwenyekiti wa kikundi hicho Hator Hassan, alisema haiwezekani kuotesha vifaranga vya idadi 3,300 kisha kuvuna kama ilivyo. ‘’Zipo changamoto kama za kufa na hasa wakati wa usafirishaji wa vifaranga kutoka eneo moja kwenda kwenye bwawa lao, wizi na wingine kufa kabla ya kufikia k...
NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ SHILINGI milioni 107,190,000 zilizotarajiwa kukusanywa na Baraza la Manispaa Chake chake Pemba, kuanzia mwezi Novemba, 2023 hadi Januari mwaka huu, hazikupatikana, baada ya wajasiriamali kugoma kukitumia kituo chao cha Michakaini, kwa wakati. Imebainika kuwa, kituo hicho kipya kilichojengwa kwa ajili yao, kina milango 63 ya maduka, ambapo kila mmoja Baraza lilikusudia kuukodisha kwa shilingi 50,000 ili lijipatie shilingi milioni 3,150,000 kwa kila mwezi mmoja. Ingawa imebainika, baada ya wajasiriamali hao kukataa kuingia kituoni humo, Baraza hilo, kuanzia mwezi Novemba, 2023 hadi Januari mwaka huu, limeshapoteza shilingi milioni 85,050,000. Aidha mapato ya shilingi ya milioni 22,140,000 nayo hayakukusanywa na Baraza hilo kwa kipindi hicho, yaliokuwa yatokane na vizimba ‘ vikuta ’ 82, ambapo kila kimoja, kilitarajiwa kukukodishwa kwa shilingi 10,000 kwa wajasiriamali. Ikafahamika kuwa, vikuta hivyo kama vyengepata wajasiriamali, kw...