NA MWANDISHI MAALUM, ZANZIBAR Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto leo Mai 07 imekaa kikao kazi na Benki ya Dunia kwa ajili ya kupitia mipango ya utekeleza ya Mradi wa Kukuza Usawa wa Kijinsia Tanzania- PAMOJA, unaotekelezwa na Wizara hiyo kwa Kushirikiana na Wakala wa Uwezeshaji KIuchumi (ZEEA). Akizungumza katika kikao kilichofanyika katika Ukumbi wa Mradi wa PAMOJA Kinazini, Unguja. Mkurugenzi Idara ya Mipango, Sera na Utafiti, Wizara ya Maendeleo, Jinsia, Wazee na Watoto Ndugu Daima Mohammed Mkalimoto amesema kilao hicho kimeleta tija kutokana na michango ya wadau iliyotolewa ili kuhakikisha utekelezaja wa Mradi unawanufaisha walengwa walikusudiwa wakiwemo wanawake na watoto. Ameeleza kwamba Mradi wa PAMOJA unalengo la kuwainua wanawake kiuchumi kupitia ZEEA, pia luwalinda na kuwahifadhi wahanga wa matukio hayo, hivyo Benki ya Dunia wametoa maelekezo kwaajili ya kuleta ufani. Naye Mratibu wa Mradi wa PAMOJA Ndugu Aisha Abbas Seif amesema k...
NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ MRATIBU Idara ya mashirikiano ya sekta ya umma na binafsi Said Salum Mohamed , amewataka waandishi wa habari kutumia vyema kalamu zao katika kutoa elimu kwa jamii kuhusiana na mashirikiano baina ya serikali na sekta binafsi, katika uwekezaji wa masuala ya kijamii na kiuchumi ili wananchi kupata huduma bora zinazosimamiwa na sekta hiyo. Ameyasema hayo alipokuwa akizungimza na wadau wa habari katika mafunzo yakuwajengea uwezo kuhusiana na mashiashirikiano baina ya sekta za umma na binafsi yaliyofanyika ukumbi wa wakala uwezeshaji wananchi kiuchumi G omban i Chakechake Pemba. Alisema kuwa sekta za umma na binafsi imekuwa na mipango ya kutoa huduma bora za kijamii na kiuchumi ili wananchi wapate huduma hizo zenye kuleta maendeleo. "Hizi taarifa ziwafikie jamii na wawekezaji katika kutoa huduma bora za kijamii na kiuchumi kwa kuyafikia malengo ya serikali ili wananchi wapate maendeleo,"alifafanua. Alifafanua kuwa uwekezaji wa umma na binafsi Pu...