Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

MRADI WA ‘PAMOJA’ WABISHA HODI PEMBA, WAANZIA WILAYA YA CHAKECHAKE KWA MAJARIBIO, WANANCHI WAUFURAHIA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ TAKWIMU kutoka Mtakwimu Mkuu wa serikali Zanzibar, zinaendelea kutishia usalama wa wanawake na watoto wa Unguja na Pemba. Maana, kwa miaka mkitatu iliyopita, imekusanya matukio 4,991 ya ukatili na udhalilishaji, ambao wengi wa waathirika ni wanawake na watoto. Ijapokuwa, namba inaonesha kupungua kila mwaka kwa miaka hiyo, lakini kwa juhudi za serikali, washirika wake wa maendeleo, taasisi binafsi na mtu mmoja mmoja, bado maumivu yapo. Maana mwaka 2023, ilikusanya matukio 1,954 ingawa mwaka uliofuata, yalishuka na kuripotiwa matukio1,8 09, na mwaka jana, yakashuka tena na kuripotiwa matukio 1,228. Utaona kuwa, mwaka 2023, matukio 1,954, yalioripotiwa, ingawa mwaka 2024 kulikuwa na mapungufu ya matukio 145, maana yalikuwa 1,809 na mwaka 2025, kukiripotiwa pungufu ya 581 kati ya yale yaliokusanywa 1,228. Hapo sasa, ndio maana kwa Zanzibar nzima, ukiyakusanya matukio hayo kwa kipindi kuanzia mwezi Januari 2023 hadi Disemba 2025, utabaini matukio ...
Recent posts

HAYA HAPA MAGUMU YA UDHALISHAJI WANAYOPITIA WANAWAKE WAJASIRIAMALI

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ UKATILI na udhalilishaji dhidi ya wanawake na wasichana unasalia kuwa kitendo cha ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu duniani kote. Ambapo kila mwaka makadirio ya wanawake milioni 316 sawa na asilimia 11 ya wanawake wenye umri wa miaka 15 hadi 45, hukutana na vitendo hivyo duniani kote, kwa mujibu wa mitandao ya kijamii. Udhalilishaji huo unaweza kua wa kimwili, kingono au kihisia. Takwimu za mwaka 2024 za Shirika la Afya Duniani (WHO), zinaonyesha mwanamke mmoja, kati ya watatu amewahi kufanyiwa ukatili huo katika kipindi cha maisha yake. Kwa mujibu wa takwimu za ukatili na udhalilishaji wa kijinsia Zanzibar, zilizotolewa na ofisi ya Mtakwimu mkuu wa serikali,   mwaka 2024 kulikuwa na 1,809 ya ukatili na udhalilishaji wameripotiwa. Takwimu hizi zinaonyesha waathirika wengi walikua watoto ambao ni asilimia 84.3 ikifuatiwa na wanawake ambao ni asilimia 11.7. Aidha utafiti uliofanywa na shirika lisilo la kiserikali, linaloendeleza us...

MABODI: ‘IPIGENI 119 KUTOA TAARIFA ZA DAWA ZA KULEVYA’

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI kisiwani Pemba, waetakiwa kuipiga nambari 119, ambayo ni bure, wanapoona kuna viashiria au mtumiaji, muuzaji, msambaazaji na muingizaji wa dawa za kulevya nchini. Ushauri huo umetolewa leo Juni 13, 2026 na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Maryam Juma Abdalla ‘ MABODI’ , wakati akizungumza na wananchi hao, uwanja wa Gombani Chakechake, kwenye uzinduzi wa siku ya kimataifa ya kupinga dawa za kulevya. Alisema, kwa upande wake serikali imeshaweka mikakati kadhaa, ikiwemo kuanzisha nambari hiyo bure kwa ajili ya kupokea taarifa, za dawa za kulevya. Alieleza kuwa, nambari hiyo iko wazi saa 24, na wananchi watakaoipiga watapokelewa na kupewa ushirikiano, ikiwa ni sehemu ya mapambano dhidi ya dawa za kulevya. ‘’Tukiwa ndani ya uzinduzi wa kampeni ya kupinga matumizi, usambaazaji, uingizaji, uuzaji wa dawa za kulevya, leo itumie nambari hiyo bure, ili kuwaokoa vijana wetu,’’alisisitiza. Aidha Katibu Mkuu huyo, alisem...

NYEZUMA: ‘MRADI WA ‘PAMOJA’ NI WA AINA YAKE KUPAMBANA NA UDHALILISHAJI’

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MTAALAMU wa Masuala la Jinsia, kupitia Mradi wa ‘Pamoja’ wa kukuza usawa wa kijinsia Zanzibar, Nyezuma Simai Issa, amesema Mradi huo, ni wa aina yake, na utapunguza wimbi la ukatili na udhalilishaji, pindi utakapomalizika. Mtaalamu huyo, aliyasema hayo leo Juni 11, 2026 ukumbi wa Samail Gombani Chakechake Pemba, wakati akielezea muhutasiri ya utekelezaji wa mradi huo, kwa Kamati teule ya wilaya ya Chakechake, ya utekelezaji wa mradi huo. Alisema, jambo jipya ambalo limo ndani ya mradi huo, ni ujenzi wa vituo vinane, vya makuzi na malezi ya awali ya mtoto, ambapo kila wilaya kitajengwa kimoja. Alisema, lengo la kituo hicho ni kuwapa nafasi wazazi na walezi, kujiendeleza kiuchumi, wakiwa na uhakika wa malezi kwa watoto wao. ‘’Kupitia mradi huu wa miaka mitano, jambo kubwa ambalo limo pamoja na mingine mazuri, tutajenga vituo vinane, kwa wilaya zote nane, zilizopotiwa na mradi huu,’’alifafanua. Aidha Mtaalamu huyo, alisema jambo jingine ambal...