NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI kisiwani Pemba, waetakiwa kuipiga nambari 119, ambayo ni bure, wanapoona kuna viashiria au mtumiaji, muuzaji, msambaazaji na muingizaji wa dawa za kulevya nchini. Ushauri huo umetolewa leo Juni 13, 2026 na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Maryam Juma Abdalla ‘ MABODI’ , wakati akizungumza na wananchi hao, uwanja wa Gombani Chakechake, kwenye uzinduzi wa siku ya kimataifa ya kupinga dawa za kulevya. Alisema, kwa upande wake serikali imeshaweka mikakati kadhaa, ikiwemo kuanzisha nambari hiyo bure kwa ajili ya kupokea taarifa, za dawa za kulevya. Alieleza kuwa, nambari hiyo iko wazi saa 24, na wananchi watakaoipiga watapokelewa na kupewa ushirikiano, ikiwa ni sehemu ya mapambano dhidi ya dawa za kulevya. ‘’Tukiwa ndani ya uzinduzi wa kampeni ya kupinga matumizi, usambaazaji, uingizaji, uuzaji wa dawa za kulevya, leo itumie nambari hiyo bure, ili kuwaokoa vijana wetu,’’alisisitiza. Aidha Katibu Mkuu huyo, alisem...
NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MTAALAMU wa Masuala la Jinsia, kupitia Mradi wa ‘Pamoja’ wa kukuza usawa wa kijinsia Zanzibar, Nyezuma Simai Issa, amesema Mradi huo, ni wa aina yake, na utapunguza wimbi la ukatili na udhalilishaji, pindi utakapomalizika. Mtaalamu huyo, aliyasema hayo leo Juni 11, 2026 ukumbi wa Samail Gombani Chakechake Pemba, wakati akielezea muhutasiri ya utekelezaji wa mradi huo, kwa Kamati teule ya wilaya ya Chakechake, ya utekelezaji wa mradi huo. Alisema, jambo jipya ambalo limo ndani ya mradi huo, ni ujenzi wa vituo vinane, vya makuzi na malezi ya awali ya mtoto, ambapo kila wilaya kitajengwa kimoja. Alisema, lengo la kituo hicho ni kuwapa nafasi wazazi na walezi, kujiendeleza kiuchumi, wakiwa na uhakika wa malezi kwa watoto wao. ‘’Kupitia mradi huu wa miaka mitano, jambo kubwa ambalo limo pamoja na mingine mazuri, tutajenga vituo vinane, kwa wilaya zote nane, zilizopotiwa na mradi huu,’’alifafanua. Aidha Mtaalamu huyo, alisema jambo jingine ambal...