NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@ MWENYEWE Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi kwenye hutuba yake ya ufunguzi wa Kituo cha wajasiriamali Chake chake, alielezea kufarajika. Mbele ya umati wa wajasiriamali na wananchi wa mkoa wa kusini Pemba, ameelezea kuwa, sasa atapa usingizi baada ya kumalizika kwa kituo hicho. ‘’Leo nimefarajika kuona sasa kituo hichi kipya na cha kisasa, nakifungua rasmi, sasa wajasiriamali wa mji wa Chake chake, waliokuwa wakihangaika huku na kule wamepata utulivu,’’akasisitiza. Eneo jingine Dk. Mwinyi wakati wa hafla ya uzinduzi wa kituo hicho, mwezi Oktoba 2023, akatoa rai kama sio maagizo kwa Baraza la Manispaa Chake chake. Moja, akaanza kusisitiza kwa watendaji, kuhakikisha usafi unafanyika kwa udhati, ili wananchi watakaofika hapo, wasishuhudie uchafu kuzagaa. Jingine akaelekeza, watendaji wa Manispaa na Halmashauri, kuhakikishe, hakuna hata mjasiriamali mmoja, anaepanga bidhaa zake nje ya soko hilo. ‘’Haiwezekani hata kidogo, kuwa w...
NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAKIKUNDI cha ufugaji wa majongoo bahari, ‘ tumuombe mola’ cha Makangaale wilaya ya Micheweni Pemba, wanatarajia kujipatia shilingi milioni 20 mwishoni mwa mwaka huu, ikiwa watafanikiwa kuuza bidhaa hiyo, baada ya kuekeza vifaranga vyenye thamani ya shilingi million 1.6 mwaka jana. Fedha hizo, ni uwekezaji wa vifaranga 3,300 vya majongoo habari, walivyovinunua kwa shilingi 1,650,000 wastani wa shilingi 500 kila kifaranga kimoja, chenye urefu kati ya nchi nne hadi tano. Wanakikundi hao cha ‘ tumuombe mola ’ wamesema kati ya vifaranga hivyo, wanatarajia kuvuna majongoo yaliokwisha pevuka 2,500 na kisha kila moja kuliuza kwa bei ya shilingi 8,000 na kujipatia shilingi milioni 20. Mwenyekiti wa kikundi hicho Hator Hassan, alisema haiwezekani kuotesha vifaranga vya idadi 3,300 kisha kuvuna kama ilivyo. ‘’Zipo changamoto kama za kufa na hasa wakati wa usafirishaji wa vifaranga kutoka eneo moja kwenda kwenye bwawa lao, wizi na wingine kufa kabla ya kufikia k...