NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MTAALAMU wa Masuala la Jinsia, kupitia Mradi wa ‘Pamoja’ wa kukuza usawa wa kijinsia Zanzibar, Nyezuma Simai Issa, amesema Mradi huo, ni wa aina yake, na utapunguza wimbi la ukatili na udhalilishaji, pindi utakapomalizika. Mtaalamu huyo, aliyasema hayo leo Juni 11, 2026 ukumbi wa Samail Gombani Chakechake Pemba, wakati akielezea muhutasiri ya utekelezaji wa mradi huo, kwa Kamati teule ya wilaya ya Chakechake, ya utekelezaji wa mradi huo. Alisema, jambo jipya ambalo limo ndani ya mradi huo, ni ujenzi wa vituo vinane, vya makuzi na malezi ya awali ya mtoto, ambapo kila wilaya kitajengwa kimoja. Alisema, lengo la kituo hicho ni kuwapa nafasi wazazi na walezi, kujiendeleza kiuchumi, wakiwa na uhakika wa malezi kwa watoto wao. ‘’Kupitia mradi huu wa miaka mitano, jambo kubwa ambalo limo pamoja na mingine mazuri, tutajenga vituo vinane, kwa wilaya zote nane, zilizopotiwa na mradi huu,’’alifafanua. Aidha Mtaalamu huyo, alisema jambo jingine ambal...
NA ASHA SALIM- WKUMM, PEMBA@@@@ SEKTA ya kilimo Zanzibar, inaendelea kutumia nyezo muhimu na mipango thabiti, katika kunyanyua wakulima waweze kujikimu na kunufaika kupitia shuhuli za kilimo. Katika kuhakikisha hilo, ushirikiano wa karibu kupitia washirika mbalimbali wa maendeleo na miradi inayosainiwa na serikali ya Mapinduzi Zanzibar, kusaidia utekelezaji wa sekta hiyo zinaonekana. Juhudi hizo, zinaendelea kwa ushirikiano wa karibu, kupitia idara zake, zinazotekeleza majukumu yake chini ya wizara hiyo, na sasa serikali kujivunia kufikia mafanikio makubwa ya kiuchumi. Eeneo ambalo, serikali imekuwa na mfano mzuri wa utendaji kazi, ni kushughulikia kwa karibu msitu wa hifadhi ya Ngezi Micheweni. KWANI MSITU WA NGEZI ULIANZIA WAPI Taarifa zilizopo kwenye tovuti ya ‘ Ngezi Vumawimbi Heritage Organization , zinaeleza kuwa, m aeneo yanayozunguka msitu wa Ngezi, kumbe yamekaliwa kwa muda mrefu sana na Waarabu au Waajemi waliowahi kuishi. Infaghamika kuwa, kupitia tovuti...