Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

TAMWA YAWAPA MAFUNZO YA UWAJIBIKAJIN MADIWANI NA WARATIBU WANAWAKE

NA MOZA SHAABAN, PEMBA MADIWANI wakuchaguliwa na waratibu wanawake na watoto kutoka wilaya nne za Pemba   wametakiwa kuwajibika ipasavyo katika utekelezaji majukumu yao ya msingi ya kiuongozi, ili kujenga imani kwa jamii juu ya uwezo alionao mwanamke katika kuongoza na kuleta maendeleo. Wito huo umetolewa na Afisa Progamu wa mradi wa kuhamasisha ushiriki wa wanawake katika masuala ya uongozi (SWIL) unaotekelezwa na TAMWA-Zanzibar Sabrina Ali Mwatanga wakati wa mafunzo   kwa madiwani na waratibu wanawake na watoto kutoka wilaya nne za Pemba, yaliolenga kuwajengea uwezo juu ya namna ya kuwajibika ipasavyo katika uongozi wao, yaliofanyika katika ukumbi wa mikutano TAMWA Mkanjuni Chake chake Pemba. Alieleza mafunzo hayo ni mwendelezo wa hamasa na kuwajengea uwezo madiwani na waratibu hao juu namna bora ya kutekeleza majukumu yao ya kiongozi, ili jamii ione ufanyaji kazi wao kivitendo. Afisa huyo alisema   TAMWA imekua ikifanya juhudi kubwa katika kuwajengea uwezo wana...
Recent posts

CANADA YAKABIDHI VIFAA VYA SH/= MILION 270 VYA UCHUMI WA BULUU

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ SERIKALI ya Canada, imesema itaendelea kushirikiana na serikali za Tanzania, katika maeneo mbalimbali, ikiwemo kwenye uchumi wa buluu, ili walengwa wakuze pato lao na taifa. Hayo yameleezwa leo Juni 23, 2026 na Balozi wa taifa hilo, nchini Tanzania Emily Burns, kwenye hafla ya ugawaji wa vitendea kazi kwa vikundi vya wajasiriamali, waliokeza kwenye bahari, na ufunguzi wa kituo cha mafunzo eneo la Chamanangwe wilaya ya Wete Pemba. Alisema, ushirikiano huo, anaamini utawasaidia wajasriamali waliokeza kwenye eneo hilo, hasa wanawake na vijana, ambao kwa muda mrefu walikuwa hawakuhusishwa moja kwa moja. Alieleza kuwa, kwa eneo la Zanzibar na baadhi ya mikoa ya Tanzania bara, ilivyozungurukwa na bahari, wakati umefika manufaa yake, yawanufaishe makundi yote. ‘’Serikali ya Canada, inaziahidi serikali zote mbili kwamba, ushirikiano huu kwenye sekta ya uchumi wa buluu, utakuwa endelevu pamoja na maeneo mingine,’’alifafanua. Katika hatua nyingine, B...

MABWENI KWA WANAFUNZI YAPUNGUZA VITISHO VYA UBAKAJI, YAWAPA UHAKIKA WA MAKAAZI

    NA MOZA SHABAN, PEMBA@@@@ SERIKALI ya awamu ya nane, imekuwa ikigeuza sekta ya elimu kwa vitendo, ikiwemo ujenzi wa dahalia. Maana lengo hasa ni kuwapunguzia umbali wa kutembea masafa marefu wanafunzi, pale wanapokwenda na kurudi skuli. Dahalia hizo, zimekuwa zikiwasaidia wanafunzi hao, katika kuongeza ufaulu na maarifa ya kujifunza, masomo yao na kupata utulivu, wa kujiepusha na vitisho vya udhalilishaji. Maana alishasema mara kadhaa, Ofisa Mdhamini wa wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba, Mohamed Nassor Salum kuwa, wamekuwa wakipokea kesi za vitisho vya ubakaji kwa wanafunzi. Anasema, wapo wanafunzi hasa kuanzia kidato cha nne, wamekuwa wakiviziwa vichakani, iwe wanapokwenda ama wanaporudi masomoni. ‘’Mazingira haya ya ujenzi wa dakhalia, ni kuwahakikishia ulinzi wao, maana mingi yapo karibu mno na skuli, wanazosoma,’’anasema. Anakiri kuwa, wahalifu wa ubakaji, walishazoea kutumia vichaka, ili kuwadhalilisha wanafunzi. ‘’Sasa wanafunzi wetu hasa wa...

WASICHANA NA ELIMU YA JUU, VIGINGI NA MASHIMO YA KUWAKATISHA TAMAA YAZIDI

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ RIPOTI ya Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto ‘UNICEF’, lile la masuala ya wanawake, UN-Women na shirika la Plan International, inaonesha idadi ya wasichana wanaoandikishwa skuli, kwa sasa ni kubwa kuliko wakati wowote. Ripoti hiyo iliotolewa mwaka 2020, inaeleza idadi ya wasichana watoro skulini tangu mwaka 1995 imepungua na sasa wasichana wana fursa ya kusoma skuli za sekondari, kuliko wavulana. HALI ILIVYO NCHINI Mitandao inaripoti, kiwango cha wanafunzi wanaojiunga na elimu ya sekondari nchini Tanzania ina uwiano nzuri, ambapo wasichana hufikia karibu nusu ya wanafunzi wanaosajiliwa. Hata hivyo, kutoka elimu ya msingi hadi sekondari kwa ujumla asilimia 56 ni ya wasichana, huku asilimia 34 pekee ndio wanaomaliza elimu ya sekondari. Huku mitandao ikiripoti, hata Zanzibar kunauwiano mzuri wa wasichana wanao jiunga na masomo ya sekondari, kati yao na wavulana. Idadi ya wanaomaliza na kufaulu ni pungufu ikilinganishwa na wavulan...

WAFANYABIASHARA WANAWAKE MASOKONI WATAKIWA KUTOVUMILIA VITENDO VYA UDHALILISHAJI

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ WANAWAKE wanaofanya biashara katika masoko ya Mjini Wete na Kifumbikai Wilaya ya Wete Kaskazini Pemba, wameshauriwa kuripoti   vitendo vya ukatili na udhalilishaji kwa viongozi wao wa masoko, ili kuchukua hatua zaidi katika kukabiliana navyo. Ushauri huo umetolewa na Msimamizi wa masoko na mazingira Wilaya ya Wete Sadri Mussa Said,   wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake Wete Kaskazini Pemba. Alise katika masoko yote kuna viongozi waliochaguliwa kwa ajili ya kusimamia wafanyabiashara na kuwatatulia changamoto zao mbali mbali za kimazingira na kinidhamu, hivyo ni vizuri kuwatumia ili kupata msaada wa changamoto hizo wanapokua katika shughuli zao za kibiashara. "Masoko yote kuna viongozi waliochaguliwa kwa ajili ya kusimamia wafanyabiashara na kuwatatulia changamoto zao mbali mbali za kimazingira na kinidhamu, hivyo   tunawashauri wanawake kuwatumia kuripoti matukio ya udhalilishaji yanapotokezea, ili kupata m...