Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

UMEWAHI KUHADITHIWA KUHUSU CHAKULA AINA YA MWATA, WANAUME WAPIGANA FOLENI SUPU YAKE

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ “NIWEKEE kisongo pawa 2000, supu weka nyingi na pili pili kwa mbali na kiungwa”, lugha za kuagizia supu ya Mwata. Sio lugha ngeni kwa wafanya biashara na watu wanaouza supu hiyo ya Mwata hususan katika maeneo ya Kangani na vitongoji vyake. Wenyewe hutumia jina la “kisongopawa”kama umaarufu lakini jina halisi ni Mwata, ndilo watu wengi kutoka maeneo mbali mbali hufahamu kwa haraka. Na jina la kisongopawa si rasmi na si lenye kufahamika isipokua kwa wenyeji wa maeneo ya Kangani na jirani ambako   ndio mwata huvuliwa na kuliwa . Mwata ni   aina   ya viumbe vipatikanavyo pwani, ambacho hutumiwa kwa ajili ya chakula au kitoweo kama ilivyo viumbe vingi vya baharini, ingawa umetofautiana navyo kwa kiasi kikubwa hata uvuvi wake. Mwata kisiwani Pemba hupatikana zaidi na kuhesabiwa kama ni kitoweo adhimu katika Pwani ya Jemele iliopo shehia ya Kangani wilaya ya Mkoani mkoa wa kusini Pemba. Ingawa baadhi ya watu hueleza yapo maeneo min...
Recent posts

KUMBE MKAMANDUME ALIKIMBIA VITA IRAN KUJIFICHA PEMBA?

      NA RAHEME MOHAMED, PEMBA   MOHAMMED bin Abrahman umaarufu "Mkamandume"   Ni mshirazi kutoka katika nchi ya Iran, mfalme ambae alifika katika kisiwa cha Pemba mwishoni mwa karne ya 15, yaani miaka 600 iliyopita.   Alifikia mji wa Pujini, kijiji cha Kijito Kame ambapo alikuwa pamoja na mke wake na mtoto wao mmoja.   Mtoto ambae alijulikana kwa jina la Haroun bin Mohammed bin Abrahman, na hadi kufikia sasa jina halisi la mke ambae alifikanae kutoka Iran halijafahamika.   Mfalme Mkamandume, walitoka nchi Iran kwa sababu kulikuwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe na kuamua kuingia katika mwambao wa Afrika Mashariki, kutafuta hifadhi.   Walifika hapo pamoja na familia yake kwa kutumia usafiri wa majini na chombo, ambacho walitumia ilikuwa ni jahazi.   Huo ndio usafiri mashuhuri ulioukitumika katika enzi hizo, kwani hakukuwa na mwingine zaidi ya jahazi.   Walifikia katika mji wa Pujini, kijiji cha ...

POSA ZA MICHEWENI ZA ZAMANI, WANAWAKE WAKIKUTANA NA WANAUME SIKU YA ARUSI

         NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ‘’NILIVUNJIKA mkono, baada ya kuparamia nyumba kumkimbia muume mtarajiwa alipokuja kwetu, ili tusionane,’’anasema Saada Khsmi Kombo (65) wa Micheweni. Hadi leo mkoni wake mmoja wa kushoto, eneo vilipootea vidole hapako sawa, baada ya ajali hiyo. Kwa utamduni ulivyokuwa enza hizo, ilikuwa mwanaume hata kwa ambae alishabisha hodi na kuweka nia ya kufunga ndoa, haikuwa rahisi, kukutana na mtarajiwa wake. Ndio maana Saada anasema, alilazimika kwenda mbio nyingi, kwani hakuwa na hamu ya kukutana na mume wake mtarajiwa, hasa kutokana na malezi yalivyokuwa. KWANINI ILIKUWA HAWAONANI? Rehema Faki Sheha (60), baada ya muume kuweka nia na posa kufuata, hapo mwanamke hukosa hamu hata ya kula, na hakukua na jambo la ushawishi la kukutana nae. Anasema huo ndio utamaduni wa Micheweni, na wao wakiurithi tokea enzi na karne, ingawa hayo anasema ilitokana na mafundisho ya wazazi wao. Walikuwa wakielezwa, kuwa mara baada ya ...

HISTORIA PANGO LA KIJIJI MAKANGALE, INASISIMUA, INATISHA

  NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ PANGO la kijij, linalopatikana shehia ya Makangale, kaskazini  mwa Pemba. Ni mojawapo ya kivutio cha kihistoria vyenye hadithi ya kipekee. Umaarufu wa pango hili, ulianza mwaka 2009 baada ya Profesa Felix Chami wa Chuo Kikuu cha Dar- es Salaam, kugundua mabaki ya kihistoria, ikiwemo mifupa ya wanyama, shanga, mkaa, na vigae vinavyoashiria uwepo wa makazi ya binadamu katika vipindi tofauti vya kihistoria kwenye pango hilo. Kwa mujibu wa historia, pango hili lilitumiwa na wapiganaji wa vita ya kwanza ya dunia 1914 hadi mwaka 1918. Na baadae vita ya pili ya dunia yam waka 1939 hadi mwaka 1945, kama maficho yao na pia sehemu ya kuficha silaha. Leo hii, pango la kijiji Makangale limekuwa kivutio kikubwa cha watalii, wanaotembelea hasa hoteli za kaskazini Pemba, hufika kushuhudia uzuri na historia ya pango hilo, lenye milango miwili wa kuingilia na wa kutokea. Idara ya Makumbusho na Mambo ya Kale Pemba imeboresha njia za kuingia pangoni ...