NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANUFAIKA wa sadaka ya nyama ya Ng’ombe, zaidi ya 189 wa shehia za Wambaa na Chumbageni wilaya ya Mkoani Pemba, wamepongeza hatua ya jumuiya ya udhu-hiya ya shehia hizo, kwa kukamilisha bila ya kasoro, zoezi la ugawaji wa sadaka hiyo. Walisema, wamefakiniwa kupata nyama hivyo kwa ajili hya kukamilisha mlo wa sikukuu, tena kwa wakati, jambo ambalo walijiona sawa na wingine, wenye uwezo wa kifedha. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, kwa mashatri ya kutochapishwa majini yao, mara baada ya kupokea sadaka hiyo, walisema walipatiwa wastani kilo 1.5, ambayo wingi wao walipata na sikukuu ya pili. Walisema, uwepo wa Jumuiya hiyo, kwa miaka mitatu mfululizo sasa, imekuwa ikiwahakikisha kupata kitoweleo, jambo ambalo kama sio sadaka hiyo, wapo wanaokula dagaa kavu ama samaki siku hiyo. Walisema, hatu hiyo imekuwa ikiwarahisishia maisha walau kwa siku mbili za sikukuu, jambo ambalo hujiona ni sawa na wingine wenye uwezo. ‘’Kwa hakika, juzi nilipokea...
NA MWANDISHI MAALUM, UNGUJA Maofisa kutoka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) ofisi ya Zanzibar, wamewapa elimu ya haki za binadamu na misingi ya utawala bora Wanafunzi 454 wa Skuli za sekondari kwa Mikoa mitatu ya Unguja. Wakizungumza kwa nyakati tofauti kupitia Serikali za wanafunzi wa Skuli 11 za mikoa hiyo, Maofisa hao waligusia zaidi katika mada za kukuza, kulinda, kuheshimu, na kuhifadhi haki za wengine. Pia maofisa hao waliwaeleza wanafunzi kwa upana kuhusu THBUB, kazi na majukumu yake katika kulinda haki za binadamu sambamba na wajibu wa wanafunzi hao katika kuzitekeleza na kuziishi haki hizo. Akiizungumzia haki ya msingi ya mwanadamu, haki ya kuisha Ofisa Sheria THBUB, Fatma Sultan Mwesimba aliwaeleza wanafunzi hao kwa haki hiyo inaaza mara moja baada ya binadamu kuzaliwa nakuongeza kuwa haki hiyo haipokonyeki ina inapaswa mtu kuendelea kuishi nayo na haipaswi kuvunjwa kwa namna yoyote ile isipokua iamuliwe kupitia sharia za nchi. Pia aliongeza kwa ...