Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

'THBUB' YAWAHIMIZA WAZAZI, WALEZI KUVUNJA UKIMYA DHIDI YA UDHALILISHAJI WA WATOTO

NA MWANDISHI MAALUM, ZANZIBAR@@@@ AFISA Uchunguzi kutoka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) Ofisi ya Zanzibar, Abdul-latif Ali Sheha amewasihi wazazi na walezi wa Shehiya ya Kinuni, kujenga utamaduni wa kuzilinda na kuziishi haki za watoto kwa vitendo. Abdullatif alitoa nasaha hizo kwa wazazi na walezi 637 katika Madrasatul Thamaraatul Jannah iliyopo Shehia ya Kinuni, Mkoa wa Mjini Magharibi wakati akiwapa hao elimu ya haki za watoto na wajibu wa jamii katika kuzuia vitendo vya ukatili wa watoto na uvunjwaji wa haki za binadamu ikiwa ni mwendelezo wa kutoa elimu na msaada wa sheria wakati wa mwendelezo wa zoezi la Kampeni ya Msaada wa Kisheria wa Mama Samia Awamu ya Pili (MSLAC II) unaoendelea katika Wilaya tatu za Mkoa wa Mjini Magharibi. “Mtoto ana haki ya kuishi katika mazingira salama, kupatiwa elimu na kulindwa dhidi ya aina zote za unyanyasaji" Alisisitiza bw. Abdullatif. Pia aliwaeleza wazazi hao kuwa jamii inapaswa kuachana na tabia ya kuoneana muhali ...
Recent posts

ANGUKO LA UCHUMI LA WANAWAKE HUANZIA HAPA

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ KATIKA zama hizi, wanawake wanakabiliwa na changamoto kadhaa, ikiwemo utelekezwaji. Ambao kwa kiasi kikubwa, unaathari za moja kwa moja katika uchumi na ustawi wa maisha yao. Mara nyingi, utelekezwaji huo hufanywa na wanaume kutokana na sababu kadhaa, huku wengi wa wanaotelekezwa, wakitupia lawama ndoa za mke zaidi ya mmoja. Katika hili, wanawake wengi waliofanya mahojiano na mwandishi wa makala hii, ambao wamewahi kutelekezwa walisema, chanzo ni ndoa za mke zaidi ya mmoja. Huku Afisa ustawi wa jamii wilaya ya Wete Salma Saleh Hamad akigongea msumari kuwa, katika idadi ya mashauri ya kesi za utelekezaji wanazopokea ofisini kwao, asilimia 90 yanaonesha chanzo ni ndoa za mke zaidi ya mmoja. NINI UTELEKEZAJI FAMILIA? Ni kule mtu kushindwa kupeleka mahitaji kwa yule unaepaswa kumpa, hali ya kuwa unauwezo wa kutoa mahitaji hayo. Utelekezaji unaweza kuwa wa moja kwa moja au katika huduma za elimu, afya na hata kihisia. Ingawa Serikali na wad...

KIZUNGUMKUTI TUHMA ZA UKATILI, UDHALILISHAJI KWA KIZIWI MICHEWENI

  SAIDA ALI, PEMBA MAMA mzazi ambae mwanawe mwenye ulemavu wa uziwi wa miaka 38, alifanyiwa vitendo vya ukatili na udhalilishaji, ameviomba vyombo vya ulinzi na usalama, kuwa haki itendeke kufuatia unyama aliodai kufanyiwa, kijana wake. Aliyasema hayo, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, shehia ya Shumba vyamboni wilaya ya Micheweni, kufuatia sitofahamu ya majibu ya hospitali na athari aliyonayo kijana wao. Alisema kuwa kitendo alichodai kufanyiwa kijana wao huyo, ambacho alimshuhudia akiwa amefungwa mikono nyuma akiwa na tambara mdomoni, ni cha kikatili na udhalilishaji. Alieleza kuwa, muda wa saa 8:00 usiku baada ya kusikia kelele za kukorota kwa kijana wake, alikimbilia chumbani kwake, na kufika alijonea maajabu. ‘’Kwanza alikuwa amevungwa mwiili mzima nguo nyeusi mithili ya beibui, nilishuhudia vichupa vidogo viwili, kimoja kikiwa na majimaji, (dawa) nusu na chingine kikiwa kitupu,’’alifafanua. Aidha mzazi huyo alisema, jingine ambalo limemshitua kwa kij...

TAMWA YAWAPA MAFUNZO YA UWAJIBIKAJIN MADIWANI NA WARATIBU WANAWAKE

NA MOZA SHAABAN, PEMBA MADIWANI wakuchaguliwa na waratibu wanawake na watoto kutoka wilaya nne za Pemba   wametakiwa kuwajibika ipasavyo katika utekelezaji majukumu yao ya msingi ya kiuongozi, ili kujenga imani kwa jamii juu ya uwezo alionao mwanamke katika kuongoza na kuleta maendeleo. Wito huo umetolewa na Afisa Progamu wa mradi wa kuhamasisha ushiriki wa wanawake katika masuala ya uongozi (SWIL) unaotekelezwa na TAMWA-Zanzibar Sabrina Ali Mwatanga wakati wa mafunzo   kwa madiwani na waratibu wanawake na watoto kutoka wilaya nne za Pemba, yaliolenga kuwajengea uwezo juu ya namna ya kuwajibika ipasavyo katika uongozi wao, yaliofanyika katika ukumbi wa mikutano TAMWA Mkanjuni Chake chake Pemba. Alieleza mafunzo hayo ni mwendelezo wa hamasa na kuwajengea uwezo madiwani na waratibu hao juu namna bora ya kutekeleza majukumu yao ya kiongozi, ili jamii ione ufanyaji kazi wao kivitendo. Afisa huyo alisema   TAMWA imekua ikifanya juhudi kubwa katika kuwajengea uwezo wana...

CANADA YAKABIDHI VIFAA VYA SH/= MILION 270 VYA UCHUMI WA BULUU

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ SERIKALI ya Canada, imesema itaendelea kushirikiana na serikali za Tanzania, katika maeneo mbalimbali, ikiwemo kwenye uchumi wa buluu, ili walengwa wakuze pato lao na taifa. Hayo yameleezwa leo Juni 23, 2026 na Balozi wa taifa hilo, nchini Tanzania Emily Burns, kwenye hafla ya ugawaji wa vitendea kazi kwa vikundi vya wajasiriamali, waliokeza kwenye bahari, na ufunguzi wa kituo cha mafunzo eneo la Chamanangwe wilaya ya Wete Pemba. Alisema, ushirikiano huo, anaamini utawasaidia wajasriamali waliokeza kwenye eneo hilo, hasa wanawake na vijana, ambao kwa muda mrefu walikuwa hawakuhusishwa moja kwa moja. Alieleza kuwa, kwa eneo la Zanzibar na baadhi ya mikoa ya Tanzania bara, ilivyozungurukwa na bahari, wakati umefika manufaa yake, yawanufaishe makundi yote. ‘’Serikali ya Canada, inaziahidi serikali zote mbili kwamba, ushirikiano huu kwenye sekta ya uchumi wa buluu, utakuwa endelevu pamoja na maeneo mingine,’’alifafanua. Katika hatua nyingine, B...