‘Aweka mikakati wanabaki daraja la kwanza na la pili tu. IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA "Nilipoteuliwa kuwa Mwalimu Mkuu, mwanzo nilipata hofu hasa pale nilipojiona, naenda kuongoza watu wenye kiwango cha elimu sawa na mimi,’’anasema. Ni maneno ya Mwalimu Mkuu skuli ya Sekondari ya Wanawake Utaani Wete, Siti Faki Ali mkaazi wa Chasasa Wete. Mwalimu huyo ambae alitokea skuli ya Chasasa akiwa Msaidizi Mwalimu Mkuu, alipata hofu mara ya kupokea barua ya kwenda kuiongoza skuli hiyo. Anasema, kwa vile ameshakaa uongozi katika mambo mbalimbali ya kijamii na Serikali kwenye nafasi ndogo ndogo, ndipo alipoona kwamba na nafasi hiyo anaweza kuiongoza. Mara baada ya kukabidhiwa madaraka, alianza kuweka mikakati, ikiwemo kuondosha zero kwa wanafunzi kuanzia kidato cha pili hadi cha...
NA ZUHURA JABIR Katika jamii, mara nyingi mafanikio hupimwa kwa kiwango cha elimu, mali au nafasi aliyonayo mtu. Hata hivyo, kuna watu ambao maisha yao yanatufundisha kwamba mafanikio makubwa huanza pale mtu anapoamua kujiamini, kupambana na changamoto na kutokubali mazingira yamzuie kufikia ndoto zake. Hii ni simulizi ya Fatma Suleiman Mussa, mwanamke mwenye ulemavu anayeishi Jumbi, Zanzibar, ambaye licha ya changamoto alizokutana nazo tangu akiwa mtoto, ameamua kutumia uwezo alionao kujiajiri, kusaidia familia yake na kuwa mfano kwa wanawake wengine wenye ulemavu. Safari yake imejaa changamoto, lakini pia ni ushahidi kwamba “ ulemavu si mwisho wa ndoto. ” SAFARI YA ELIMU NA MAISHA Fatma ni mtoto wa pili katika familia ya watoto wanne, wote wakiwa wa kike. Alianza elimu ya msingi katika Skuli ya Tunguu na baadaye aliendelea hadi kidato cha pili mwaka 2015. Alipata nafasi ya kuendelea na kidato cha tatu katika Skuli ya Kibele, lakini changamoto mbalimbali zil...