Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

NJUMA ALI JUMA: MJASIRIAMALI ANAEJIAMINISHA KIMAISHA SASA, AWAPA WOSIA WENZAKE

NA TATU MAKAME. ZANZIBAR@@@ UNAPOZUNGUMZIA ujasiri na ucheshi alionao mwanamke utagundua kuwa ni kiungo muhimu katika jamii hasa kwenye nafasi za uongozi. Aidha wanawake wenye uthubutu wa kufanya harakati za jamii wamekuwa na uwezo mkubwa wa kushawishi jamii kufanya harakati za maisha ili kuendeleza maisha yao katika jamii. Hata hivyo serikali na taasisi binafsi nazo zimekuwa mfano mkubwa kuwahamasisha wananwake kuingia kwenye nafasi za uongozi baada ya kuwapatia mafunzo ya kuwania nafasi za uongozi ili kuachana na mfumo dume wa kuwa mwanamke uwezo wake mdogo kuwa kiongozi. Hata hivyo Mradi wa SWIL unaoimarisha uongozi wa wanawake unaoendeshwa na Chama cha waandishi wa habari Tanzania Tamwa ZNZ nao umekuwa mfano bora wa kuwahamasisha wanawake kuingia kwenye nafasi za uongozi na kuwa kioo kwa jamii. Kwa mujibu wa Mkufunzi kutoka Chuo kikuu cha taifa cha Zanzibar (SUZA) Imane Duwe alisema kiongozi sio lazima awe mwanasiasa au mtu maarufu kama wengine. Hata hivyo alisema wanawake wanaoing...
Recent posts

DIWANI FATMA ''KITOTO'' WADI YA TIBIRINZI: NA SAFARI YA UONGOZI HILI ALITAHADHARISHA KWA WENZAKE

    NA MARYAM SALUM, PEMBA@@@@ ‘ MWA NASIASA hatakiwi kuwa mbaguzi, watu wote ni sawa, ili mwisho wa siku, jamii ikuelewe tu,’’anasema Fatma Khamis Juma Diwani wadi ya Tibirinzi.   ‘’Tabia yangu hupenda kujichanganya iwe kwenye kijiwe cha kahawa, sokoni nipo, masikani za vijana nipo, na makundi mengine yenye rika tofauti. Hii ni kauli ya Fatma Juma Khamis, anayehudumu udiwani wadi ya Tibirinzi, Jimbo la Chake chake, kwa kipindi cha pili mfululizo sasa. Katika siasa, mtu hatakiwi kuwa mbaguzi na badala yake awe kuwa karibu na jamii iliyomzunguruka, kwa maslahi mapana. Anakiri kuwa kuingia kwenye kinyang’anyiro cha siasa, watu wote hupitia changamoto, ikiwemo kuitwa majina mabaya hasa kwa wanawake. Kwenye jamii iliyo kubwa, tafsiri iliyopo, pindi mwanamke akiingia kwenye siasa hubandikwa majina maovu na yenye kukatisha tamaa, au kuwindwa na washindani wake. Diwani Fatma anasema, kwa awamu ya kwanza ya udiwani wake, hakuishia kuomba kura kwa mikutanao ya hadha...

-MKUNGA, MWANAMKE KIONGOZI ALIYEANZA MBALI, AVIRUKA VIGINGI, 2030 KURUDI TENA JIMBONI

  NA MARYAM SALUM, PEMBA@@@@ ‘……kidogo kidogo ndio mwendo……’. Ni msemo wa kiswahili unao maanisha kufanya mambo hatua kwa hatua, subira na umakini   ndiyo njia bora na salama ya kufanikisha malengo. Msemo huu unaenda sambamba na safari ya Mkunga kutoka kazi ya Ualimu, hadi     ulingo wa kisiasa kuwa Makamo Mwenyekiti ngome ya Wanawake Taifa wa ACT.                      TUMJUE MKUNGA. Mkunga Hamad Sadala (65) ni mwanandoa, mchakarikaji, mwenye kujiami asiyekubali kuyumbishwa kwani anajitambua na anajikubali popote. Alizaliwa mwaka 1961 katika Kijiji cha Uvumbi shehia ya Chanjaani Chake Chake, ni mtoto wa tano (5) na wa mwisho katika familia ya mzee Hamad Sadala. Anasema kuwa mnamo mwaka 1966 hadi 1967   wazazi wake walimsomesha elimu   ya awali darasa la kwanza skuli ya Shamiani hadi mwaka 1978 kumaliza kidato cha tatu skulini hapo. Anafahamisha kuwa mwa...

HUYU HAPA MWANAMKE WA ZANZIBAR ALIYEANZISHA CHUO CHA UDEREVA, AELEZEA ALIVYOANZA HADI SASA

  NA TATU MAKAME, ZANZIBAR@@@ UNAPOZUNGUMZIA ukakamavu alionao mwanamke huwezi kusahau jinsia yake kutokana na kazi wanazofanya wanawake katika jamii kutokana na mchango wao kwa taifa. Hata hivyo wanawake wamekuwa na mchango mkubwa wa kuelimisha jamii katika mambo mbalimbali bila kusahahu kuwa wao ni viongozi katika majukumu wanayoyasimamia. Mtazamo wa jamii ni kuwa mwanamke ni kiumbe dhaifu na hawezi kufanya jambo la maendeleo katika jamii inayomzunguuka. Hata hivyo kwa kuwa serikali imekuwa ikitoa kipaumbele kwa viongozi wanawake kuona asilimia 50 kwa 50 inafikiwa jamii imekuwa na mtazamo tofauti kuhusu mwanamke hasa katika kuanzisha mambo mbalimbali katika jamii. Aidha unapozungumzia nafasi za uongozi katika ngazi za jamii huwezi kumsahau Zainab Abdi Salum ambae ni dereva aliyeamua kuanzisha chuo cha udereva kuwaokoa madereva vijana na ajali za barabarani. Zainab alizaliwa mwaka 1984 katika mtaa wa Kisauni Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja na kuanza skuli ya msingi Kiembe Samaki mn...

HANUNA IBRAHIM: KUTOKA SEKRETARI HADI DC. ALIMBWAGA WAZIRI AKAUKWAA UWAKILISHI CHAKECHAKE

    NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@ KATIKATI ya giza nene lililogubika haki ya mwanamke kuwa kiongozi kwa wakati huo, kuna mwanamke alielishinda?. Alisimama kidedea, yeye na waliomzunguka walihakikisha anafanikiwa na kweli alishika nafasi mbalimbali za uongozi, mpaka kuwa mmoja wa viongozi wanawake walioweka alama isiyofutika katika jamii. Ni Hanuna Ibrahim Massoud, alieanza kuliona jua mwaka 1959, Kisiwani kwa Binti Abedi wilaya ya Wete kaskazini Pemba. Alianza kusaka elimu yake ya msingi, mwaka 1965, ambapo aliipata katika skuli tofauti kama Ziwani, Shamiani na Utaani. Mnamo mwaka 1974, alikamilisha elimu yake ya sekondari kidato cha nne, katika skuli ya Fidel Castro. “Safari yangu ya masomo haikuwa na kituo kimoja, nilisoma maeneo mengi, lakini huku kulinifanya kuyajuwa na kuyatawala vizuri mazingira,’’anahadithia. Kumbe wakati huo kuelimika kwa mtoto wa kike hadi kidato cha nne, ilikuwa fursa adimu na nimsingi mkubwa wa ukombozi. Safari yake ya kutafuta elimu, ...