NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ UMEWAHI kuwaza maisha bila kuona, kusikia, kusema au kusimama. Basi hayo ndio maisha ya kila siku ya watu, wenye ulemavu, aidha wa viungo, uoni, uziwi na aina nyengine. Lakini watu wenye ulemavu ni sawa na watu wengine, wanahaki zote za msingi, kama ilivyo kwa wengine. Miongoni mwa haki hizo ni kushiriki katika shughuli za kiuchumi, kama ilivyoelezwa katika mikataba na sheria mbalimbali. Mkataba wa kimataifa wa haki za watu wenye ulemavu wa 2006, ambao ibara yake ya 27 (f) inasisitiza ushiriki na ushirikishwaji wao kiuchumi. “Nchi wanachama wakuze fursa za watu wenye ulemavu kujiajiri, kuanzisha na kuendesha shughuli za ujasiamali, vyama vya ushirika na mtu binafsi kuanzisha biashara zake”, inaeleza sehemu ya mkataba huo. Sheria ya watu wenye ulemavu ya Zanzibar nambari 8 ya mwaka 2022, kifungu cha 28 (e) inaeleza, watu wenye ulemavu wanastahiki haki zote za msingi za kibinaadamu sawa nawatu wengine ikiwemo kujitegemea na kujumuishw...
NA ZUHURA JABIR, ZNAIBAR “Usafi ni nusu ya afya." Haya sio msemo wa utani, bali ni ukweli unaogusa maisha ya kila siku ya wananchi. Mazingira safi yanamaanisha afya bora, heshima ya makazi na maendeleo ya jamii, lakini pale ambapo mifumo ya usimamizi haieleweki, wananchi hubeba mzigo ambao haukupaswa. Majadiliano yaliyowakutanisha masheha, wahamasishaji wa jamii na wataalamu wa Baraza la Manispaa Mjini, yameonesha wazi kuwa changamoto za usafi wa mazingira bado zinahitaji mshikamano. Methali isemayo, "Kidole kimoja hakivunji chawa," inaakisi hali halisi ya mapambano dhidi ya uchafu wa mazingira. MGONGANO WA MAMLAKA KATIKA UKUSANYAJI WA TAKA Moja ya hoja zilizojitokeza kwa uzito mkubwa ni mgongano wa mamlaka katika ukusanyaji wa taka ndani ya shehia ya Mchangani. Kwa mujibu wa sheha Nassir Mohammed Ali, wananchi wanakabiliwa na hali ya kuchanganyikiwa, kutokana na taasisi mbili, Baraza la Manispaa Mjini na Mamlaka ya Mji Mkongwe, kufanya kazi katika ene...