NA TATU MAKAME, ZANZIBAR @@@@ MAMLAKA ya mapato Tanzania (TRA) Tanzania imesema itaimarisha mazingira mazuri kwa wafanyabiashara kuondosha vikwazo kwao. Kamisha mkuu wa Mamlaka hiyo Salehe Juma Mwenda alisema hayo wakati wa kikao cha pamoja kilichowashirikisha watendaji wa mamlaka za kodi Tanzania pamoja na wafa nyabiashara hao kilichofanyika huko hoteli ya Madinat Al bahri Mbweni Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja wenye lengo kusikiliza changamoto za wafanyabiashara. Alisema miongoni mwa mikakati hiyo kuondosha vikwazo kwa wafanyabiashara kwa kutoa ushirikiano kwa wafanyabiashara kila kunapotokuwa vikwazo kwenye uingizaji wa biashara hapa nchini. Mwenda alitumia nafasi hiyo kueleza kuwa mkakati mwengine kuziruhusu bandari za Fumba Unguja na Mkoani Pemba kushusha mizigo inayotoka moja kwa moja nje ya nchi kinyume ilivyo sasa mizigo hiyo kushushwa Mombasa Kenya. Alisema ujenzi wa bandari hizo unakwenda kwa kasi na zitakapokamilika bandari hiyo zitafanya kazi kama ban...
NA TATU MAKAME, ZANZIBAR@@@@ WAZIRI wa fedha Tanzania Balozi Khamis Mussa Omar amesema Mamlaka hiyo inatarajia kukusanya shilingi trilioni 42 kwa mwaka wa fedha 2026/2027 katika maeneo mbalimbali ya Tanzania ili kuimarisha ukuaji wa uchumi hapa nchini. Alisema hayo Kizimkazi Mkoa wa Kusini Unguja kwenye hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) ikiwa ni muendelezo wa tamasha la Kizimkazi fastival. Alisema mapato hayo kutoka vyanzo vya ndani kwa robo tatu ikiwemo ulipaji kodi kwa wafanyabiashara na kueleza kuwa kwa mwezi ulioanzia Julai mwaka huu mamlaka hiyo ilikusanya zaidi ya bilioni 800 sawa na ongezeko la asilimia 21 ya makusanyo. Alisema ukusanyaji mapato unaimarika kila mwaka kwani mwaka wa fedha 2024,2025 Mamlaka ilifikia asilimia 1003 huku mwaka 2025_2026 kiwango cha mapato kilifikia asilimia 1005 kwa Tanzania nzima katika maeneo yote ya yanayokusanywa kodi. Aidha aliwataka wafanyabiashara kulipa kodi kwa hiar...