Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

SITI FAKI ALI WA WETE: Ndie Mwalimu Mkuu alieondosha ‘sifuri’ skuli ya Utaani

                                   ‘Aweka mikakati wanabaki daraja la kwanza na la pili tu. IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA "Nilipoteuliwa kuwa Mwalimu Mkuu, mwanzo nilipata hofu hasa pale nilipojiona, naenda kuongoza watu wenye kiwango cha elimu sawa na mimi,’’anasema.    Ni maneno ya Mwalimu Mkuu skuli ya Sekondari ya Wanawake Utaani Wete, Siti Faki Ali mkaazi wa Chasasa Wete.   Mwalimu huyo ambae alitokea skuli ya Chasasa akiwa Msaidizi Mwalimu Mkuu, alipata hofu mara ya kupokea barua ya kwenda kuiongoza skuli hiyo.   Anasema, kwa vile ameshakaa uongozi katika mambo mbalimbali ya kijamii na Serikali kwenye nafasi ndogo ndogo, ndipo alipoona kwamba na nafasi hiyo anaweza kuiongoza.   Mara baada ya kukabidhiwa madaraka, alianza kuweka mikakati, ikiwemo kuondosha zero kwa wanafunzi kuanzia kidato cha pili hadi cha...
Recent posts

FATMA SULEIMAN, MWENYE ULEMAVU ALIYEFANYA MAAMUZI YA KIMAENDELEO

  NA ZUHURA JABIR   Katika jamii, mara nyingi mafanikio hupimwa kwa kiwango cha elimu, mali au nafasi aliyonayo mtu. Hata hivyo, kuna watu ambao maisha yao yanatufundisha kwamba mafanikio makubwa huanza pale mtu anapoamua kujiamini, kupambana na changamoto na kutokubali mazingira yamzuie kufikia ndoto zake.   Hii ni simulizi ya Fatma Suleiman Mussa, mwanamke mwenye ulemavu anayeishi Jumbi, Zanzibar, ambaye licha ya changamoto alizokutana nazo tangu akiwa mtoto, ameamua kutumia uwezo alionao kujiajiri, kusaidia familia yake na kuwa mfano kwa wanawake wengine wenye ulemavu. Safari yake imejaa changamoto, lakini pia ni ushahidi kwamba “ ulemavu si mwisho wa ndoto. ”   SAFARI YA ELIMU NA MAISHA Fatma ni mtoto wa pili katika familia ya watoto wanne, wote wakiwa wa kike. Alianza elimu ya msingi katika Skuli ya Tunguu na baadaye aliendelea hadi kidato cha pili mwaka 2015. Alipata nafasi ya kuendelea na kidato cha tatu katika Skuli ya Kibele, lakini changamoto mbalimbali zil...

'ZRA' YAFANYA MABADILIKO SHERIA ZA KODI KUONGEZA UFANISI

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ MAMLAKA ya Mapato Zanzibar 'ZRA' imesma, imezifanyia mabadiliko   sheria saba   za kodi kwa mwaka wa fedha 2026/2027, yanalenga kuleta ufanisi katika makusanyo na kuwapa ahuweni wananchi. Hayo yameelezwa leo August 28, 2026  na Mkuu wa Kitengo cha Habari Makame Khamis Mohamed  wakati akiwailisha mabadiliko ya sheria hizo kwa wahariri na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali kisiwani Pemba, katika ukumbi wa mikutano wa Mamlaka hiyo Gombani Chake chake Pemba. Alisema kua mabadiliko hayo, yanalenga kuleta ufanisi kwa mlipa kodi na serikali, kwani yamezingatia kupunguza kasoro mbalimbali, zinazojitokeza pande zote mbili wakati wa kulipa na kukusanya kodi hizo. Alieleza kua mabadiliko ya sheria hizo pia yamezingatia mabadiliko na mwenendo wa sayansi na teknolojia,   pamoja na kuzingatia unafuu kwa walipakodi na kuongeza mapato kwa serikali kuu. "Sababu ya madiliko ya sheria mbalimbali za kodi kwa mwaka wa fedha 2026/2027...

ARABIA: DAKTARI DHAMANA KIGOMANI MATEMWE CHACHU YA WANAWAKE KUVITUMIA VITUO VYA AFYA

  NA TATU MAKAME HARAKATI za usawa wa kijinsia na ukombozi wa sauti ya mwanamke visiwani Zanzibar zimepitia vikwazo vingi, zikikabiliwa na mifumo dume, mila na mazingira ya kitamaduni yaliyomweka mtoto wa kike nyuma kwa miaka mingi. Katika muktadha wa kale wa kijamii, wanawake walionekana zaidi kama wasindikizaji wa kisiasa na kijamii, huku sauti zao zikisikika kwa uchache na mara nyingi zikibaki pembezoni mwa meza kuu za maamuzi. Fikra hizi zilizaa dhana potofu kuwa uongozi ni haki ya wanaume pekee na kumfanya mtoto wa kike kuziangalia nafasi za juu kama ndoto isiyoweza kufikika. Hata hivyo, mabadiliko ya nyakati na ukuaji wa uelewa wa kijamii unathibitisha kuwa uongozi kwa mwanamke sio lazima awe mwanasiasa au kiongozi mashuhuri ambae pia anaweza kutokea katika jamii ambayo bado inafikra finyu juu ya uongozi kwa mwanamke. Tunapozungumzia suala la uongozi tunabaini kuwa viongozi mbalimbali wamepiga gatua na kuwa mfano wa viongozi waliobeba sauti za wengi katika jamii inayomzunguuk...