NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ KWA sasa wazanzibar wote, wamo katika shamra shamra za miaka sita ya uongozi war ais kipendwa Dk. Hussein Ali Mwinyi, tokea alipowasili Ikulu ya Zanzibara mwaka 2020. Lengo kuu la yeye kuingia Ikulu, ilikuwa ni kumboa mzalendo wa Zanzibar, ili azidi kuwaletea neemaa, baada ya kupokea kijiti za uongozi kutoka kwa mtangulizi wake Dk. Ali Mohamed Shein. Si unajua ndani ya Chama cha Mapinduzi CCM, iko demokrasia iliyokomaa, kwa kuhakikisha viongozi wanapishana, ili kuomba ridhaa kwa wananchi, kila baada ya miaka mitano. Mwenye Dk. Mwinyi tokea awamu yake ya kwanza n ahata hii ya pili, ambapo sasa ameshatimiza miaka sita ya uongozi, alipita kwa wananchiu kuwaomba ridhaa. Nakumbuka vyema, alipokuwa ndani ya Jimbo la Konde, aliwaomba wananchi kwanza kumpa ridhaa, ili azidi kunogesha maendeleo ya kielimu, ikiwemo ujenzi wa skuli za kisasa. ‘’Nawaombeni kura, nikifika Ikulu miongoni mwa ahadi zangu moja wapo ni kuwajengea skuli ya ghorofa hapa Konde, ...
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar@@@ SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar, kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), imezindua rasmi Muongozo wa Mawasiliano kati ya Mzazi na Mtoto kuhusu Haki ya Afya ya Uzazi (PCC Toolkit), unaolenga kuimarisha malezi, mawasiliano, ulinzi na ustawi wa watoto na vijana. Uzinduzi wa muongozo huo umefanyika jana katika Hoteli ya Verde na kuzinduliwa na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Zawadi Amour Nassor, kwa niaba ya Waziri wa Wizara hiyo, Anna Athanas Paul. Akizungumza katika hafla hiyo, Zawadi alisema wazazi na walezi wanapaswa kuvunja ukimya katika kujadili masuala ya afya ya uzazi na watoto wao kwa kutumia lugha sahihi, yenye heshima na inayozingatia umri wa mtoto. Alisema watoto na vijana wanahitaji kupata taarifa sahihi zinazolingana na umri wao ili kuwasaidia kuelewa mabadiliko wanayopitia, kutambua hatari, kujilinda dhidi ya ukatili na kufanya maamuzi sahihi kuhusu ...