NA FATMA HAMAD,PEMBA @@@@ SEKTA ya uvuvi, ufugaji wa samaki na kilimo cha mwani iznaendelea kuwa nguzo muhimu ya ajira na kipato kwa wananchi wa Zanzibar huku Serikali na taasisi binafsi ikiweka mkazo katika matumizi ya rasilimali za baharini kama fursa ya biashara na uwekezaji. Hayo yalisemwa na jana Septemba 1, 2026 na Ofisa Mdhamini wizara ya Uchumi wa Bulu DK Salim Mohamed Hamza wa kati akizungumza katika mkutano wa wadau wa Mradi wa Kuimarisha Usimamizi Endelevu wa Uvuvi na Ufugaji wa Mazao ya Baharini Tanzania, TASFAM, huko katika ukumbi wa ZRA Gombani Chakechake Kusini Pemba. Alisemesema ushirikiano wa wadau ni muhimu katika kuongeza uzalishaji, ajira na kipato kwa wananchi. ALisema kwa Sasa serikali imeelekeza zaidi katika sekta ya Bahari, hivyo imeamua kuleta Mardi huo wa kuimarisha usimamizi endelevu wa uvuvi na ufugajibwa mazao baharini, ili wadau muunge mkono Mardi huo na lile lengo la serikali liweze kutimia la kujipatia kipa...
‘Aweka mikakati wanabaki daraja la kwanza na la pili tu. IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA "Nilipoteuliwa kuwa Mwalimu Mkuu, mwanzo nilipata hofu hasa pale nilipojiona, naenda kuongoza watu wenye kiwango cha elimu sawa na mimi,’’anasema. Ni maneno ya Mwalimu Mkuu skuli ya Sekondari ya Wanawake Utaani Wete, Siti Faki Ali mkaazi wa Chasasa Wete. Mwalimu huyo ambae alitokea skuli ya Chasasa akiwa Msaidizi Mwalimu Mkuu, alipata hofu mara ya kupokea barua ya kwenda kuiongoza skuli hiyo. Anasema, kwa vile ameshakaa uongozi katika mambo mbalimbali ya kijamii na Serikali kwenye nafasi ndogo ndogo, ndipo alipoona kwamba na nafasi hiyo anaweza kuiongoza. Mara baada ya kukabidhiwa madaraka, alianza kuweka mikakati, ikiwemo kuondosha zero kwa wanafunzi kuanzia kidato cha pili hadi cha...