NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ UNAPOZUNGUMZIA juhudi za serikali, katika kuiletea Pemba maendeleo ya kiuchumi, huwezi kuacha uimarishaji miundombinu ya bandari ya Mkoani Pemba. Bandari ambayo ni sehemu muhimu katika uchumi wa watu wa kusini Pemba na kisiwa kizima kwa ujumla. Kutokana na umuhimu wa bandari hiyo, serikali imekuwa ikiimarisha kwa kuifanya kuwa ya kisasa zaidi, ili kutoa huduma bora kwa wananchi. Kwani kumekuwa na maboresho makubwa, yanayo husisha gati ya kisasa, ujenzi wa jengo la abiria, njia ya kupitia abiria na kuongezwa kwa eneo la bandari kavu, kwa kuwekwa eneo maalumu la kutunzia makontena ya mizigo. Mkurugenzi wa Shirika la Bandari Pemba Abdalla Salim Abdalla, anasema bandani ya Mkoani ni ya pili kwa ukubwa visiwani humo, ikipokea meli kubwa za mizigo kutoka nchi mbalimbali na kukuza uchumi wa kisiwa hicho. Anasema, maboresho hayo yanalenga kuziwezesha meli za kisasa za mwendokasi, kuegesha kwa urahisi na usalama na kurahisisha safari za boti bai...
NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ KAIMU Ofisa Mdhamini Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Pemba, Sharifa Hamad Shapandu, amezitaka kamati za kufanikisha tamasha la 31 la utamaduni wa mzanzibari, kuhakikisha zinafanyakazi kwa kushirikiana, ili kufanikisha tamasha hilo. Ameyasema hayo August 18, 2026, ofisini kwake Gombani Chakechake Pemba, mara baada ya kuzizindua kamati hizo tano, kuelekea uzinduzi wa tamasha hilo mwishoni mwa mwezi ujao, kisiwani humo. Alisema kuwa, kuwepo kwa kamati hizo anataka iwe ni njia rahisi ya kufanikiwa kwa tamasha hilo, ambalo kwa awamu hii, linatarajiwa kuwa la aina yake. Alieleza kuwa, njia ya kuzigawa kwa kamati hizo, ni namna ya kuwa na na urahisi wa ufuatuliaji, ingawa isiwe chanzo cha kukosa kushirikiana. ‘’Najua kuwa zipo kamati tano, zinawajumbe wenye uwezo na maarifa yasiofanana, lakini hili sasa muwe na ushirikiano kwa pamoja, ili kulifanikisha hili,’’alifafanua. Aidha Kaimu Ofisa Mdhamini huy...