NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ SIFUNI Ali Haji ni Katibu Mkuu na ni kiongozi wa mwanzo, anaefanya kazi na mtandao wa asasi za kiraia katika kisiwa cha Pemba, akiwa wa kwanza mwanamke. Anasema mtandao huo unaojulikana kwa jina la PACSO, ni Umoja wa Jumuiya zisizo za kiserikali uliyoanzishwa mwaka 2005. Katika safari ya uongozi wake, anaendelea kuzisimamia jumuiya na wanachama waliokuwa Pemba ikiwemo Pegao, Juwauza, na Tamwa. Sifuni anaendelea kuvunja vikwazo vyake, katika Jumuiya hiyo kwa zaidi ya miaka sita, akilenga macho yake katika mkoa wa kusini na kaskazini mwa mji wa Pemba. Kutokana na juhudi zake na moyo wa kujituma, amekuwa akilenga uwezo wa kusimamia maendeleo endelevu kwa jamii ya kisiwa hicho. ‘’Nafasi hii haikuja tu, baada ya juhudi zangu nilizokuwa nikizifanya katika uwanachama wangu, ndipo nilipopigiwa kura kwa asilimia zote kushika nafasi ya katibu, anafafanua. Zaidi ya mwaka mmoja taasisi hiyo, haikuwa na mafaniko yoyote baada ya kusimamiwa na wanaume, ndip...
NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ UNAPOZUNGUMZIA juhudi za serikali, katika kuiletea Pemba maendeleo ya kiuchumi, huwezi kuacha uimarishaji miundombinu ya bandari ya Mkoani Pemba. Bandari ambayo ni sehemu muhimu katika uchumi wa watu wa kusini Pemba na kisiwa kizima kwa ujumla. Kutokana na umuhimu wa bandari hiyo, serikali imekuwa ikiimarisha kwa kuifanya kuwa ya kisasa zaidi, ili kutoa huduma bora kwa wananchi. Kwani kumekuwa na maboresho makubwa, yanayo husisha gati ya kisasa, ujenzi wa jengo la abiria, njia ya kupitia abiria na kuongezwa kwa eneo la bandari kavu, kwa kuwekwa eneo maalumu la kutunzia makontena ya mizigo. Mkurugenzi wa Shirika la Bandari Pemba Abdalla Salim Abdalla, anasema bandani ya Mkoani ni ya pili kwa ukubwa visiwani humo, ikipokea meli kubwa za mizigo kutoka nchi mbalimbali na kukuza uchumi wa kisiwa hicho. Anasema, maboresho hayo yanalenga kuziwezesha meli za kisasa za mwendokasi, kuegesha kwa urahisi na usalama na kurahisisha safari za boti bai...