NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ MALEZI bora na makuzi ya mtoto, ni jambo muhimu kwa maendeleo yake,kimwili na kiakili. Hili linajumuisha huduma zote muhimu anazostahili kupewa mtoto, kuanzia miaka 0 hadi 8, ili kumuwezesha kukuwa na kufikia utimilifu wake. Ikiwa ni kimwili, kiakili, kijamii, kihisia na kimaadili, ilikushiriki kikamilifu katika ujenzi wa taifa na kuyamudu mazingirayake. Mara nyingi ni rahisi kupata haya yote, kutoka kwa wazazi au walezi,lakini wengi wao husahau kwamba matumizi ya lugha nzuri kwa watoto,inamchango mkubwa katika ustawi wao. Na zipo sheria zinazopinga ukatili wa aina zote dhidi ya watoto, kwamsingi kwamba malezi bora kwa mtoto, ndio msingi imara kwa makuzi yake. Mfano, Mkataba wa kimataifa wa haki za watoto duniani ( Conventionoftherightsofthechildren ) wa mwaka 1989, ambao umeanza kutumikarasmi mwaka 1990. Ibara yake ya 19 inasisitiza, kuwa‘ nchi wanachama kuhakikishawanakuwa na sheria nzuri zitakazo mlinda mtoto juu ya aina zote zau...
NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ UDHALILISHAJI katika vyombo vya usafiri ni pamoja na ukatili wa kijinsia, inayoashiria uvunjifu wa haki za binaadamu. Kwa wenzetu wenye ulemavu, wao wamekuwa nambari moja kudhalilishwa, wakati wanapokwenda ama kurudi kwenye mipango yao ya maisha. Hali hiyo hujumuisha kuguswa mwili bila ridhaa, matusi, kauli za kubaguliwa au kulazimishwa kukaa katika mazingira yanayoshusha heshima na utu wao. Mkurugenzi wa Jumuiya ya watu wenye ulemavu Juma Kombo Hija Pemba anasema, vyombo vya usafiri havipo rafiki kwao. Anasema ukiangalia Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo zimeridhia mikataba mbalimbali ya kimataifa, inayolenga kuweka mazingira rafiki kwa watu wenye ulemavu, pamoja kusimamia haki zao. Katika kuweka mazingira mazuri ni pamoja kusimamia haki zao na ujumuishwaji katika vyombo vya usafiri, hususana watu wenye ulemavu wa viungo. Anasema yapo matukio matatu yaliyoripotiwa kwa mwezi Juni na Jualai mwaka huu, katika jumuiya hiyo amabapo mt...