NA TATU MAKAME HARAKATI za usawa wa kijinsia na ukombozi wa sauti ya mwanamke visiwani Zanzibar zimepitia vikwazo vingi, zikikabiliwa na mifumo dume, mila na mazingira ya kitamaduni yaliyomweka mtoto wa kike nyuma kwa miaka mingi. Katika muktadha wa kale wa kijamii, wanawake walionekana zaidi kama wasindikizaji wa kisiasa na kijamii, huku sauti zao zikisikika kwa uchache na mara nyingi zikibaki pembezoni mwa meza kuu za maamuzi. Fikra hizi zilizaa dhana potofu kuwa uongozi ni haki ya wanaume pekee na kumfanya mtoto wa kike kuziangalia nafasi za juu kama ndoto isiyoweza kufikika. Hata hivyo, mabadiliko ya nyakati na ukuaji wa uelewa wa kijamii unathibitisha kuwa uongozi kwa mwanamke sio lazima awe mwanasiasa au kiongozi mashuhuri ambae pia anaweza kutokea katika jamii ambayo bado inafikra finyu juu ya uongozi kwa mwanamke. Tunapozungumzia suala la uongozi tunabaini kuwa viongozi mbalimbali wamepiga gatua na kuwa mfano wa viongozi waliobeba sauti za wengi katika jamii inayomzunguuk...
NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ SIFUNI Ali Haji ni Katibu Mkuu na ni kiongozi wa mwanzo, anaefanya kazi na mtandao wa asasi za kiraia katika kisiwa cha Pemba, akiwa wa kwanza mwanamke. Anasema mtandao huo unaojulikana kwa jina la PACSO, ni Umoja wa Jumuiya zisizo za kiserikali uliyoanzishwa mwaka 2005. Katika safari ya uongozi wake, anaendelea kuzisimamia jumuiya na wanachama waliokuwa Pemba ikiwemo Pegao, Juwauza, na Tamwa. Sifuni anaendelea kuvunja vikwazo vyake, katika Jumuiya hiyo kwa zaidi ya miaka sita, akilenga macho yake katika mkoa wa kusini na kaskazini mwa mji wa Pemba. Kutokana na juhudi zake na moyo wa kujituma, amekuwa akilenga uwezo wa kusimamia maendeleo endelevu kwa jamii ya kisiwa hicho. ‘’Nafasi hii haikuja tu, baada ya juhudi zangu nilizokuwa nikizifanya katika uwanachama wangu, ndipo nilipopigiwa kura kwa asilimia zote kushika nafasi ya katibu, anafafanua. Zaidi ya mwaka mmoja taasisi hiyo, haikuwa na mafaniko yoyote baada ya kusimamiwa na wanaume, ndip...