Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

UTAMADUNI WA KUTOBOA, KUWEKA KIPINI CHA PUA, WAIBEBA MICHEWENI, WANAUME WAKIRI KUVUTIWA

      NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@   ‘’TUMESHAWAHI kusimamisha shughuli ya harusi kwa dakika 10, mke asichukuliwe, baada ya kugundua hatujamtia pambo la kipini cha pua,’’anasema Rehema Faki Shehe (60) wa Kwale Micheweni Pemba. Ilishazoelekea kuwa, kuwa mapambo ni aina ya mafuta, podari, pete, mkufu, udi, wanja na hina, ingawa kwa wanawake wilaya ya Micheweni, kipaumbele ni utoboaji wa pua kwa ajili ya utiaji wa kipini. Utamaduni wa utoboaji (utomoaji) wa pua tena ya upande wa kushoto, wenyewe wanawake wa Micheweni waliurithi zaidi ya miaka 200 iliyopita. Kwa mfano, Rehema Faki Shehe (60) alimkuta bibi yake wakati akiwa huo akiwa na miaka 50, akiwa ametobolewa tundu la upande wa kushoto ya pua, akiwa na kipini. KINA MAAGA GANI KIPINI CHA PUA? Sharifu Massoud Hamad (60) wa Kwale Micheweni mkoa wa kaskazini Pemba, anasema moja ni tofauti kati ya mwanamke na mwanamme. Anaona hata unapokuta wamevaa mavazi yenye kufanana, lakini dalili kubwa ya tofauti hiyo...
Recent posts

SHEHA FATMA WA KENDWA, AIDHIHIRISHIA DUNIA WANAWAKE WANAPOPATA UONGOZI.....

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ "UONGOZI sio cheo, ni matendo na matokeo yanayobadilisha maisha ya watu" ni maneno ya wananchi wa shehia ya Kendwa wilaya ya Mkoani. Wanasema sheha wao ni mwanamke aliyethibitisha kuwa, uongozi wa mwanamke una nguvu ya kubadilisha kabisa muelekeo wa jamii. Wanakendwa ni kama wanaungana na Mkataba wa umoja wa Mataifa wa kutokomeza aina zote za udhalilishaji (CEDAW) wa 1979 hasa ibara ya 7. Ibara inayozitaka “ Nchi wanachama zihakikishe zinawapa wanawake fursa za kushiriki katika uongozi’’. Aidha lengo namba 5.5 la maendeleo endelevu ‘SDGs’ ya mwaka 2015 hadi 2030, lililozitaka nchi zote kuhakikisha ushiriki kamili wa wanawake na fursa sawa za uongozi katika ngazi zote, iwe kisiasa, kiuchumi na kijamii. Pia Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 ibara yake ya 21 (1) inayoeleza kila Mzanzibari anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia Wawakilishi waliochaguliwa kwa hiari. Sera ya Maendeleo ya...

'NGUVU MOJA' USHIRIKA WA WATU WENYE ULEMAVU PEMBA, WALIA KUFANYIWA UKATILI WA KIUCHUMI

    NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ UMEWAHI kuwaza maisha bila kuona, kusikia, kusema au kusimama. Basi hayo ndio maisha ya kila siku ya watu, wenye ulemavu, aidha wa viungo, uoni, uziwi na aina nyengine. Lakini watu wenye ulemavu ni sawa na watu wengine, wanahaki zote za msingi, kama ilivyo kwa wengine. Miongoni mwa haki hizo ni kushiriki katika shughuli za kiuchumi, kama ilivyoelezwa katika mikataba na sheria mbalimbali. Mkataba wa kimataifa wa haki za watu wenye ulemavu wa 2006, ambao ibara yake ya 27 (f) inasisitiza ushiriki na ushirikishwaji wao kiuchumi. “Nchi wanachama wakuze fursa za watu wenye ulemavu kujiajiri, kuanzisha na kuendesha shughuli za ujasiamali, vyama vya ushirika na mtu binafsi kuanzisha biashara zake”, inaeleza sehemu ya mkataba huo. Sheria ya watu wenye ulemavu ya Zanzibar nambari 8 ya mwaka 2022, kifungu cha 28 (e) inaeleza, watu wenye ulemavu wanastahiki haki zote za msingi za kibinaadamu sawa nawatu wengine ikiwemo kujitegemea na kujumuishw...

USAFI LIFANYWE JUKUMU LA WOTE, MASHEHA WATOA RAI

  NA ZUHURA JABIR, ZNAIBAR “Usafi ni nusu ya afya." Haya sio msemo wa utani, bali ni ukweli unaogusa maisha ya kila siku ya wananchi. Mazingira safi yanamaanisha afya bora, heshima ya makazi na maendeleo ya jamii, lakini pale ambapo mifumo ya usimamizi haieleweki, wananchi hubeba mzigo ambao haukupaswa. Majadiliano yaliyowakutanisha masheha, wahamasishaji wa jamii na wataalamu wa Baraza la Manispaa Mjini, yameonesha wazi kuwa changamoto za usafi wa mazingira bado zinahitaji mshikamano. Methali isemayo, "Kidole kimoja hakivunji chawa," inaakisi hali halisi ya mapambano dhidi ya uchafu wa mazingira. MGONGANO WA MAMLAKA KATIKA UKUSANYAJI WA TAKA Moja ya hoja zilizojitokeza kwa uzito mkubwa ni mgongano wa mamlaka katika ukusanyaji wa taka ndani ya shehia ya Mchangani. Kwa mujibu wa sheha Nassir Mohammed Ali, wananchi wanakabiliwa na hali ya kuchanganyikiwa, kutokana na taasisi mbili, Baraza la Manispaa Mjini na Mamlaka ya Mji Mkongwe, kufanya kazi katika ene...

LUGHA CHAFU ZA WAZAZI KWA WATOTO, ZINAVYOWARUGIA MIFUMO YAO YA MAISHA

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ MALEZI bora na makuzi ya mtoto, ni jambo   muhimu kwa maendeleo yake,kimwili na kiakili. Hili linajumuisha huduma zote muhimu anazostahili kupewa mtoto, kuanzia miaka 0 hadi 8, ili kumuwezesha kukuwa na kufikia utimilifu wake. Ikiwa ni kimwili, kiakili, kijamii, kihisia na kimaadili, ilikushiriki kikamilifu katika ujenzi wa taifa na kuyamudu mazingirayake. Mara nyingi ni rahisi kupata haya yote, kutoka kwa wazazi au walezi,lakini wengi wao husahau kwamba matumizi ya lugha nzuri kwa watoto,inamchango mkubwa katika ustawi wao. Na zipo sheria zinazopinga ukatili wa aina zote dhidi ya watoto, kwamsingi kwamba malezi bora kwa mtoto, ndio msingi imara kwa makuzi yake. Mfano, Mkataba wa kimataifa wa haki za watoto duniani ( Conventionoftherightsofthechildren ) wa mwaka 1989, ambao umeanza kutumikarasmi mwaka 1990. Ibara yake ya 19 inasisitiza, kuwa‘ nchi wanachama kuhakikishawanakuwa na sheria nzuri zitakazo mlinda mtoto juu ya aina zote zau...