Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa Ataka Wadau Kuongeza Weledi Katika Kutokomeza Ukatili

  Na Muandishi Wetu Zanzibar Mwenyekiti wa Kamati yaMapngo wa   Kitaifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto, ambaye pia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora, Mhe. Haroun Ali Suleiman, amewataka wadau wanaojihusisha na masuala ya ukatili na udhalilishaji kufanya kazi kwa weledi na ushirikiano ili kutokomeza vitendo hivyo katika jamii. Mhe. Haroun alitoa wito huo jana wakati wa uzinduzi wa Kamati ya Kitaifa ya ngazi ya Mawaziri uliofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip Airport, Zanzibar. Alisema kuwa lengo la kuundwa kwa kamati hiyo ni kuimarisha ushirikiano kati ya taasisi mbalimbali katika kupambana na vitendo vya ukatili na udhalilishaji dhidi ya wanawake na watoto, kwa lengo la kupunguza na hatimaye kuvimaliza kabisa. Aidha, aliitaka kamati hiyo kutekeleza majukumu yake kwa bidii, kuweka mikakati madhubuti na kuhakikisha sheria pamoja na sera zilizopo zinatekelezwa ipasavyo ili kulinda haki za wanawake na ...
Recent posts

KIZUNGUMKUTI TUHMA ZA UKATILI, UDHALILISHAJI KWA KIZIWI MICHEWENI

  SAIDA ALI, PEMBA MAMA mzazi ambae mwanawe mwenye ulemavu wa uziwi wa miaka 38, alifanyiwa vitendo vya ukatili na udhalilishaji, ameviomba vyombo vya ulinzi na usalama, kuwa haki itendeke kufuatia unyama aliodai kufanyiwa, kijana wake. Aliyasema hayo, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari, shehia ya Shumba vyamboni wilaya ya Micheweni, kufuatia sitofahamu ya majibu ya hospitali na athari aliyonayo kijana wao. Alisema kuwa kitendo alichodai kufanyiwa kijana wao huyo, ambacho alimshuhudia akiwa amefungwa mikono nyuma akiwa na tambara mdomoni, ni cha kikatili na udhalilishaji. Alieleza kuwa, muda wa saa 8:00 usiku baada ya kusikia kelele za kukorota kwa kijana wake, alikimbilia chumbani kwake, na kufika alijonea maajabu. ‘’Kwanza alikuwa amevungwa mwiili mzima nguo nyeusi mithili ya beibui, nilishuhudia vichupa vidogo viwili, kimoja kikiwa na majimaji, (dawa) nusu na chingine kikiwa kitupu,’’alifafanua. Aidha mzazi huyo alisema, jingine ambalo limemshitua kwa kij...

TAMWA YAWAPA MAFUNZO YA UWAJIBIKAJIN MADIWANI NA WARATIBU WANAWAKE

NA MOZA SHAABAN, PEMBA MADIWANI wakuchaguliwa na waratibu wanawake na watoto kutoka wilaya nne za Pemba   wametakiwa kuwajibika ipasavyo katika utekelezaji majukumu yao ya msingi ya kiuongozi, ili kujenga imani kwa jamii juu ya uwezo alionao mwanamke katika kuongoza na kuleta maendeleo. Wito huo umetolewa na Afisa Progamu wa mradi wa kuhamasisha ushiriki wa wanawake katika masuala ya uongozi (SWIL) unaotekelezwa na TAMWA-Zanzibar Sabrina Ali Mwatanga wakati wa mafunzo   kwa madiwani na waratibu wanawake na watoto kutoka wilaya nne za Pemba, yaliolenga kuwajengea uwezo juu ya namna ya kuwajibika ipasavyo katika uongozi wao, yaliofanyika katika ukumbi wa mikutano TAMWA Mkanjuni Chake chake Pemba. Alieleza mafunzo hayo ni mwendelezo wa hamasa na kuwajengea uwezo madiwani na waratibu hao juu namna bora ya kutekeleza majukumu yao ya kiongozi, ili jamii ione ufanyaji kazi wao kivitendo. Afisa huyo alisema   TAMWA imekua ikifanya juhudi kubwa katika kuwajengea uwezo wana...

CANADA YAKABIDHI VIFAA VYA SH/= MILION 270 VYA UCHUMI WA BULUU

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ SERIKALI ya Canada, imesema itaendelea kushirikiana na serikali za Tanzania, katika maeneo mbalimbali, ikiwemo kwenye uchumi wa buluu, ili walengwa wakuze pato lao na taifa. Hayo yameleezwa leo Juni 23, 2026 na Balozi wa taifa hilo, nchini Tanzania Emily Burns, kwenye hafla ya ugawaji wa vitendea kazi kwa vikundi vya wajasiriamali, waliokeza kwenye bahari, na ufunguzi wa kituo cha mafunzo eneo la Chamanangwe wilaya ya Wete Pemba. Alisema, ushirikiano huo, anaamini utawasaidia wajasriamali waliokeza kwenye eneo hilo, hasa wanawake na vijana, ambao kwa muda mrefu walikuwa hawakuhusishwa moja kwa moja. Alieleza kuwa, kwa eneo la Zanzibar na baadhi ya mikoa ya Tanzania bara, ilivyozungurukwa na bahari, wakati umefika manufaa yake, yawanufaishe makundi yote. ‘’Serikali ya Canada, inaziahidi serikali zote mbili kwamba, ushirikiano huu kwenye sekta ya uchumi wa buluu, utakuwa endelevu pamoja na maeneo mingine,’’alifafanua. Katika hatua nyingine, B...

MABWENI KWA WANAFUNZI YAPUNGUZA VITISHO VYA UBAKAJI, YAWAPA UHAKIKA WA MAKAAZI

    NA MOZA SHABAN, PEMBA@@@@ SERIKALI ya awamu ya nane, imekuwa ikigeuza sekta ya elimu kwa vitendo, ikiwemo ujenzi wa dahalia. Maana lengo hasa ni kuwapunguzia umbali wa kutembea masafa marefu wanafunzi, pale wanapokwenda na kurudi skuli. Dahalia hizo, zimekuwa zikiwasaidia wanafunzi hao, katika kuongeza ufaulu na maarifa ya kujifunza, masomo yao na kupata utulivu, wa kujiepusha na vitisho vya udhalilishaji. Maana alishasema mara kadhaa, Ofisa Mdhamini wa wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba, Mohamed Nassor Salum kuwa, wamekuwa wakipokea kesi za vitisho vya ubakaji kwa wanafunzi. Anasema, wapo wanafunzi hasa kuanzia kidato cha nne, wamekuwa wakiviziwa vichakani, iwe wanapokwenda ama wanaporudi masomoni. ‘’Mazingira haya ya ujenzi wa dakhalia, ni kuwahakikishia ulinzi wao, maana mingi yapo karibu mno na skuli, wanazosoma,’’anasema. Anakiri kuwa, wahalifu wa ubakaji, walishazoea kutumia vichaka, ili kuwadhalilisha wanafunzi. ‘’Sasa wanafunzi wetu hasa wa...

WASICHANA NA ELIMU YA JUU, VIGINGI NA MASHIMO YA KUWAKATISHA TAMAA YAZIDI

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ RIPOTI ya Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto ‘UNICEF’, lile la masuala ya wanawake, UN-Women na shirika la Plan International, inaonesha idadi ya wasichana wanaoandikishwa skuli, kwa sasa ni kubwa kuliko wakati wowote. Ripoti hiyo iliotolewa mwaka 2020, inaeleza idadi ya wasichana watoro skulini tangu mwaka 1995 imepungua na sasa wasichana wana fursa ya kusoma skuli za sekondari, kuliko wavulana. HALI ILIVYO NCHINI Mitandao inaripoti, kiwango cha wanafunzi wanaojiunga na elimu ya sekondari nchini Tanzania ina uwiano nzuri, ambapo wasichana hufikia karibu nusu ya wanafunzi wanaosajiliwa. Hata hivyo, kutoka elimu ya msingi hadi sekondari kwa ujumla asilimia 56 ni ya wasichana, huku asilimia 34 pekee ndio wanaomaliza elimu ya sekondari. Huku mitandao ikiripoti, hata Zanzibar kunauwiano mzuri wa wasichana wanao jiunga na masomo ya sekondari, kati yao na wavulana. Idadi ya wanaomaliza na kufaulu ni pungufu ikilinganishwa na wavulan...