NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WIZARA ya Ujenzi na Uchukuzi kisiwani Pemba, imewataka wananchi watakaodaiwa nauli mpya iwe kwenye dalala, bajaji au bodaboda kwa kisingizio cha kupanda bei ya mafuta, kuripoti katika vyombo vya sheria, kwani serikali haijatangaaza nauli mpya. Kauli hiyo, imetolewa na Ofisa Mdhamini wa wizara hiyo, Ibrahim Saleh Juma, wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi, kufuatia malalamiko ya wananchi, kulipishiwa nauli mpya hivi sasa. Alisema, serikali inaelewa vyema juu ya changamoto ya kupanda kwa nishati hiyo ya mafuta duniani, ingawa bado, tamko la kupandishwa nauli halijatolewa. Alieleza kuwa, serikali imekuwa na utaratibu wa kupokea mapendekezo ya upandishwaji wa nauli hiyo kutoka kwa madereva hao, na kisha kukaa pamoja, ili kuangalia uwezekono wa kupandisha ama laa. Ibrahimu alieleza kuwa, hadi sasa na tokea kupanda kwa nishati hiyo, serikali haijatangaaza nauli mpya, hivyo ni marufuku kwa dereva yeyote, kupandisha nauli hiyo. Alifafanua...
IMEANDIKWA NA TATU MAKAME MAHUJAJI watarajiwa wameaswa kuacha kushughulikia simu wanapokuwa katika ibada ya Hijja, ili waweze kuitekeleza kwa utulivu, unyenyekevu na kupata radhi za Mwenyezi Mungu. Wito huo umetolewa na Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Ali Abdulghulam Hussein, wakati akifunga mafunzo kwa Mahujaji watarajiwa iliyofanyika katika Ukumbi wa Shantimba, Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja yaliandaliwa na Taasisi ya Khairat Hajj and Umra Travel. Alisema, ni muhimu kwa mahujaji kufuata miongozo wanayopewa na viongozi wa Hijja na kuepuka vitendo vinavyoweza kuharibu ibada hiyo, ikiwemo kutumia simu bila ulazima au kujihusisha na mambo yasiyo na tija. “Niwaase mahujaji watarajiwa msijishughulishe na mambo yasiyo na faida kama kuangalia michezo wakati wa ibada, hilo linaweza kuharibu utekelezaji wa nguzo ya tano ya Uislamu,” alisema Abdulghulam. Aidha, aliwataka kuwa wavumilivu katika kipindi chote cha ibada hiyo ili waweze kuitekeleza kikamilifu na...