NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ‘’TUMESHAWAHI kusimamisha shughuli ya harusi kwa dakika 10, mke asichukuliwe, baada ya kugundua hatujamtia pambo la kipini cha pua,’’anasema Rehema Faki Shehe (60) wa Kwale Micheweni Pemba. Ilishazoelekea kuwa, kuwa mapambo ni aina ya mafuta, podari, pete, mkufu, udi, wanja na hina, ingawa kwa wanawake wilaya ya Micheweni, kipaumbele ni utoboaji wa pua kwa ajili ya utiaji wa kipini. Utamaduni wa utoboaji (utomoaji) wa pua tena ya upande wa kushoto, wenyewe wanawake wa Micheweni waliurithi zaidi ya miaka 200 iliyopita. Kwa mfano, Rehema Faki Shehe (60) alimkuta bibi yake wakati akiwa huo akiwa na miaka 50, akiwa ametobolewa tundu la upande wa kushoto ya pua, akiwa na kipini. KINA MAAGA GANI KIPINI CHA PUA? Sharifu Massoud Hamad (60) wa Kwale Micheweni mkoa wa kaskazini Pemba, anasema moja ni tofauti kati ya mwanamke na mwanamme. Anaona hata unapokuta wamevaa mavazi yenye kufanana, lakini dalili kubwa ya tofauti hiyo...
NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ "UONGOZI sio cheo, ni matendo na matokeo yanayobadilisha maisha ya watu" ni maneno ya wananchi wa shehia ya Kendwa wilaya ya Mkoani. Wanasema sheha wao ni mwanamke aliyethibitisha kuwa, uongozi wa mwanamke una nguvu ya kubadilisha kabisa muelekeo wa jamii. Wanakendwa ni kama wanaungana na Mkataba wa umoja wa Mataifa wa kutokomeza aina zote za udhalilishaji (CEDAW) wa 1979 hasa ibara ya 7. Ibara inayozitaka “ Nchi wanachama zihakikishe zinawapa wanawake fursa za kushiriki katika uongozi’’. Aidha lengo namba 5.5 la maendeleo endelevu ‘SDGs’ ya mwaka 2015 hadi 2030, lililozitaka nchi zote kuhakikisha ushiriki kamili wa wanawake na fursa sawa za uongozi katika ngazi zote, iwe kisiasa, kiuchumi na kijamii. Pia Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 ibara yake ya 21 (1) inayoeleza kila Mzanzibari anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia Wawakilishi waliochaguliwa kwa hiari. Sera ya Maendeleo ya...