Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

HANUNA IBRAHIM: KUTOKA SEKRETARI HADI DC. ALIMBWAGA WAZIRI AKAUKWAA UWAKILISHI CHAKECHAKE

    NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@ KATIKATI ya giza nene lililogubika haki ya mwanamke kuwa kiongozi kwa wakati huo, kuna mwanamke alielishinda?. Alisimama kidedea, yeye na waliomzunguka walihakikisha anafanikiwa na kweli alishika nafasi mbalimbali za uongozi, mpaka kuwa mmoja wa viongozi wanawake walioweka alama isiyofutika katika jamii. Ni Hanuna Ibrahim Massoud, alieanza kuliona jua mwaka 1959, Kisiwani kwa Binti Abedi wilaya ya Wete kaskazini Pemba. Alianza kusaka elimu yake ya msingi, mwaka 1965, ambapo aliipata katika skuli tofauti kama Ziwani, Shamiani na Utaani. Mnamo mwaka 1974, alikamilisha elimu yake ya sekondari kidato cha nne, katika skuli ya Fidel Castro. “Safari yangu ya masomo haikuwa na kituo kimoja, nilisoma maeneo mengi, lakini huku kulinifanya kuyajuwa na kuyatawala vizuri mazingira,’’anahadithia. Kumbe wakati huo kuelimika kwa mtoto wa kike hadi kidato cha nne, ilikuwa fursa adimu na nimsingi mkubwa wa ukombozi. Safari yake ya kutafuta elimu, ...
Recent posts

"JE, UNAJUA MTOTO WAKO ANAANZA KUJIFUNZA TANGU AKIWA TUMBONI?

      NA SULEIMAN SAID, PEMBA “Fikiria mtoto anapokuwa tumboni, macho yake bado yamefumba,’’inafahamika.   Ingawa ndani ya kichwa chake kuna mabilioni ya seli zilizo tayari kumsaidia kujifunza .   Cha kushangaza ni kwamba, msingi wa seli hizo, uliwekwa wiki chache, tu baada ya mama kutunga mimba.   Lakini cha kujiuliza je, unajua kipindi hiki ndicho kinachoweka msingi muhimu wa maendeleo yake ya baadaye?’’.   Mtaalamu wa eneo hilo hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani, anasema wazazi wengi huamini kuwa elimu ya mtoto huanza siku ya kwanza, anapoingia darasani, lakini ukweli wa kisayansi ni kwamba kujifunza huanza sambamba na safari ya ukuaji wa ubongo.   Tena inafahamika kuwa ni, wiki chache baada ya mimba kutungwa, na kadiri ujauzito unavyokuwa mtoto huanza pia kuitikia na kujifunza kutokana na mazingira yake akiwa tumboni.   Anasema kuanzia takribani wiki ya tatu, baada ya mimba kutungwa, ubongo wa mtoto huanza kukua ...

JUMAZA INAUNGA MKONO MARIDHIANO VYAMA VYA SIASA ZANZIBAR

  NA AMRAT KOMBO, ZANZIBAR@@@@ JUMUIYA ya Maimamu Zanzibar    (JUMAZA) imesema inaunga mkono tamko la maridhiano ya chama cha CCM  na ACT Wazalendo kwani ni hatua   ya msingi katika kuimarisha  amani, umoja na maendeleo ya  Zanzibar. Katibu Mtendaji wa Jumuiya hiyo,  Shekh Ali Abdalla Amour, aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Jamatkhan Vuga mjini Unguja. Alisema jumuiya hiyo imepokea kwa faraja na furaha maridhiano yaliyotangazwa hadharani  Julai 9, katika viwanja vya Ikulu  Zanzibar mbele ya Rais wa Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia  Suluhu Hassan. Aidha alisema ni vyema kwa   viongozi hao kutofanya khiyana katika  utekelezaji wa makubaliano hayo ili  kuendelea kujenga amani, umoja   na mshikamano kwa wananchi wa Z anzibar. Alieleza kuwa jambo hilo limeonesha  utayari wa viongozi kuweka mbele maslahi ya Zanzibar na wananchi wake badala ya ...

UNDP, PACSO WAWAPA DOZI YA KISHERIA WANANACHI UWANDANI, WENYEWE WAFURAHIA

    NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ MWANASHERIA wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara Maalum ‘SMZ’ Aziza Suleiman Mohamed amesema, jamii imekuwa ikifahamu udhalilishaji, unaopelekea madhara ya kimwili, bali unajumuishwa madhara ya  kingono, kihisia, kutelekezwa pamoja na kumnyima mtu usalama wake. Ameyasema hayo jana August 3, 2026 alipokuwa akizungumza na wananchi wa shehia ya Uwandani wilaya ya Chake chake, juu ya elimu iliyoandaliwa na Mwemvuli wa Asasi za Kiraia Pemba PACSO na kufanyika skuli ya Uwandani. Alisema kuwa upo udhalilishaji mbalimbali unaojumuishwa madhara ya kingono, kihisia, kutelekezwa pamoja na kumnyima mtu usalama wake. Alisema matokeo ya udhalilishaji ni makubwa kiasi ambacho, kunaweza kusababisha majaraha, kifo kuenea kwa maradhi tabia hatarishi na matokeo mabaya kwa wanaofanyiwa. Alifafanua kuwa wahanga wakubwa wanaothirika na vitendo hivyo ni wanawake, watoto na watu wenye ulemavu, hivyo ipo sheria ya Mtoto nambari 6 ya mwaka 2011,...

UTAMADUNI WA KUTOBOA, KUWEKA KIPINI CHA PUA, WAIBEBA MICHEWENI, WANAUME WAKIRI KUVUTIWA

      NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@   ‘’TUMESHAWAHI kusimamisha shughuli ya harusi kwa dakika 10, mke asichukuliwe, baada ya kugundua hatujamtia pambo la kipini cha pua,’’anasema Rehema Faki Shehe (60) wa Kwale Micheweni Pemba. Ilishazoelekea kuwa, kuwa mapambo ni aina ya mafuta, podari, pete, mkufu, udi, wanja na hina, ingawa kwa wanawake wilaya ya Micheweni, kipaumbele ni utoboaji wa pua kwa ajili ya utiaji wa kipini. Utamaduni wa utoboaji (utomoaji) wa pua tena ya upande wa kushoto, wenyewe wanawake wa Micheweni waliurithi zaidi ya miaka 200 iliyopita. Kwa mfano, Rehema Faki Shehe (60) alimkuta bibi yake wakati akiwa huo akiwa na miaka 50, akiwa ametobolewa tundu la upande wa kushoto ya pua, akiwa na kipini. KINA MAAGA GANI KIPINI CHA PUA? Sharifu Massoud Hamad (60) wa Kwale Micheweni mkoa wa kaskazini Pemba, anasema moja ni tofauti kati ya mwanamke na mwanamme. Anaona hata unapokuta wamevaa mavazi yenye kufanana, lakini dalili kubwa ya tofauti hiyo...