NA ZUHURA JABIR Katika jamii, mara nyingi mafanikio hupimwa kwa kiwango cha elimu, mali au nafasi aliyonayo mtu. Hata hivyo, kuna watu ambao maisha yao yanatufundisha kwamba mafanikio makubwa huanza pale mtu anapoamua kujiamini, kupambana na changamoto na kutokubali mazingira yamzuie kufikia ndoto zake. Hii ni simulizi ya Fatma Suleiman Mussa, mwanamke mwenye ulemavu anayeishi Jumbi, Zanzibar, ambaye licha ya changamoto alizokutana nazo tangu akiwa mtoto, ameamua kutumia uwezo alionao kujiajiri, kusaidia familia yake na kuwa mfano kwa wanawake wengine wenye ulemavu. Safari yake imejaa changamoto, lakini pia ni ushahidi kwamba “ ulemavu si mwisho wa ndoto. ” SAFARI YA ELIMU NA MAISHA Fatma ni mtoto wa pili katika familia ya watoto wanne, wote wakiwa wa kike. Alianza elimu ya msingi katika Skuli ya Tunguu na baadaye aliendelea hadi kidato cha pili mwaka 2015. Alipata nafasi ya kuendelea na kidato cha tatu katika Skuli ya Kibele, lakini changamoto mbalimbali zil...
NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ MAMLAKA ya Mapato Zanzibar 'ZRA' imesma, imezifanyia mabadiliko sheria saba za kodi kwa mwaka wa fedha 2026/2027, yanalenga kuleta ufanisi katika makusanyo na kuwapa ahuweni wananchi. Hayo yameelezwa leo August 28, 2026 na Mkuu wa Kitengo cha Habari Makame Khamis Mohamed wakati akiwailisha mabadiliko ya sheria hizo kwa wahariri na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali kisiwani Pemba, katika ukumbi wa mikutano wa Mamlaka hiyo Gombani Chake chake Pemba. Alisema kua mabadiliko hayo, yanalenga kuleta ufanisi kwa mlipa kodi na serikali, kwani yamezingatia kupunguza kasoro mbalimbali, zinazojitokeza pande zote mbili wakati wa kulipa na kukusanya kodi hizo. Alieleza kua mabadiliko ya sheria hizo pia yamezingatia mabadiliko na mwenendo wa sayansi na teknolojia, pamoja na kuzingatia unafuu kwa walipakodi na kuongeza mapato kwa serikali kuu. "Sababu ya madiliko ya sheria mbalimbali za kodi kwa mwaka wa fedha 2026/2027...