Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

BANDARI YA FUMBA KUANZA KAZI JANUARI MWAKANI

  NA TATU MAKAME, ZANZIBAR@@@@ SERIKALI imesema bandari ya Fumba itakuwa na uwezo wa kushusha na kupakia kontena 40 kwa wakati mmoja ifikapo Januari mwakani hali itakayorahisisha ushushaji wa mizigo katika bandari hiyo na kuondosha usumbufu kwa wafanyabiashara. Mkurugenzi wa Shirika la Bandari Zanzibar Akif Ali Khamis alisema hayo Fumba wakati akitoa maelezo ya ujenzi wa gati ya bandari hiyo kufuatia ziara iliyofanywa na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Yussuph Juma Mwenda aliyefika bandarini kukagua ujenzi wa bandari hiyo. Alisema ujenzi wa bandari utakapokamilika utarahisisha usafirishaji wa mizigo kwa wafanyabiashara na kuongeza mapato kupitia mamlaka ya mapato TRA hasa usafirishaji wa mizigo.  Alitumia nafasi hiyo kueleza kuwa bandari hiyo itakuwa na uwezo wa kushusha vyombo 750 kwa wakati mmoja kutokana na ukubwa wa bandari na kueleza kuwa bandari itarahisisha ushushaji wa mizigo kutofautisha na bandari ya Malindi ambayo inashusha kontena 10 hadi 12 kwa w...
Recent posts

FATMA MGWALI: ULEMAVU HAIKUA KIKWAZO KUISAIDIA JAMII YAKE

  NA TATU MAKAME, ZANZIBAR@@@@ LICHA ya ulemavu alionao hakuwahi kukata tamaa katika kupambania maisha yake na jamii inayomzunguuka katika kupata huduma za jamii ikiwemo maji safi na salama katika jamii yake. Unapomuona hali yake na ushujaa wake ni tofauti na uwezo wake kutokana na tatizo la uoni hafifu wa macho aliokuwa nao lakini ana ndoto za kufanikisha yale aliyojipangia katika maisha yake hasa kuwapatia wananchi wa eneo lake huduma ya maji safi na salama ili waondokane na adha ya maji. Unapomuona huwezi amini kama anauwezo na ujasiri wa kusimama akapigania haki yake licha ya umaskini wake pamoja na kubezwa na kudharauliwa kwa sababu ya ulemavu wake. Huyo si mwengine ni Fatma Mgwali Khamis mkaazi wa kijiji cha Fukuchuchani Mkoa wa Kaskazini Unguja. Fatma alizaliwa mnamo mwaka 1977 katika kijiji cha Fukuchani ni mtoto wa tano katika watoto wanane wa Mama mzazi wa Fatma aliyefahamika kwa jina la Tatu Haji Khamis ambae alijaaliwa kupata watoto watatu wanaume na watoto watato wanaw...

TRA: 'TUNAENDELEA KUIMARISHA MAZINGIRA RAFIKI KWA WAFANYABIASHARA WAOTE'

  NA TATU MAKAME, ZANZIBAR @@@@  MAMLAKA ya mapato Tanzania (TRA) Tanzania imesema itaimarisha mazingira mazuri kwa wafanyabiashara kuondosha vikwazo kwao.  Kamisha mkuu wa Mamlaka hiyo Salehe Juma Mwenda alisema hayo wakati wa kikao cha pamoja kilichowashirikisha watendaji wa mamlaka za kodi Tanzania pamoja na wafa nyabiashara hao kilichofanyika huko hoteli ya Madinat Al bahri Mbweni Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja wenye lengo kusikiliza changamoto za wafanyabiashara.  Alisema miongoni mwa mikakati hiyo kuondosha vikwazo kwa wafanyabiashara kwa kutoa ushirikiano kwa wafanyabiashara kila kunapotokuwa vikwazo kwenye uingizaji wa biashara hapa nchini. Mwenda alitumia nafasi hiyo kueleza kuwa mkakati mwengine kuziruhusu bandari za Fumba Unguja na Mkoani Pemba kushusha mizigo inayotoka moja kwa moja nje ya nchi kinyume ilivyo sasa mizigo hiyo kushushwa Mombasa Kenya. Alisema ujenzi wa bandari hizo unakwenda kwa kasi na zitakapokamilika bandari hiyo zitafanya kazi kama ban...

WAZIRI WA FEDHA TANZANIA ''TRA' KUKUSANYA SH/= 42 TRILIONI MWAKA 2026/2027

  NA TATU MAKAME, ZANZIBAR@@@@ WAZIRI wa fedha Tanzania Balozi Khamis Mussa Omar amesema Mamlaka hiyo inatarajia kukusanya shilingi trilioni 42 kwa mwaka wa fedha 2026/2027 katika maeneo mbalimbali ya Tanzania ili kuimarisha ukuaji wa uchumi hapa nchini. Alisema hayo Kizimkazi Mkoa wa Kusini Unguja kwenye hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) ikiwa ni muendelezo wa tamasha la Kizimkazi fastival.  Alisema mapato hayo kutoka vyanzo vya ndani kwa robo tatu ikiwemo ulipaji kodi kwa wafanyabiashara na kueleza kuwa kwa mwezi ulioanzia Julai mwaka huu mamlaka hiyo ilikusanya zaidi ya bilioni 800 sawa na ongezeko la asilimia 21 ya makusanyo. Alisema ukusanyaji mapato unaimarika kila mwaka kwani mwaka wa fedha 2024,2025 Mamlaka ilifikia asilimia 1003 huku mwaka 2025_2026 kiwango cha mapato kilifikia asilimia 1005 kwa Tanzania nzima katika maeneo yote ya yanayokusanywa kodi. Aidha aliwataka wafanyabiashara kulipa kodi kwa hiar...

AWENA SALIM KOMBO: MWANAMKE ANAEPAMBANIA UONGOZI KWENYE JIMBO LAKE

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA   "SIKATI tamaa ipo siku nitafanikiwa lengo langu nililolikusudia kwa sababu kila kitu kimepangwa kwa muda maalumu, hivyo naamini bado wangu haujafika"   Sio maneno ya mtu mwengine bali ni Awena Salim Kombo mwenye umri wa miaka 50 mkaazi wa shehia ya Kangagani Wadi ya Kiuyu, Jimbo la Kojani Wilaya ya Wete Pemba.   Awena ni mwanamke shupavu mwenye ndoto ya kuwa kiongozi tangu akiwa kijana mdogo, na ndipo mwaka 1990 alipoamua kujiunga kwenye chama cha Mapinduzi CCM, ili kusudi apate nafasi ya kuwa kiongozi.   Lengo lake la kusaka uongozi ni kutaka kusaidia jamii kwenye mambo mbalimbali ikiwemo kutatua changamoto zinazowakabili.   "Hivi sasa baadhi ya wanajamii wenye matatizo hunifuata kutaka msaada, hivyo wakati mwengine nashindwa kutokana na hali yangu kutomudu" anaeleza.   Mwaka 2017 Awena alianza kupata nafasi za uongozi katika chama chake, ambapo alijiona tayari anaenda kutimiza ndoto zake ...

BIZUME: MWANAMKE ANAEPAMBANA KUFIKIA TAIFA KIUONGOZI

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA    BIZUME Haji Zume, mkaazi wa shehia ya Kinyasini Jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, ni miongoni mwa wanawake mashuhuri wenye nia ya kufika mbali kiuongozi.   Ingawa matarajio yake yeye mpaka sasa, ni kugombea nafasi za ndani ya chama tu kuanzia tawi hadi Taifa, na sio Jimboni kwa kile anachodai kwamba ni lazima kwanza ushikilie nafasi hizo ili uwe imara zaidi.   Atapojijenga zaidi kwa nafasi za ndani ya chama, hapo ndipo ataanza kutafuta njia ya kusonga mbele kwani, huwezi tu kufika huko ikiwa hukuanza nafasi za chini.   "Nataka na mimi nifikie kugombea Uwakilishi na Ubunge katika Jimbo lakini, huwezi kufika huko ikiwa bado kwenye chama hujashika nafasi yeyote," anasema Bizume.   Lengo la mama huyo kugombea nafasi hizo, ni kuhakikisha anajijengea uwezo zaidi wa kiuongozi, kujenga mahusiano mazuri na wanachama, pamoja na kukubalika kwenye chama chake.   Anasema, hiyo itampa fursa ya kus...