NA TATU MAKAME. ZANZIBAR@@@ UNAPOZUNGUMZIA ujasiri na ucheshi alionao mwanamke utagundua kuwa ni kiungo muhimu katika jamii hasa kwenye nafasi za uongozi. Aidha wanawake wenye uthubutu wa kufanya harakati za jamii wamekuwa na uwezo mkubwa wa kushawishi jamii kufanya harakati za maisha ili kuendeleza maisha yao katika jamii. Hata hivyo serikali na taasisi binafsi nazo zimekuwa mfano mkubwa kuwahamasisha wananwake kuingia kwenye nafasi za uongozi baada ya kuwapatia mafunzo ya kuwania nafasi za uongozi ili kuachana na mfumo dume wa kuwa mwanamke uwezo wake mdogo kuwa kiongozi. Hata hivyo Mradi wa SWIL unaoimarisha uongozi wa wanawake unaoendeshwa na Chama cha waandishi wa habari Tanzania Tamwa ZNZ nao umekuwa mfano bora wa kuwahamasisha wanawake kuingia kwenye nafasi za uongozi na kuwa kioo kwa jamii. Kwa mujibu wa Mkufunzi kutoka Chuo kikuu cha taifa cha Zanzibar (SUZA) Imane Duwe alisema kiongozi sio lazima awe mwanasiasa au mtu maarufu kama wengine. Hata hivyo alisema wanawake wanaoing...
NA MARYAM SALUM, PEMBA@@@@ ‘ MWA NASIASA hatakiwi kuwa mbaguzi, watu wote ni sawa, ili mwisho wa siku, jamii ikuelewe tu,’’anasema Fatma Khamis Juma Diwani wadi ya Tibirinzi. ‘’Tabia yangu hupenda kujichanganya iwe kwenye kijiwe cha kahawa, sokoni nipo, masikani za vijana nipo, na makundi mengine yenye rika tofauti. Hii ni kauli ya Fatma Juma Khamis, anayehudumu udiwani wadi ya Tibirinzi, Jimbo la Chake chake, kwa kipindi cha pili mfululizo sasa. Katika siasa, mtu hatakiwi kuwa mbaguzi na badala yake awe kuwa karibu na jamii iliyomzunguruka, kwa maslahi mapana. Anakiri kuwa kuingia kwenye kinyang’anyiro cha siasa, watu wote hupitia changamoto, ikiwemo kuitwa majina mabaya hasa kwa wanawake. Kwenye jamii iliyo kubwa, tafsiri iliyopo, pindi mwanamke akiingia kwenye siasa hubandikwa majina maovu na yenye kukatisha tamaa, au kuwindwa na washindani wake. Diwani Fatma anasema, kwa awamu ya kwanza ya udiwani wake, hakuishia kuomba kura kwa mikutanao ya hadha...