NA TATU MAKAME, ZANZIBAR@@@@ SERIKALI imesema bandari ya Fumba itakuwa na uwezo wa kushusha na kupakia kontena 40 kwa wakati mmoja ifikapo Januari mwakani hali itakayorahisisha ushushaji wa mizigo katika bandari hiyo na kuondosha usumbufu kwa wafanyabiashara. Mkurugenzi wa Shirika la Bandari Zanzibar Akif Ali Khamis alisema hayo Fumba wakati akitoa maelezo ya ujenzi wa gati ya bandari hiyo kufuatia ziara iliyofanywa na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Yussuph Juma Mwenda aliyefika bandarini kukagua ujenzi wa bandari hiyo. Alisema ujenzi wa bandari utakapokamilika utarahisisha usafirishaji wa mizigo kwa wafanyabiashara na kuongeza mapato kupitia mamlaka ya mapato TRA hasa usafirishaji wa mizigo. Alitumia nafasi hiyo kueleza kuwa bandari hiyo itakuwa na uwezo wa kushusha vyombo 750 kwa wakati mmoja kutokana na ukubwa wa bandari na kueleza kuwa bandari itarahisisha ushushaji wa mizigo kutofautisha na bandari ya Malindi ambayo inashusha kontena 10 hadi 12 kwa w...
NA TATU MAKAME, ZANZIBAR@@@@ LICHA ya ulemavu alionao hakuwahi kukata tamaa katika kupambania maisha yake na jamii inayomzunguuka katika kupata huduma za jamii ikiwemo maji safi na salama katika jamii yake. Unapomuona hali yake na ushujaa wake ni tofauti na uwezo wake kutokana na tatizo la uoni hafifu wa macho aliokuwa nao lakini ana ndoto za kufanikisha yale aliyojipangia katika maisha yake hasa kuwapatia wananchi wa eneo lake huduma ya maji safi na salama ili waondokane na adha ya maji. Unapomuona huwezi amini kama anauwezo na ujasiri wa kusimama akapigania haki yake licha ya umaskini wake pamoja na kubezwa na kudharauliwa kwa sababu ya ulemavu wake. Huyo si mwengine ni Fatma Mgwali Khamis mkaazi wa kijiji cha Fukuchuchani Mkoa wa Kaskazini Unguja. Fatma alizaliwa mnamo mwaka 1977 katika kijiji cha Fukuchani ni mtoto wa tano katika watoto wanane wa Mama mzazi wa Fatma aliyefahamika kwa jina la Tatu Haji Khamis ambae alijaaliwa kupata watoto watatu wanaume na watoto watato wanaw...