NA ZUHURA JABIR, ZNAIBAR “Usafi ni nusu ya afya." Haya sio msemo wa utani, bali ni ukweli unaogusa maisha ya kila siku ya wananchi. Mazingira safi yanamaanisha afya bora, heshima ya makazi na maendeleo ya jamii, lakini pale ambapo mifumo ya usimamizi haieleweki, wananchi hubeba mzigo ambao haukupaswa. Majadiliano yaliyowakutanisha masheha, wahamasishaji wa jamii na wataalamu wa Baraza la Manispaa Mjini, yameonesha wazi kuwa changamoto za usafi wa mazingira bado zinahitaji mshikamano. Methali isemayo, "Kidole kimoja hakivunji chawa," inaakisi hali halisi ya mapambano dhidi ya uchafu wa mazingira. MGONGANO WA MAMLAKA KATIKA UKUSANYAJI WA TAKA Moja ya hoja zilizojitokeza kwa uzito mkubwa ni mgongano wa mamlaka katika ukusanyaji wa taka ndani ya shehia ya Mchangani. Kwa mujibu wa sheha Nassir Mohammed Ali, wananchi wanakabiliwa na hali ya kuchanganyikiwa, kutokana na taasisi mbili, Baraza la Manispaa Mjini na Mamlaka ya Mji Mkongwe, kufanya kazi katika ene...
NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ MALEZI bora na makuzi ya mtoto, ni jambo muhimu kwa maendeleo yake,kimwili na kiakili. Hili linajumuisha huduma zote muhimu anazostahili kupewa mtoto, kuanzia miaka 0 hadi 8, ili kumuwezesha kukuwa na kufikia utimilifu wake. Ikiwa ni kimwili, kiakili, kijamii, kihisia na kimaadili, ilikushiriki kikamilifu katika ujenzi wa taifa na kuyamudu mazingirayake. Mara nyingi ni rahisi kupata haya yote, kutoka kwa wazazi au walezi,lakini wengi wao husahau kwamba matumizi ya lugha nzuri kwa watoto,inamchango mkubwa katika ustawi wao. Na zipo sheria zinazopinga ukatili wa aina zote dhidi ya watoto, kwamsingi kwamba malezi bora kwa mtoto, ndio msingi imara kwa makuzi yake. Mfano, Mkataba wa kimataifa wa haki za watoto duniani ( Conventionoftherightsofthechildren ) wa mwaka 1989, ambao umeanza kutumikarasmi mwaka 1990. Ibara yake ya 19 inasisitiza, kuwa‘ nchi wanachama kuhakikishawanakuwa na sheria nzuri zitakazo mlinda mtoto juu ya aina zote zau...