Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

JUMAZA INAUNGA MKONO MARIDHIANO VYAMA VYA SIASA ZANZIBAR

  NA AMRAT KOMBO, ZANZIBAR@@@@ JUMUIYA ya Maimamu Zanzibar    (JUMAZA) imesema inaunga mkono tamko la maridhiano ya chama cha CCM  na ACT Wazalendo kwani ni hatua   ya msingi katika kuimarisha  amani, umoja na maendeleo ya  Zanzibar. Katibu Mtendaji wa Jumuiya hiyo,  Shekh Ali Abdalla Amour, aliyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Jamatkhan Vuga mjini Unguja. Alisema jumuiya hiyo imepokea kwa faraja na furaha maridhiano yaliyotangazwa hadharani  Julai 9, katika viwanja vya Ikulu  Zanzibar mbele ya Rais wa Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia  Suluhu Hassan. Aidha alisema ni vyema kwa   viongozi hao kutofanya khiyana katika  utekelezaji wa makubaliano hayo ili  kuendelea kujenga amani, umoja   na mshikamano kwa wananchi wa Z anzibar. Alieleza kuwa jambo hilo limeonesha  utayari wa viongozi kuweka mbele maslahi ya Zanzibar na wananchi wake badala ya ...
Recent posts

UNDP, PACSO WAWAPA DOZI YA KISHERIA WANANACHI UWANDANI, WENYEWE WAFURAHIA

    NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ MWANASHERIA wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Idara Maalum ‘SMZ’ Aziza Suleiman Mohamed amesema, jamii imekuwa ikifahamu udhalilishaji, unaopelekea madhara ya kimwili, bali unajumuishwa madhara ya  kingono, kihisia, kutelekezwa pamoja na kumnyima mtu usalama wake. Ameyasema hayo jana August 3, 2026 alipokuwa akizungumza na wananchi wa shehia ya Uwandani wilaya ya Chake chake, juu ya elimu iliyoandaliwa na Mwemvuli wa Asasi za Kiraia Pemba PACSO na kufanyika skuli ya Uwandani. Alisema kuwa upo udhalilishaji mbalimbali unaojumuishwa madhara ya kingono, kihisia, kutelekezwa pamoja na kumnyima mtu usalama wake. Alisema matokeo ya udhalilishaji ni makubwa kiasi ambacho, kunaweza kusababisha majaraha, kifo kuenea kwa maradhi tabia hatarishi na matokeo mabaya kwa wanaofanyiwa. Alifafanua kuwa wahanga wakubwa wanaothirika na vitendo hivyo ni wanawake, watoto na watu wenye ulemavu, hivyo ipo sheria ya Mtoto nambari 6 ya mwaka 2011,...

UTAMADUNI WA KUTOBOA, KUWEKA KIPINI CHA PUA, WAIBEBA MICHEWENI, WANAUME WAKIRI KUVUTIWA

      NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@   ‘’TUMESHAWAHI kusimamisha shughuli ya harusi kwa dakika 10, mke asichukuliwe, baada ya kugundua hatujamtia pambo la kipini cha pua,’’anasema Rehema Faki Shehe (60) wa Kwale Micheweni Pemba. Ilishazoelekea kuwa, kuwa mapambo ni aina ya mafuta, podari, pete, mkufu, udi, wanja na hina, ingawa kwa wanawake wilaya ya Micheweni, kipaumbele ni utoboaji wa pua kwa ajili ya utiaji wa kipini. Utamaduni wa utoboaji (utomoaji) wa pua tena ya upande wa kushoto, wenyewe wanawake wa Micheweni waliurithi zaidi ya miaka 200 iliyopita. Kwa mfano, Rehema Faki Shehe (60) alimkuta bibi yake wakati akiwa huo akiwa na miaka 50, akiwa ametobolewa tundu la upande wa kushoto ya pua, akiwa na kipini. KINA MAAGA GANI KIPINI CHA PUA? Sharifu Massoud Hamad (60) wa Kwale Micheweni mkoa wa kaskazini Pemba, anasema moja ni tofauti kati ya mwanamke na mwanamme. Anaona hata unapokuta wamevaa mavazi yenye kufanana, lakini dalili kubwa ya tofauti hiyo...

SHEHA FATMA WA KENDWA, AIDHIHIRISHIA DUNIA WANAWAKE WANAPOPATA UONGOZI.....

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ "UONGOZI sio cheo, ni matendo na matokeo yanayobadilisha maisha ya watu" ni maneno ya wananchi wa shehia ya Kendwa wilaya ya Mkoani. Wanasema sheha wao ni mwanamke aliyethibitisha kuwa, uongozi wa mwanamke una nguvu ya kubadilisha kabisa muelekeo wa jamii. Wanakendwa ni kama wanaungana na Mkataba wa umoja wa Mataifa wa kutokomeza aina zote za udhalilishaji (CEDAW) wa 1979 hasa ibara ya 7. Ibara inayozitaka “ Nchi wanachama zihakikishe zinawapa wanawake fursa za kushiriki katika uongozi’’. Aidha lengo namba 5.5 la maendeleo endelevu ‘SDGs’ ya mwaka 2015 hadi 2030, lililozitaka nchi zote kuhakikisha ushiriki kamili wa wanawake na fursa sawa za uongozi katika ngazi zote, iwe kisiasa, kiuchumi na kijamii. Pia Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 ibara yake ya 21 (1) inayoeleza kila Mzanzibari anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia Wawakilishi waliochaguliwa kwa hiari. Sera ya Maendeleo ya...

'NGUVU MOJA' USHIRIKA WA WATU WENYE ULEMAVU PEMBA, WALIA KUFANYIWA UKATILI WA KIUCHUMI

    NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ UMEWAHI kuwaza maisha bila kuona, kusikia, kusema au kusimama. Basi hayo ndio maisha ya kila siku ya watu, wenye ulemavu, aidha wa viungo, uoni, uziwi na aina nyengine. Lakini watu wenye ulemavu ni sawa na watu wengine, wanahaki zote za msingi, kama ilivyo kwa wengine. Miongoni mwa haki hizo ni kushiriki katika shughuli za kiuchumi, kama ilivyoelezwa katika mikataba na sheria mbalimbali. Mkataba wa kimataifa wa haki za watu wenye ulemavu wa 2006, ambao ibara yake ya 27 (f) inasisitiza ushiriki na ushirikishwaji wao kiuchumi. “Nchi wanachama wakuze fursa za watu wenye ulemavu kujiajiri, kuanzisha na kuendesha shughuli za ujasiamali, vyama vya ushirika na mtu binafsi kuanzisha biashara zake”, inaeleza sehemu ya mkataba huo. Sheria ya watu wenye ulemavu ya Zanzibar nambari 8 ya mwaka 2022, kifungu cha 28 (e) inaeleza, watu wenye ulemavu wanastahiki haki zote za msingi za kibinaadamu sawa nawatu wengine ikiwemo kujitegemea na kujumuishw...