Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

UJENZI BANDARI YA MICHEWENI NI JUHUDI ZA DK. MWINYI KUIFUNGUA PEMBA KIUCHUMI

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, amedhamiria kwa vitendo kuleta maendeleo ya kiuchumi kisiwani Pemba. Na ndio maana, anachukua juhudi mbalimbali kuhakikisha wananchi wa Pemba, wanakuwa na maisha bora kiuchumi, kwa kuendelea kuwapelekea miradi ya kimaendeleo ya kimkakati. Lengo ni kuona kwamba, kila mwananchi anajiajiri na kuajiriwa kupitia fusra za kiuchumi, ambazo zinaendelea kuletwa na Dk. Mwinyi katika kila sekta. Hayo ni ya kujivunia katika kisiwa hiki, kwani kinaenda kufunguka na kuleta maendeleo endelevu kwa wananchi wake. Moja ya miradi mikubwa ambayo itakuza uchumi wa wananchi kisiwani Pemba, ni ujenzi wa bandari za kitaifa ambazo zitawaingizia kipato wananchi, kwa namna moja ama nyingine na kupata maendeleo. Katika ahadi zake Dk. Mwinyi alizoziweka kwa wananchi kwa ajili ya kukuza kipato chao, ni ujenzi wa Bandari ya Shumba Mjini, iliyoko wilaya ya Micheweni mkoa wa kaskazini Pemba. Ba...
Recent posts

UCHUMI WA BULUU YAJA NA MRADI WA AINA YAKE KWA UVUVI, UFUGAJI ENDELEVU WA MAZAO YA BAHARINI

  NA FATMA HAMAD,PEMBA @@@@ SEKTA ya uvuvi, ufugaji wa samaki na kilimo  cha mwani iznaendelea kuwa nguzo muhimu ya ajira na kipato kwa wananchi wa Zanzibar huku Serikali  na taasisi binafsi ikiweka mkazo katika matumizi ya rasilimali za baharini kama fursa ya biashara na uwekezaji.  Hayo yalisemwa na  jana Septemba 1, 2026 na Ofisa Mdhamini wizara ya Uchumi wa Bulu DK Salim Mohamed Hamza wa kati akizungumza katika mkutano wa wadau wa Mradi wa Kuimarisha Usimamizi Endelevu wa Uvuvi na Ufugaji wa Mazao ya Baharini Tanzania, TASFAM,  huko katika ukumbi wa ZRA Gombani Chakechake Kusini Pemba.  Alisemesema ushirikiano wa wadau ni muhimu katika kuongeza uzalishaji, ajira na kipato kwa wananchi.  ALisema kwa Sasa serikali imeelekeza zaidi katika sekta ya Bahari, hivyo imeamua kuleta Mardi huo wa kuimarisha usimamizi endelevu wa uvuvi na ufugajibwa mazao baharini, ili wadau muunge mkono Mardi huo na lile lengo la serikali liweze kutimia la kujipatia kipa...

SITI FAKI ALI WA WETE: Ndie Mwalimu Mkuu alieondosha ‘sifuri’ skuli ya Utaani

                                   ‘Aweka mikakati wanabaki daraja la kwanza na la pili tu. IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA "Nilipoteuliwa kuwa Mwalimu Mkuu, mwanzo nilipata hofu hasa pale nilipojiona, naenda kuongoza watu wenye kiwango cha elimu sawa na mimi,’’anasema.    Ni maneno ya Mwalimu Mkuu skuli ya Sekondari ya Wanawake Utaani Wete, Siti Faki Ali mkaazi wa Chasasa Wete.   Mwalimu huyo ambae alitokea skuli ya Chasasa akiwa Msaidizi Mwalimu Mkuu, alipata hofu mara ya kupokea barua ya kwenda kuiongoza skuli hiyo.   Anasema, kwa vile ameshakaa uongozi katika mambo mbalimbali ya kijamii na Serikali kwenye nafasi ndogo ndogo, ndipo alipoona kwamba na nafasi hiyo anaweza kuiongoza.   Mara baada ya kukabidhiwa madaraka, alianza kuweka mikakati, ikiwemo kuondosha zero kwa wanafunzi kuanzia kidato cha pili hadi cha...

WALISEMA SIWEZI, LAKINI SIKUACHA”: FATMA AIBADILISHA CHANGAMOTO YA ULEMAVU KUWA NGUVU YA KUJITEGEMEA

  NA ZUHURA JABIR, ZANZIBAR @@@@   JUMBI, Wilaya ya Magharibi B, Unguja Kwa Fatma Suleiman Mussa, safari ya kujitegemea haikuanza na biashara. Ilianza akiwa mtoto, katika mazingira ambayo ulemavu wake uliifanya safari ya elimu kuwa ngumu na kumlazimu kukabiliana mapema na mitazamo ya watu waliodhani hawezi kufikia ndoto zake.  Licha ya changamoto hizo, Fatma hakukubali ulemavu uwe sababu ya kuachana na elimu au ndoto zake.   Alianza safari yake ya elimu akiwa na changamoto ambazo watoto wengi wasio na ulemavu huenda wasizikabili. Katika kipindi chake cha masomo, alikutana na vikwazo mbalimbali vilivyohusiana na hali yake, lakini aliendelea kusoma kadiri alivyoweza.   Kwa Fatma, shule haikuwa sehemu ya kupata elimu pekee. Ilikuwa pia sehemu ambayo alijifunza kuvumilia, kujiamini na kukataa kuamini kwamba uwezo wa mtu unaweza kupimwa kwa kuangalia mwili wake.   Safari yake ya elimu ilimfundisha somo ambalo limeendelea kuwa sehemu ya maisha yake hadi leo: kwam...