Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

FATMA SULEIMAN, MWENYE ULEMAVU ALIYEFANYA MAAMUZI YA KIMAENDELEO

  NA ZUHURA JABIR   Katika jamii, mara nyingi mafanikio hupimwa kwa kiwango cha elimu, mali au nafasi aliyonayo mtu. Hata hivyo, kuna watu ambao maisha yao yanatufundisha kwamba mafanikio makubwa huanza pale mtu anapoamua kujiamini, kupambana na changamoto na kutokubali mazingira yamzuie kufikia ndoto zake.   Hii ni simulizi ya Fatma Suleiman Mussa, mwanamke mwenye ulemavu anayeishi Jumbi, Zanzibar, ambaye licha ya changamoto alizokutana nazo tangu akiwa mtoto, ameamua kutumia uwezo alionao kujiajiri, kusaidia familia yake na kuwa mfano kwa wanawake wengine wenye ulemavu. Safari yake imejaa changamoto, lakini pia ni ushahidi kwamba “ ulemavu si mwisho wa ndoto. ”   SAFARI YA ELIMU NA MAISHA Fatma ni mtoto wa pili katika familia ya watoto wanne, wote wakiwa wa kike. Alianza elimu ya msingi katika Skuli ya Tunguu na baadaye aliendelea hadi kidato cha pili mwaka 2015. Alipata nafasi ya kuendelea na kidato cha tatu katika Skuli ya Kibele, lakini changamoto mbalimbali zil...
Recent posts

'ZRA' YAFANYA MABADILIKO SHERIA ZA KODI KUONGEZA UFANISI

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ MAMLAKA ya Mapato Zanzibar 'ZRA' imesma, imezifanyia mabadiliko   sheria saba   za kodi kwa mwaka wa fedha 2026/2027, yanalenga kuleta ufanisi katika makusanyo na kuwapa ahuweni wananchi. Hayo yameelezwa leo August 28, 2026  na Mkuu wa Kitengo cha Habari Makame Khamis Mohamed  wakati akiwailisha mabadiliko ya sheria hizo kwa wahariri na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali kisiwani Pemba, katika ukumbi wa mikutano wa Mamlaka hiyo Gombani Chake chake Pemba. Alisema kua mabadiliko hayo, yanalenga kuleta ufanisi kwa mlipa kodi na serikali, kwani yamezingatia kupunguza kasoro mbalimbali, zinazojitokeza pande zote mbili wakati wa kulipa na kukusanya kodi hizo. Alieleza kua mabadiliko ya sheria hizo pia yamezingatia mabadiliko na mwenendo wa sayansi na teknolojia,   pamoja na kuzingatia unafuu kwa walipakodi na kuongeza mapato kwa serikali kuu. "Sababu ya madiliko ya sheria mbalimbali za kodi kwa mwaka wa fedha 2026/2027...

ARABIA: DAKTARI DHAMANA KIGOMANI MATEMWE CHACHU YA WANAWAKE KUVITUMIA VITUO VYA AFYA

  NA TATU MAKAME HARAKATI za usawa wa kijinsia na ukombozi wa sauti ya mwanamke visiwani Zanzibar zimepitia vikwazo vingi, zikikabiliwa na mifumo dume, mila na mazingira ya kitamaduni yaliyomweka mtoto wa kike nyuma kwa miaka mingi. Katika muktadha wa kale wa kijamii, wanawake walionekana zaidi kama wasindikizaji wa kisiasa na kijamii, huku sauti zao zikisikika kwa uchache na mara nyingi zikibaki pembezoni mwa meza kuu za maamuzi. Fikra hizi zilizaa dhana potofu kuwa uongozi ni haki ya wanaume pekee na kumfanya mtoto wa kike kuziangalia nafasi za juu kama ndoto isiyoweza kufikika. Hata hivyo, mabadiliko ya nyakati na ukuaji wa uelewa wa kijamii unathibitisha kuwa uongozi kwa mwanamke sio lazima awe mwanasiasa au kiongozi mashuhuri ambae pia anaweza kutokea katika jamii ambayo bado inafikra finyu juu ya uongozi kwa mwanamke. Tunapozungumzia suala la uongozi tunabaini kuwa viongozi mbalimbali wamepiga gatua na kuwa mfano wa viongozi waliobeba sauti za wengi katika jamii inayomzunguuk...

KUMBE SIFUNI NDIE KATIBU MKUU WA MWANZO PACSO MWANAMKE

  NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ SIFUNI Ali Haji ni Katibu Mkuu na ni kiongozi wa mwanzo, anaefanya kazi na mtandao wa asasi za kiraia katika kisiwa cha Pemba, akiwa wa kwanza mwanamke. Anasema mtandao huo unaojulikana kwa jina la PACSO, ni Umoja wa Jumuiya zisizo za kiserikali uliyoanzishwa mwaka 2005. Katika safari ya uongozi wake, anaendelea kuzisimamia jumuiya na wanachama waliokuwa Pemba ikiwemo Pegao, Juwauza, na Tamwa. Sifuni anaendelea kuvunja vikwazo vyake, katika Jumuiya hiyo kwa zaidi ya miaka sita, akilenga macho yake katika mkoa wa kusini na kaskazini mwa mji wa Pemba. Kutokana na juhudi zake na moyo wa kujituma, amekuwa akilenga uwezo wa kusimamia maendeleo endelevu kwa jamii ya kisiwa hicho. ‘’Nafasi hii haikuja tu, baada ya juhudi zangu nilizokuwa nikizifanya katika uwanachama wangu, ndipo nilipopigiwa kura kwa asilimia zote kushika nafasi ya katibu, anafafanua. Zaidi ya mwaka mmoja taasisi hiyo, haikuwa na mafaniko yoyote baada ya kusimamiwa na wanaume, ndip...

MBINU ZA DK. MWINYI UIMARISHAJI BANDARI YA MKOANI PEMBA, MATUNDA YAONEKANA KWA MACHO SASA

    NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ UNAPOZUNGUMZIA juhudi za serikali, katika kuiletea Pemba maendeleo ya kiuchumi, huwezi kuacha uimarishaji miundombinu ya bandari ya Mkoani Pemba. Bandari ambayo ni sehemu muhimu katika uchumi wa watu wa kusini Pemba na kisiwa kizima kwa ujumla. Kutokana na umuhimu wa bandari hiyo, serikali imekuwa ikiimarisha kwa kuifanya kuwa ya kisasa zaidi, ili kutoa huduma bora kwa wananchi. Kwani kumekuwa na maboresho makubwa, yanayo husisha gati ya kisasa, ujenzi wa jengo la abiria, njia ya kupitia abiria na kuongezwa kwa eneo la bandari kavu, kwa kuwekwa eneo maalumu la kutunzia makontena ya mizigo. Mkurugenzi wa Shirika la Bandari Pemba Abdalla Salim Abdalla, anasema bandani ya Mkoani ni ya pili kwa ukubwa visiwani humo, ikipokea meli kubwa za mizigo kutoka nchi mbalimbali na kukuza uchumi wa kisiwa hicho. Anasema, maboresho hayo yanalenga kuziwezesha meli za kisasa za mwendokasi, kuegesha kwa urahisi na usalama na kurahisisha safari za boti bai...