NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@ KATIKATI ya giza nene lililogubika haki ya mwanamke kuwa kiongozi kwa wakati huo, kuna mwanamke alielishinda?. Alisimama kidedea, yeye na waliomzunguka walihakikisha anafanikiwa na kweli alishika nafasi mbalimbali za uongozi, mpaka kuwa mmoja wa viongozi wanawake walioweka alama isiyofutika katika jamii. Ni Hanuna Ibrahim Massoud, alieanza kuliona jua mwaka 1959, Kisiwani kwa Binti Abedi wilaya ya Wete kaskazini Pemba. Alianza kusaka elimu yake ya msingi, mwaka 1965, ambapo aliipata katika skuli tofauti kama Ziwani, Shamiani na Utaani. Mnamo mwaka 1974, alikamilisha elimu yake ya sekondari kidato cha nne, katika skuli ya Fidel Castro. “Safari yangu ya masomo haikuwa na kituo kimoja, nilisoma maeneo mengi, lakini huku kulinifanya kuyajuwa na kuyatawala vizuri mazingira,’’anahadithia. Kumbe wakati huo kuelimika kwa mtoto wa kike hadi kidato cha nne, ilikuwa fursa adimu na nimsingi mkubwa wa ukombozi. Safari yake ya kutafuta elimu, ...
NA SULEIMAN SAID, PEMBA “Fikiria mtoto anapokuwa tumboni, macho yake bado yamefumba,’’inafahamika. Ingawa ndani ya kichwa chake kuna mabilioni ya seli zilizo tayari kumsaidia kujifunza . Cha kushangaza ni kwamba, msingi wa seli hizo, uliwekwa wiki chache, tu baada ya mama kutunga mimba. Lakini cha kujiuliza je, unajua kipindi hiki ndicho kinachoweka msingi muhimu wa maendeleo yake ya baadaye?’’. Mtaalamu wa eneo hilo hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani, anasema wazazi wengi huamini kuwa elimu ya mtoto huanza siku ya kwanza, anapoingia darasani, lakini ukweli wa kisayansi ni kwamba kujifunza huanza sambamba na safari ya ukuaji wa ubongo. Tena inafahamika kuwa ni, wiki chache baada ya mimba kutungwa, na kadiri ujauzito unavyokuwa mtoto huanza pia kuitikia na kujifunza kutokana na mazingira yake akiwa tumboni. Anasema kuanzia takribani wiki ya tatu, baada ya mimba kutungwa, ubongo wa mtoto huanza kukua ...