Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

DONGO MSANII MWENYE NDOTO ZA KUFIKA MBALI KWENYE FANI YA UIGIZAJI

  -Asema, changamoto ya kifedha inawarudisha nyuma kwenye kazi zao NA ZUHURA JUMA, PEMBA    KHAMIS Ali Omar (32), umaarufu ‘dongo’, ni mkaazi wa Kambini Kichokochwe wilaya ya Wete Pemba.   Yeye ni msanii wa kizazi kipya mwenye ndoto za kufika mbali kwenye uigizaji wake.   Alianza fani hiyo mwaka 2017, wakati huo haikuwa moyoni mwake, wala haikuwa katika malengo yake aliyojiwekwea kwenye maisha.   Kipindi hicho alikuwa kwenye kikundi cha mchezo wa sarakasi cha 'Kambini Art Group' , hivyo kulikuwa na maonyesho yanayofanyika kila mwezi wa mwisho kabla ya kuingia kwenye funga, kijijini kwao, ambapo walikutana na vikundi mbalimbali ikiwemo vya uigizaji.   "Hapa kwetu kila mwaka mwezi wa ‘ mrisho’ , ( siku moja kabla ya ramadhan ), kulikuwa kunafanyika onesho 'show' , hivyo vikundi mbalimbali vya burudani vilialikwa na kuonyesha vipaji vyetu," anaeleza Dongo.   Wakati wapo kwenye sarakasi, mmoja wao alizaa wazo la kutaka kuigiz...
Recent posts

BANDARI YA FUMBA KUANZA KAZI JANUARI MWAKANI

  NA TATU MAKAME, ZANZIBAR@@@@ SERIKALI imesema bandari ya Fumba itakuwa na uwezo wa kushusha na kupakia kontena 40 kwa wakati mmoja ifikapo Januari mwakani hali itakayorahisisha ushushaji wa mizigo katika bandari hiyo na kuondosha usumbufu kwa wafanyabiashara. Mkurugenzi wa Shirika la Bandari Zanzibar Akif Ali Khamis alisema hayo Fumba wakati akitoa maelezo ya ujenzi wa gati ya bandari hiyo kufuatia ziara iliyofanywa na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Yussuph Juma Mwenda aliyefika bandarini kukagua ujenzi wa bandari hiyo. Alisema ujenzi wa bandari utakapokamilika utarahisisha usafirishaji wa mizigo kwa wafanyabiashara na kuongeza mapato kupitia mamlaka ya mapato TRA hasa usafirishaji wa mizigo.  Alitumia nafasi hiyo kueleza kuwa bandari hiyo itakuwa na uwezo wa kushusha vyombo 750 kwa wakati mmoja kutokana na ukubwa wa bandari na kueleza kuwa bandari itarahisisha ushushaji wa mizigo kutofautisha na bandari ya Malindi ambayo inashusha kontena 10 hadi 12 kwa w...

FATMA MGWALI: ULEMAVU HAIKUA KIKWAZO KUISAIDIA JAMII YAKE

  NA TATU MAKAME, ZANZIBAR@@@@ LICHA ya ulemavu alionao hakuwahi kukata tamaa katika kupambania maisha yake na jamii inayomzunguuka katika kupata huduma za jamii ikiwemo maji safi na salama katika jamii yake. Unapomuona hali yake na ushujaa wake ni tofauti na uwezo wake kutokana na tatizo la uoni hafifu wa macho aliokuwa nao lakini ana ndoto za kufanikisha yale aliyojipangia katika maisha yake hasa kuwapatia wananchi wa eneo lake huduma ya maji safi na salama ili waondokane na adha ya maji. Unapomuona huwezi amini kama anauwezo na ujasiri wa kusimama akapigania haki yake licha ya umaskini wake pamoja na kubezwa na kudharauliwa kwa sababu ya ulemavu wake. Huyo si mwengine ni Fatma Mgwali Khamis mkaazi wa kijiji cha Fukuchuchani Mkoa wa Kaskazini Unguja. Fatma alizaliwa mnamo mwaka 1977 katika kijiji cha Fukuchani ni mtoto wa tano katika watoto wanane wa Mama mzazi wa Fatma aliyefahamika kwa jina la Tatu Haji Khamis ambae alijaaliwa kupata watoto watatu wanaume na watoto watato wanaw...

TRA: 'TUNAENDELEA KUIMARISHA MAZINGIRA RAFIKI KWA WAFANYABIASHARA WAOTE'

  NA TATU MAKAME, ZANZIBAR @@@@  MAMLAKA ya mapato Tanzania (TRA) Tanzania imesema itaimarisha mazingira mazuri kwa wafanyabiashara kuondosha vikwazo kwao.  Kamisha mkuu wa Mamlaka hiyo Salehe Juma Mwenda alisema hayo wakati wa kikao cha pamoja kilichowashirikisha watendaji wa mamlaka za kodi Tanzania pamoja na wafa nyabiashara hao kilichofanyika huko hoteli ya Madinat Al bahri Mbweni Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja wenye lengo kusikiliza changamoto za wafanyabiashara.  Alisema miongoni mwa mikakati hiyo kuondosha vikwazo kwa wafanyabiashara kwa kutoa ushirikiano kwa wafanyabiashara kila kunapotokuwa vikwazo kwenye uingizaji wa biashara hapa nchini. Mwenda alitumia nafasi hiyo kueleza kuwa mkakati mwengine kuziruhusu bandari za Fumba Unguja na Mkoani Pemba kushusha mizigo inayotoka moja kwa moja nje ya nchi kinyume ilivyo sasa mizigo hiyo kushushwa Mombasa Kenya. Alisema ujenzi wa bandari hizo unakwenda kwa kasi na zitakapokamilika bandari hiyo zitafanya kazi kama ban...

WAZIRI WA FEDHA TANZANIA ''TRA' KUKUSANYA SH/= 42 TRILIONI MWAKA 2026/2027

  NA TATU MAKAME, ZANZIBAR@@@@ WAZIRI wa fedha Tanzania Balozi Khamis Mussa Omar amesema Mamlaka hiyo inatarajia kukusanya shilingi trilioni 42 kwa mwaka wa fedha 2026/2027 katika maeneo mbalimbali ya Tanzania ili kuimarisha ukuaji wa uchumi hapa nchini. Alisema hayo Kizimkazi Mkoa wa Kusini Unguja kwenye hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) ikiwa ni muendelezo wa tamasha la Kizimkazi fastival.  Alisema mapato hayo kutoka vyanzo vya ndani kwa robo tatu ikiwemo ulipaji kodi kwa wafanyabiashara na kueleza kuwa kwa mwezi ulioanzia Julai mwaka huu mamlaka hiyo ilikusanya zaidi ya bilioni 800 sawa na ongezeko la asilimia 21 ya makusanyo. Alisema ukusanyaji mapato unaimarika kila mwaka kwani mwaka wa fedha 2024,2025 Mamlaka ilifikia asilimia 1003 huku mwaka 2025_2026 kiwango cha mapato kilifikia asilimia 1005 kwa Tanzania nzima katika maeneo yote ya yanayokusanywa kodi. Aidha aliwataka wafanyabiashara kulipa kodi kwa hiar...