NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, amedhamiria kwa vitendo kuleta maendeleo ya kiuchumi kisiwani Pemba. Na ndio maana, anachukua juhudi mbalimbali kuhakikisha wananchi wa Pemba, wanakuwa na maisha bora kiuchumi, kwa kuendelea kuwapelekea miradi ya kimaendeleo ya kimkakati. Lengo ni kuona kwamba, kila mwananchi anajiajiri na kuajiriwa kupitia fusra za kiuchumi, ambazo zinaendelea kuletwa na Dk. Mwinyi katika kila sekta. Hayo ni ya kujivunia katika kisiwa hiki, kwani kinaenda kufunguka na kuleta maendeleo endelevu kwa wananchi wake. Moja ya miradi mikubwa ambayo itakuza uchumi wa wananchi kisiwani Pemba, ni ujenzi wa bandari za kitaifa ambazo zitawaingizia kipato wananchi, kwa namna moja ama nyingine na kupata maendeleo. Katika ahadi zake Dk. Mwinyi alizoziweka kwa wananchi kwa ajili ya kukuza kipato chao, ni ujenzi wa Bandari ya Shumba Mjini, iliyoko wilaya ya Micheweni mkoa wa kaskazini Pemba. Ba...
NA FATMA HAMAD,PEMBA @@@@ SEKTA ya uvuvi, ufugaji wa samaki na kilimo cha mwani iznaendelea kuwa nguzo muhimu ya ajira na kipato kwa wananchi wa Zanzibar huku Serikali na taasisi binafsi ikiweka mkazo katika matumizi ya rasilimali za baharini kama fursa ya biashara na uwekezaji. Hayo yalisemwa na jana Septemba 1, 2026 na Ofisa Mdhamini wizara ya Uchumi wa Bulu DK Salim Mohamed Hamza wa kati akizungumza katika mkutano wa wadau wa Mradi wa Kuimarisha Usimamizi Endelevu wa Uvuvi na Ufugaji wa Mazao ya Baharini Tanzania, TASFAM, huko katika ukumbi wa ZRA Gombani Chakechake Kusini Pemba. Alisemesema ushirikiano wa wadau ni muhimu katika kuongeza uzalishaji, ajira na kipato kwa wananchi. ALisema kwa Sasa serikali imeelekeza zaidi katika sekta ya Bahari, hivyo imeamua kuleta Mardi huo wa kuimarisha usimamizi endelevu wa uvuvi na ufugajibwa mazao baharini, ili wadau muunge mkono Mardi huo na lile lengo la serikali liweze kutimia la kujipatia kipa...