Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

MBINU ZA DK. MWINYI UIMARISHAJI BANDARI YA MKOANI PEMBA, MATUNDA YAONEKANA KWA MACHO SASA

    NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ UNAPOZUNGUMZIA juhudi za serikali, katika kuiletea Pemba maendeleo ya kiuchumi, huwezi kuacha uimarishaji miundombinu ya bandari ya Mkoani Pemba. Bandari ambayo ni sehemu muhimu katika uchumi wa watu wa kusini Pemba na kisiwa kizima kwa ujumla. Kutokana na umuhimu wa bandari hiyo, serikali imekuwa ikiimarisha kwa kuifanya kuwa ya kisasa zaidi, ili kutoa huduma bora kwa wananchi. Kwani kumekuwa na maboresho makubwa, yanayo husisha gati ya kisasa, ujenzi wa jengo la abiria, njia ya kupitia abiria na kuongezwa kwa eneo la bandari kavu, kwa kuwekwa eneo maalumu la kutunzia makontena ya mizigo. Mkurugenzi wa Shirika la Bandari Pemba Abdalla Salim Abdalla, anasema bandani ya Mkoani ni ya pili kwa ukubwa visiwani humo, ikipokea meli kubwa za mizigo kutoka nchi mbalimbali na kukuza uchumi wa kisiwa hicho. Anasema, maboresho hayo yanalenga kuziwezesha meli za kisasa za mwendokasi, kuegesha kwa urahisi na usalama na kurahisisha safari za boti bai...
Recent posts

KAMATI KUFANIKISHA TAMASHA LA 31 UTAMADUNI WA MZANZIBARI ZAZINDULIWA PEMBA

  NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ KAIMU Ofisa Mdhamini Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Pemba, Sharifa Hamad Shapandu, amezitaka kamati za kufanikisha tamasha la 31 la utamaduni wa mzanzibari, kuhakikisha zinafanyakazi kwa kushirikiana, ili kufanikisha tamasha hilo.   Ameyasema hayo August 18, 2026, ofisini kwake Gombani Chakechake Pemba, mara baada ya kuzizindua kamati hizo tano, kuelekea uzinduzi wa tamasha hilo mwishoni mwa mwezi ujao, kisiwani humo.   Alisema kuwa, kuwepo kwa kamati hizo anataka iwe ni njia rahisi ya kufanikiwa kwa tamasha hilo, ambalo kwa awamu hii, linatarajiwa kuwa la aina yake. Alieleza kuwa, njia ya kuzigawa kwa kamati hizo, ni namna ya kuwa na na urahisi wa ufuatuliaji, ingawa isiwe chanzo cha kukosa kushirikiana.   ‘’Najua kuwa zipo kamati tano, zinawajumbe wenye uwezo na maarifa yasiofanana, lakini hili sasa muwe na ushirikiano kwa pamoja, ili kulifanikisha hili,’’alifafanua.   Aidha Kaimu Ofisa Mdhamini huy...

DONGO MSANII MWENYE NDOTO ZA KUFIKA MBALI KWENYE FANI YA UIGIZAJI

  -Asema, changamoto ya kifedha inawarudisha nyuma kwenye kazi zao NA ZUHURA JUMA, PEMBA    KHAMIS Ali Omar (32), umaarufu ‘dongo’, ni mkaazi wa Kambini Kichokochwe wilaya ya Wete Pemba.   Yeye ni msanii wa kizazi kipya mwenye ndoto za kufika mbali kwenye uigizaji wake.   Alianza fani hiyo mwaka 2017, wakati huo haikuwa moyoni mwake, wala haikuwa katika malengo yake aliyojiwekwea kwenye maisha.   Kipindi hicho alikuwa kwenye kikundi cha mchezo wa sarakasi cha 'Kambini Art Group' , hivyo kulikuwa na maonyesho yanayofanyika kila mwezi wa mwisho kabla ya kuingia kwenye funga, kijijini kwao, ambapo walikutana na vikundi mbalimbali ikiwemo vya uigizaji.   "Hapa kwetu kila mwaka mwezi wa ‘ mrisho’ , ( siku moja kabla ya ramadhan ), kulikuwa kunafanyika onesho 'show' , hivyo vikundi mbalimbali vya burudani vilialikwa na kuonyesha vipaji vyetu," anaeleza Dongo.   Wakati wapo kwenye sarakasi, mmoja wao alizaa wazo la kutaka kuigiz...

BANDARI YA FUMBA KUANZA KAZI JANUARI MWAKANI

  NA TATU MAKAME, ZANZIBAR@@@@ SERIKALI imesema bandari ya Fumba itakuwa na uwezo wa kushusha na kupakia kontena 40 kwa wakati mmoja ifikapo Januari mwakani hali itakayorahisisha ushushaji wa mizigo katika bandari hiyo na kuondosha usumbufu kwa wafanyabiashara. Mkurugenzi wa Shirika la Bandari Zanzibar Akif Ali Khamis alisema hayo Fumba wakati akitoa maelezo ya ujenzi wa gati ya bandari hiyo kufuatia ziara iliyofanywa na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Yussuph Juma Mwenda aliyefika bandarini kukagua ujenzi wa bandari hiyo. Alisema ujenzi wa bandari utakapokamilika utarahisisha usafirishaji wa mizigo kwa wafanyabiashara na kuongeza mapato kupitia mamlaka ya mapato TRA hasa usafirishaji wa mizigo.  Alitumia nafasi hiyo kueleza kuwa bandari hiyo itakuwa na uwezo wa kushusha vyombo 750 kwa wakati mmoja kutokana na ukubwa wa bandari na kueleza kuwa bandari itarahisisha ushushaji wa mizigo kutofautisha na bandari ya Malindi ambayo inashusha kontena 10 hadi 12 kwa w...