NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi, katika uzinduzi wa tamasha la 31 la utamaduni wa mzanzibari, linalotarajiwa kufanyika leo hii, uwanja wa michezo Gombani Chake chake Pemba. Uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika, kuanzia majira ya saa 8:00 jioni ya leo, na shamara shamara na maandalizi ya tamasha hilo zitaanzaa mapema, uwanjani hapo. Akizungumza na mwandishi wa habari, Kamishna wa Utamaduni Zanzibar Dk. Omar Salum Mohamed alisema, maandalizi yote yameshakamilika, kwa ajili ya uzinduzi wa tamasha hilo. Alisema kuwa, lengo kuu la kuanzishwa tamasha hilo, ni kuhakikisha wazanzibari wanaendelea kukumbushwa, kuelimishwa na kushajiishwa, kuzingatia mila silka, desturi, maadili na mambo mengine yote yanayohusu utamaduni wao. "Katika tamasha hili hapa kisiwani Pemba mchana wa leo, tunatarajia sana, kuwa mgeni rasmi awe Rais wetu wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi, maana...
IMEANDIKWA NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ MAAFISA Utumishi kwenye taasisi za Serikali na binafsi wametakiwa kutokuchelewesha mafaili ya watumishi wanaohitaji stahiki zao za mafao ZSSF, ili kuondosha usumbufu unaojitokeza wakati wa utekelezaji wa kazi hiyo. Akizungumza na maafisa hao katika Ukumbi wa kiwanja cha kufurahishia watoto Tibirinzi Chake Chake Pemba, Mkurugenzi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (ZSSF) Pemba, Msabah Massoud Msabah alisema, kuna haja ya kuwa na Ofisa maalumu ambae atashughulikia mafaili hayo na sio kubadilishwa. Alisema kuwa, kumekuwa na ucheleweshwaji mkubwa wa mafaili ya watumishi ambao wanastahiki kupatiwa mafao yao kwa namna moja ama nyengine, jambo ambalo linaweza kuchukua muda mrefu kupatikana kwa haki, na wakati mwengene wanaweza kuikosesha kabisa, kwani kuna muda maalumu uliopangwa kwa ajili ya kuwasilisha vielelezo. “Tushirikiane pamoja katika hili kuhakikisha wanapatikana watendaji maalumu, ambao hata kwenye mafunzo watakuwa wanakuja hao hao kwa aj...