Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

DK. MWINYI KULIZINDUA TAMASHALA LA UTAMADUNI WA MZANZIBARI PEMBA LEO

    NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi, katika uzinduzi wa tamasha la 31 la utamaduni wa mzanzibari, linalotarajiwa kufanyika leo hii, uwanja wa michezo Gombani Chake chake Pemba. Uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika, kuanzia majira ya saa 8:00 jioni ya leo, na shamara shamara na maandalizi ya tamasha hilo zitaanzaa mapema, uwanjani hapo. Akizungumza na mwandishi wa habari, Kamishna wa Utamaduni Zanzibar Dk. Omar Salum Mohamed alisema, maandalizi yote yameshakamilika, kwa ajili ya uzinduzi wa tamasha hilo. Alisema kuwa, lengo kuu la kuanzishwa tamasha hilo, ni kuhakikisha wazanzibari wanaendelea kukumbushwa, kuelimishwa na kushajiishwa, kuzingatia mila silka, desturi, maadili na mambo mengine yote yanayohusu utamaduni wao. "Katika tamasha hili hapa kisiwani Pemba mchana wa leo, tunatarajia sana, kuwa mgeni rasmi awe Rais wetu wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi, maana...
Recent posts

ZSSF YATAKA MAFAILI YA WATUMISHI WANAOSTAHIKI KUPATA MAFAO YASICHELEWESHWE

  IMEANDIKWA NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ MAAFISA Utumishi kwenye taasisi za Serikali na binafsi wametakiwa kutokuchelewesha mafaili ya watumishi wanaohitaji stahiki zao za mafao ZSSF, ili kuondosha usumbufu unaojitokeza wakati wa utekelezaji wa kazi hiyo. Akizungumza na maafisa hao katika Ukumbi wa kiwanja cha kufurahishia watoto Tibirinzi Chake Chake Pemba, Mkurugenzi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (ZSSF) Pemba, Msabah Massoud Msabah alisema, kuna haja ya kuwa na Ofisa maalumu ambae atashughulikia mafaili hayo na sio kubadilishwa. Alisema kuwa, kumekuwa na ucheleweshwaji mkubwa wa mafaili ya watumishi ambao wanastahiki kupatiwa mafao yao kwa namna moja ama nyengine, jambo ambalo linaweza kuchukua muda mrefu kupatikana kwa haki, na wakati mwengene wanaweza kuikosesha kabisa, kwani kuna muda maalumu uliopangwa kwa ajili ya kuwasilisha vielelezo. “Tushirikiane pamoja katika hili kuhakikisha wanapatikana watendaji maalumu, ambao hata kwenye mafunzo watakuwa wanakuja hao hao kwa aj...

UKWELI WA DK. MWINYI BAADA YA KUINGIA IKULU, SASA WANAFUNZI 1,236 KONDE WATELEZA KWENTE '''TAIZ' WAKIWA GHOROFANI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ KWA sasa wazanzibar wote, wamo katika shamra shamra za miaka sita ya uongozi war ais kipendwa Dk. Hussein Ali Mwinyi, tokea alipowasili Ikulu ya Zanzibara mwaka 2020. Lengo kuu la yeye kuingia Ikulu, ilikuwa ni kumboa mzalendo wa Zanzibar, ili azidi kuwaletea neemaa, baada ya kupokea kijiti za uongozi kutoka kwa mtangulizi wake Dk. Ali Mohamed Shein. Si unajua ndani ya Chama cha Mapinduzi CCM, iko demokrasia iliyokomaa, kwa kuhakikisha viongozi wanapishana, ili kuomba ridhaa kwa wananchi, kila baada ya miaka mitano. Mwenye Dk. Mwinyi tokea awamu yake ya kwanza n ahata hii ya pili, ambapo sasa ameshatimiza miaka sita ya uongozi, alipita kwa wananchiu kuwaomba ridhaa. Nakumbuka vyema, alipokuwa ndani ya Jimbo la Konde, aliwaomba wananchi kwanza kumpa ridhaa, ili azidi kunogesha maendeleo ya kielimu, ikiwemo ujenzi wa skuli za kisasa. ‘’Nawaombeni kura, nikifika Ikulu miongoni mwa ahadi zangu moja wapo ni kuwajengea skuli ya ghorofa hapa Konde, ...

ZANZIBAR YAZINDUA MUONGOZO WA MAWASILIANO KATI YA MZAZI, MTOTO

  Na Mwandishi Wetu, Zanzibar@@@ SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar, kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), imezindua rasmi Muongozo wa Mawasiliano kati ya Mzazi na Mtoto kuhusu Haki ya Afya ya Uzazi (PCC Toolkit), unaolenga kuimarisha malezi, mawasiliano, ulinzi na ustawi wa watoto na vijana. Uzinduzi wa muongozo huo umefanyika jana katika Hoteli ya Verde na kuzinduliwa na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Zawadi Amour Nassor, kwa niaba ya Waziri wa Wizara hiyo, Anna Athanas Paul. Akizungumza katika hafla hiyo, Zawadi alisema wazazi na walezi wanapaswa kuvunja ukimya katika kujadili masuala ya afya ya uzazi na watoto wao kwa kutumia lugha sahihi, yenye heshima na inayozingatia umri wa mtoto. Alisema watoto na vijana wanahitaji kupata taarifa sahihi zinazolingana na umri wao ili kuwasaidia kuelewa mabadiliko wanayopitia, kutambua hatari, kujilinda dhidi ya ukatili na kufanya maamuzi sahihi kuhusu ...

KUELEKEA TAMASHA LA 31 LA UTAMADUNI WA MZANZIBARI MWAKA 2026 PEMBA, RESI ZA NGALAWA KUSHUHUDIWA

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ UTAMADUNI, ni neno la lugha ya kiswahili, ambalo kwa lugha ya kiingereza ni ‘ culture ’, lenyewe likitokana na neneo la kilatini, lenye maana ‘ Cultura’ .   Mitandao ya kijamii, inaripoti kuwa, neneo hilo usuli wake ni neno ‘ colere’,  linalomaanisha "kulima, kustawisha.   Ikifafanua kuwa, neno hili linafafanuliwa kwa namna nyingi, ikiwemo tokea mwaka 1952, na Alfred Kroeber  na  Clyde Kluckhohn ,  walikusanya orodha ya vijelezi 164 vya neno hilo, katika kazi yao.   Miongoni mwa vijelezi hivyo ni ‘ c ulture:a’, critical, Review , ambapo lengo ni kuonesha mzizi wa neno, utamaduni kwa lugha ya Kiswahili, ama ‘ culture’ kwa lugha ya kiingereza. KWANINI MATAIFA YAWE NA UTAMADUNI? Inafahamika katika maandishi mbalimbali, kikiwemo kitabu cha ‘ukombozi wa kiutamaduni’ kuwa, utamaduni ni kielelezo cha uhai wa watu. Kwa mfano Tanzania pekee, imeundwa na mchanganyiko wa zaidi ya makabila 120, yenye mila, lugha ...

MRADI MKAKATI UJENZI WA MATANGI YA KUHIFADHIA MAJI PEMBA, NI NJIA YA KUJIKWAMUA NA KIPATO

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ MAJI ni rasilimali muhimu kwa maisha ya viumbe wote wanaoishi. Kwa mujibu wa mitandao ya kijamii lita trillion 11 hadi 12.5 za maji, hutumika kwa siku duniani kote. Itambulike maendeleo yote duniani, hutegemea upatikanaji huduma muhimu za kijamii, ikiwemo maji safi na salama. Mitandao ya kijamii imeripoti sekta ya kilimo pekee inachukua karibu lita trillion 8.0 za maji kwa siku, ikifuatwa na ya viwanda inayokisiwa kutumia lita trillion 2.3, huku matumizi ya nyumbani yakikisiwa kuchukua lita trillion 1.2 duniani kote. Ndio maana, serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar huchukua juhudi za makusudi, kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji safi na salama, kila siku. Miongoni mwa juhudi hizo ni utekelezaji mradi wa kimkakati, wa ujenzi wa matangi makubwa ya kuhifadhia maji, katika maeneo ya mikoa miwili ya kisiwa cha Pemba. Ofisa Mdhamini Ofisi ya Rais Pemba Shuweikha Abdallah Omar anasema, mbali na kusogeza huduma ya maji kwa wananchi, mradi ...