Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

KUCHELEWA KUHAMIA WAJASIRIAMALI KITUO CHA MICHAKAINI, WALIKOSESHA BARAZA LA MANISPAA MILIONI 100

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ SHILINGI milioni 107,190,000 zilizotarajiwa kukusanywa na Baraza la Manispaa Chake chake Pemba, kuanzia mwezi Novemba, 2023 hadi Januari mwaka huu, hazikupatikana, baada ya wajasiriamali kugoma kukitumia kituo chao cha Michakaini, kwa wakati.   Imebainika kuwa, kituo hicho kipya kilichojengwa kwa ajili yao, kina milango 63 ya maduka, ambapo kila mmoja Baraza lilikusudia kuukodisha kwa shilingi 50,000 ili lijipatie shilingi milioni 3,150,000 kwa kila mwezi mmoja. Ingawa imebainika, baada ya wajasiriamali hao kukataa kuingia kituoni humo, Baraza hilo, kuanzia mwezi Novemba, 2023 hadi Januari mwaka huu, limeshapoteza shilingi milioni 85,050,000. Aidha mapato ya shilingi ya milioni 22,140,000 nayo hayakukusanywa na Baraza hilo kwa kipindi hicho, yaliokuwa yatokane na vizimba ‘ vikuta ’ 82, ambapo kila kimoja, kilitarajiwa kukukodishwa kwa shilingi 10,000 kwa wajasiriamali. Ikafahamika kuwa, vikuta hivyo kama vyengepata wajasiriamali, kw...
Recent posts

THBUB YAFIKA DUNGA KUWAPA ELIMU YA HAKI ZA BINAADAMU WANANCHI

  NA MWASHAMBA JUMA, (THBUB)@@@@ Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, THBUB ofisi ya Zanzibar, imewajengea uelewa mpana wanakijiji wa Dunga Kiembeni kuhusu masuala ya uvunjifu wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora. Akizungumza na wanakijiji hao kwenye mkutano wa pamoja baina ya Tume na wananchi wa Shehia ya Dunga Kiembeni iliopo Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja, Afisa Sheria wa THBUB Bw. Wilfred Msagati aliwahimiza wananchi hao kutambua haki zao na kuzipambania pale zinapovunjwa. Sambamba na kuwaelekeza kufika Tume kwa lengo la kuwasilisha malalamiko yao endapo watakupamba na masuala ya uvunjwaji wa haki na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora. Wilfred aliyasema hayo wakati akiwasilisha mada ya “Majukumu ya THBUB” kwa wanajijiji hao pamoja ya kuwaelimisha haki mbalimbali ambazo binaadamu zinamstahikia na kumuwajibikia huku akiwafahamisha jinsi ya Tanzania ilivyoridhia mikataba ya kimataifa kutekeleza haki za binadamu zikiwemo haki za watoto...

UN-WOMEN YAAHIDI KUENDELEA KUFANYAKAZI NA FAWE-ZANZIBAR

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ SHIRIKA la Umoja wa mataifa la UN-Women, limesema litaendelea kufanyakazi na taasisi ya FAWE Zanzibar, kwa maslahi ya kuwasaidia wajasiriali wa mazao, yanayolimwa baharini na nchi kavu. Hayo yameelezwa jana Febuari 17, 2026 na Mwakilishi wa shirika hilo upande wa Tanzania Emile Kivugo Mwakafundu, alipokuwa akiwasalimia wajasiriamali, wanaoendelea na mafunzo ya mnyonyoro wa thamani, yanayofanyika kituo cha elimu mbadala Wingwi Micheweni Pemba. Alisema UN-Women ni mdau mkuu wa maendeleo ya jamii, wakiwemo wajasiriamali wa uzalishaji muhogo, majongoo bahari, mwani pamoja na wakulima wa migomba, ili kuziongezea thamani biadhaa hizo. Alisema, shirika hilo linawajali wajasiriamali hao, ili kuhakikisha wanaziongezea thamani bidhaa zao kwa lengo la kukuza pato lao. Alieleza kuwa, haiwezekani kwa mkulima, baada ya kuvuna mazao yake, kwenda kuyauza sokoni kama yalivyo, bali ni kuyachakata, ili aongeze pato lake. ‘’UN-Women inaendesha maradi huu ...

UMEWAHI KUHADITHIWA KUHUSU CHAKULA AINA YA MWATA, WANAUME WAPIGANA FOLENI SUPU YAKE

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ “NIWEKEE kisongo pawa 2000, supu weka nyingi na pili pili kwa mbali na kiungwa”, lugha za kuagizia supu ya Mwata. Sio lugha ngeni kwa wafanya biashara na watu wanaouza supu hiyo ya Mwata hususan katika maeneo ya Kangani na vitongoji vyake. Wenyewe hutumia jina la “kisongopawa”kama umaarufu lakini jina halisi ni Mwata, ndilo watu wengi kutoka maeneo mbali mbali hufahamu kwa haraka. Na jina la kisongopawa si rasmi na si lenye kufahamika isipokua kwa wenyeji wa maeneo ya Kangani na jirani ambako   ndio mwata huvuliwa na kuliwa . Mwata ni   aina   ya viumbe vipatikanavyo pwani, ambacho hutumiwa kwa ajili ya chakula au kitoweo kama ilivyo viumbe vingi vya baharini, ingawa umetofautiana navyo kwa kiasi kikubwa hata uvuvi wake. Mwata kisiwani Pemba hupatikana zaidi na kuhesabiwa kama ni kitoweo adhimu katika Pwani ya Jemele iliopo shehia ya Kangani wilaya ya Mkoani mkoa wa kusini Pemba. Ingawa baadhi ya watu hueleza yapo maeneo min...

KUMBE MKAMANDUME ALIKIMBIA VITA IRAN KUJIFICHA PEMBA?

      NA RAHEME MOHAMED, PEMBA   MOHAMMED bin Abrahman umaarufu "Mkamandume"   Ni mshirazi kutoka katika nchi ya Iran, mfalme ambae alifika katika kisiwa cha Pemba mwishoni mwa karne ya 15, yaani miaka 600 iliyopita.   Alifikia mji wa Pujini, kijiji cha Kijito Kame ambapo alikuwa pamoja na mke wake na mtoto wao mmoja.   Mtoto ambae alijulikana kwa jina la Haroun bin Mohammed bin Abrahman, na hadi kufikia sasa jina halisi la mke ambae alifikanae kutoka Iran halijafahamika.   Mfalme Mkamandume, walitoka nchi Iran kwa sababu kulikuwa na vita vya wenyewe kwa wenyewe na kuamua kuingia katika mwambao wa Afrika Mashariki, kutafuta hifadhi.   Walifika hapo pamoja na familia yake kwa kutumia usafiri wa majini na chombo, ambacho walitumia ilikuwa ni jahazi.   Huo ndio usafiri mashuhuri ulioukitumika katika enzi hizo, kwani hakukuwa na mwingine zaidi ya jahazi.   Walifikia katika mji wa Pujini, kijiji cha ...