Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

'NGUVU MOJA' USHIRIKA WA WATU WENYE ULEMAVU PEMBA, WALIA KUFANYIWA UKATILI WA KIUCHUMI

    NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ UMEWAHI kuwaza maisha bila kuona, kusikia, kusema au kusimama. Basi hayo ndio maisha ya kila siku ya watu, wenye ulemavu, aidha wa viungo, uoni, uziwi na aina nyengine. Lakini watu wenye ulemavu ni sawa na watu wengine, wanahaki zote za msingi, kama ilivyo kwa wengine. Miongoni mwa haki hizo ni kushiriki katika shughuli za kiuchumi, kama ilivyoelezwa katika mikataba na sheria mbalimbali. Mkataba wa kimataifa wa haki za watu wenye ulemavu wa 2006, ambao ibara yake ya 27 (f) inasisitiza ushiriki na ushirikishwaji wao kiuchumi. “Nchi wanachama wakuze fursa za watu wenye ulemavu kujiajiri, kuanzisha na kuendesha shughuli za ujasiamali, vyama vya ushirika na mtu binafsi kuanzisha biashara zake”, inaeleza sehemu ya mkataba huo. Sheria ya watu wenye ulemavu ya Zanzibar nambari 8 ya mwaka 2022, kifungu cha 28 (e) inaeleza, watu wenye ulemavu wanastahiki haki zote za msingi za kibinaadamu sawa nawatu wengine ikiwemo kujitegemea na kujumuishw...
Recent posts

USAFI LIFANYWE JUKUMU LA WOTE, MASHEHA WATOA RAI

  NA ZUHURA JABIR, ZNAIBAR “Usafi ni nusu ya afya." Haya sio msemo wa utani, bali ni ukweli unaogusa maisha ya kila siku ya wananchi. Mazingira safi yanamaanisha afya bora, heshima ya makazi na maendeleo ya jamii, lakini pale ambapo mifumo ya usimamizi haieleweki, wananchi hubeba mzigo ambao haukupaswa. Majadiliano yaliyowakutanisha masheha, wahamasishaji wa jamii na wataalamu wa Baraza la Manispaa Mjini, yameonesha wazi kuwa changamoto za usafi wa mazingira bado zinahitaji mshikamano. Methali isemayo, "Kidole kimoja hakivunji chawa," inaakisi hali halisi ya mapambano dhidi ya uchafu wa mazingira. MGONGANO WA MAMLAKA KATIKA UKUSANYAJI WA TAKA Moja ya hoja zilizojitokeza kwa uzito mkubwa ni mgongano wa mamlaka katika ukusanyaji wa taka ndani ya shehia ya Mchangani. Kwa mujibu wa sheha Nassir Mohammed Ali, wananchi wanakabiliwa na hali ya kuchanganyikiwa, kutokana na taasisi mbili, Baraza la Manispaa Mjini na Mamlaka ya Mji Mkongwe, kufanya kazi katika ene...

LUGHA CHAFU ZA WAZAZI KWA WATOTO, ZINAVYOWARUGIA MIFUMO YAO YA MAISHA

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ MALEZI bora na makuzi ya mtoto, ni jambo   muhimu kwa maendeleo yake,kimwili na kiakili. Hili linajumuisha huduma zote muhimu anazostahili kupewa mtoto, kuanzia miaka 0 hadi 8, ili kumuwezesha kukuwa na kufikia utimilifu wake. Ikiwa ni kimwili, kiakili, kijamii, kihisia na kimaadili, ilikushiriki kikamilifu katika ujenzi wa taifa na kuyamudu mazingirayake. Mara nyingi ni rahisi kupata haya yote, kutoka kwa wazazi au walezi,lakini wengi wao husahau kwamba matumizi ya lugha nzuri kwa watoto,inamchango mkubwa katika ustawi wao. Na zipo sheria zinazopinga ukatili wa aina zote dhidi ya watoto, kwamsingi kwamba malezi bora kwa mtoto, ndio msingi imara kwa makuzi yake. Mfano, Mkataba wa kimataifa wa haki za watoto duniani ( Conventionoftherightsofthechildren ) wa mwaka 1989, ambao umeanza kutumikarasmi mwaka 1990. Ibara yake ya 19 inasisitiza, kuwa‘ nchi wanachama kuhakikishawanakuwa na sheria nzuri zitakazo mlinda mtoto juu ya aina zote zau...

TAMU, CHUNGU USAFIRI WA UMMA KWA WATU WENYE ULEMAVU, HADI VIGARI VYAO WALIPISHWA KAMA MZIGO

  NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ UDHALILISHAJI katika vyombo vya usafiri ni pamoja na ukatili wa kijinsia, inayoashiria uvunjifu wa haki za binaadamu. Kwa wenzetu wenye ulemavu, wao wamekuwa nambari moja kudhalilishwa, wakati wanapokwenda ama kurudi kwenye mipango yao ya maisha. Hali hiyo hujumuisha kuguswa mwili bila ridhaa, matusi, kauli za kubaguliwa au kulazimishwa kukaa katika mazingira yanayoshusha heshima na utu wao. Mkurugenzi wa Jumuiya ya watu wenye ulemavu Juma Kombo Hija Pemba anasema, vyombo vya usafiri havipo rafiki kwao.   Anasema ukiangalia Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo zimeridhia mikataba mbalimbali ya kimataifa, inayolenga kuweka mazingira rafiki kwa watu wenye ulemavu, pamoja kusimamia haki zao. Katika kuweka mazingira mazuri ni pamoja kusimamia haki zao na ujumuishwaji katika vyombo vya usafiri, hususana watu wenye ulemavu wa viungo. Anasema yapo matukio matatu yaliyoripotiwa kwa mwezi Juni na Jualai mwaka huu, katika jumuiya hiyo amabapo mt...

NADYA JUMA : KIJANA ANAEANZA POLE POLE KUUSAKA UONGOZI, ALIPOANZIA PATAMU

  NA ZUHURA JABIR, ZANZIBAR@@@@ "Uongozi hauanzi unapopewa cheo; huanza pale unapokuwa tayari kuwahudumia wengine,’’ kauli hii inaelezea kwa ukamilifu safari ya Nadya Juma Idrissa, kijana ambaye ameonyesha kuwa uongozi wa kweli hujengwa kwa kujituma, nidhamu na huduma kwa jamii.   Katika kipindi ambacho vijana wengi bado husita kushiriki katika masuala ya uongozi, Nadya, aliamua kuchukua hatua mapema.   Alianza kama mwanachama wa kawaida wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), lakini leo ni Katibu wa Hamasa wa Tawi la ‘UVCCM’ katika Chuo Kikuu cha Zanzibar (ZU). Safari yake ni ushahidi kwamba mafanikio hayaji kwa bahati, bali hujengwa hatua kwa hatua.   MWANZO WA SAFARI YA UONGOZI Nadya anasimulia kuwa, safari yake ilianza akiwa bado mwanafunzi, alipokuwa akishiriki kwa hiari, katika shughuli mbalimbali za CCM kwenye tawi la eneo analoishi. Hakuwa na cheo wala mamlaka, lakini alijitokeza kila mara, kushiriki shughuli za chama, mikutano na kazi za kujitolea. ...