NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ‘’NILIVUNJIKA mkono, baada ya kuparamia nyumba kumkimbia muume mtarajiwa alipokuja kwetu, ili tusionane,’’anasema Saada Khsmi Kombo (65) wa Micheweni. Hadi leo mkoni wake mmoja wa kushoto, eneo vilipootea vidole hapako sawa, baada ya ajali hiyo. Kwa utamduni ulivyokuwa enza hizo, ilikuwa mwanaume hata kwa ambae alishabisha hodi na kuweka nia ya kufunga ndoa, haikuwa rahisi, kukutana na mtarajiwa wake. Ndio maana Saada anasema, alilazimika kwenda mbio nyingi, kwani hakuwa na hamu ya kukutana na mume wake mtarajiwa, hasa kutokana na malezi yalivyokuwa. KWANINI ILIKUWA HAWAONANI? Rehema Faki Sheha (60), baada ya muume kuweka nia na posa kufuata, hapo mwanamke hukosa hamu hata ya kula, na hakukua na jambo la ushawishi la kukutana nae. Anasema huo ndio utamaduni wa Micheweni, na wao wakiurithi tokea enzi na karne, ingawa hayo anasema ilitokana na mafundisho ya wazazi wao. Walikuwa wakielezwa, kuwa mara baada ya ...
NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ PANGO la kijij, linalopatikana shehia ya Makangale, kaskazini mwa Pemba. Ni mojawapo ya kivutio cha kihistoria vyenye hadithi ya kipekee. Umaarufu wa pango hili, ulianza mwaka 2009 baada ya Profesa Felix Chami wa Chuo Kikuu cha Dar- es Salaam, kugundua mabaki ya kihistoria, ikiwemo mifupa ya wanyama, shanga, mkaa, na vigae vinavyoashiria uwepo wa makazi ya binadamu katika vipindi tofauti vya kihistoria kwenye pango hilo. Kwa mujibu wa historia, pango hili lilitumiwa na wapiganaji wa vita ya kwanza ya dunia 1914 hadi mwaka 1918. Na baadae vita ya pili ya dunia yam waka 1939 hadi mwaka 1945, kama maficho yao na pia sehemu ya kuficha silaha. Leo hii, pango la kijiji Makangale limekuwa kivutio kikubwa cha watalii, wanaotembelea hasa hoteli za kaskazini Pemba, hufika kushuhudia uzuri na historia ya pango hilo, lenye milango miwili wa kuingilia na wa kutokea. Idara ya Makumbusho na Mambo ya Kale Pemba imeboresha njia za kuingia pangoni ...