Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

DK. MWINYI KUINGIA KWENYE HISTORIA UZINDUZI MWENGE WA UHURU PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa, utakaofanyika Aprili 2 mwka huu katika Uwanja wa  michezo Gombani Chake Chake Pemba. Taarifa hiyo imetolewa na Mkuu wa  Mkoa wa Kusini Pemba, Rashid Hadid Rashid, wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya uzinduzi wa mbio za mwenge wa uhuru kwa mwaka 2026 ofisini kwake  Chake Chake Pemba. Alisema kuwa, katika uzinduzi huo Dk. Mwinyi atahutubia wananchi pamoja na kuzindua rasmi mbio za mwenge wa uhuru na kuendelezwa kwa ufunguzi wa miradi mbali mbali ya maendeleo katika wilaya nne kisiwani Pemba. Alisema, mwenge wa uhuru hukimbizwa nchi nzima ikiwa ni sehemu ya kuenzi uhuru wa taifa, kuenzi maendeleo ya nchi sambamba na kudumisha Amani, mshikamano na maelewano ya wananchi katika shughuli mbali mbali za maendeleo ya taifa. "Mwenge wa uhuru mwaka huu 2026 unatarajiwa kuzinduliwa P...
Recent posts

SIKU YA WANAWAKE DUNIANI, KILIO, KIGUGUMIZI KWA WANAWAKE WENYE ULEMAVU NA UONGOZI, KATIJA AELEZEA MAGUMU

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WIKI iliyopita, ilikuwa ni siku ya wanawake duani kote.   Kwao na jamii, siku ya kimataifa, yenye lengo la kuchanbua matamu na mchungu wanayoyapitia katika maisha yao.   Wanawake, ni jamii na jamii ni wanawake, hivyo kila nyanja na ukumbi nao wapo, maana ni binaadamu.   Iwenye kwenye uongozi, uchumi, ajira, siasa, uongozi, utamaduni na udumishaji amani na utulivu.   Hapa ni Kiuyu Wete, mbele yangu namuoba mjasiriamali, kwa aina ya mwendo wake ambao sio wa kawaida, bila shaka ni mtu mwenye ulemavu wa viungo.   Niliharakia, kutaka kumjua ni nani, nilipomkaribia ana nadisha haya…kangaa…kangaaa…na wale wa wapenzi wa madira na vipodozi nipo njooo ujichagulie.   Kauli hizo, zilinifanya nisimame pembeni kidogo, mwa nyumba ya Asha Haji Makame, nae mjasiriamali huyo, aligeuka nyuma ghafla, kwa kule kutafuta wateja na alinifuata.   …..assalama alyekum, baada ya kuitikia mjasiriamali huyo, alimuuliz...

‘ZIC’ YAGAWA CHAKULA MAANDALIZI YA SIKUKUU KWA MAYATIMA, WAFUTARI NAO PAMOJA MTAMBWE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MKUU wa wilaya ya Wete Rashid Abdalla Rashid, amesema jambo la kugawa chakula kwa mayatima, lililofanywa na Shirika la Bima Zanzibar ‘ZIC’ ni la kiutu na linafaa kuigwa na mashirika mingine. Mkuu huyo wa wilaya, aliyasema hayo jana, kwenye kijiji cha kulelea mayatima, Bwagayamoyo Mtambwe Wete, mara baada ya kumaliza hafla ya ugawaji wa chakula kwa ajili ya sikukuu, iliyoandaliwa na ‘ZIC’. Alisema, ‘ZIC’ imefikiria jambo jema kwa watoto hao, kwani wameondokewa na baba zao, hivyo wanapopata mashirika kama hayo, hurejesha matumaini na furaha. Alieleza kuwa, ijapokuwa kuondokewa na jambo kubwa na linalochelewa kusahaualika, lakini ugawaji huo wa chakula hicho, na kwa uhakika, inawapunguzia machungu watoto hao. ‘’Kwanza niwapongeza sana wenzetu wa ‘ZIC’ kwa uamuzi wao, kwanza kuwagawiya futari mayatima tena hawa, waliopo hapa Mtambwe,’’alisema. Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa wilaya ya Wete, aliwataka wazazi na walezi wanaowalea watoto hao m...