Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

NYEZUMA: ‘MRADI WA ‘PAMOJA’ NI WA AINA YAKE KUPAMBANA NA UDHALILISHAJI’

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MTAALAMU wa Masuala la Jinsia, kupitia Mradi wa ‘Pamoja’ wa kukuza usawa wa kijinsia Zanzibar, Nyezuma Simai Issa, amesema Mradi huo, ni wa aina yake, na utapunguza wimbi la ukatili na udhalilishaji, pindi utakapomalizika. Mtaalamu huyo, aliyasema hayo leo Juni 11, 2026 ukumbi wa Samail Gombani Chakechake Pemba, wakati akielezea muhutasiri ya utekelezaji wa mradi huo, kwa Kamati teule ya wilaya ya Chakechake, ya utekelezaji wa mradi huo. Alisema, jambo jipya ambalo limo ndani ya mradi huo, ni ujenzi wa vituo vinane, vya makuzi na malezi ya awali ya mtoto, ambapo kila wilaya kitajengwa kimoja. Alisema, lengo la kituo hicho ni kuwapa nafasi wazazi na walezi, kujiendeleza kiuchumi, wakiwa na uhakika wa malezi kwa watoto wao. ‘’Kupitia mradi huu wa miaka mitano, jambo kubwa ambalo limo pamoja na mingine mazuri, tutajenga vituo vinane, kwa wilaya zote nane, zilizopotiwa na mradi huu,’’alifafanua. Aidha Mtaalamu huyo, alisema jambo jingine ambal...
Recent posts

MSITU WA NGEZI PEMBA NA SAFARI YA UHIFADHI, WATIMIZA MIAKA 67, ILIANZA NA WAKOLONI

  NA ASHA SALIM- WKUMM, PEMBA@@@@ SEKTA ya kilimo Zanzibar, inaendelea kutumia nyezo muhimu na mipango thabiti, katika kunyanyua wakulima waweze kujikimu na kunufaika kupitia shuhuli za kilimo. Katika kuhakikisha hilo, ushirikiano wa karibu kupitia washirika mbalimbali wa maendeleo na miradi inayosainiwa na serikali ya Mapinduzi Zanzibar, kusaidia utekelezaji wa sekta hiyo zinaonekana. Juhudi hizo, zinaendelea kwa ushirikiano wa karibu, kupitia idara zake, zinazotekeleza majukumu yake chini ya wizara hiyo, na sasa serikali kujivunia kufikia mafanikio makubwa ya kiuchumi. Eeneo ambalo, serikali imekuwa na mfano mzuri wa utendaji kazi, ni kushughulikia kwa karibu msitu wa hifadhi ya Ngezi Micheweni. KWANI MSITU WA NGEZI ULIANZIA WAPI Taarifa zilizopo kwenye tovuti ya ‘ Ngezi Vumawimbi Heritage Organization , zinaeleza kuwa, m aeneo yanayozunguka msitu wa Ngezi, kumbe yamekaliwa kwa muda mrefu sana na Waarabu au Waajemi waliowahi kuishi. Infaghamika kuwa, kupitia tovuti...

CFP, CFI, ‘GLOBAL AFFAIRS CANADA WAWATANGAAZIA NEEMA WANAOLIMA KILIMO MSITU

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@   ….kilimo ni maji, na maji ni kilimo… Maji ndio mama wa taifa wa kilimo, bila ya maji hakuna kilimo.   Ni maneno ya mtafiti wa kilimo kutoka Afrika Kusini, Mr. Rugeng Mjinja Zuma, wakati akiwasilisha utafiti wa kilimo mwaka 1999, chuo cha kilimo, nchini humo.   Akasema, kama mataifa yana baba wa taifa, basi kwenye kilimo, baba wa taifa ni maji.   Kelvin John Musetepe wa Burundi mtaalamu wa kilimo cha umwagiliaji, mwaka 2000, alimwambia Waziri wa kilimo nchini humo, kama hakuna maji, basi hakuna kilimo.   Waziri huyo, alikuwa ameshaondolewa kwenye nafasi ya uwaziri wa maji, miezi mitatu iliyopita, jambo lililomkasirisha.   Rais wa awamu ya nane ya Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, wakati akilihutubia Baraza la Wawakilishi, aliiagiza wizara husika, kuhakikisha huduma ya maji, iko vizuri.   ‘’Sasa huduma ya maji sio tu kwa ajili ya matumizi ya ndani, kama kupikia na kunywa, sasa ni kwa ajili ya ku...