NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ SHILINGI milioni 107,190,000 zilizotarajiwa kukusanywa na Baraza la Manispaa Chake chake Pemba, kuanzia mwezi Novemba, 2023 hadi Januari mwaka huu, hazikupatikana, baada ya wajasiriamali kugoma kukitumia kituo chao cha Michakaini, kwa wakati. Imebainika kuwa, kituo hicho kipya kilichojengwa kwa ajili yao, kina milango 63 ya maduka, ambapo kila mmoja Baraza lilikusudia kuukodisha kwa shilingi 50,000 ili lijipatie shilingi milioni 3,150,000 kwa kila mwezi mmoja. Ingawa imebainika, baada ya wajasiriamali hao kukataa kuingia kituoni humo, Baraza hilo, kuanzia mwezi Novemba, 2023 hadi Januari mwaka huu, limeshapoteza shilingi milioni 85,050,000. Aidha mapato ya shilingi ya milioni 22,140,000 nayo hayakukusanywa na Baraza hilo kwa kipindi hicho, yaliokuwa yatokane na vizimba ‘ vikuta ’ 82, ambapo kila kimoja, kilitarajiwa kukukodishwa kwa shilingi 10,000 kwa wajasiriamali. Ikafahamika kuwa, vikuta hivyo kama vyengepata wajasiriamali, kw...
NA MWASHAMBA JUMA, (THBUB)@@@@ Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, THBUB ofisi ya Zanzibar, imewajengea uelewa mpana wanakijiji wa Dunga Kiembeni kuhusu masuala ya uvunjifu wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora. Akizungumza na wanakijiji hao kwenye mkutano wa pamoja baina ya Tume na wananchi wa Shehia ya Dunga Kiembeni iliopo Wilaya ya Kati, Mkoa wa Kusini Unguja, Afisa Sheria wa THBUB Bw. Wilfred Msagati aliwahimiza wananchi hao kutambua haki zao na kuzipambania pale zinapovunjwa. Sambamba na kuwaelekeza kufika Tume kwa lengo la kuwasilisha malalamiko yao endapo watakupamba na masuala ya uvunjwaji wa haki na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora. Wilfred aliyasema hayo wakati akiwasilisha mada ya “Majukumu ya THBUB” kwa wanajijiji hao pamoja ya kuwaelimisha haki mbalimbali ambazo binaadamu zinamstahikia na kumuwajibikia huku akiwafahamisha jinsi ya Tanzania ilivyoridhia mikataba ya kimataifa kutekeleza haki za binadamu zikiwemo haki za watoto...