Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

WANANCHI PEMBA, WAMPA TANO DK. MWINYI KWA HUTUBA YA UJENZI WA AMANI

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI wa mkoa wa kusini Pemba, wameipongeza hutuba ya uzinduzi wa mwenge wa uhuru kitaifa kwa mwaka 2026, iliyotolewa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi. Walisema, hutuba hiyo ilitoa mwelekeo wa umoja, mshikamano, upendo miongoni mwa wananchi wa Tanzania, jambo linalofaa kuungwa mkono. Wakizungumza mara baada ya kumalizika kwa hafla ya uzinduzi wa mwenge huo, jana uwanja wa michezo Gombani, walisema hutuba imewakumbusha watanzania wajibu wao, kwa maslahi mapana ya taifa. Mmoja kati ya wananchi hao Ali Ameir Haji wa Mchangamdogo, alisema hutuba hiyo kama wananchi waliifuatilia kwa makini, basi ni darasa tosha wa ujenzi wa amani. Alieleza kuwa, hutuba nyingi anazozitoa Dk. Mwinyi kwenye hafla kadhaa za kitaifa, huwa na mwelekeo mpana, ingawa hiyo ya kwenye uzinduzi wa mwenge wa uhuru, imeongezeka mara dufu. ‘’Kwa hakika hutuba hiyo, ilijaa kila kitu mfano, imehamasisha upendo, nidhamu, umo...
Recent posts

ANGALIA HAFLA YA UZINDUZI WA MWENGE WA UHURU KITAIFA MKOA WA KUSINI PEMBA MWAKA 2026

 

DK. MWINYI KUZINDUA MWENGE WA UHURU ASUBUHI HII UWANJA WA GOMBANI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, asubuhi ya leo April 2, 2026, anatarajiwa kuwa mgeni, rasmi katika uzinduzi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa, utakaofanyika, uwanja wa michezo Gombani Chake Chake Pemba. Taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa kusini Pemba, Rashid Hadid Rashid, kwa vyombo vya habari, ilieleza kuwa, tayari maandalizi yote yameshakamilika kwa shughuli hiyo ya kitaifa. Taarifa hiyo ilieleza kuwa, Dk. Mwinyi ataingia kwenye kitabu cha kumbukumbu kwa zoezi hilo, ambapo kwa mara ya kwanza, lilifanyika zaidi ya miaka 10 iliyopita kisiwani humo. Mkuu huyo wa mkoa katika taarifa yake, ilifafanua kuwa, Dk. Mwinyi atawahutubia wananchi watakaohudhuria, pamoja na kuzindua rasmi mbio za mwenge wa uhuru kitaifa, kwa mwaka 2026. Alieleza kuwa, wananchi watakaohudhuria kwenye zoezi hilo la kitaifa, kabla ya Dk. Mwinyi kufanya uzinduzi huo, watashuhudia burudani kadhaa uwanjani hapo. Alisema, m...

UNAIFAHAMU KAULIMBIU YA MWENGE WA UHURU WA MWAKA HUU?

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ……..MWENGE wa uhuru ni chombo cha kitaifa. Baada ya taifa la Tanzania kupata huru, kilianzisha chombo hicho, kikiwa na malengo kadhaa ndani yake. Kwa wakati huo, taarifa zinaeleza ni hayati Rais wa kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ndie aliyeuasisi. Kumbe unaweza kuthibitisha kuwa, chimbo la mwenge huo wa uhuru, ni maono ya Baba wa taifa, hasa pale alipousimamisha juu ya mlima Kilimanjaro. Akatamka kuwa, ‘ lengo ni kuleta matumaini pale pasipo na matumaini, upendo pale penye chuki na heshima pale palipojaa dharau’ . Mwenge huo, kwa mara ya kwanza, uliwashwa mwaka 1961, baada ya Mwalimu Nyerere kumteua Luteni Alexander Gwebe Nyirenda kutekeleza azma hiyo iliyoitwa “Operesheni Mwangaza”. Kwa mwaka jana, aliyekua Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Philipi Isdori Mpango, wakati akiwahutubia wananchi wa Mkoa wa Pwani, kwenye uzinduzi, alisema mwenge ni kielelezo cha umoja na mshikamano. Akafafanua kuwa, tangu ...

CFP YAANZA KUMALIZA KIU YA UKOSEFU WA MAJI KWA WAKULIMA KILIMO MSITU PEMBA, FATMA BAKAR AANZA KUUAGA UMASKINI

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@ ….nilianza na shamba moja la ekari moja, na sasa nimeongeza mawaili yenye ukubwa na nusu nusu eka kila moja, ndio maneno ya mkulima kilimo msitu Fatma Bakari wa Chato. Chato hiyo, sio ile ya Mkoani Dodoma Tanzania bara, hapana ipo kijiji cha Gombeume, shehia ya Mchanga mdogo wilaya ya Wete Pemba. Hapo ndio anapoishi mkulima huyo, ambae kwa sasa anajiita mtaalamu wa kilimo msitu, ama kilimo mchanganyiko wa miti ya biashara na chakula. ALIANZAJE KILIMO MSITU Alianza kuwataja Jumuiya ya Uhifadhi yaw a Misutu Pemba ‘CFP’ na Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar, kwamba ndio waliomzua yeye na sasa kuwa mkulima mtaalam wa kilimo msitu. Alijifunza nini maana ya kilimo hicho, kinalimwaje na faida zake za muda mfupi na mrefu, katika maisha ya kila siku. Baada ya mafunzo, huku na muume, akiwa ameshafariki, ndipo mwaka 2024 mwezi wa August, alipoanza kilimo hicho ndani ya shamba la urithi la aliyekuwa muume wake. Hapo akiwa na utaalamu, ...

UZINDUZI MBIO ZA MWENGE WA UHURU KITAIFA 2026, NI ZAMU YA MKOA WA KUSINI PEMBA

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ CHIMBO la mwenge wa Uhuru, ni nia ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, kuweka mwenge juu ya kilele cha mlima Kilimanjaro. Lengo ni kuleta matumaini pale pasipo na matumaini, upendo pale penye chuki na heshima pale palipojaa dharau. Ambapo nia hiyo, aliitoa kwa mara ya kwanza mwaka 1959 huko New York, alipohutubia Baraza la Udhamini la Umoja wa Mataifa. Kwa wakatu huo, alimteua Luteni Alexander Gwebe Nyirenda kutekeleza azma hiyo iliyoitwa “Operesheni Mwangaza”, ambapo yeye na wenzake, walianza maandalizi mwezi Novemba 1961. Kabla ya Tanganyika kupata uhuru, ambapo hatimaye usiku wa mkesha wa sherehe za uhuru tarehe 9 Desemba 1961, Luteni Nyirenda na wenzake, waliwasha na kusimika mwenge wa uhuru na Bendera ya Tanganyika kwenye kilele cha mlima Kilimanjaro. Hiyo ilikuwa kama ishara ya kuwa huru, kwa kupandisha mwenge kileleni ilikuwa kwanza, ni kuonesha kazi ngumu iliyoko mbele ya kulijenga taifa changa la Tanganyika. Pili, ilikuwa ni ku...

DK. MWINYI KUINGIA KWENYE HISTORIA UZINDUZI MWENGE WA UHURU PEMBA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa, utakaofanyika Aprili 2 mwka huu katika Uwanja wa  michezo Gombani Chake Chake Pemba. Taarifa hiyo imetolewa na Mkuu wa  Mkoa wa Kusini Pemba, Rashid Hadid Rashid, wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya uzinduzi wa mbio za mwenge wa uhuru kwa mwaka 2026 ofisini kwake  Chake Chake Pemba. Alisema kuwa, katika uzinduzi huo Dk. Mwinyi atahutubia wananchi pamoja na kuzindua rasmi mbio za mwenge wa uhuru na kuendelezwa kwa ufunguzi wa miradi mbali mbali ya maendeleo katika wilaya nne kisiwani Pemba. Alisema, mwenge wa uhuru hukimbizwa nchi nzima ikiwa ni sehemu ya kuenzi uhuru wa taifa, kuenzi maendeleo ya nchi sambamba na kudumisha Amani, mshikamano na maelewano ya wananchi katika shughuli mbali mbali za maendeleo ya taifa. "Mwenge wa uhuru mwaka huu 2026 unatarajiwa kuzinduliwa P...