Skip to main content

Posts

UWE KARIBU NASI KWA HABARI NA MATUKIO

POSA ZA MICHEWENI ZA ZAMANI, WANAWAKE WAKIKUTANA NA WANAUME SIKU YA ARUSI

         NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ‘’NILIVUNJIKA mkono, baada ya kuparamia nyumba kumkimbia muume mtarajiwa alipokuja kwetu, ili tusionane,’’anasema Saada Khsmi Kombo (65) wa Micheweni. Hadi leo mkoni wake mmoja wa kushoto, eneo vilipootea vidole hapako sawa, baada ya ajali hiyo. Kwa utamduni ulivyokuwa enza hizo, ilikuwa mwanaume hata kwa ambae alishabisha hodi na kuweka nia ya kufunga ndoa, haikuwa rahisi, kukutana na mtarajiwa wake. Ndio maana Saada anasema, alilazimika kwenda mbio nyingi, kwani hakuwa na hamu ya kukutana na mume wake mtarajiwa, hasa kutokana na malezi yalivyokuwa. KWANINI ILIKUWA HAWAONANI? Rehema Faki Sheha (60), baada ya muume kuweka nia na posa kufuata, hapo mwanamke hukosa hamu hata ya kula, na hakukua na jambo la ushawishi la kukutana nae. Anasema huo ndio utamaduni wa Micheweni, na wao wakiurithi tokea enzi na karne, ingawa hayo anasema ilitokana na mafundisho ya wazazi wao. Walikuwa wakielezwa, kuwa mara baada ya ...
Recent posts

HISTORIA PANGO LA KIJIJI MAKANGALE, INASISIMUA, INATISHA

  NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ PANGO la kijij, linalopatikana shehia ya Makangale, kaskazini  mwa Pemba. Ni mojawapo ya kivutio cha kihistoria vyenye hadithi ya kipekee. Umaarufu wa pango hili, ulianza mwaka 2009 baada ya Profesa Felix Chami wa Chuo Kikuu cha Dar- es Salaam, kugundua mabaki ya kihistoria, ikiwemo mifupa ya wanyama, shanga, mkaa, na vigae vinavyoashiria uwepo wa makazi ya binadamu katika vipindi tofauti vya kihistoria kwenye pango hilo. Kwa mujibu wa historia, pango hili lilitumiwa na wapiganaji wa vita ya kwanza ya dunia 1914 hadi mwaka 1918. Na baadae vita ya pili ya dunia yam waka 1939 hadi mwaka 1945, kama maficho yao na pia sehemu ya kuficha silaha. Leo hii, pango la kijiji Makangale limekuwa kivutio kikubwa cha watalii, wanaotembelea hasa hoteli za kaskazini Pemba, hufika kushuhudia uzuri na historia ya pango hilo, lenye milango miwili wa kuingilia na wa kutokea. Idara ya Makumbusho na Mambo ya Kale Pemba imeboresha njia za kuingia pangoni ...

KUTOKA SKULI YA MWANZO JAMBANGOME HADI MSITU, ILIHAMISHIWA UWELENI MIAKA 300 ILIYOPITA

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ KISIWANI Pemba, kuna kijiji kimoja chenye historia ya pekee, kijuilikanacho kwa jina la Jambangome. Kijiji hicho kipo katika maeneo ya karibu na Wambaa, wilaya ya Mkoani, mkoa wa kusini Pemba. Kipo umbali wa kilometa 31 kutoka mji mkuu wa Pemba wa kisasa Chake chake, ambapo ni umbali wa dakika 49   hadi saa moja, kwa usafiri wa gari   ambayo si ya abiria. Jambangome ina historia kubwa na yakuvutia inapoelezwa kwa vizazi vya sasa na wageni wanaoingia na kutaka kuujuwa kiundani mji huo. Kwani inaaminika mji huo, ndio wa kwanza kuhamiwa na kukaliwa na watu katika kisiwa hicho cha Pemba. Historia inatueleza kuwa, Jambangome ilikaliwa na wahindi wa jamii ya Mabohora, ambao asili yao ni “Wagujurati” kutoka India. Walihamia, baada ya kushauriwa na mababu zao kutafuta fursa mpya za kibiashara, katika ukanda wa Afrika mashariki, baada ya kupatwa na njaa kali huko katika jamii zao. Neno hili “Bohora” linatokana na neno la kigujurati le...

MAKABURI YA MAZRUI NA HADITHI INAYOTIA HURUMA PEMBA, MABAKI YAISHI KWA MIAKA 300 SASA

     NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@ MAKABURI ya Mazrui, ni sehemu ya kihistoria inayopatikana   Chwaka, shehia ya Tumbe mashariki wilaya ya Micheweni Kaskazini Pemba. Ni sehemu moja wapo ya kivutio cha kihistoria, hutembelewa na wageni wa ndani na nje ya nchi, ili kulinda urithi na utamaduni unaopatikana humo. Makaburi ya mazrui ni eneo la tatu la sehemu ya kihistoria, katika eneo hilo na lenye mabaki   ya utawala wa Mazrui waliohamia katika karne ya 18. Ni miongoni mwa mabaki yaliyopo hapo ni hayo makaburi yaliyokuwepo sehemu hiyo. Tukisema makaburi ni sehemu maalum ,iliyotengwa kwa ajili ya kuzikwa kiumbe kilichokufa na kuhifadhiwa, kwa safari yake ya milele. MAZRUI KUHAMA KWAO KUINGIA PEMBA Mohamed Yussuf Khamis, ni Afisa Mambo ya Kale anasema   Wamazrui kwa jina jengine wanaitwa (Waarabu), wa kabila la kimazrui, wanatokana na asili ya taifa la Oman. Anasema, walihama kwao na kuja katika upwa wa Afrika Mashariki kwa lengo la kufanya biashara na...

WATUMISHI WAPYA WIZARA YA ELIMU PEMBA WAPEWA NENO

NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ WATUMISHI  wapya wa   wizara ya elimu na mafunzo ya Amali Pemba, wametakiwa kufanya kazi kwa kufuata misingi ya sheria na kanuni za utumishi wa Umma ili kuongeza uwajibikaji katika utendaji wao. Kauli hiyo imetolewa na Mratibu Idara ya uratibu na Utumishi kutoka wizra ya elimu na mafunzo ya Amali Zanzibar Harith Bakari Ali, wakati akifungua mafunzo ya kuthibitishwa kazi kwa waajiriwa wapya yaliofanyika katika ukumbi wa Skuli ya Michakaini Chake chake Pemba. Alisema ufanisi wa kazi hutokana na kufuatwa ipasavyo kwa Sheria, miiko na maadili ya kazi ambayo humtengeneza mtumishi kua muawajibikaji katika utendaji wake wa kila siku ndani na nje ya eneo la kazi. "Sheria,   maadili,   kanuni na miiko ya kazi ndio kichocheo muhimu cha uwajibikaji kwa mtumishi wa Umma, hivyo ni muhimu kuyazingatia yote haya ili kufanya kazi zenu vizuri na si katikamaeneoyakazi tu bali hata nje ya kazi, alieleza. Alisema kua   kipengele chengine muhimu ...

Mkurugenzi TAMWA–Zanzibar Dk. Mzuri Aaga Rasmi, Aweka Alama Kubwa ya Mageuzi ya Kijinsia

  Baada ya zaidi ya miongo miwili ya kujitolea, uongozi na harakati za kutetea haki za wanawake, watoto na uhuru wa vyombo vya habari, Mkurugenzi wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania, Tawi la Zanzibar (TAMWA–ZNZ), Dk. Mzuri Issa Ali ameaga rasmi waandishi wa habari kutokana na kuondoka katika wadhifa wake, akiacha taasisi imara yenye mifumo thabiti na mafanikio yanayotambulika kitaifa na kimataifa. Akizungumza mbele ya waandishi wa habari, viongozi wa serikali, wadau wa maendeleo na wanachama wa TAMWA–ZNZ, Mkurugenzi huyo amesema waandishi wa habari ndio nguzo kuu ya taasisi hiyo licha ya changamoto kubwa wanazokumbana nazo lakini bado waliendelea kushirikiana na Tamwa Zanzibar katika kutumia kalamu zao kuelezea harakati za shughuli za Tamwa Zanzibar. “Kama kuna kundi la watu wanaojua kuuliza maswali magumu, kufuatilia ukweli bila kuchoka, na bado malipo yakawa madogo au hakuna kabisa, basi hao ni waandishi wa habari. Na cha kufurahisha zaidi, hao ndio nguzo kuu ya TAMWA...