NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MKURUGENZI wa Baraza la Mjia Mkoani Muumini Abeid Salum, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi, katika mashindani ya sita ya tahafidhil-quran, ya kanda ya Wambaa wilayani humo asubuhi ya kesho Machi 14, 2026. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Katibu wa Jumuiya ya tahafidhil qur-an kanda ya Wambaa, Mwalimu Abdalla Haji Ali, alisema tayari maandalizi ya shughuli hiyo, yameshakamilika. Alisema, Mkurugenzi huyo, atawashuhudia wanafunzi wakishindana kwa juzuu ya kwanza, pili, tatu, tano, saba, 10 na 20, wakiwemo wanafunzi wa kike na kiume. Alieleza kuwa, mashindani hayo ya aina yake kwa mwaka huu, yanatarajiwa kufanyika msikiti wa Ijumaa Wambaa wilayani humo. Alisema, baada ya majaji kukamilisha kazi yao hiyo na kutoa matokeo, mgeni rasmi huyo atatoa zawadi ikiwemo fedha taslimu, kwa washindi na washiriki wote 45. ‘’Ni kweli asubuhi hii, Mkurugenzi wetu wa Baraza la mji la Mkoani, atayashuhudia mashindani ya sita ya tahafidhi qur-an, yanayoandaliwa ...
KUCHELEWA KUHAMIA KWA WAJASIRIAMALI KITUO CHA MICHAKAINI, MANISPAA CHAKE CHAKE ILIKOSA 'BUNDA' LA MAPATO
NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@ MWENYEWE Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi kwenye hutuba yake ya ufunguzi wa Kituo cha wajasiriamali Chake chake, alielezea kufarajika. Mbele ya umati wa wajasiriamali na wananchi wa mkoa wa kusini Pemba, ameelezea kuwa, sasa atapa usingizi baada ya kumalizika kwa kituo hicho. ‘’Leo nimefarajika kuona sasa kituo hichi kipya na cha kisasa, nakifungua rasmi, sasa wajasiriamali wa mji wa Chake chake, waliokuwa wakihangaika huku na kule wamepata utulivu,’’akasisitiza. Eneo jingine Dk. Mwinyi wakati wa hafla ya uzinduzi wa kituo hicho, mwezi Oktoba 2023, akatoa rai kama sio maagizo kwa Baraza la Manispaa Chake chake. Moja, akaanza kusisitiza kwa watendaji, kuhakikisha usafi unafanyika kwa udhati, ili wananchi watakaofika hapo, wasishuhudie uchafu kuzagaa. Jingine akaelekeza, watendaji wa Manispaa na Halmashauri, kuhakikishe, hakuna hata mjasiriamali mmoja, anaepanga bidhaa zake nje ya soko hilo. ‘’Haiwezekani hata kidogo, kuwa w...