NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ WANAWAKE wanaofanya biashara katika masoko ya Mjini Wete na Kifumbikai Wilaya ya Wete Kaskazini Pemba, wameshauriwa kuripoti vitendo vya ukatili na udhalilishaji kwa viongozi wao wa masoko, ili kuchukua hatua zaidi katika kukabiliana navyo. Ushauri huo umetolewa na Msimamizi wa masoko na mazingira Wilaya ya Wete Sadri Mussa Said, wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake Wete Kaskazini Pemba. Alise katika masoko yote kuna viongozi waliochaguliwa kwa ajili ya kusimamia wafanyabiashara na kuwatatulia changamoto zao mbali mbali za kimazingira na kinidhamu, hivyo ni vizuri kuwatumia ili kupata msaada wa changamoto hizo wanapokua katika shughuli zao za kibiashara. "Masoko yote kuna viongozi waliochaguliwa kwa ajili ya kusimamia wafanyabiashara na kuwatatulia changamoto zao mbali mbali za kimazingira na kinidhamu, hivyo tunawashauri wanawake kuwatumia kuripoti matukio ya udhalilishaji yanapotokezea, ili kupata m...
NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ S ERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ime sema inae ndelea kuchukua hatua mbalimbali za kuimarisha ustawi na ulinzi wa watoto nchini. Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa wizara hiyo Zawadi Amour Nassor, wakati akifungua kongamano la maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika, leo tarehe 16 Juni 2026 katika ukumbi wa ZSSF Tibirinzi Chake chake Pemba. Alisema hatua hizo ni pamoja na kuimarisha mifumo ya ulinzi wa mtoto , kuendeleza kampeni za kupinga ukatili dhidi ya watoto, kuimarisha huduma za afya na lishe, kuhamasisha malezi chanya pamoja na kuendeleza ushiriki wa watoto katika masuala yanayowahusu. " Serikali inae ndelea kuchukua hatua mbali m bali za kuimarisha ustawi na ulinzi wa watoto , ikiwa ni pamoja na kuimarisha mifumo ya ulinzi wa mtoto , kuendeleza kampeni za kupinga ukatili dhidi ya watoto, kuimarisha huduma za afya na kuhamasisha malezi chanya " alisema. A...