Skip to main content

Posts

Showing posts from February 18, 2024

SHUNGI: 'WATAKA KUJENGEWA BARABARA YAO KWA KIWANGO CHA LAMI'

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI wa shehia ya Shungi wilaya ya Chake chake Pemba, wameikumbusha serikali, kuwajengea barabara yao ya Chanjamjawiri- Tundaua kwa kiwango cha lami, ili wapate kuitumia kwa utulivu. Walisema, kwa sasa imesambaa mashimo na msingi yenye kina kirefu, jambo ambalo haliwapi utulivu, wakati wanapokwenda kwenye shughuli zao za kimaisha. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi shehiani hapo, walisema barabara hiyo ambayo awali ilikuwa na lami, kwa sasa zaidi ya miaka minne imekuwa ikihataraisha waenda kwa miguu, achia mbali wanaotumia vyombo vya moto. Mmoja kati ya wananchi hao Moza Suleiman Mohamed wa Misooni alisema, hasa wao akinamama wamekuwa wakipata usumbufu mara pale wanapokuwa wajawazito. ‘’Hutokezea sisi kutakiwa kuripoti hospitali ya Chake chake kwa huduma na uchunguuzi zaidi, lakini tunapoitumia barabara kutokana na mashimo yaliomo, hupata mtikisiko,’’alieleza. Nae Asma Said Abdalla wa Chanjamjawiri, alisema barabara hiyo ndio wanayoitum

JAJI IBRAHIM ATUPILIA MBALI RUFAA KESI DAWA ZA KULEVYA

  NA MARYAM NASSOR, PEMBA @@@@        HUKUMU ya rufaa ya dawa za kulevya inayohusisha kete 1,678 iliyowasilishwa mahakama kuu Zanzibar, kanda ya Pemba, imekataliwa na Jaji wa mahakama hiyo, Ibrahim Mzee Ibrahim, baada ya kubaini kuwa, upande wa mashtaka tokea awali, ulithibitisha kosa pasi na shaka yoyote. Jaji Ibrahim akitoa uamuzi wa rufaa hiyo na baada ya kujiridhisha, aliamuru mshtakiwa huyo Zubeir Jerad Said wa Bopwe Pemba, kutumikia chuoa cha mafunzo, kwa muda wa miaka 10, kama alivyohukumiwa awali mahakama ya mkoa.   Alisema kuwa, mahakama yake imeitupilia mbali rufaa hiyo, kutokana na kuwa upande wa mashtaka, ulikuwa na mashahidi ambao walitoa ushahidi wa wazi na wakuaminika, hivyo hawezi kuipindua hukumu hiyo.   Jaji huyo alisema kuwa, mshtakiwa alikamatwa na na dawa hizo na kupewa jina la kielelezo ‘pw3 na pw4’, ambacho ni mfuko wa dawa za kulevya aina ya heroin kete uliokuwa na 1, 678   zenye uzito wa   gramu 41.53.   Alieleza kuwa, wakili wa utetezi Abeid Mohamed