Skip to main content

Posts

Showing posts from February 23, 2025

MARYAM THANI: MWAKILISHI ALIEPANIA KUMALIZA CHANGAMOTO KATIKA JIMBO LAKE, Anasema, ataendelea kugombea uongozi kuhakikisha jimbo lake linapata maendeleo zaidi

  NA ZUHURA JUMA, P EMBA@@@@ KATIKA jamii inayokuwa kwa kasi, uongozi wa wanawake umekuwa muhimu zaidi kuliko wakati mwengine wowote. Leo tunazungumza na mwakilishi wa Jimbo la Gando wilaya ya Wete kupitia chama cha Mapinduzi CCM, Maryam Thani Juma ambae aliepania kuleta mabadiliko ya kimaendeleo katika jamii. Mwanamama huyo amefanya mambo mengi katika vipindi viwili vya uongozi wake tangu mwaka 2015 hadi sasa ambapo wananchi wa jimbo lake wanannufaika nayo. Maryam ni mwanamke jasiri alieweza kuvuka vikwanzo vingi na hatimae kufanikiwa kuingia kwenye chombo cha maamuzi baada ya kuchaguliwa na wananchi kwa kishindo. Baada ya kuwafikishia wananchi wake maendeleo, ilipofika mwaka 2020 alipoingia tena kwenye kinyang’anyiro cha kugombea, alifanikiwa pia. HARAKATI ZAKE UONGOZI ZILIANZIA WAPI? Mwakilishi huyo alianza uongozi kwenye chama akiwa kama Katibu wa Uchumi na Fedha katika tawi la Kizimbani Wete Pemba, baadae akawa Mjumbe wa Kamati Tekelezaji ya Vijana Wilaya ya Wete kwa wakati hu...

EMPOWERING COMMUNITIES: CFP TRAINS MANGROVE CONSERVATION COMMITTEES IN GOVERNANCE AND LEADERSHIP

  BY KHELEF NASSOR, ZANZIBAR@@@ In a significant step towards bolstering local conservation efforts, Community Forests Pemba (CFP), through the ZanzADAPT project, conducted a vital training session for Mangrove Conservation Committee members from Uzi and Unguja Ukuu. The session, facilitated by John Ngonyani, CFP’s COFMA Officer, focused on governance, leadership, and legal frameworks surrounding mangrove conservation. As climate change increasingly threatens coastal ecosystems, empowering local communities with the right knowledge and tools is crucial for ensuring the sustainable management and protection of mangrove forests. Speaking during the training, John Ngonyani emphasized the importance of community-driven conservation initiatives. “Mangrove forests are more than just trees; they are life-supporting ecosystems that protect our coastlines, provide breeding grounds for marine species, and sustain livelihoods. By equipping you with the right skills and knowledge, we are ens...

WAGOMBEA WANAWAKE WATAJA ATHARI ZINAZOWEZA KUWAKUMBA IWAPO WATADHALILISHWA

NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ KILA kukicha Seirikali, taasisi binafsi na jamii zinapaza sauti zao ili kuhakikisha wanaondoa vitendo vya udhalilishaji ambavyo kwa asilimia kubwa hufanyiwa wanawake na watoto. Suala la kukemea vitendo vya udhalilishaji sasa limejaa kwenye mioyo ya watu kwa sababu halipewi nafasi katika jamii zetu, licha ya wachache wanaolifanya na kutia aibu Taifa letu. Tayari wanajamii waliowengi wameshapatiwa elimu na wanajua athari zinazojitokeza iwapo mwananchi atafanyiwa vitendo vya udhalilishaji na ndio maana wapo tayari kuyazungumzia na kuyakemea kwa nguvu zote. Wanawake wanaogombea ni miongoni mwa wanakumbwa na changamoto za udhalilishaji ambazo hupelekea kuwaathiri kisaikolojia, kimwili, kijamii, kisiasa na kiuchumi. Mwandishi wa makala haya alitaka kujua ni athari gani zinazowakumba wanawake wanaogombea nafasi za uongozi iwapo watadhalilishwa. Ibrahim Mustafa Mussa ambae ni Mjumbe wa Kamati ya Siasa wilaya ya Wete kupitia chama cha Mapinduzi CCM anasema, udhalilisha...

UDHALILISHAJI KWENYE VYAMA UNAVYOWEZA KUKATISHA NDOTO ZA WAGOMBEA WANAWAKE, 'Wanasema: kama una moyo mwepesi hutoboi

  IMEANDIKWA NA  ZUHURA JUMA, PEMBA HAKIKA… hakuna safari ya mafanikio iliyokosa vikwazo na misukosuko ndani yake. Lakini kama mwanadamu hatakiwi kuvunjika moyo ama kukata tamaa kwa kile kinachoitwa kukumbana na vikwazo katika safari yake ya kutafuta mafanikio. Na ndio maana tumeumbwa na tabia ya kujaribu kila upande, ili tu kuhakikisha unafanikiwa katika maisha yako. Ili ufanikiwe katika maisha yako lazima uwe tayari kupambana na kuvishinda vikwazo vyote vinavyokupitia mbele yako. Kwani hakuna mafanikio ya njia rahisi na ndio maana wahenga walisema… ‘jitihada wajada’ wakimaanisha ukijitahidi utafanikiwa. UDHALILISHAJI UNAOWAKUMBA WAGOMBEA WANAWAKE Saada Saleh Ali mkaazi wa Chwale ni miongoni mwa wanawake wapambanaji katika kuusaka uongozi bila kujali vikwazo anavyokutana navyo katika kila hatua anayopitia. Hiyo imemfanya kuwa jasiri na kujiamini huku akifanikiwa kujinyakulia nafasi mbali mbali ndani ya chama chake. Saada ambae ni Mwenyekiti wa Vijana Wilaya ya Wete kupitia ch...

MWAKILISHI CHWAKA AKABIDHI VIFAA VYA KIELIMU

  Mwakilishi wa Jimbo la Chwaka Issa Haji Ussi, amesema ataendelea kutoa misaada mbali mbali ya  vifaa vya kielimu katika Jimbo hilo. Kauli hiyo ameitowa huko Ndijani wakati akikabidhi vifaa mbali mbali vya kielimu. Alisema vifaa hivyo vimekuja wakati muafaka ambapo vitatumika zaidi msimu huu wa mwezi mtukufu wa Ramadhani unao tarajiwa hivi karibuni. Alieleza viongozi wa Jimbo Hilo wako pamoja na wanchi katika kuwafikishia kile wanacho kitaka katika sehemu zao. Aidha mwakilishi huyo alisema wako tayari kusaidia katika Kila sekta ambayo imekuwa na changa moto ya miundo mbinu husika. Vifaa hivyo vilivyo tolewa  vimegharimu zaidi ya shilingi miloni Hamsini huku ahadi ikitolewa kwa imamu atakae swalisha tarawehe atalipwa elfu Hamsini Mmoja wanafunzi Haisam Juma kwa niaba ya wanafunzi wenzake alieleza msaada huo wameupokea kwa mikono miwili na watautumia kama wali vyo jipangia.                             ...