Skip to main content

Posts

Showing posts from April 13, 2025

NAOMBA: MKULIMA ALIYEJIKITA NA KILIMO MSITU, AELEZEA KILICHOMVUTIA

HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@ NI majira ya saa 4:00 asubuhi, nilipofika katika bonde la Kigawani kijiji cha Chwale Wilaya ya Wete Pemba, nikitokea Mkoani.  Katika safari  hiyo niliyochukuwa muda usiopunguwa saa 1:30 kwa usafiri wa umma, nikiwa na lengo la kutaka kujuwa changamoto na maendeleo ya kilimo msitu ambacho kinalimwa shehiani humo.   Ilikuwa ni safari yenye kheri kubwa, kwani kukutana na wakulima  wa kilimo msitu, ambao wameamuwa kujikita na kilimo hicho wakiwa na malengo ya kujikwamua kimaisha. Pamoja na wakulima wengine kuzungumza nao  nilipata hamu na shauku kubwa ya kuzungumza na mkulima Naomba Shaaban Mbarouk, baada ya kumsikia kuwa alikotokea  hakuwa na hamu ya kujiingiza katika kilimo hicho.    Wala sikufanya ajizi nilimvuta pembeni, chini ya muembe huku upepo ukitupepea taratibu akiielezea makala haya, kinaga ubaga kuhusu kilimo hicho kilichomvutia hadi kujiingiza.   Alijiingiza katika kilimo hicho, baada ya kupata mafun...

KAIMU MKURUGENZI "ZSSF" ATOA NENO KWA WAAJIRI

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ K AIMU  Mkurugenzi Mwendeshaji Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Pemba Msabah Masoud Msabah, aliwataka waajiri kufuata sheria zilizowekwa na Mfuko huo ili kuhakikisha upatikanaji wa haki za msingi za wanachama wao. Aliyasema hayo April 16 2025, wakati akizungumza na wadau wanaohusika na uandaaji wa malipo ya michango katika mfuko huo kutoka taasisi binafsi, huko Tibinzi Chake Chake Pemba. Alisema iwapo waajiri watafuata sheria zilizowekwa na mfuko huo, itasaidia kupata haki zao zote za msingi ndani ya mda husika, jambo ambalo ni kipaombele cha mfuko huo. Alisema kwa sasa mfuko umeanzisha mfumo maalumu, utakaomuwezesha mwanachama kuweka pamoja na kupata taarifa zake zote za mwenendo wa uchangiaji wake, hivyo ni vyema kwa waajiri kutumia mfumo huo ili kurahisisha upatikanaji wa taarifa. "Mfuko wa hifadhi ya Jamii (ZSSF) umeandaa mfumo  maalumu utakaomuwezesha mwanachama kupata taarifa zake kwa urahisi ( employers potlal), basi ni vyema kwa waajiri kutum...

WANANCHI MJANANZA WATAKA OFISI YA ‘ZLSC’ IHAMIE KWAO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI wa shehia ya Wingwi Mjananza wilaya ya Wete Pemba, wamekishauri Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ kuhamishia ofisi kwenye shehia yao, ili kila wanapokuwa na changamoto zao za kisheria wawe karibu nao. Walisema, huduma walizopewa za ushauri wa kisheria bila ya malipo, zimewavutia na kuona ipo haja kwa sasa, kwa kituo hicho kujenga ofisi shehiani mwao. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi leo April 18, 2025  mara baada ya kufungwa kwa kambi ya siku tatu ya utoaji elimu, ushauri na msaada wa kisheria, walisema wanatamani ZLSC ijenga ofisini eneo la Mjananza. Walisema kuwa, wengi wao walikuwa hawana uwelewa wa utaratibu wa kufuatilia nyaraka kama za vyeti vya ndoa, talaka, vyeti vya kuzaliwa, vitambulisho jambao ambalo wamelipata ndani ya kambi hiyo. Mwananchi Salim Hamad Faki, alishauri kuwa, ni vyema kwa ZLSC ikawa na ofisini ngazi ya shehia, ili kupunguzia dhiki za wananchi kuwafuata mjini wanasheria, wanapokuwa na changamoto za...

‘ZLSC’ CHAPIGA HODI YA KISHERIA WINGWI MJANAZA

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ KITUO cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ sasa kimeelekeza nguvu yake kwa wananchi wa shehia ya Wingwi Mjananza wilaya ya Wete Pemba, kwa kambi ya siku tatu, ya kutoa elimu, ushauri na msaada wa sheria bila ya malipo. Kambi hiyo, ipo ndani ya skuli ya Msingi ya Mjananza, ambayo ilianza jana April, 16, na ikitarajiwa kumalizika kesho majira ya saa 8:15 jioni. Akizungumza na wananchi hao, juu ya utaratibu wa utoaji wa msaada huo, leo April 17, 2025  skulini hapo, Afisa Miradi wa ‘ZLSC’ Beny Louis Mlingi, alisema kwanza, mwananchi atapaswa asajiliwe, kwenye fomu maalum kambini hapo. Alieleza kuwa, baada ya hapo atakutana na wanasheria nguli pamoja na mawakili na Vakili , wanaofanyakazi Kituo cha Huduma za Sheria, kwa ajili ya kusikilizwa lalamiko lake. Alifahamisha kuwa, katika kambi hiyo, inawakaribisha wananchi wenye changamoto za kisheria, kama vile migogoro ya mipaka, ardhi, matunzo kwa watoto, waliokosa vyeti vya ndoa, vya kuzaliwa. Eneo j...

‘ZLSC’ CHAWAFIKIA WANANCHI 112, KWA MSAADA WA KISHERIA UWANDANI

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANANCHI 112, wakiwemo wanawake 80 na wanaume 32 wa shehia ya Uwandani wilaya ya Chake chake, wamejitokeza na kupewa elimu, ushauri na msaada wa kisheria, uliotolewa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ katika kambi ya siku tatu. Akizungumza na blog ya pemba today juzi, Afisa Miradi wa ‘ZLSC’ Beny Louis Mlingi, alisema wengi wao ni wale waliolalamikia ukosefu wa vyeti vya kuzaliwa, vyeti vya ndoa, vitambulisho vya ukaazi pamoja na migogoro ya ardhi. Alieleza kuwa, kwa sasa wamepanga kulifuatilia hilo, ili kuona wanawasaidia wananchi hao, ili kupata nyaraka hizo muhimu kwa ajili ya shughuli nyingine. ‘’Ni kweli hapa Uwandani wananchi wameitikia wito wa kufika kwenye kambi yetu ya siku tatu, na tumegundua shida zipo za wananchi kulalamikia ukosefu wa nyaraka muhimu,’’alifafanua. Mapema Mwenyekiti wa Kituo hicho Pfrofesa: Chriss Maina Peter, alisema wanakusudia kukutana na watendaji wakuu wa serikali, ili kuona wananchi hoa wasiokuwa na uwez...

WADAU UANDAAJI MALIPO 'ZSSF' PEMBA TUMIENI MIFUMO KURAHISISHA TAARIFA

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ AFISA Mdhamini Wizara ya Fedha na Mipango Pemba, Abdulwahab Said Abuu-bakar aliwataka wadau wanaohusika na uandaaji wa malipo ya michango katika mifumo ya Mfuko wa hifadhi ya jamii (ZSSF) kutumia mifumo hiyo kwa usahihi ili kurahisisha upatikanaji wa taarifa kwa wanachama wake. Aliyasema hayo April 15, 2025 katika mkutano wa kuwajengea uwezo wadau hao uliofanyika katika ukumbi wa (ZSSF) Tibirinzi Chake Chake Pemba. Alisema kumekua na malalamiko ya ucheleweshwaji wa upatikanaji wa mafao ya ustaafu kutoka kwa wanachama, yanayosababishwa na taasisi kushindwa kuweka kumbukumbu vizuri, katika mifumo hiyo. Hivyo alisema ni vyema kwakila taasisi kuhakikisha inatimiza majukumu yake vizuri ili kupunguza malalamiko hayo kwa wastaafu wa serikali na taasisi binafsi. "Ni vyema  taasisi zihakikishe  zinatimiza majukumu yake vizuri ili kupunguza malalamiko kutoka kwa wastaafu wa serikali na taasisi binafsi" alisema. Alieleza kua  serikali imeandaa utara...