Skip to main content

Posts

Showing posts from October 8, 2023

WAZIRI ZANZIBAR AKEMEA MILA ZINAZOKIUKA HAKI ZA BINAADAMU

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Zanzibar Riziki Pembe Juma amesema hakuna sababu ya kuendelea na ukiukwaji wa haki za binadamu na ukatili dhidi ya wanawake na wasichana kutokana na mila zenye madhara.   Kauli hiyo ameitowa jana wakati wa   kufunga mkutano wa kimataifa wa ukeketaji, uliofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, Dar es salaam, amesema hakuna sababu kuendelea na ukiukwaji wa haki za binadamu na ukatili dhidi ya wanawake na wasichana kutokana na mila zenye madhara katika makundi hayo.   Aidha amesema mapendekezo yaliyotolewa katika mkutano huo yakitekelezwa vizuri yataokoa na kuwalinda wanawake na wasichana dhidi ya vitendo hivyo   viovu katika mataifa mbali mbali.   Waziri huyo ametaja baadhi ya mapendekezo yaliyopendekezwa katika mkutano huo ikiwemo ushirikishwaji wa jinsia zote pamoja kuwajengea uwezo wavulana na wasichana kukataa ukeketaji, Tume ya Umoja wa Afrika kuratibu mikutano mikuu pamoja na Mawaziri wa Nchi W

WAANDISHI WA HABARI, WASAIDIZI WA SHERIA, WATETEZI HAKI ZA BINAADAMU WAAHIDI KUIFIKIA JAMII PEMBA

  ASHA ABDALLA NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WAANDISHI wa habari, wasaidizi wa sheria na watetezi wingine wa haki za binadamu kisiwani Pemba, wamesema baada ya kumalizika kwa mafunzo ya siku nne, sasa wako tayari kuisaidia jamii, namna bora ya kuzilinda haki za binaadamu. Walisema kazi iliyofanywa na Mwemvuli wa asasi za kirais Pemba ‘PACSO’ kwa kushirikiana kwa na Shirika la kimaendeleo ulimwengini ‘UNDP’ ni jambo jema na lililobakia ni wao kuwafikia wananachi. Wakizungumza mara baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo, yaliyofanyika ukumbi wa Chuo cha Amali Vitongoji Chake chake, walisema wamepata elimu ya kutosha kwa ajili ya kuifikisha kwa jamii. Watetezi hao wa haki za binaadamu walisema, PACSO na UNDP wameshatimiza wajibu wao kwa kuwapa mafunzo hayo, sasa kilichobakia kwao wao, ni kuhakikisha wanakutana na makundi kadhaa ndani ya vijiji mbali mbali. Mmoja kati ya washiriki hao Mwalimu Mwache Juma Abdalla, alisema kazi iliyoko mbele yao ni kukutana na makundi kama vile wanafunzi

WAZIR PEMBE ATAKA UZINGATIAJI AFYA YA AKILI

  Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Riziki Pembe Juma amewataka wananchi kuzingatia umuhimu wa Afya ya akili ili kuzuia maafa ambayo yanayoweza kutokea na kupelekea athari kubwa kwa katika mwili wa binadamu. Akizungumza katika   bonanza la kuadhimisha kuelekea siku ya afya ya akili na maafa duniani lilofanyika katika jengo la Chuo cha Afya Zanzibar Wilaya ya Magharib “B” Unguja, amesema   kila mwananchi anapaswa kutambua umuhimu wa afya ya akili kama ilivyo afya ya mwili ili kujikinga na maafaa ambayo yanawezakujitokeza. Amesema afya ya akili ni muhimu kwa kila mtu kwani inamuwezesha kuishi maisha yenye furaha, tija na kujisikia vizuri ulimwenguni. Lakini mara nyingi suala hili halipewi kipaumbele kinachostahili.   Hivyo Waziri huyo   amehimiza suala la afya ya akili kupewa kipaumbele na kila mtu, kutambua kwamba   ni sehemu muhimu ya afya kwa ujumla. “Afya ya Akili ni muhimu kwa kila mmoja wetu, kwani maafa hayachagui   mtu wa kumuathiri, yanaweza kumu

DK. MZURI AONESHA UMUHIMU WA SHERIA BORA ZA HABARI

  Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Tanzania (TAMWA ZNZ) Dkt. Mzuri Issa amesema ni muhimu kuwa na sheria bora za habari ambazo zinapelekea kuwepo kwa uhuru wa habari na uhuru wa kujieleza kwa jamii. Amesema hayo wakati wa mkutano wa kutoa mapendekezo ya marekebisho ya sheria ya tume ya utangazaji ya Zanzibar (No. 7, 1997), ambao uliwashirikisha kamati ya masuala ya habari (ZAMECO), Asasi za kiraia na Tume ya kurekebisha ya Sheria uliofanyika   Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Mazizini. Dkt.  Mzuri aliongeza  kuwa ipo haja ya kufanyiwa marekesbiso sheria hiyo ili kutoa fursa ya uhuru wa kujieleza ambao ndio chanzo kikuu cha maendeleo ya nchi. “ Uhuru wa habari na haki ya kupata habari pamoja na uhuru wa kujieleza ni mambo ya msingi katika maendeleo ya nchi na inaleta   furaha ya mtu binafsi”, amesisitiza Dkt. Mzuri Issa. Kwa upande wake,  Mwenyekiti wa tume ya kurekebisha sheria Zanzibar, Ndugu  Khadija Shamte amesema kuwa muda umefika sasa kuwa na sheria zinazokwen

JAMII YAKUMBUSHWA KUILINDA HAKI KUU YA BINAADAMU

  NA ASHA ABDALLA, PEMBA@@@@ JAMII imekumbushwa kuwa, moja ya haki kuu ya msingi kwa kila mwanadamu ni ile ya kuishi, hivyo ni kosa kwa mtu mwengine yeyote kumuondolea mwenzake . Hayo yalielezwa na mtoa mada mwanasheria kutoka Shirika la Msaada na Haki za Binaadamu Siti Habib Mohamed, wakati akiendesha mafunzo ya siku nne kwa waandishi wa habari, wadau wa habari na wasaidizi wa sheria, yanayofanyika Chuo cha Amali Vitongoji Chake chake na kuandaliwa na Mwemvuli wa asasi za Kirai Pemba PACSO kwa ufadhili wa UNDP. Alisema kua zana ya haki za binadamu ilianzishwa mnamo  mwaka 1948 baada ya vita vya kwanza vya dunia, hivyo ni wajibu wa kila mmoja hadi leo hii, kuhakikisha anailinda na kuitetea haki ya kuishi ya mwanzake. Alieleza kuwa, haki za binadamu kimsingi ni yale madai au haki zote ambazo anadai binamu mara baada ya kuzaliwa, na kwa kawida hakuna taasisi yoyote ambayo inaweza kuzuia. ‘’Ni kweli haki ya msingi kwa kila mwanadamu ni ile ya kuishi, hivyo ni wajibu wa kila mmoj

TAMWA-ZANZIBAR YATOA RAI WAKATI WA UANDAAJI SERA, SHERIA

  NA NAFDA HINDI, ZANZIBAR Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa habari wanawake Tanzania Zanzibar Dk. Mzuri Issa  Ali ameishauri Serikali pamoja na Taasisi binafsi kuandaa Sera na Sheria za nchi kwa kuzingatia usawa na jinsia zote ili kuwepo usawa wakati wa teuzi mbali mbali zinazofanywa. Akizinduwa waraka maalumu naoainisha changamoto zinazowakumba wanawake na watu wenye ulemavu katika kugombea nafasi za Uongozi hafla iliyofanyika Ofisi za ukumbi wa bima Mperani mjini Unguja. Dk.Mzuri amesema kwa miaka mingi wanawake na watu wenye ulemavu wamekosa nafasi muhimu katika ngazi za maamuzi jambo ambalo linawanyima haki yao ya msingi ya kidemokrasia ya kutoa mawazo yao na uhuru wa kujieleza. “Elimu ndio ngazi kubwa ya kuwapeleka wanawake katika Uongozi kwa miaka mingi iliyopita walinyimwa fursa ya elimu na baadhi ya wazee ama walezi kutishwa na kuwa na dhana potofu ya kuharibiwa watoto wao katika masuala ya udhalilishaji na kwa bahati mbaya fursa hizo kupata wanaume pekee,”   alisem