Skip to main content

Posts

Showing posts from September 24, 2023

RAIS MAHKAMA YA AFRIKA AWAPA NENO WANAOWAKINZA WAANDISHI

  NA HAJI NASSOR, ARUSHA RAIS wa Mahkama ya Afrika ya haki za binaadamu na haki za watu Imani Daud Aboud, amesema kama waandishi wa habari wanafanyakazi zao chini ya vitisho kutoka kwa mamlaka kunahatarisha kudhoofisha uhuru wao na ule wa kujieleza na kutoa maoni. Rais huyo aliyasema hayo jana ukumbi wa mahakama hiyo mkoani Arusha alipokuwa akifungua mkutano wa kikanda kwa waandishi wa habari juu ya ulinzi na usalama wao uliondaliwa na Baraza la habari Tanzania MCT. Alisema vipo vyombo au mamlaka vimekuwa vikiingilia na kuwatisha waandishi wa habari wanpokuwa kazini jambo ambalo halisidii kuimarisha uhuru wa kujieleza na ule wa habari. Alieleza kuwa,  haki ya kupata na kusambaaza habari ni haki ya kikatiba hivyo ni kosa kwa mamlaka nyingine kuviingilia vyombo vya habari pasi na dai la haki. 'Waandishi wa habari ni sauti ya wsiokuwa na sauti na ni sauti kwa waliokata tamaa hivyo ni jukwaa muhimu na linapaswa lilindwe na sio kushambuliwa,'alieleza. Katika hatua nyingine rais huyo

KAMANDA MCHOMVU AWAPA NENO WAZAZI

  KAMANDA   wa polisi Mkoa wa Mjini Magharibi kamishina Msaidizi wa P olisi Richard (ACP), Thadei Mchomvu, amewataka wazazi na walezi   kushirikiana kwa pamoja katika kuwalea na kuwatunza watoto wao kwa ajili ya kuwalinda    na vitendo vya ukatili na udhalilishaji. Akizungumza na mwandishi wa gazeti hili ofisini kwake Muembe Madema M jini Zanzibar, amesema baadhi ya wazazi   hushughulikia   shughuli zao zaidi na hawana utamaduni wa   kuwa   karibu na watoto wao jambo ambalo hupelekea kuendelea vitendo hivyo. "Wapo wazazi wakitoka asub u h i ndo wametoka kurudi kwao ni usiku watoto wakiwa wamelala, mtindo ambao unachangia watoto kukosa elimu ya kujitambua   iliyo muhimu katika kuwasaidia kuepuka kufanyiwa vitendo viovu vya kudhalilishwa," a lisema Richard " Na baadhi ya kina mama wanawacha watoto kudhurura ovyo bila ya kuwavisha nguo kamili na kupelekea mtoto kufanyiwa vitendo vya ukatili na udhalilishaji." Aliongezea Richard Aidha alisema kuna faida mbalimb

WANACHAMA WAMCHAGUA TENA MLAY KUWA RAIS MCT

    NA HAJI NASSOR, ARUSHA@@@@ WANACHAMA wa Baraza la Habari Tanzania MCT, wamemrejesha tena Rais wa Baraza hilo, Jaji Mstaafu: Juxon Isaac Mlay kwa miaka mengine mitatu ijayo, kupitia mkutano mkuu wa 25, uliofanyika Septemba 28, 2023 mkoani Arusha. Mkutano huo, pia umemchagua Yussauf Khamis Yussuf kuwa Makamu wa rais   na wingine waliochaguliwa katika mkutano huo ni wawakilishi wa vyombo vya habari, akiwemo Tido Mhando. Wawakilishi wingine ni Rose Rouben, Ali Haji Mwadini samba mba na kupatikana kwa wawakilishi watatu, kundi la umma wakiongozwa na CPA: Happiness Nkya, Jaji Robert Makaramba na Mwajaa Said. Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi huo, rais aliyerejea tena madarakani Juxon Isaac Mlay, alisema kasi na ari iliyokuwepo kwa miaka mitatu, ni vyema ikaongezeka. Aliwataka viongozi wenzake, waliorudi kutetea nafasi zao, kuhakikisha wanaendelea kufanya makubwa, wakiwa ndani ya Baraza la Habari Tanzania, ili kuwalipa wanachama waliowachagua. ‘’Niwaombe wa