Skip to main content

Posts

Showing posts from July 7, 2024

FIDEL CASTRO, WANANCHI WAPIGA MARUFUKU UZURURAJI HOLELA ENEO LA SKULI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ UONGOZI wa skuli ya sekondari ya Fidel Castro, wananchi kijijini hapo, pamoja na uongozi wa shehia ya Wawi wilaya ya Chake chake, umekubaliana kupiga marufuku kuanzia sasa, kutoingia kwa mtu yeyote bila ya kazi ya halali, ndani ya eneo la skuli, ili kuepusha athari ambazo zimeanza kujitokeza. Wakizungumza kwenye kikao cha pamoja, kilichofanyika skulini hapo, walisema tayari athari kama za wizi wa vifaa vya wanafunzi, umeanza kujitokeza, hivyo wamekubaliana kuanzia sasa kupiga marufuku, uingiaji kiholela. Mwalimu mkuu wa skuli hiyo Seif Hamad, alisema ameridhishwa na uamuzi uliofikiwa na pande mbili hizo, kwani wamekuwa na hofu kubwa ya kutokezea vitendo vya udhalilishaji hapo baadae. Alieleza kuwa, uamuzi huo unaweza kusaidia sana kuondosha uingiaji holela ndani ya skuli hiyo, ambao kwa kiasi kikubwa, ulikuwa unaanza kutishia hata mali za skuli. ‘’Mimi nimeridhishwa na uamuzi ambao umefikiwa kati yetu, wazazi na uongozi wa shehia, kwamba sasa tuwaz

KAMATI KITAIFA 'GEF' YAZITAKA TAASISI ZA UWEZESHAJI WANANCHI KUTATUA VIKWAZO UFIKIAJI USAWA KIUCHUMI

  NA MWANDISHI WETU, ZANZIBAR @@@@ KAMATI ya Kitaifa ya Ushauri kuhusu utekelezaji wa Programu ya Kizazi chenye usawa, imezitaka taasisi zinazohusika na uwezeshaji wananchi kiuchumi kuweka mkakati wa kuungana kufanya kazi kwa pamoja, ili kuzitafutia ufumbuzi changamoto zinazokwaza ufikiaji wa haki na usawa wa kiuchumi kwa wanawake. Wito huo umetolewa kufuatia ziara ya wajumbe wa kamati, yenye lengo la kufuatilia utekelezaji wa Programu hiyo Zanzibar kubaini kuwepo kwa baadhi ya changamoto zinazowakwaza wanawake kupata haki na usawa wa kiuchumi. Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye pia ni Naibu Spika wa Baraza la wawakilishi Zanzibar, Mhe. Mgeni Hassan Juma, alieleza licha ya wananchi hasa wanawake kuonesha utayari wa kujishughulisha na shughuli za kiuchumi hasa kilimo cha mwani lakini wanakabiliwa na vikwazo vingi vinavyowakatisha tamaa zaidi. Alibainisha kutokana na changamoto hizo kugusa sekta mbalimbali ni muhimu  taasisi husika kama Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Zanziba

'WEPO' YAZINDUA MRADI KUSAIDIA MAPAMBANO DHIDI YA UDHALILLISHAJI

  SALIM HAMAD, PEMBA@@@@ HAKIMU wa Mahkama ya Mkoa wa Kaskazini Pemba, Zuwena Mohamed Abdul-kadir amewataka wadau wa mapambano dhidi ya vitendo vya udhalilishaji, kuongeza kasi katika mapambano hayo, ili kuwakinga watoto wasiharibiwe, ambao ndio kundi kubwa linalokabiliwa na shida hizo. Kauli hiyo ya Hakim wa Mkoa, imetolewa kwaniaba yake na Hakimu wa Mahkama ya Mwanzo Wete Adam Abdalla Faki wakati akizungumza na Wadau wa Mambano ya Udhalilishaji, katika hafla ya uzinduzi wa Mradi wa uwezeshaji wa Kisheria na upatikanaji wa haki unaofadhiliwa na UNDP uliofanyika Baraza la Mji Wete. Alisema  katika kumaliza shidha hizo, wadau kila mmoja kwa nafasi yake anapaswa kusimama imara na kutoa ushirikiano katika kupiga vita vitendo hivyo visiendelee. ‘’Bado vitendo hivi vinaendelea kujitokeza pamoja na juhudi zote zinazochukulia lakini tunatakiwa kuwa wamoja na mashiriano kupiga vita vitendo hivyo,’’alisema . Kwa upande wake Mratibu wa Mradi huo kutoka Jumuia ya wasaidizi wa sheria Wete WEPO, Ra

'CONNECTING CONTINENT' YAWAONESHA NJIA WAZAZI KUONGEZA UFAULU

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ UONGOZI wa skuli ya sekondari ya Connecting Continent iliyopo Mgogoni wilaya ya Chake chake, umesema kama wazazi na walezi wataongeza ushirikiano, kati yao na waalimu, uwezekano wa kuondoa daraja la nne na la tatu kwa kidato cha nne upo. Mwalimu mkuu skulini hapo, Mwache Juma Abdalla, alisema waalimu wanaosomesha skuli hiyo, wamekuwa na moyo mmoja wa kuondoa daraja la nne na la tatu kwa wanafunzi wa kidato cha nne, hasa kwa mitihani ya taifa. Alisema, hilo linaweza kuwa rahisi mno, ikiwa kuanzia sasa   wazazi na walezi, watajenga msingi madhubuti ya ushirikiano kati yao na waalimu, skulini hapo. Alieleza kuwa, wapo wazazi na walezi, hawapiti skulini hapo jambo ambalo linalowapa ukakasi waalimu na kuhisi wameachiwa majukumu peke yao ya ulezi. Mwalimu mkuu huyo, aliyasema hayo Julai 6, 20204 kwenye kikao cha kwanza kwa mwaka huu, cha kuwasilisha matokeo ya muhula wa kwanza kwa wanafunzi wa kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne. Alifahamisha kuwa,