Skip to main content

Posts

Showing posts from May 5, 2024

MDHAMINI HABARI PEMBA, AWAKUMBUSHA JAMBO MUHIMU WAFANYAKAZI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WATENDAJI wa wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Pemba, wamekumbushwa kufanyakazi kwa ushirikiano katika taasisi zao, ikiwa ni njia moja wapo, ya kupeleka huduma bora kwa wananchi. Hayo yameelezwa na Afisa Mdhamini wa wizara hiyo, Mfamau Lali Mfamau, wakati akizungumza na watendaji hao, hivi karibuni uwanja wa michezo Gombani, na kusema kuwa ushirikiano ndio silaha ya ushindi. Alisema, wizara hiyo na vitengo vyake ni muhimu kwa jamii, hivyo hawana budi kwa watendaji, kulijua hilo na kuongeza ushirikiano miongoni mwao. Alieleza kuwa, hakuna mafanikio yoyote ambayo hayatachagizwa pasi na kuwepo kwa umoja, mshikamano na kupendana, na kinyume chake ni kujidhoofisha katika utoaji huduma kwa wananchi. ‘’Tujitahidi mno kushirikiana katika utendaji kazi zetu, tukifanya hivyo hata wale wananchi wanaokuja kutaka huduma kwetu, itakuwa rahisi hata kama mtendaji mmoja hayupo,’’alieleza. Katika hatua nyingine Afisa Mdhamini huyo, amewakumbusha wak

MKAGUZI WA POLISI MJANANZA, 'WAVUVI FUATILIENI TAARIFA ZA HALI YA HEWA'

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@   JESHI la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, limesema haliko tayari kuona maisha ya wavuvi yako hatarini, kwa kule kutofuatilia taarifa za wataalamu wa mamlaka ya hali ya hewa nchini.   Hayo yameelezwa bandari ya Tanda Tumbi, kwa nyakati tofauti na Mkaguzi wa shehia ya Mjananza kutoka Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Inspekta Khalfan Ali Ussi, wakati akizungumza na wavuvi hao, kwenye bandari za shehia hiyo, alipofanya ziara maalum.   Alisema, Jeshi la Polisi linawajibu wa kuwakumbusha wavuvi hao, kufuatilia kila siku taarifa za utabiri wa hali ya hewa, kwani Jeshi halipendi kuona maisha yao yako hatarini.   Alieleza, kuwa, wavuvi ni moja ya kundi lenye thamani kubwa katika jamii, hasa la kukuza pato la taifa, na ndio maana Jeshi la Polisi, likaamua kukutana nao, ili kuwakumbusha jambo hilo.   Aidha Inspekta huyo alifahamisha kuwa, hasa kwa kipindi hichi cha kuvuma upepo wenye kasi ya ajabu, ambao unauwezo mkubwa, ni vyema wavuvi wak

JAJI DHAMANA PEMBA, ATAKA MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA KWA VITENDO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ JAJI Dhamana wa Mahkama kuu Zanzibar kisiwani Pemba, Salim Hassan Bakari, amewataka wahitimu ya mafunzo ya sheria, kuwa mstari wa mbele, kuongoza mapambano dhidi ya rushwa katika taasisi za umma, ili kwenda samba mba na kasi serikali ya awamu ya nane.   Jaji huyo aliyasema hayo leo Mei 10, 2024 , ukumbi wa Maktaba Chake chake, wakati akiyafunga mafunzo ya sheria, yalioendeshwa na Kituo cha Mafunzo na Utafiti Zanzibar ’ZLRC’ kilichopo chini ya Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar, kwa upande wa Pemba.   Alisema, sasa wameshaongeza uwelewa wa mapambano dhidi ya rushwa hasa baada ya kuisoma sheria husika zikiwemo za manunuzi, ni vyema baada ya kuhitimu mafunzo hayo, wakawe mstari wa mbele katika eneo hilo.   Alieleza kua, serikali ya awamu ya nane, nayo imekuwa ikikemea kwa nguvu zote, juu ya utoaji na upokeaji wa rushwa, hivyo nao wanaojibu huo, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha utawala bora.   ‘’Leo mmehitimu mafunzo ya kisheria, na bila sha

BODI YA USHAURI YA WATOTO YA TAIFA YATAKIWA KUWA NA UMOJA- WAZIRI PEMBE

  Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mhe Riziki Pembe Juma ameitaka Bodi ya Ushauri ya Watoto Taifa kuwa na umoja moja katika mapambano ya vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia dhidi ya   Wanawake na Watoto. Ameyasema hayo jana wakati alipokutana na bodi hiyo Ofisini kwake Kinazini Mjini Unguja. Amesema hivi sasa inaonekana watoto wa kiume kuharibiwa kwa kasi. Hivyo Mhe. Riziki amewataka wajumbe wa bodi hiyo kunganisha nguvu ya pamoja katika mapambano ya vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia dhidi ya   wanawake na Watoto . Mhe. Riziki amefahamishwa kwamba Wizara anayoisimamia imeundwa kwa ajili ya kushughulikia masuala   mbalimbali ya kijamii nchini, ikiwemo masuala yanayowahusu watoto, hivyo ameitaka bodi hiyo kuhakikisha changamoto zinazowakabili watoto   kuziwasilisha katika Wizara hiyo ili kuweza kupatiwa ufumbuzi. Aidha amewataka kuhakikisha wanabadilisha mitazamo ya baadhi ya watoto wanokataa kushiriki katika vikao au wito wowote kwa kuona kwamba hakuna mal

RC: MATTAR AHIMIZA KUFUATWA MAADILI KWA WAUGUZI

NA ASHA ABDALLA, PEMBA@@@@  WAUGUZI wameshauriwa kuwa na maadili mazuri katika kufanya kazi zao, ili kuendelea kutoa huduma nzuri zinazo stahiki na kuwapa faraja wagonjwa wakati wanapohudhuria katika vituoni mwao.  Hayo yameelezwa jana Mei 9, 2024 na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, ukumbi wa chuo cha Samail Gombani Chake Chake, Pemba wakati alipokua akizungumza na wauguzi katika kuelekea kuadhimisha siku ya wauguzi duniani, ambayo kilele chake rasmi ni Mei, 12 mwezi huu. Amesema kuwa na maadili, mazuri katika kufanya kazi ni muhimu, kwani kunapelekea kupata umaarufu  kwa watu  na kuitia hadhi mzuri taasisi kwa ujumla.  "Tujitahidi tuwe na maadili, kwani tunapokuwa kazini taasisi tunazo zifanyia kazi zina tudai maadili mazuri na watu ambao tunawapatia huduma katika Taasisi hizo na kujijengea umaarufu mzuri katika kazi zetu", alieleza.  Kwaupande wake Mkurugenzi Idara ya Uuguzi na Ukunga Wizaraya Afya Mwanaisha Juma Fakih  aliwataka wauguzi hao  kufanya kazi

MATAYARISHO WIKI YA MSAADA WA KISHERIA PEMBA YAANZA KWA KISHINDO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ LEO Mei 7, mwaka 2024, Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar ofisi ya Pemba, imekutana na wadau wake mbali mbali wakiwemo watoa msaada wa kisheria na wasaidizi wa sheria, ili kupanga mikakati ya kuelekea, wiki ya msaada wa kisheria hapa Zanzibar . Kwenye kikao hicho kilichofanyika Gombani Chake chake, na kuongozwa na Afisa Mdhamini, Ofisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Pemba, Halima Khamis Ali, kwanza kilipokea ripoti ya wiki ya msaada ya mwaka 2023, iliyotolewa na Mkuu wa Divisheni ya Katiba na Msaada wa Kisheria Pemba, Bakar Omar Ali. Ambae kwenye ripoti hiyo, alielezea mafanikio yaliopatikana ikiwa ni pamoja na kuwafikia wananchi waliokuwa wakihitaji msaada wa kisheria katika makaazi yao. Alisema jingine ni waendesha boda boda kutoa malalamiko yao, juu ya madai ya kunyanyaswa na askari wa usalama barabarani pamoja na faini kubwa wanazopigwa kwa makosa madogo. Mkuu huyo wa Divisheni, alieleza kuwa jingine ni kuwakuta

KONGAMANO MAADHIMISHO SIKU YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI, SHERIA MPYA ZANZIBAR IKO JIKONI

  NA MARYAM NASSOR, UNGUJA@@@ @ SERIKALI ya Mapinduzi   ya Zanzibar,   imesema   mageuzi ya sera na sheria za habari nchini yaendane   sambamba na kanuni   na maadili ya vyombo vya habari. Akizungumza katika kongamano la madhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari, Katibu mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Fatma Hamad Rajab, akimuakilisha waziri wa wizara hiyo alisema hilo litafanikiwa. Alisema, Serikali   ya awamu ya nane, inafanya juhudi kubwa   ya kuweka mazingira rafiki kwa uhuru wa vyombo vya   habari nchini,    bila ya kuathiri uhuru wa mtu mwingine. Alieleza kuwa, hivyo wandishi wa habari wanatakiwa kufanya kazi zao   kwa kuzingatia sheria, weledi   na maadili,   ili kunufaika na sekta hiyo. Nae Afisa sheria kutoka Tume ya Utangazaji Zanzibar Khadija Mabrouk Hassan, alisema   rasimu ya sheria ya habari tayari inafanyiwa kazi kwa sasa   na iko katika hatua za mwisho katika afisi ya Mwanasheria mkuu kwa hatua zaidi. Alisema, sheria zilizofanyiwa k

KWA SHERIA HII UHURU WA HABARI ZANZIBAR NI NDOTO

  NA NIHIFADHI ISSA, ZANZIBAR.@@@@     WAANDISHI wa habari wanajukumu la kuendelea kufanya uchechemuzi wa mabadiliko ya sheria zenye mapungufu na ambazo sio rafiki kwa tasnia ya habari ili kutoa fursa ya upatikanaji wa sheria zilizo bora. Yamebainishwa hayo na Mkurugenzi wa Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania TAMWA Zanzibar      Dkt. Mzuri Issa   nakusema kuwa     Sheria nambari 5 ya Wakala wa Habari, Magazeti na Vitabu ya mwaka 1988, ambayo imefanyiwa marekebisho sheria namba 8 mwaka 1997 sheria hii licha yakuwa ni kongwe imekuwa na mapungufu mengi yanayokwamisha haki na uhuru wa vyombo vya habari Zanzibar. Akizungumza katika kikao cha kujadili    mapungufu ya sheria zinazokwamisha uhuru wa habari huko katika ukumbi wa TAMWA Tunguu amesema Demokrasia sahihi hutegemea uhuru wa vyombo vya habari unavyoweza kusimamia maslahi ya jamii,     ikiwemo   uhuru wa kutoa maoni na kujieleza bila ya kuingiliwa pamoja   kusambaza taarifa na mawazo ya aina mbalimbali kwa kufuata