NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WATENDAJI wa wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Pemba, wamekumbushwa kufanyakazi kwa ushirikiano katika taasisi zao, ikiwa ni njia moja wapo, ya kupeleka huduma bora kwa wananchi. Hayo yameelezwa na Afisa Mdhamini wa wizara hiyo, Mfamau Lali Mfamau, wakati akizungumza na watendaji hao, hivi karibuni uwanja wa michezo Gombani, na kusema kuwa ushirikiano ndio silaha ya ushindi. Alisema, wizara hiyo na vitengo vyake ni muhimu kwa jamii, hivyo hawana budi kwa watendaji, kulijua hilo na kuongeza ushirikiano miongoni mwao. Alieleza kuwa, hakuna mafanikio yoyote ambayo hayatachagizwa pasi na kuwepo kwa umoja, mshikamano na kupendana, na kinyume chake ni kujidhoofisha katika utoaji huduma kwa wananchi. ‘’Tujitahidi mno kushirikiana katika utendaji kazi zetu, tukifanya hivyo hata wale wananchi wanaokuja kutaka huduma kwetu, itakuwa rahisi hata kama mtendaji mmoja hayupo,’’alieleza. Katika hatua nyingine Afisa Mdhamini huyo, amewakumbusha wak