Skip to main content

KILANGI AIVUTIA PUMZI KAMPUNI UJENZI WA TANGI LA KUHIFADHI MAJI

 



Na Salma Lusangi, Zanzibar:

KATIBU Mkuu Wizara ya Maji, Nishati na Madini Zanzibar Joseph Kilangi  ameahidi kusitisha  mkataba na Kampuni ya Simba Developa inayojenga mradi wa tangi la kuhifadhia maji safi na salama  eneo la Mgeni Haji Wilaya ya Maghari ‘A’ Unguja, kwa kutoridhishwa  na utendaji kazi wa kampuni hiyo.

Aliyasema hayo wakati alipofanya ziara yake ya kiutendaji ya kukagua miradi hiyo inayotekelezwa na kampuni mbalimbali ikiwemo  kampuni ya Afcon,  Simba developa na Shanjo.

Alisema utekelezaji wa kampuni hiyo, haujafikia hata asilimia 30 ya ufanyaji kazi, hivyo endapo ujenzi huo utaendelea kudorora, atashauriana na mwasheria wa wizara yake, ili kuandaa utaratibu wa kusitisha mkataba pamoja na kuwatoza fidia kampuni hiyo.

“Mradi wa ujenzi la tangi ni mradi wa miezi minane, lakini hadi sasa miezi minne imepita wamechimba shimo na kufunga nondoo chini basi, hakuna kazi inayoendelea na hatuwezi kuendelea na kampuni hii,’’alieleza.

Alisema hatua ya kukatisha mkataba itafanyika kwa kampuni zote ambazo zitashindwa kutimiza ahadi kama walivyokubaliana, na kila kampuni ina muda waliyokubaliana katika kutekeleza mradi.

Alielezea Mradi wa Maji unayotekelezwa na kampuni ya Afcon kupitia fedha za Benki ya Exim, ambapo ni mkopo nafuu wa dola milioni 92.18 unajukumu la kuchimba visima, kujenga matangi ya kuhifadhia maji, kufukia maboba pamoja kujenga nyumba ya kuhifadhi Maji (Maji House) unaendelea vizuri.

Naye Meneja Mradi huo, Rashid Mohamed kutoka Mamlaka ya Maji Zanzibar ‘ZAWA’ alisema mradi wa kisima kupitia fedha za ahuweni za UVIKO-19, unajukumu la kujenga matangi 10 kwa Unguja na Pemba, kuchimaba visima vipya 38 pamoja kufanya kazi ya kutandika mabomba.

Kwa upande wake Mhandisi Hassan Khamis Hassan kutoka ‘ZAWA’, alisema kisima cha Bubwisudi, hakina tatizo kimefungwa  mashine kubwa ya kusukumia maji, ila wanahitaji usalama wa mashine hiyo na wameshafanya utaratibu wa kuwaomba ZECO wasaidie kifaa hicho cha usalama wa mashine (mota).

Mapema Mhadisi wa kampuni ya Simba Develop Hassan Hamad, alisema utekelezajwi wa mradi wa tangi la maji kupitia kampuni hiyo unatokana na mshauri elekezi ambapo alifelisha kokoto zilizoagizwa mwanzo kutona na ardhi ya hapo ina maji maji isingeweza kukidhi vigezo vilivyohitajika lakini  tayari wameshaagiza kokoto zinanostahiki na kuendelea na kazi.

Ziara ya katibu Mkuu Kilangi ni ziara ya siku mbili, ambapo siku ya kwanza alitembelea Mradi wa maji shehiya ya Masingini, Dimani, Nyumba ya kuhifadhia maji eneo la Miembeni ( Madema) ambapo shughuli hizo zinatekelezwa na fedha za Exim Benki. Pia alitembea mradi wa maji Mbuzini unaotekelezwa kwa fedha za ahuweni za UVIKO-19 na mradi wa ujenzi wa tangi la kuhifadhia maji Mgeni haji linalojengwa na kampuni ya Simba Developa.

Mwisho.

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...