Skip to main content

WATAALAMU 'ECD' PEMBA WATAJA NJIA 5 KUKUZA UBONGO WA MTOTO

 

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA

WATAALAMU wa malezi ya kisayansi, makuzi na uchangamshi wa mtoto katika hatua za awali ‘ECD’ kisiwani Pemba, wametaja njia tano ambazo familia ikizifuata, itakuwa ni chachu ya ukuaji wa ubongo kwa matoto na kuongeza ufahamu.

Moja ya njia hizo ni chakula bora ikiwa ni pamoja na mboga mboga, matunda na samaki kwa mama mjamzito, tokea siku ya kwanza baada ya kubeba ujazito.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, walisema kwa mfano katika samaki, kuna kirutubisho kinachoitwa ‘omega three’ ambacho chenyewe kimebaba chembe chembe zinazoitwa ‘rids’ ambazo kazi yake kubwa, ni kujenga ubongo wa mtoto.

Mmoja kati ya wataalamu hao Dk. Omar Adam Mohamed anayesomea matibabu ya watoto nchini China, alisema hatua nyingine, ni mama mjamzito kunywa maji kwa wingi.

Alisema chumvi chumvi na kalshiam zilizomo ndani ya maji safi na salama, humsadiai mtoto kukukua kwa haraka na kujenga ubongo wake tokea akiwa tumboni.

Mtaalamu huyo alisema, mama mjamzito anapopuuzia unywaji maji kwa wingi, hujikaribishia magonjwa ambayo yanaweza kusababish kusinyaa kwa ukuaji wa mtoto na kuathiri ubongo wake.

‘’Suala la lishe nzuri wala halinauhusiano na utajiri, bali familia ni kujipanga kwa mboga za majani na matunda ya kawaida, kufanya hivyo ni kukuza ubongo wa mtoto,’’anaeleza.

Nae Kaimu Mkuu wa Idara ya Ustawi wa Jamii Pemba Omar Mohamed Ali, alisema njia nyengine ya kukuza ubongo wa mtoto, ni wazazi kujenga utamaduni wa kumzungumzisha mtoto akiwa tumboni.

‘’Inawezekana jamii haiamini kuwa, mtoto akiwa tumboni anaskikia sauti, milio, kelele n ahata kupata msongo, hivyo ni wajibu kufanya hivyo ili aanze kuzoea mazingira yake mapema,’’alishauri.

Aidha Afisa huyo alisema, mara mtoto anapozaliwa katika miezi yake mitatu ya kwanza, familia ziwe na utamaduni wa kumtolea hadithi na kufanya uchangamshi nae.

‘’Hatua nyingine ni watoto kabla hawajafikia miaka minane ‘8’ jamii iwashirikishe kwa mambo kadhaa, ikiwa ni pamoja kumfundisha majina ya vitu, hasa yalio karibu nao,’’alishauri.

Aidha alifafanua kuwa, sio busara jamii kuanza kuwandaa watoto baada ya kufikia miaka minane, na kuiacha siku moja baada ya kuzaliwa hadi miaka minane.


‘’Mtoto anaanza kupata ufahamu toka akiwa tumboni mwa mama yake, na hata siku moja baada ya kuzaliwa, sasa ni wajibu kwa wazazi, kutenga muda kila siku ili kushirikiana na mtoto wao, hiyo itajenga ubongo wake mapema,’’alieleza.

 Muwezeshaji kwenye mafunzo ya Kitaifa ya Sayansi ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto ‘SECD’ Everlyne Okeyo, anasema tafiti zinaonesha kuwa, mtoto akiwa tumboni anasikia zaidi ya lugha 600.

Alisema, watoto wanakosa ukuaji mzuri wa kutengeneza ubongo wao, kwa kule wazazi kutowashughulika kuzungumza nao, wakidhani hawana uwezo wa kufahama lugha zao.

Alieleza kuwa, makuzi mazuri ya awali ya mtoto, ni baina ya siku moja baada ya kuzaliwa, hadi miaka minane, ambapo hapo huwa rahisi kwa wazazi na walezi, kuweka mwelekeo wa maisha ya mtoto.

Katika hatua nyingine, Everlyne alisema, ubongo wa binadamu una nyuroni bilioni 100, na ndio maana mtoto mara anapozaliwa, huwa na asilimi 25 ya ubongo wake ni mtu mzima.

‘’Mtoto anapofikia mwaka mmoja, hufikia asilimia 60, wakati miaka miwili huwa na asilimia 75 na kuanzia miaka minne hadi sita, hubeba asilimia 90 ya uwelewa,’’alieleza.

Akizungumza kwenye ufunguzi wa mafunzo hayo, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dk. Dorothy Gwajima, aliwataka waandishi wa habari, kuifikisha kwa jamii, dhana ya malezi ya kisayansi ‘SECD.

 

Mzazi Mwajuma Haji Makame wa Chake chake, ambae ameshapata watoto sita, anasema amekuwa akiwasemesha watoto wake wachanga, ingawa sio kwa kurudia rudia.

 

‘’Nilikuwa nadhani hadi mtoto aanze kufikia mwaka mmoja na kuendelea, ndio nianze kumfundisha na kuchangamana naye, nikiamini ndio anafahamu,’’anasema.

 

Wazazi Khamis Hija Kassim na Othman Himid Omar wanasema, wanaume waliowengi wamekuwa wakikamilisha majukumu ya familia na yaliobakia likiwemo la uchangamshi wa mtoto ni la mama pekee.

 

‘’Elimu ya ECD bado haijafika kwa wananchi tuliowengi, maana wapo baadhi yetu tunadhani wajibu ni kuakikisha milo imepatikana na sio kutenga muda kucheza na watoto na hasa mama wajawazito,’’anasema.

 

Hivi karibuni akizungumza kwenye kilele cha maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika, Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, aliwataka wanaume kutenge muda wa kucheza na watoto wao.

 

                              Mwisho   

    

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch