Skip to main content

KAMA TAMTHILIA VILE KESI YA DAKTARI IS-HAKA PEMBA KUACHIWA HURU

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA:::


MTOTO wa miaka 16, ambae awali aliliambia Jeshi la Polisi kuwa, amebakwa na daktari Is-haka Rashid Hadid, na kisha kumkana mahakamani na kuondolewa kwa kesi hiyo, sasa mtoto huyo, anashikiliwa na Jeshi hilo, kwa kutoa taarifa za uongo.

KESI HII ILIANZIA WAPI?

Itakumbukwa kuwa, mtoto huyo miezi mitatu iliyopita, ndie aliyeliambia Jeshi la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, kuwa ni daktari huyo pekee, ndie aliyemtorosha na kisha kumbaka zaidi ya mara moja.

Baada ya maelezo ya mtoto huyo, ndipo Jeshi la Polisi lilipojitayarisha kirasilimali na kumfuata daktari huyo kijijini kwao Kangagani wilaya ya Wete, na kumkamata na kuanza kumuhoji.

Baada ya kuhojiwa juu ya tuhma zinazomkabili, kisha daktari huyo, kuanzia Mei 18, mwaka huu alipandishwa Mahakamani na kuswekwa rumande, hadi Mahakama ya mkoa Wete ilipomuondoshea shataka dhidi yake juzi Julai 13, mwaka 2022.



Ambapo Hakimu wa mahakama maalum ya makosa ya udhalilishaji mkoani humo, Ali Abdur-haman Ali, alisema sababu ya kumuondoshea kesi hiyo daktari huyo, ni muathirika (mtoto) wa tukio hilo, kumkana mtuhumiwa.

Alisema kila mtoto anapoulizwa juu ya kumfahamu mtuhumiwa aliyemtaja akiwa Polisi, alikana zaidi ya mara tatu, na ndio sababu ya kuondoshwa kwa kesi hiyo mahakamani hapo.

JESHI LA POLISI KWA SASA

Hapo ndipo Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi ambae pia ni mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai mkoani humo, Gerome Felix Ngoi, alipoamua kumshikilia mtoto huyo.

Alieleza kuwa, kwa sasa wanaendelea kumuhoji juu ya kutoa kwake taarifa za uongo kwa Jeshi la Polisi, na kusababisha usumbufu kwa daktari huyo.



‘’Ni kweli baada ya kesi ya ubakaji, iliyokuwa ikimuhusisha daktari Is-haka Rashid Hadid kuondolewa, kwa sababu ya mtoto kumkana, sasa tunamshikilia kwa tuhuma za kulidanganya Jeshi la Polisi,’’alieleza.

Aidha alieleza kuwa, tayari jalada lenye namba ‘IR 367’ ya mwaka 2022 limeshafunguliwa na Jeshi la Polisi la mtoto huyo na upelelezi utakapomilika atafikishwa mahakamani.

Hata hivyo, amewataka wananchi mkoani humo, kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi na vyombo vyengine vya sheria, ili kukomesha matendo hayo.

KESI ILIPOKUA MAHAKAMANI

Ilidaiwa mahakamani kuwa, mtuhumiwa Is-haka Rashid Hadid April 21 mwaka huu, majira ya saa 8:30 mchana, alimtorosha mtoto mwenye miaka 16, kutoka nyumbani kwao, na kumpeleka nyumbani kwake Kagangani.

Kufanya hivyo ni kosa kinyume na kifungu cha 113 (1) (a) cha sheria ya Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018, sheria ya Zanzibar.

Kosa la pili kwa mtuhumiwa huyo lilikuwa ni baada ya kumtorosha, siku hiyo hiyo majira ya saa 3:00 usiku alimbaka, kinyume na kifungu cha 108 (1), (2), (e) na 109 (1) cha sheria ya Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018.


Kosa la tatu ambalo lilitokea Aprili 22 na la nne ambalo lilitokea Aprili 23, mwaka huu pia, alilitenda kwa nyakati tofauti za usiku, kwa kudaiwa kumbaka.

Ambapo pia kufanya hivyo, ni kinyume na kifungu cha 108 (1), (2), (e) na 109 (1) cha sheria ya Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018 sheria ya Zanzibar.

KESI ZINAZOFANANA NA HIZI

Tukio linalofafana hilo, liliwahi kutokea Novemba 21, mwaka 2019, katika hospitali ya Chake chake, baada ya daktari wa kitengo cha Atrasaund, kudaiwa kuomba rushwa ya ngono kwa mjamzito, kama sharti la kumpa huduma. Ambapo kesi hii nayo ilifutwa Januari mwaka 2021.

Aidha Kesi nyingine ya ubakaji ni ya mwaka huu, ya daktari Hassan Said Hassan ambayo ilifunguliwa mahakamani Disemba 16, mwaka jana na kisha baada ya mtoto kumkana mahakamani ilifutwa JUuni 29, mwaka huu, kwenye mahakama ya mkoa Chake chake.

Aidha Disemba 18, mwaka mwaka 2019, TBC 1, iliripoti Afisa Muuguzi Msaidizi wa kituo cha Afya Mamba mkoani Katavi kushikiliwa na Jeshi la Polisi, kwa tuhuma za kumbaka mjamzito, wakati alipokuwa akimsaidia kujifungua.

                    Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch