Skip to main content

WADAU PEMBA WATAJA MWARUBAINI WA AMANI ZANZIBAR

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA

WADAU wa ujenzi wa amani kisiwani Pemba, wamesema kama haki itatendeka katika sekta kadhaa zilizopo Zanzibar, suala la uvunjifu wa amani, litabaki kwenye vitabu vya kumbu kumbu pekee.

Walisema, bado kuna tasisi ndani ya serikali zimekuwa zikisababisha uvujifu wa amani, kwa kule kutotenda haki ipasavyo, wakati wanapowahudumia wananchi.

Wakizungumza kwenye kongamano la amani na mashirikiano lililoandaliwa na tasisi ya Search for Common Ground ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa ‘dumisha amani Zanzibar’ na kufanyika ukumbi Greef Foullege Chake chake Pemba, walisema msingi wa amani ni haki.

Walieleza kuwa, kazi inayofanywa na ‘SCG’ kwa kushirikiana na ‘the foundation for Civil Society’ kwa ufadhili wa Umoja wa nchi za Ulaya ‘EU’ ni nzuri, ingawa sasa kazi iliyobakia kwa watendaji ni kutekeleza haki.

Mmoja kati ya wadau hao, kutoka Jumuiya ya Maimamu Zanzibar ‘JUMAZA’ Yussuf Ramadhan Abdalla, alisema uvunjifu wa amani hujitokeza baada ya mwenye haki kukoseshwa na kupewa mtu mwengine.

‘’Wenzetu wa Search, wamekuja na mradi mzruri mno wa kutuamsha juu ya kuidumisha amani iliyopo, sasa ni kazi kwa wasimamizi wa haki, kuitekeleza,’’alisema.

Nae mdau Tatu Abdalla Msellem, alisema sio kweli kuwa uvunjifu wa amani Zanzibar, husababishwa na uchaguzi pekee, bali zipo changamoto nyingine kama migogoro ya ardhi, ndoa na udhalilishaji, hupelekea kukosekana kwa amani.

Kwa upande wake mjumbe kutoka chama cha Ualbino Pemba Mudathiri Khamis Sharif, alisema suala la amani linafaa kuchungwa na kila mmoja, kwani athari yake, huwakumba zaidi wanawake, wazee, watoto na wenye ulemavu.

Nae Suleiman Juma Suleiman na Salim Hamad Simba, walisema vyombo vya habari, visipotumika vyema, vinaweza kuwa chanzo cha uvujifu wa amani.



Akizungumza kwenye kongamano hilo, Afisa Mawasiliano kutoka Search for Common Ground Zanzibar, Khelef Nassor Rashid , alisema ujio wa mradi huo, ni kuona Zanzibar kuna kuwa na amani endelevu.

‘’Mradi huu ambao tuliuzindua tokea mwaka jana, na kutarajia kuutia nanga mwishoni wa mwaka huu, ni kuhakikisha wanasiasa, viongozi wa dini, waandishi wa habari na jamii inaendelea kuelimisha faida za ujenzi wa amani,’’alieleza.



Akifungua kongamano hilo, Afisa Mdhamini wizara ya Nchi, Afisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Pemba, Thabit Othman Abdalla, alisema mradi huo, umekuwa msaada mkubwa kwa serikali kuu.

Alisema, viongozi wote wamekuwa wakisisitiza kudumisha amani, na ndio vivyo hivyo tasisi ya search kwa kushirikiana na the foundation, wameibua mradi huo kwa wakati mwafaka.

‘’Zanzibar kwa sasa inaendeshwa kwa mfumo wa serikali ya Umoja wa Kitaifa, ambapo suala la amani ni jambo la mwanzo, na huku tasisi hizi zinakuja na mradi huu, ni jambo jema kwetu,’’alieleza.

Mapema akiwasilisha mada ya vyombo vya habari na ujenzi wa amani, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya waandishi wa habari Pemba, ‘PPC’ Ali Mbarou Omar, alisema mradi huo umesaidia kuifikia jamii, katika nyanja mbali mbali.

‘’Tulitengeneza vipindi, uandishi wa habari za kawaida, makala na hata kuwatumia wasanii kufikisha ujumbe wa amani kwa jamii, hili tunaona tumefanikiwa,’’alifafanua.

Wakati huo huo Afisa program kutoka ‘the foundation for Civil Society’ ya Tanzania bara Eveline Mchau, alisema kila mmoja anayonafasi ya kuchagiza na kufanya uchechemuzi wa ujenzi wa amani.

‘’Tunatarajia hata mradi huu ukimalizika mwishoni mwa mwaka 2022, basi wadau nyinyi na wengine, tuone mnaendeleza wajibu wenu wa kudumisha amani, katika maeneo yenu,’’alifafanua.

Mradi wa dumisha amani Zanzibar ambao ulizinduliwa mwaka 2021, unatekelezwa kwa pamoja kati ya search for Common Ground, the foundation for Civil Society, kwa ufadhili wa Jumuiya ya nchi za Ulaya ‘EU’.

                              Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch