Skip to main content

NOELA: MTAALAMU WA KUZIDARZI NYWELE, SALUNI YAKE YAMPA UHAKIKA WA MAISHA

 


NA MARYAM SALUM, PEMBA

 “SHIDA, dhiki na maneno makali niliyoyapata wakati naishi kwa mjomba wangu, ndio chanzo cha kuamua kujiajiri,’’ndio maneno ya kwanza ya mjasiriamali Noela Alfred Majia mmiliki wa saluni ya Crassiana hair salun liyopo Gereji Wawi- Chake chake.

Hapa ndio msemo ‘mtegemea cha ndugu hufa maskini’ ulipotafsirika kwa vitendo kwa mjasiriamali huyo mzaliwa wa Dar-es Salaam na sasa mkaazi wa Wawi Chake chake Pemba.

HISTORIA YAKE

Alikuwa anaishi na mama yake mzazi na mjomba wake, akimtegemea kwa kila kitu kwa wakati huo, huku mama yake akiwa na uwezo mdogo wa kuendesha familia.

Noela alijihisi mtoto wa maana sana mbele ya mjomba wake, na aliamini anaweza kuwa mwanga wa maisha yake, hasa kwa vile ni mjomba anayetokana na mama yake mzazi.

‘’Kwa hakika tamaa ya kukaa na mjomba na kisha kuwa na maisha mazuri hapo baadae, nilifikiria sana, na sikutarajia kuwa iko siku mjomba engegeuka adui wa maisha yangu,’’anasema.

Wakati Noela akiwa na miaka 17 alishamaliza darasa la kumi, siku moja alichokipata kutoka kwa mjomba wake, juu ya kauli kali na chafuzu bila ya kujali umari wake.

‘’Toka hapa kwangu, ondoka haraka sana, wewe mtu gani tafuta pahala uende, mimi sikutaki kukuona hapa kwangu,’’ndio maneno anayoyakumbuka Noela kutoka kwa mjambo wake.

Huku akitakiwa kuhama na mjomba wake, naye sasa baada ya kuona hilo limesimama, alianza kubuni na kufikiria namna ya kutokana hapo na kuelekea eneo jengine kujiendesha kimaisha.

 “Kutokana na hali ilivyokuwa sikujali udogo wangu wala umri wangu, nilikimbia na hapo nikaona bora nifanye uamuzi wa haraka kama msichana yakutafuta njia yakupata maisha kabla familia yangu haijagombana kwa ajili yangu,” anaeleza.

BAADA YA KUTIMULIWA NA MJOMBA WAKE

Noela aliwasili kisiwani Pemba mwaka 2015, akiwa hana uhakika wa kula, kulala lakini nia yake ni kupata kazi ambayo itamuwezesha kusonga mbele kimaisha.

“Mimi ni msichana ambaye nilikuwa naishi na mama na mjomba, lakini baada tu ya kumaliza masomo yangu mjombo alinikaripia na kuamua kufika Pemba kutafuta kazi,’’anasema.

Baada ya kutua Pemba, alishikwa mkono na kijana mmoja, na kumpeleka kufanyakazi za ndani, eneo la Machomane Chake chake, ingawa hakudumu.

‘’Sikudumu maana, haikua lengo langu hasa kuendelea kufanya kazi za ndani, nilipopata shida yangu ya shilingi 700,000 kama miezi minne niliacha kufanya,’’anasema.

UANZISHWAJI WA SALUNI YAKE

Shilingi 700,000 alipozipata zilimtosha kuanzisha ujasiriamali wa kuzipakasa nywele za wanawake wenzake na kuwatia urembo mwengine kichwani.

Noela anasema licha ya changamoto alizozipata ikiwa ni pamoja na kutokuwa na sehemu rasmi ya malazi, lakini kisha alifanikiwa kupata malengo wa kukodia kuanzisha saluni.

Alisema kuwa mtaji wake wa kusuka nakuwa mmiliki wa saluni  umemfanya kuwa mwanamke anayeweza kutafuta maisha popote katika nchi yake bila woga.

“Kazi yangu ya mkono inanifanya nijiamini na kuaminiwa na kila mtu kwa chochote ambacho nitahitaji bila ya kubugudhiwa,” alieleza.

AINAYA MITINDO YA NYWELE



Kwenye saluni yake, Noela anasema ipo zaidi ya mitindo saba, anayoweza kuwasuka wateja wake, na hivyo hivyo inatofautiana bei.

‘’Kwa mfano msuko aina ya roketi, minyoosho, mbinjuo na machana ya ndizi haya yote huwahudumia wateja wake kwa shilingi 2000,’’anasema.



Lakini anayomitindo kama ya yebo yebo kwa gharama ya shilingi 16,000 matubutu ya uzi ni shilingi 20,000, crochet kwa gharama ya shilingi 10,000 na mabutu ya rasta ni shilingi 30,000 na mtindo , kubiip ni shilingi 15000.

FAIDA YA SALUNI

Kwake anasema kuaminiwa na wenzake, sio jambo katika maisha hasa ya siku hizi yaliojaa watu matapeli na wengine wakishindwa kujiamini wenyewe.

Jengine analoona kama faida kubwa kwake ni kujiamini kukopa, kuazima fedha kwa kiwango chake anachokihitaji, jambo ambalo kabla yam waka 2015 hilo hakuwa na uwezo nalo.

“Sasa hivi naweza kujikwamua kimaisha kutokana na changamoto mbali mbali zinazonikabili mimi na familia yangu bila kumtegemea mume au mtu mwengine”, alieleza.

Kutokana na saluni yake kuwa ni ya kwaida, siku ambayo wateja wamekwenda wengine hujipatia kati ya shilingi 40,000 hadi shilingi 50,000 ingawa kwa siku za uhafifu huingiza shilingi kati ya 25,000 hadi shilingi 30,000.

Hata kuongeza mtaji wa shilingi 700,000 aliaonza nao na sasa kujimilikisha mtaji wa shilingi milioni 1, kwake sio jambo dogo.

CHANGAMOTO

Moja baadhi ya bidhaa za rasta, wigi na dawa za kulainisha nywele au kupaka usoni humalizimu kuzifuata Dar-es-Salaam, kutokana wafanyabiashara wa kisiwani Pemba kutochukua bidhaa hizo.

 Kuhusu wateja, anasema hutegemeana na mwezi au siku, maana suala la urembo pia huendana na siku au mwaka mwenye shughuli maalum.

‘’Hutegemeana kwa mfano mwisho wa mwezi hupata wateja kati ya 10 hadi 15, ingawa kwa siku za kawaida huwa ni katia ya watano hadi sita,’’anasema.

 “Namshukuru mwenza wangu mashirikiano kwenye  kazi yangu wananipa mazuri, hunipa maneno mazuri, ili nisikate tamaa kutokana na ugumu uliopo kwenye kazi yangu,” anafahamisha.

 ULIPAJI KODI

Anasema mazingira yaliwekwa kwao wajasiriamali wadogo, juu ya ulipaji kodi kwa biashara yake, anaufurahia mno na kumpongeza rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi.

‘’Kodi yangu hapa kwa udogo wa biashara yangu nalipa shilingi 50,000 serikali, ambapo hii ni wastani maana sasa Pemba imevamiwa na milango ya saluni,’’anasema.

OMBI LAKE

Anasema kama kuna mashirika, makampuni na tasisi za serikali ni vyema zikamuangalia, kwa kumpa mikopo yenye masharti nafuu ili kukuza biashara yake.

Kwake anaona mikopo wakati mwengine humpitia upande, kutokana na kuwa na masharti makubwa, na kumuacha akiwa mnyonge kwenye eneo hilo.

MALENGO YAKE YA BAADAE

Noela ambaye kwa sasa yumo kwenye ndoa kwa muda zaidi ya mika mine, hajabahatika mtoto, ingawa malengo yake ni kuongeza ujuzi wa aina nyingine ya mitindo ya nywele.

Jengine anasema ni kuwasaidia wanawake wenzake vijana, kupata ajira na hilo litawezekana ikiwa, dhamiri yake ya kuomba mikopo yenye masharti nafuu atafanikiwa


WATEJA WA NOELA

‘’Sipendi kutaja jina langu, lakini kwa hakika huduma za Noela za ususi wa nywele na uwekaji dawa na urembo mwengine, yuko vizuri mno na sihami kwake,’’anasema.

Hata mwengine aliyakataa kutoa jina lake, anasema Saluni ya Noela kwanza inautulivu na kisha huduma zake sio ghali kama wengine, lakini kubwa zaidi ameonesha kubobea.

Mwamtatu Hilmin Yassiri anasema Noela ana sifa za kipekee kwenye kazi yake, ambazo hajawahi kuzipata kwenye saluni nyingine alizowahi kupata huduma.

ALIKOTOKA NOLEA KIELIMU/MAISHA

Noela alipata elimu yake ya msingi katika Skuli ya Mchangani Dares-Salaam, na baada ya kumaliza, aliendelea na  elimu ya sekondari mwaka 2012 skuli ya Makumbusho,’’anasema.

 Kazi hiyo ya saluni (ususi wa nywele), alianza kuipenda tokea akiwa  darasa la nne, kwa vile ndani alimokuwa anaishi walikuwemo na wadada wakisuka na kupamba maharusi.

“Hivyo kutokana na ufahamu wangu niliokuwa nao na jinsi nilivyokuwa napenda hivyo vitu, sikuwa tayari kujiweka nyuma kama mfuko wa suruali, na leo najivunia nipo na changu,’’anasema.

                                  MWISHO.

 

 

 

 

                                                      

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch