Skip to main content

WANAWAKE TANZANIA WAWEZESHWA MANUNUZI YA UMMA KIELEKTRONIKI

 


 

Na Salma Lusangi, New York@@@@

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesema imewawezesha wanawake kupata fursa za manunuzi ya umma kwa kutoa mafunzo ya kiufundi ili kuongeza uwezo wa zabuni na matumizi bora ya mifumo ya ununuzi wa kielektroniki.

Taarifa hiyo imetolewa na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Mhe. Riziki Pembe Juma mwishoni mwa wiki iliyopita wakati akifunga kikao cha pembeni (side Event) huko New York, Nchini Marekani katika ukumbi wa Umoja wa Mataifa.

Mhe Riziki amesema Serikali imefanya juhudi hiyo ili kuwezesha kila raia wa Tanzania kumudu faida sawa kutokana na fursa za manunuzi, hasa zile zinazohusiana na biashara ndogo ndogo zinazoendeshwa na kumilikiwa na wanawake.

Amefahamisha kwamba  jitihada hiyo inafanywa na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) na Mamlaka za Serikali za Mitaa (LGAs).



Alieleza Serikali yaTanzania inasisitiza matumizi ya mfumo wa kitaifa wa ununuzi wa kielektroniki ili kuweka mazingira mazuri ambayo pia yanaiwezesha Serikali kufuatilia idadi ya mikataba ya manunuzi inayotolewa kwa wanawake.

 

Pia alisema ili kuhakikisha wanawake wanawezeshwa na ujuzi mdogo wa lugha ya Kiingereza, Serikali inatayarisha na kuhakikisha nyaraka za zabuni zimeandikwa katika Lugha yetu ya Taifa (Kiswahili) ili ziweze kueleweka kwa urahisi na kunufaisha makundi maalum fursa za manunuzi.

 

Mhe Riziki alifahamisha kwamba, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeanza safari ya ubunifu wa kuendeleza Dira yake mpya ya Maendeleo 2050 itakayoendesha Ajenda ya Maendeleo ya Taifa kwa miaka 25 ijayo ili kuhakikisha maono yanafafanuliwa vyema na mienendo ya kijamii na kiuchumi pamoja na mitazamo ya kijinsia, itazingatiwa.

 


“Safari ya ubunifu wa kuendeleza Dira yake mpya ya Maendeleo 2050 itakayoendesha Ajenda ya Maendeleo ya Taifa kwa miaka 25 itasaidia usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake na wasichana katika mipango ya maendeleo ya kitaifa “ Alisema Pembe.

 

Aidha waziri huyo ametoa shukrani za pekee kwa Wizara, Idara na Wakala za Serikali, maafisa wa Umoja wa Mataifa, Taasisi za Utafiti na wadau wa elimu juu, sekta binafsi na vyombo vya habari kwa kufanikisha mkutano huo.

 

Mapema akifungua kikao hicho Mshauri wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan katika masuala ya Wanawake na Makundi Maalum Bi Sophia Mjema alisema Tanzania Bara na Zanzibar, imeandaa sera, mikakati, mipango, na programu kadhaa za kuwawezesha wanawake na wasichana  na kuhakikisha usawa wa kijinsia katika shughuli  mbali mbali.

 

Alielezea Sera ya Taifa ya Biashara ya mwaka  2003 imetaja haja ya "kuunga mkono ushirikishwaji wa wanawake katika michakato ya maendeleo ya biashara kupitia upatikanaji wa usawa zaidi wa mali za uzalishaji, hasa ardhi yenye hati miliki, miundombinu, fedha, elimu na ujuzi".

 

Pia, kuongeza mafunzo na kurekebisha taratibu za uendeshaji ili kuruhusu na kukuza matumizi ya mfumo wa manunuzi ya umma; kushughulikia vikwazo vya kifedha na upatikanaji wa taarifa za manunuzi ya umma.

 

Mkutano wa Hadhi ya Wanawake (CSW68) ulianza  tarehe 11 hadi 22 Machi 2024, New York nchini Marekani ambapo ya kikao cha pembeni kilikuwa na mada isemayo Kufadhili Usawa wa kijinsia: Kuwawezesha Wanawake na Wasichana Kupata Huduma za Umma na Kuendeleza Ahadi za Kizazi chenye Usawa nchini Tanzania.
 
Mwisho
 
 
 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch