Skip to main content

MKUTANO WA MDIPAO, WAZAA MRADI WA MAJI SAFI NA SALAMA MKOANI

 

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

‘’TUNA mwaka mmoja sasa, shida ya maji sisi wananchi wa kijiji cha Kinyasini wilaya ya Mkoani, tunaisikia kwenye vyombo vya habari,’’wanasema wananchi hao.

Nilipotaka kujua kulikoni, wananchi hawa wanaishi kwenye vivuli vya raha na burudani, hasa kupitia haki ya msingi ya huduma ya maji safi na salama, hawakuwa wachoyo kusema ukweli.

Rukia Ramadhan Bakari, akizungumza kwa shauku anasema, mkutano uliofanyika mwezi Febuari 2023, ulioitwisha na wasaidizi wa sheria wa wilaya ya Mkoani, ndio chanzo kikuu cha kuzaliwa kwa mradi huo.

Mkutano huo pamoja mambo mingine ya kisheria, wananchi na hasa wanawake, walielezea changamoto yao ya ukosefu wa uhakika wa huduma ya maji safi na salama.

‘’Tulielezea changamoto yetu ya ukosefu wa huduma hiyo, mbele ya wasaidizi wa sheria, na wao walituahidi kwamba changamoto hiyo wataifuatilia,’’anakumbushia.

Baada ya kimnya kirefu cha wiki tatu, waliitwa tena kupewa mrejesho na wasaidizi hao wa sheria, ingawa anasema wengi wao akiwemo yeye, hakuamini.

‘’Unaju dhiki tulionayo hapa kijiji cha Kinyasini wilaya ya Mkoani ya ukosefu wa huduma ya maji safi na salama, hatukuwa tukimuamini yeyote, na hata wao wengine tulishindwa kuamini,’’anasema.

Awena Nassor Ali, anasema muda sasa ukafika wa kuanza kuiyaga shida na dhiki ya maji, baada ya wasaidizi hao wa sheria kuwaleta kijijini kwao, wafadhili ya mradi wa uchimbaji kisima, ujenzi wa mnara wa tanki la kuhifadhi maji na usambaazaji pia.

‘’Lililonifurahisha leo na kusahau dhiki, ni kuona changamoto zetu zimefuatiliwa na kutekelezwa kwa vitendo, maana hadi mipira ya kusambaazia huduma hiyo, tumewekewa na wafadhili,’’anaeleza.

Kumbe wananchi wa kijiji cha Kinyasani, na hasa kundi kubwa la wanawake, ambao walikuwa wanategemea maji yanayozalishwa na kusambaazwa na Mamlaka ya Maji Zanzibar ‘ZAWA’ walikuwa wanaishi kwenye wingu, la kusaka maji.

‘’Sisi na watoto wetu, mpango wa kuamka saa 8:00 za usiku ilikuwa ni jambo la kawaida, kuifuata huduma ya maji, mabondeni umbali ya kilomita mbili hadi tatu,’’anafafanua.

Anakumbuka vyema, kuwa matumizi ya maji ya kutosha hawakuwa na nafasi hiyo, kwani visima walivyokuwa wakivitumia vilikuwa na ujazo mdogo wa chini ya lita 15,000 kwa saa.



Mradi huo uliobuliwa na wasaidizi wa sheria wilaya ya Mkoani, anasema umekuja kuzima na kuzika kabisa shida na dhiki waliokuwa nayo kwa muda mrefu, na sasa wanaishi kwa utulivu.

‘’Haki zote za kibinaadamu na kinyumba zimetulia kwa wananchi wa kijiji cha Kinyasani, kwani huduma ya maji, imerudi upya tena kwa kasi,’’anasema.

Mwanaisha Makama Haji, anaona sasa kila nyumba wananchi wanafua, kukoga na hata kumwagilia bustani kwa utulivu, kufuatia kilio chao kupata mnyamazishaji.

‘’Kama wasiaidizi wa sheria wote Tanzania, watakuwa na juhudi kama walizonazo hawa wa Mkoani, hakuna kijiji ambacho kitakuwa na shida ya mradi wa maendeleo, na ufumbuzi usipatikane,’’anasema.

Kwake anaona, mkutano huo ulizaa matunda mengine, lakini la kupatiwa ufumbuzi wa huduma ya maji safi na salama kwake, ni ndoto iliyopata jibu.

Ndio maana sasa, anatoa rai kwa wananchi wenzake, kwanza kuuenzi mradi huo, pamoja na kuuelea kwa nguvu zote, ili vizazi vijavyo, vifaidike nao.

Mwananchi Hamad Mzee Hamad nae wa Kinyasini anasema, kazi iliyofanywa na wasaidizi wa sheria, sasa kwake binafsi imemsaidia kupata utulivu na mpangilio mzuri wa maisha yake.

‘’Sasa unalala na kuamka kwa wakati uutakao, maana huduma ya maji safi na salama imo ndani ya nyumba yetu, maana wasadizi wa sheria, wametusaidia kupatikana kwa mfadhili,’’anafafanua.

Msaidizi fundi mkuu wa mradi huo, Khatib Issa Maalim, anasema wasaidizi wa sheria wa wilaya ya Mkoani, kupitia mradi huo, wamefanikiwa kupunguza makali kwa wananchi wa Kinyasini.





‘’Anakiri kuwa maji ya ‘ZAWA’ wakati mkubwa hukumbwa na changamoto zinazowakwaza wananchi, hivyo kupatikana kwa mradi huo, ni faraja kwao,’’anasema.

Hata hivyo anawashauri wasimamizi wa mradi huo, kuongeza idadi ya matenki ya kuhifadhi maji, ili kulisaidia tenki la sasa lenye uwezo wa kubeba lita 5000 pekee.

‘’Zuri zaidi lililomo ndani ya mradi huu, ni kwamba hata kama huduma ya umeme itazimika, wanaweza kufungua tanki lao na kupata huduma,’’anasema.

Mkurugenzi wa Jumuiya ya wasadizi wa sheria wilaya ya Mkoani ‘MDIPAO’, Nassor Hakim Haji, anasema mradi huo ulitokana na mkutano walioutisha kwa wananchi hao, na kisha kutaja changamoto yao hiyo.



‘’Kwa kushirikiana na wananchi, tulifanikiwa kuuibua mradi huu, baada ya wenyewe kukiri kuwa, changamoto kubwa ni kutokuwa na uhakika wa huduma ya maji safi na salama katika maisha yao,’’anaeleza.

Anakiri kuwa, baada ya kuundwa kamati na yeye kuwa mjumbe, kazi ya kuanza kumtafuta mfadhili ilipamba moto, na kisha kufanikiwa kuwapata, wanamkoani wanaoishi nje ya nchi.

‘’Baada ya kuwasiliana nao, walitaka mchanganuo wa gharama na kuwatumia, na baada ya wiki tatu, ujumbe wao ulifika na kuanza kazi ya uchimbaji kisima,’’anaeleza.

Kisima hicho, kina zalisha wastani wa lita 35,000 kwa saa, ambayo maji yake huvutwa kwa mashine, kutoka kisimani hadi kwenye tenki la lita 5000 kila siku, na kisha kusambaazwa kwa wananchi.

Mkurugenzi huyo anakiri kuwa, haikuwa kazi rahisi kupatikana kwa mradi huo, ambao wafadhili waligharamia hadi utandaazaji mipira midogo, iliyoingia nyumbani kwa wananchi.




‘’Hivi sasa nyumba 30 kati ya nyumba 52 zenye wakaazi wastani wa 210, wananufaika na mradi huu, kupitia awamu hii ya kwanza, ambapo awamu nyingine, itamalizia nyumba 22 zilizobakia na kufikia wananchi 450 kwa mradi wote,’’anasema.

Kwa sasa anasema mradi huo, unalelewa na kamati maalum, ambayo wasaidizi wa sheria ni wajumbe, na kukutana kila baada ya muda, ili kuelezea changamoto zao.

Mkurugenzi huyo, anasema wamejipanga vyema kwa kuanzisha mfuko maalum, kwa ajili kuulinda na kuimarisha mradi huo, ikiwemo michango kwa ajili ya umeme wa kusukumia maji, hadi kwenye tenki.

Afisa sheria kutoka Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Zanzibar ofisi ya Pemba, Bakari Omar Ali, anasema uibuaji wa miradi hiyo, ndio miongoni mwa mafanikio ya kuwepo kwa wasaidizi wa sheria Zanzibar.

Anasema, wapo wananchi waliokwisha kata tamaa, sio kwenye kufuatilia masuala ya haki zao za kisheria pekee, bali hata huduma za kijamii kama maji safi na salama.

‘’Kwa mfano, kuna hao wananchi wa kijiji cha Kinyasini, walikuwa na kilio cha ukosefu wa huduma ya maji safi na salama, lakini wapo wingine, wanalalamikia ukosefu wa vitambulisho vya mzanzibari mkaazi na vyeti vya kuzaliwa,’’anasema.

Hapa akawataka wongeze juhudi, ili kuhakikisha wanaibua changamoto nyingine, zilizowazungumka wananchi, ili kuondoa hisia za kuishi kwa matabaka.

Waziri wa Nchi Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Zanzibar, Haroun Ali Suleiman, akizungumza hivi karibuni, alisema, wasaidizi wa sheria wataendelea kuwekewa mazingira rafiki kila hali inaporuhusu.

‘’Kwanza, tutaendelea kufuatilia ahadi ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, ya kuwapatia usafiri wa bajaji kila jumuia,’’anafafanua.

‘’Hili litawapa hamasa na nguvu wasaidizi wa sheria, kwa kuendelea kuibua changamoto zinazowakwaza wananchi wa Unguja na Pemba.

Wakili Alphonce Gura, kutoka tasisi ya LSF anasema, ikiwa wasaidizi wa sheria watafanyakazi kwa bidii, manufaa yake kwa jamii hayachelewi kuonekena.

Mkuu wa wilaya ya Mkoani Khatib Juma Mjaja, anasema ‘MDIPAO’ ni moja ya jumuia za wasaidizi wa sheria, zinazofanyakazi zake, kwa hamu ya kutatua changamoto za wananchi.

                           Mwisho   

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch