Skip to main content

WAJUMBE BARAZA LA WAWAKILISHI WAJIFUNZA MAFUTA, GESI ASILIA MTWARA

 



 NA MWANDISHI MAALUM, @@@@

Wajumbe wa Kamati ya Bajeti ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar Wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mwanaasha Khamis Juma wamefanya ziara mkoani Mtwara ya kutembelea miradi ya gesi asilia kwa lengo la kujifunza. 

 

Wakiwa katika ziara hiyo ya siku Moja wametembelea visima mbalimbali ikiwemo miundombinu ya gesi  ya Mnazibay pamoja na kiwanda cha kuchakata gesi Madimba. 

 

Akizungumza mara baada ya kuwakaribisha Mkoani Mtwara Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mwanahamis  Munkunda amesema kuwa gesi asilia imekuwa chachu kwa maendeleo ya mikoa ya lindi, mtwara na Tanzania kwa ujumla.



 

Amesema uwepo wa gesi hiyo ni fursa kubwa ambayo watajifunza na wataiona jinsi inavyofanyakazi ambapo ndio malighafi inayotumika viwandani, majumbani na pia ni nishati inayotumika kuzalishia umeme. 

 

"Gesi kwetu ni fursa kubwa ambayo inatumika majumbaji, kwenye magari, viwandani na pia ni nishati muhiimu viwandani uwepo wa nishati hiyo umeongeza fursa nyingi za uwekezaji mkoani hapa nafasi tunazo na tunakaribisha wawekezaji wengi zaidi  mkoa huu ni kitovu cha uwekezaji naimani mtatembea na mtajione" amesema Munkunda 

 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mwanaasha Khamis Juma amesema kuwa wamefika mkoani hapa kujifunza katika sekta ya mafuta na gesi asilia.

"Tumekuja kujifunza kwenye miundombinu ya gesi asilia na sisi kwa sasa tunayo mamlaka inayosimamia gesi asilia tumefurahishwa na tumeona miundombinu ya kuzalisha na kuchakata gesi  sisi kama wawakilishi wa wananchi tunaenda kuishauri serikali ili sekta ya gesi iweze kuwa chanzo kizuri cha mapato"




 

Kwa upande wake Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Mkondo wa Juu Pura Mussa Ryoba Itumbo (Mjioligia) amesema kuwa ziara hii Ina lengo la kubadilishana uzoefu na Mamlaka ya Udhibiti wa Utafutiji wa Uchimbaji wa Mafuta na Gesi asilia Zanzibar-ZPRA ili kujifunza kujifunza zaidi. 

“Ziara hii ina lengo la kujifunza na kubadilishana uzoefu kwa pande zote mbili ambapo Tanzania bara tayari gesi ipo na tunauzoefu wakati Zanzibar wako kwenye utafiti ambapo tayari baadhi ya vitaru vimeshatangazwa kwaajili ya utafiti” amesema Itumbo

 

“Mpaka sasa tunayo gesi zaiidi ya futi za ujazo 57 jitihada kubwa zinafanywa na serikali ili kuhakikisha kuwa gesi iliyopo kwenye kina kirefu chini ya bahari inafikiwa na kuanza kutumika kwkauwa ndio eneo pekee lenye kiwango kikubwa cha gesi asilia” amesema Itumbo

 

Mkurugenzi wa Mwendeshaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Utafutiji wa Uchimbaji wa Mafuta na Gesi asilia Zanzibar Adam Abdulla Makame  amesema kuwa kwa sasa wamejipanga kuboresha sheria kwa upande wa mafuta na gesi asilia pamoja na mikataba ya utafutaji wa mafuta na gesi asilia ili kuhakikisha kuwa wanavutia wawekezaji.

“Tumeshaanza kutangaza baadhi ya vitalu ambapo mapkaa sasa kimoja cha pemba mnazi tayari kina mwekezaji na vingine jitihada kubwa zinafanyika ili kuweza kuwapata na kuanza utafuti wa mafuta na gesi asili” amesema Makame.






Nae Yusuph Hassan Idd(Masharubu) mwakilishi  wa jimbo la Fuoni ambaye ni mjumbe wa kamati ya bajeti amesema kuwa wamekuja kutembelea mahali ambapo gesi asilia inazalishwa na kuchakatwa ili  kuona shughuli mbalimbali zinazofanyika katika matumizi ya gesi asilia ambayo kwa kiasi kikubwa yanananyua uchumi wa taifa.

Kikubwa kilichonifurahisha ni kuwa gesi asilia inatumika kwa wingi mtwara hizi ni fursa kuwa ambazo na sisi Zanzibar tunatamani kuwa nazo ili tuweze kutumia kama umeme na pia kwenye magari, viwandani”

nae Rukia Omary Ramadhan Mwakilishi wa Jimbo la Amani Zanzibar amesema kuwa gesi asilia tunaiona ina faida kubwa na pia ina kuza uchumi pamoja na kupunguza gharama nyingi ikiwemo  za kupika kwa wanawake ambapo itapugnuza matumizi ya mafuta kwenye magari.

“Serikali  imefanyakazi kubwa niipongeze tumekuja kujifunza lakiani pia sasa tumefungua milango ya wawekezaji kwaajili ya uchimbaji wa gesi asilia kwakeli naona mafuta na gesi asilia ni fursa nzuri tukiwa na uchumi wa juu itatusaidia na kutunyanyua kiuchumi kama nchi” amesema Ramadhan

MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch