Skip to main content

HATA HILI LA KUWASINDIKIZA WENZA KLINIKI WANAUME WANASUBIRI WATUNGIWE SHERIA?

 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

INGAWA kwa karne moja iliyopita, suala la wanaume kuhimizwa kuwasindikiza wenzao wao kliniki, halikuwa likisikika, na inawezekana ni kwa sababu ya afya zilivyokuwa za wajawazito hao.

Maana tunaelezwa na kusifiwa kuwa, wajawazito wa enzi hizo za mababu na mabibi, walikuwa ‘fiti’ afya zao, hali iliyopelekea, hata siku moja kabla ya kujifungua, alikuwa anakwenda shambani kulima.

Na ukweli unabakia pale pale kuwa, hata kwa wakati huo vyakula vyenye siha, rutba, damu na kuongeza nguvu kwa wajawazito, vilikuwa bwerere.

Kwa miaka hii ya sasa, afya za wajawazito walio wengi na hasa ikiwemo ukosefu wa damu, ndio habari ya mjini, na ndio maana sasa wanaume wakatakiwa wawasindikize wenzao wao, kliniki.

Tena, kwani ni kila siku, hapana walau kwa wiki ya kwanza ya kuripoti kliniki, ili sasa zile changamoto anazokabiliana nazo, na yule mwenza apate kuzijua, ingawa wapo waliowasugu.

Hapa wacha niwaulize wale wasugu wa kusindikiza wenzao wao, hilo kwao ni zito, au wanasubiri hadi itungwe sheria na kanuni ndio watekeleze?

Mbona ni jambo jema, wanalohimiza wataalamu wa afya, tena bahati nzuri, mwanamme anaemsindikiza mwenza wake, hata kwenye msusuru yeye hakai.

Hili je ni dogo, sasa hapa wewe mwanamme unakwamishwa na nini, hata ushindwe kumsindikiza mwenza wako kliniki?

Naendelea kusema kuwa, wataalamu wanavyowapenda wanaume, huwataka kufanya hivyo kwa walau siku moja tu, tena pale tu mwanamke anapojigundua na ujauzito, sasa wapi wanakwama?

Au ndio wanaume hawa ili kuwasindikiza wenzao wao wanasubiri wizara ya Afya itunge kanuni, sheria na sera juu ya jambo hili?

Mbona kama vile ni jambo la kawaida, na pia ndio kunogesha upendo wenu, na hasa ikizingatiwa kuwa, kilichomo tumboni ni mali yenu pamoja.

Kwani unadhani ukifika huko kliniki kuna jambo kubwa, hapana ni kuelezwa maendeleo ya mtoto wenu mtarajiwa, kazi zipi afanye mjamzito huyo, chakula gani atumie na namna ya kuishi nae kwa kipindi cha ujauzito wake.

Kama ulionesha mahaba, mapenzi, utulivu, upendo na masikilizano wakati wa kuitafuta mimba hiyo, sasa iweje ushindwe kumsindikiza kliniki?

Si dhani kuwa jambo hilo, lazima wanaume wasubiri utungwaji wa sheria na kanuni, eti ndio sasa hapo waanze kuwasindikiza wenzao wao kliniki.

Hivyo wewe mwanamme, husijiskii faraja na furaha unapomsindikiza mwenza wako kliniki, na kisha mtaalamu wa afya ya uzazi, akakwambia kuwa mtoto wenu uko na afya nzuri.

Au hupati furaha, mtaalamu huyo akakuelezea njia na namna bora ya kumuendeo mwenza wako huyo, hasa kipindi cha ujauzito wake.

Maana, haya na mengine, ndio maendeleo yanayotolewa huko kiliniki, ambako wewe unasubiri hadi utungiwe sheria, pengine ndio utekeleze.

Kwa hakika haipendezi, kuona kila siku mwanamke anaharibu ujauzito wake, na pengine sababu ikiwa ni utendaji wa kazi kupitiliza, ukosefu wa damu au kuendewa kinyama na mwenza wake, ikiwemo kulaliwa tumboni.

Yote kwa yote, wanaume ambao hamjaamka, msisubiri kutungwa na sheria wala sera, ya kuwataka kuwasikindikiza wenza wenu kliniki, bali sasa iwe ndio utamaduni wa lazima.

Wajawazito endeleeni kuwapa darsa wenza wenu, waliowapa ujauzito kuhakikisha wanaambatana na nyinyi hadi kliniki, ili wajue maendeleo ya mtoto wenu mtarajiwa.

Viongozi wa dini na asasi za kirai kama vile TAMWA, TGNP endeleeni kuwaelimisha wanaume, kuwa mimba ni ya jamii, ila mtoto amehifadhiwa na mtu mmoja tumboni mwake.

                         Mwisho  

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch