Skip to main content

WANANCHI KIJIJI CHA MNAZI MMOJA, KWA MBURI MAKAANI WAFURAHIA KUPATA UMEME

 





HABIBA ZARALI KU@@@PEMBA
NISHATI  ya umeme imekuwa ni mkombozi kwa wakulima kwani kunawawezesha kulima kilimo cha uhakika wakati wowote na aina yoyote.
Kauli hiyo ilitolewa na mkulima wa mbogamboga na matunda Mohamed Abdalla Khamis huko Vitongoji Makaani Wilaya ya Chake Chake alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi.
Mkulima huyo mwenye shamba lenye ukubwa wa ekari saba alisema  kabla ya kupata nishati ya umeme aliyopelekewa kupitia juhudi za mradi wa Swil alikuwa hana uhakika wa kilimo chake licha ya kwamba alikitegemea  kwa ajili ya kujiongezea kipato.
Alielekeza kuwa kupitia mradi huo ameweza kupiga hatuwa moja kwenda nyengine kutokana na uhakika wa kilimo kwa vile umeme utamsaidia kuweza kupata maji  ya kumwagilia katika mashamba yake.


Alifahamisha wananchi wengi wamejikita katika kilimo hususan cha mbogamboga lakini wamekuwa wakikata tamaa kutokana na kukosekana kwa huduma ya umeme ambayo huwakosesha fursa ya kupata maji kwa ajili ya kumwagilia màhamba.
"Kilimo bila maji ya uhakika ni kubahatisha na maji ya uhakika huwezi kuyapata bila ya umeme kwa maana hiyo basi mimi sasa nna uhakika wa kilimo changu Kwa vile tayari umeme nimeshapata", alisema.
Akizungumza suala la soko mkulima huyo alisema soko la ndani la  mbogamboga kwa sasaivi inaonekana kukuwa lakini ingawaje kunahitajika mbinu mbadala ya kuweza kusarifu mboga hizo na kuweza kuziuza katika soko la nje.
Kuhusu changamoto inayowakabili kipindi kirefu sasa ni kuwepo kwa joto ambalo linasababisha baadhi ya mboga mboga kutokuzaa na nyengine kufa kabisa pamoja na mabwana shamba kutowatembelea wakulima Kwa muda mrefu jambo ambalo ni tatizo.
"Kama izi tungule kipindi cha nyuma hazitoi kutokana na  juwa kali , migomba nayo  haizai sasa tazama huku ikiwa huna umeme ambao utaweza kupata maji ya uhakika unadhani kilimo kitaimarika apo",alisema.
Alifahamisha kuwa maji kupitia Mamlaka ya maji ZAWA hayawezi kutosheleza Kwa umwagiliaji asipokuwa wamwagilie kutoka katika visima ambapo bila ya umeme huwezi kufanikisha.
Nae mkulima Hamad Smail Faki alisema  ni jambo moja la faraja kuona mradi wa swil kupitia TAMWA na PEGAO umelipigia mbio suala la umeme na hadi sasa wakaweza kupata.



Alisema anaamini kuwepo kwa umeme huo ni chachu ya kuleta mabadiliko ya kilimo kwani watazalisha na kupata kipato na hatimae kuondokana na umaskini .
"Tulikuwa tuna kilio Kwa muda mrefu lakini sasa kimenyamazika tunaahidi kufanya vizuri kama lengo lililokusudiwa,alisema.
Nae Salma Ali mwalimu ambae anajishughulisha na kilimo hicho alisema baada ya kupata maji kupitia umeme huo tayari ameshapanda mbogamboga ikiwemo michicha, mitungule na hata matunda yanayoingiza damu kwa maarufu mikarakadee.
Ujasiri wa kupanda mbogamboga umekuja baada ya huu umeme tulioupata kupitia mradi wa swil maana mashamba tulikushayaacha hayo kwa vile ata tukilima hamna faida mimea hufa",alisema.
"Pamoja na umeme huo  kuwasaidia wakulima hata sisi  ambao tunajishugjulisha na biashara pia ni mkombozi wetu alisema Khamis Shaame Makame na Juma Khamis Mwalim.
Alielekeza kuwa wake zao majumbani sasa wanaweza kutengeneza malai wakauza na kujipatia kijipato cha kujiendeshea na kuepuka utegemezi mkubwa .


"Awa wanawake wanahitaji kuwa na shughuli japo ndogo ndogo za kufanya wakajiingizia kipato sio kukaa tu na kusubiria kuletewa lakini wakati mwengine ndo wanarudi nyuma Kwa kukosa nyenzo muhimu ila sasaivi kwa kweli tumefarijika kupata umeme tumekomboka",alisema.
Hivyo waliyaomba mashirika na taasisi mbalimbali kuiga mfano huo wa Tamwa na Pegao wa kusaidia jamii katika masuala ya kujiletea kipato na kuondokana na dhiki katika maisha yao.
MWISHO 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch