Skip to main content

TUMIENI MATOKEO YA SENSA KUFANYA UTAFITI-BALOZI HAMZA

 




IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA

WALIMU na wanafunzi wa vyuo vikuu kisiwani Pemba wametakiwa kuyatumia matokeo ya sensa katika kufanya shughuli za utafiti, ili kuwarahisishia katika kazi zao za kimasomo na kufundishia.

Akifungua kikao cha usambazaji wa matumizi ya matokeo ya viashiria vya sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 kwa wanafunzi na walimu wa vyuo vikuu kisiwani hapa, Kamisaa wa Sensa Zanzibar Balozi Mohamed Haji Hamza alisema, takwimu za matokeo ya sensa zitawarahisishia kufanya utafiti wa haraka.

Alisema kuwa, ni vyema sensa ikatumika kwa ajili ya kufanya utafiti wa baadae kutokana na matokeo yaliyopatikana, hivyo ipo haja kila wanapofanya utafiti kutumia takwimu hizo kwa maendeleo yao na taifa kwa ujumla.

‘’Sensa ina vitu vingi sana tunavyoweza kuvitumia katika mambo yetu mbali mbali, ikiwemo ya kiutafiti, hivyo tuzitumie takwimu hizi za sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 kwa ajili ya kazi zetu,’’ alisema Balozi huyo.

Aidha aliwahamasisha walimu na wanafunzi hao kuelimisha jamii ili ihamasike kuyatumia matokeo ya sensa kufanya utafiti na vitu vyengine vya kimaendeleo, kwani bila ya takwimu utafiti hauwezi kuwa wa kiwango kizuri.



Kwa upande wake Mtakwimu Mkuu wa Serikali Salum Kassim Ali alisema kuwa, kawaida wanafunzi wanatumia tafiti kwa ajili ya mazoezi (field) katika vyuo vyao, hivyo aliwashauri walimu kuwahamasisha wanafunzi wao kutumia sekondari data kwani ni rahisi.

‘’Tumewaita hapa kuwafahamisha kwamba mnapopewa kazi za utafiti kule vyuoni basi mjitahidi kutumia takwimu ambazo zimepatikana kutokana na matokeo ya sensa, hivyo zitakuwa na thamani na wengine pia watatumia,’’ alieleza.

Akiwasilisha mada katika kikao hicho, Meneja Viwango na Utafiti Zanzibar Hamisa Suleiman alifahamisha kuwa, data zote za hatua ya sekondari zitapatikana kwa kufuata utaratibu unaotakiwa, hivyo ni vyema kwanza kupata kibali ambacho kinahitaji kulipiwa.



‘’Tufuate utaratibu mzuri wakati wa kufanya tafiti zetu na sisi tunaangalia data hizo unazitaka kwa lengo gani, ikiwa utafiti huo una maslahi na nchi yetu kwa maendeleo basi tunakupatia,’’, alisema Meneja huyo.

Nae Mwenyekiti wa sensa Balozi Amina Salim Ali alisema, matokeo ya sensa ni muhimu kwa kufanya tafiti mbali mbali, kwani kuna takwimu ambazo zitawasaidia katika masomo yao.

Kwa upande wao washiriki wa mkutano huo walisema, baada ya kuwasilishwa matokeo hayo ya sensa walibaini kwamba, viashiria vingi vya hatari vinatoka Mkoa wa Kaskazini Pemba, hali ambayo imewapa wasiwasi, hivyo kunahitajika utafiti wa hali ya juu kuweza kujua tatizo.



Mkutano huo wa siku moja umefanyika katika ukumbi wa ZRA Gombani Chake Chake ambao umeandaliwa na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar kwa lengo la kuihamasisha jamii kutumia matokeo ya sensa kufanya mambo yao ya kimaendeleo.

                                                     MWISHO.                                                              

                                                              

                                

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch