Skip to main content

WAZAZI WATAKIWA KUSHIRIKIANA KUDHIBITI UTORO MASOMONI

 



IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@

WAZAZI na walezi wametakiwa kushirikiana pamoja na walimu, kamati ya skuli na kamati ya shehia katika kuhakikisha wanadhibiti utoro kwa wanafunzi, jambo ambalo litasaidia kunyanyua viwango vya ufaulu.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, wananchi wa shehia ya Mjiniole Wilaya ya Chajke Chake walisema, kuna baadhi ya wazazi huchangia watoto wao kuwa watoro kutokana na kuwa anapokaa nyumbani hamuulizi jambo lolote.

Walisema kuwa, ushirikiano wa dhati unahitajika katika kudhibiti utoro maskulini kwa lengo la kustawisha maendeleo ya mtoto kielimu, jambo ambalo litasaidia kusoma na kufaulu vizuri kwenye mitihani yake.

Mwananchi Fatma Ali Hamad mkaazi wa kijiji cha Simaongwe alisema kuwa, ni vyema kwa wazazi kuwa tayari kuwashughulikia watoto ili wapate elimu ambayo itawasaidia katika maisha yao yote.

Kwa upande wake mwananchi Hamad Khatib Hamad alieleza kuwa, ingekuwa wazazi wana mashirikiano kama ilivyokuwa zamani basi suala la utoro lisingekuwepo na watoto wangekwenda skuli kupata elimu.

‘’Zamani nilikuwa nikimkuta mtoto anazurura nampeleka skuli na bakora mbili nampiga, siku ya pili hasubiri kuambiwa, lakini mtoto wa leo ukimuuliza tu hujaenda skuli au madrasa kwa nini, mzazi wake anakujia juu na kukuambia kwani unampa kula yako huyu? Kwa kweli hatuendelei,’’ alieleza baba huyo.

Nae Hadia Ali Hamad alieleza kuwa, ipo haja ya kuwa na mikakati maalumu pamoja na sheria ndogo ndogo katika shehia yao, ili mtoto akionekana anazurura wakati wa skuli au madrasa apelekwe kwa lazima na endapo mzazi wake atakaidi basi achukuliwe hatua.

‘’Tutakapofanya hivi itasaidia sana watoto kupata elimu na kuziondoa familia katika dimbwi la umasikini, kwa sababu ikiwa huna elimu unakuwa na umasikini wa mawazo, kifikra na umasikini wa kipato, hivyo unakosa fursa za kujiendeleza kimaisha,’’ alifafanua mama huyo.

Mratibu wa wanawake na watoto shehia hiyo Khadija Henock Maziku alisema, utoro katika shehia yao upo kwa kiasi kikubwa kutokana na kuwa wazazi kutokuwashughulikia watoto wao na wanapoambiwa wanakuwa wakali.

Alifahamisha kuwa, iwapo watoto wataendelea kutoroka skuli na madrasa, shehia yao itakuwa haina maendeleo kwa sababu watajiingiza katika makundi ya wizi, utumiaji wa madawa ya kulevya na kujiingiza kwenye ajira za kukata matofali na kuchimba mawe.

Sheha wa shehia hiyo Hamad Said Mgau alisema kuwa, wameunda kamati wa skuli na wamekuwa wakilizungumzia kwa kila suala la utoro na namna ya kulidhibiti, ambapo kwa hatua ya mwanzo wamewaomba walimu wakuu kuwapa majina ya wanafunzi wote watoro ili kuwafuata majumbani mwao.

Mwalimu Mkuu wa skuli ya Sekondari Kangagani Omar Kombo Hamad alisema, skuli hiyo inachukua wanafunzi wa shehia ya Mjiniole na Kangagani ambapo baadhi yao wamekuwa watoro sana licha ya kuwapa adhabu ya bakora na adhabu mbadala.

‘’Tunawapiga bakora mbili au tunawapa adhabu mbadala lakini bado hali ni mbaya, ila utoro zaidi unachangiwa na wazazi kwa sababu anamuona mtoto wake amekaa nyumbani hamuulizi na wala sisi hapewi taarifa kwamba ana dharura au la,’’ alieleza mwalimu huyo.

Afisa Mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba Mohamed Nassor Salim alisema, Wizara ina mikakati mbali mbali kuhakikisha wanadhibiti utoro kwa wanafunzi ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa kampeni maalumu ya kuwarudisha wanafunzi watoro skuli, ambapo kwa sasa wameshawarudisha wanafunzi elfu 31,000 kati ya 35,000 waliokuwa nao kwa Unguja na Pemba.

Aidha alisema kuwa, mkakati mwengine ni kuongeza madarasa na matundu ya vyoo kwa sababu wakati mwengine watoto wanapokwenda vichakani kujisaidia hawarudi tena skuli, ambapo kwa sasa wanatarajia kuongeza matundu 60 katika skuli mbali mbali kisiwani Pemba.

‘’Pia tunaajiri walimu ili waweze kuwazibiti wanafunzi, kwa sababu wanapokuwa wachache wanashindwa kuwadhibiti watoto na hatimae wanakuwa watoro, mwaka jana tumeajiri walimu 1,444 na mwaka huu tunataraji kuajiri walimu wasiopungua 400, pia tunashirikiana na OCD kuhakikisha tunadhibiti hali hii,’’ alifafanua.

Afisa Mdhamini huyo aliwataka wazazi kushirikiana pamoja na Serikali katika suala la kumpatia mtoto elimu, kwani ndio urithi pekee utakaodumu na kumletea maendeleo katika maisha yake ya baadae.

                                                          MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch