Skip to main content

IWEJE UVUNJIKA NDOA IWE MACHUNGU, MAUMIVU KWA WATOTO, WENGI WAELEMEWA NA MZIGO WA MTUNZO

 



NA FATMA HAMAD, PEMBA

……………..SIRI ya mtungi aijuaye ni kata………

……Wahenga wengine wakasema hasira hasara…...

Misemo yote hii inasadifu mno pale ndoa inapovunjika baada ya wana ndoa kuamua lipasuke tugawane mbao.

Ingawa misumari ya hizo mbao, huwachoma na kuwaumiza wengi, wakiwemo wana familia na hasa watoto wao.

Mara nyingi pale wazazi wakiwa wametengana, baada ya ndoa kuvunjika watoto hukosa huduma muhimu za maisha na kuathirika kimwili na kiakili.

Mwana harakati maarufu wa kulinda na kutetea haki za watoto kisiwani Pemba,Tatu Abdala Msellem, mara kwa mara amekuwa akitoa tanbihi kuwa, kuvunjika kwa ndoa isiwe sababu ya kila mzazi kufumbia macho wajibu wake wa malezi ya watoto.

Hii ni kwa sababu, mtoto  anapokosa huduma za lazima sio tu huwa mnyonge na kujiona kama yatima, bali huwa hana furaha anapocheza, na akili yake huwa haifuatilii vizuri masomo.

‘’Kama ndoa imevunjika, kwanini watoto waingizwe katika shida wakati wao sio walioingia kwenye mkataba wa ndoa, wala kupelekea wazazi watenngane,’’anahoji.

Sheihk Said Ahmad Mohmed kutoka Ofisi ya Mufti kisiwani Pemba, aliwataka wanaume wasimame kwenye nafsi zao, watulize akili zao na inapobidi ndoa kuparaganyika, basi waelewe bado wanayo dhima ya kuhakikisha watoto wanapata huduma zote muhimu.

’Ndoa ikifikia mwisho wake kwa kuvunjika ,sio kuvunjika kwa wajibu wa kulea na kuhudumia watoto, kwa mke huduma zinapaswa kuendelea mpaka inapomalizika eda, lakini kwa watoto lazima ziendelee kwa ukamilifu,’’ anafafanua.

Rashid Said Nassor, Afisa Hifadhi ya Watoto Wilaya ya Chake chake anashangaa kuona inapovunjika ndoa, wathirika wakubwa wawe watoto wakati wao hawakuhusika na kutengana kwa hao wana ndoa?

WATOTO WANASEMAJEE

Mwanafunzi mmoja wa darasa la kwanza wa Skuli ya Kangagani, nilimkuta akiwa kwao nyumbani kwa takriban wiki mbili akiwa amepiga  kambi kwenye eneo la uvunjaji  wa kokoto bila ya kuhudhuria masomoni.

Akinieleza kilichomsibu kuwa, amelazimika kufanya kazi hio ya sulubu, ili ajipatie mahitaji ya shuleni  na nyumbani kwao, baada ya baba yao kutowajali kimaisha na kisha kuingizwa kwenye dimbwi la utelekezaji.

‘’Kwa sasa nabanja kokoto, ili kujipatia vifaa vya skuli, kama viatu na sare, kwani mama yangu hapatiwi huduma na baba yangu’’, anasema.

Mtoto huyu anaeleza kuwa, sasa ni mwaka  wa  saba  hajaitia machoni sura ya baba yake, na amekuwa akisikia tu habari zake kutoka kwa mama yake, lakin hamjui kwa sura.

‘’Nasikia baba yangu anaishi Unguja, lakini sijawahi kumuona wala kupata huduma yake yoyote, tena kwa wadogo zake, (baba mdogo na mkuu),’’anasimulilia.

Kwa hivyo ikifika karibu na kipindi cha sikukuu za kiimani, huenda kubanja kokoto kwa ajili ya kujinunulia nguo n ahata kumsaidia mama yake chakula,’’analeza.

Mtoto Juma mwenye umri wa miaka [15] mkaazi wa Mjini Wingwi (hilo sio  jina lake halisi), anaefanya kazi ya uvuvi wa samaki, amesema baba yao amewatelekeza takriban kwa miaka minane sasa na   hawaulizi cha asubuhi wala cha jioni.

‘’Nimejingiza kwenye shughuli hizi za uvuvi, ili nipate fedha kwa ajili ya matumizi ya nyumbani kwetu na mimi binafsi,’’anasema.

Ali Khamis Kombo mwenye umri wa [15] mkazi wa kijiji cha Mijini Kiuyu aliacha kusoma na kufanya shughuli ndogo ndogo za kibiashara, kwa ajili ya kumsaidia mama yake, baada ya kubaina baba yake hana mpango nao.



‘’Nyumbani tuko watoto sita (9), na mama hana kazi yoyote, hivyo nafanya kazi ili niendeshe familia yangu baada ya baba kutupa kisogo cha kutuhudumia,’’anafafanua.

WAZAZI WANASEMAJE

Asha Ali, mkaazi wa Mjini Kiuyu Wete Pemba, mwenye watoto tisa anasema, huduma zote anajitegemea, ingawa bado yuko kwenye ndoa ya mume alieongeza mke wa pili hivi karibuni.

 ‘’Sio kama naona raha mwanangu kufanya biashara, lakini nitafanyaje sasa, sina budi ila kumtaka anisaidie kimaisha na anafanya hivyo,’’anassimulia.

Bikombo Khamis mkaazi wa mjini Wingwi anaeleza kuwa, mume wake aliondoka kwenda uvuvini [dago ] Dar es- Saalam karibu miaka minane sasa iliopita, na hurudi wakati wa  mwezi mtukufu wa Ramadhani pekee.



 ‘’Ameniachia watoto  wanane [8] na huenda pwani na  watoto wangu  kupanda mwani,  ili tupate pesa za kujinunulia mahitaji, mana baba yao amenitelekeza,’’anafahamisha.

Mratibu wa wanawake na watoto wa Shehia ya Kangagani, Awena Salim Kombo, anaesema wanawake wengi walioachiwa mzigo wa ulezi peke yao, huwauzisha biashara watoto wao, ili wapate chakula.

‘’Ukimuuliza mama kwa nini hawa watoto hawaendi skuli na madarassa na badala yake wanatembeza biashara, anakwambia afanye nini na hana uwezo wa kuwahudumia,’’anaeleza.

SHERIA MBALI MBALI

Sheria ya Ajira na Mahusiano Kazini nambari 8 ya mwaka 2005 inakataza mtoto mwenye umri wa chini ya miaka 14, kuajiriwa na kukataza ajira kwa watoto wa chini ya miaka 18, katika maeneo ya migodi, viwanda, ubaharia katika meli au kazi nyingine yeyote inayotambulika kuwa hatarishi.

Hata hivyo, sheria inaruhusu ajira kwa watoto wa miaka 14 katika kazi nyepesi, ambazo sio hatarishi kwa afya yake, lakini haiathiri mahudhurio ya watoto masomoni.

WANAHARAKATI WANASEMAJE

Semeni Ali Khamis, mwanaharakati kutoka Jumuiya ya Wanawake katika wilaya ya Micheweni, anaeleza kuwa watoto wengi wanaojiajiri ni wale ambao kuwa hawapati matunzo, kutoka kwa wazazi wao.

‘’Katika kijiji cha Konde baadhi ya wanaume hujiingiza kwenye masuala ya ulevi tu, hawana habari ya kushughulikia familia zao,’’analeza.



Fat-hiya Mussa Said Mratibu wa Chama cha Wandishi wa habari wanawake Tanzania [TAMWA] ofisi ya Pemba, anasema anapoachwa mwanamke anaachwa na watoto wote kihuduma, hivyo shida na dhiki  zinawakumba zaidi watoto.

‘’Utawakuta watoto muda wa kuwepo masomoni wamebebeshwa mabakuli ya Mchicha, chaza, kwa ajili ya kutembeza mitaani, jambo ambalo linasababisha kufanyiwa udhalilishaji hapo baadae,’’ anasema.

OFISI YA MUFTI

Afisa kutoka Ofisi ya Mufti iliopo Pemba, Abdalla Muhamed Abdalla, anasema utelekezaji wa wanawake unachangia kwa kiasi kikubwa watoto kujiingiza katika ajira.

Kwa bahati mbaya, siku hizi kumekuwa na ongezeko la talaka ambapo kwa kipindi  cha Juni  hadi Agosti mwaka 2023,  kupitia ofisi ya Mufti wamepokea maombi 18 ya talaka, na malalamiko tisa (9) ya utelekezaji wa familia.

Alisisitiza ni vyema watoto, wakapatiwa huduma muhimu na malezi ya familia ili wakuwe vizuri kwa faida ya taifa kwa ujumla.

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu wa Jamuhuri ya Mungano wa Tanzania, Patrobas Katambi, amesema  serikali haitavumilia kuona watoto wanakosa haki zao za msingi .

‘’Ni kosa kuajiri watoto kinyume na sheria inavyosema na adhabu inatolewa chini ya kifungu cha 102 (2) ambacho kinampa Hakimu kutoa adhabu sawa na faini isiyozidi shilingi milioni 5 au kifungo cha mwaka mmoja au vyote,’’ anafafanua.

Kwa mujibu wa takwimu  kuna watoto milioni 152 wanatumikishwa duniani hivi sasa na kati yao 25,803 ( asilimia 5.6) wapo katika ajira  Zanzibar.

 

Hali hii imebainishwa katika taarifa ya Waziri wa Nchi, Afisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji, Mudrik Ramadhan Soraga, katika maadhimisho ya Siku ya Kupambana na Ajira za watoto mjini Zanzibar.

 

Siku hii huadhimishwa rasmi kila ifikapo Juni 12 ya kila mwaka.

 

KITENGO CHA HIFADHI YA MTOTO

Kwa mujibu wa takwimu za kitengo cha hifadhi ya mtoto Pemba katika wilaya ya Micheweni kwa mwaka 2022, malalamiko yalioripotiwa ya utelekezwaji wa wanawake ni 71, ambapo yamehusisha watoto 185, wanawake 92 na wanaume  93.

Kuanzia mwezi  Januari hadi Agosti mwaka 2023 malalamiko yaliyopokelwa ni 28,watoto walioripotiwa kutelekezwa ni 84 ( wanaume ni  49 na wanawake 35).



Shirika la Kazi Duniani (ILO) linakadiria kuwepo watoto  152 milioni  katika ajira duniani na kati yao  73  milioni wamo  katika kazi ambazo ni hatari.

Karibu asilimia 70 ya ajira  hizi za watoto ni katika  kilimo na sababu kubwa ni kutokana na umasikini na ugumu wa wazazi kupata ajira zenye hadhi.

Sheria ya Elimu Zanzibar ya 1982, kifungu cha 20, cha sheria hiyo kinamtaka kila mzazi kuhakikisha anampatia mtoto wake elimu ya lazima, pale anapofikia umri wa miaka saba.

Katiba ya Zanzibar ya 1984, inaeleza wazi katika kifungu cha 15[1] kuwa kila mtu ana stahili kuheshimiwa na kupata hifadhi kwa nafasi yake, maisha yake binafsi naya nyumbani kwake, na pia heshima na hifadhi ya maskani yake na mawasiliano yake.

Nacho kifungu cha 12[1] kikasisitiza kuwa, watu wote ni sawa mbele ya sharia, na wanayo haki, bila ya ubaguzi wowote, kulindwa na kupata haki sawa mbele ya sheria.

MIKATABA

Kwa mujibu wa Mkataba wa Afrika wa Haki na Ustawi wa Mtoto wa mwaka 1999, Ibara ya15, kinafafanua kuwa, mtoto ana haki ya kulindwa dhidi ya kazi au ajira zitakazoathiri afya, elimu na maendeleo yake.

Serikali inatakiwa kuweka sheria za kima cha chini cha mshahara, muda wa  kufanya kazi, mazingira ya kazi na adhabu kwa wasio tekeleza haki hii.

Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Mtoto wa mwaka 1989 ibara ya 32, kinaeleza mtoto ana haki ya kulindwa dhidi ya kazi au ajira zitakazoathiri afya au elimu yake.

                  Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch