Skip to main content

ZSTC LAKABIDHI VIFAA VYA UOTESHAJI MICHE YA MIKARAFUU





NA HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@

SHIRIKA la Biashara la Taifa Zanzibar (ZSTC) limekabidhi vifaa vyenye thamani ya shilingi 53,900,000 kwa ajili ya kusaidia uoteshaji wa miche ya mikarafuu  kwa wizara ya kilimo na baadhi ya wakulima kisiwani Pemba.

Vifaa hivyo vilivyokabidhiwa ni pamoja vyandarua vya kivuli 35, roli ya vifuko vya kuatikia miche kilogramu 3100 pamoja na fedha taslimu shilingi milioni mbili kwa ajili ya ununuzi wa matende ya mikarafuu.

Akizungumza kwa nyakati tofauti wakati wa makabidhiano hayo, Mkurugenzi wa Mfuko wa Karafuu wa Shirika la ZSTC Ali Suleiman Mussa kwa niaba ya Mkurugenzi Mwezeshaji wa shirika hilo alisema  vifaa hivyo vitasaidia upatikanaji wa miche ya mikarafuu kwa wingi na kuondowa usumbufu kwa wakulima.

Alifahamisha kuwa shirika la ZSTC linathamini na kuwajali sana wakulima wa zao la karafuu kutokana na umuhimu wao wa kulikuza  zao hilo  ambalo ni tegemeo katika kukuza uchumi wa taifa.

Alieleza kuwa shirika hilo litaendelea na jitihada zake zote kuhakikisha linawainuwa wakulima hao ili waweze kupata nguvu zaidi wa kuliendeleza na kuinuwa kipato cha wananchi na nchi yao kwa ujumla.



"Vifaa hivi hatukuvielekeza kwa wizara ya kilimo pekee bali tumewaangalia na wakulima wetu  ili nao waweze kuatika miche hii kwa wingi na kuondokana na  matatizo yasiyo ya lazima wanapohitaji miche ",alisema.

Mapema akipokea msaada huo Mkuu wa Idara ya Kilimo Pemba Asha Omar Ali kwa niaba ya Ofisa Mdhamini wa wizara ya Kilimo Pemba, alisema vifaa hivyo vitawasaidia sana katika shughuli zao za uoteshaji wa miche kwani baadhi ya vifaa vyao ikiwemo vyandarua vilikuwa vimeshachakaa


Aidha Mkuu huyo alibainisha kuwa, changamoto kubwa waliyonayo ni uhaba wa mabwana shamba, hivyo aliwataka wakulima kuendelea kuwatumia mabwana shamba waliopo mpaka pale tatizo hilo litakapotatuliwa.




Akizungumzia suala la ugawaji wa miche ya mikarafuu kwa wakulima, Afisa huyo alieleza kuwa hivi sasa wamekuwa na mpango mzuri kuhakikisha wakulima wa zao hilo wanapata miche hiyo. 

"Kwa sasa mpango  tulionao wakuwapatia wakulima miche ya mikarafuu ni kupata orodha ya idadi ya wakulima kutoka kwa masheha, ndipo tuanze kugawa miche hiyo," alisema.

Alieleza kuwa, matarajio yeo ni kuona uzalishaji wa miche ya mikarafuu inaongezeka kwa wingi, ili na wananchi wapate miche mingi itakayosaidia kupata zao la karafuu kwa winging hapo baadae. 

Nae mkulima aliyepata vifaa hivyo Abdalla Mohamed Salim wa Kijiji cha Kuungoni Wilaya ya Micheweni alisema ni matarajio yake kufanya kazi ya uoteshaji miche ya mikarafuu ili kufikisha malengo yaliyokusudiwa na shirika ikiwemo kuliimarisha zao la karafuu na kuleta maendeleo ya nchi.

" Hapo nyuma nilikuwa na changamoto ya vifaa kwani havikuwepo Pemba ilibidi nivifuata Bara lakini sasa nitazalisha miche zaidi ya ile niliyokubaliana na shirika kwani sina sababu vifaa nnavo"alisema.



Nae Mwenyekiti wa kikundi cha ushirika cha umoja wa Tangaani Wilaya ya Mkoani Abdalla Ali Salim baada ya kupokea vifaa hivyo aliahidi kuvifanyia kazi kwa malengo yaliyokusudiwa na kuliomba shirika la ZSTC kuendelea na ushirikiano wa kuwatembelea mara kwa mara ili kujuwa matatizo yanayowakabili katika kilimo cha karafuu.

Hivyo aliiomba Serikali kuwapekekea mabwana shamba mara Kwa mara ili waweze kuwatatulia changamoto zinapotokezea katika kilimo hicho.



                   MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch