Skip to main content

WANAFUNZI 274 WA MINUNGWINI WASOMA CHINI YA MITI

 






IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA

WANAFUNZI 274 wa skuli ya msingi Minungwini wilaya ya Wete Pemba, wanaendelea kusoma chini ya miti baada ya vyumba vinne vya madarasa walivyokuwa wakitumia kuchimbuka na kuvuja kwa muda wa zaidi ya miezi sita sasa.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi wazazi na walezi wenye watoto skulini hapo walisema, wanafunzi hao wanaendelea kukosa mtiririko mzuri wa masomo kutokana na kutumia eneo hilo kwa siku za kiangazi pekee huku siku za mvua zikiwa ni changamoto.

Wazazi hao walisema kuwa, kutokana na kuharibika kwa madarasa hayo wana hofu ya kuporomoka kwa elimu skulini hapo kutokana na changamoto ya wanafunzi hao kusoma chini ya miti.

Mmoja kati ya wazazi hao Fatma Jaffar Faki alisema kuwa hali hiyo haimpi usingizi kutokana na watoto wao kutokuwa na mazingira rafiki ya kusomea.

"Tunapenda watoto wetu wapate elimu bora lakini kwa hali hii ya kuwekwa chini ya miti ni mtihani kwa sababu wakati wa upepo ni hatari, kwani hata tawi linaweza kukatika na kuwaangukia," alisema. 

Mzazi Asha Omar Rashid ameiomba Wizara ya elimu kuchukua hatua za haraka kujenga ili kuwarejesha wanafunzi madarasani. 

Akizungumzia kuwepo kwa vyumba hivyo chakavu alisema, vinaweza kuhatarisha maisha ya wanafunzi, walimu na wapita njia.

"Banda hili lina hatari mbili, moja ya wanafunzi kukosa kulitumia na nyengine linaweza kuwaangukia kwa sababu kuta zimeinama na zimepasuka, ikinyesha mvua viambaza huroana na watoto kama tunavyowajua pale kwenye hatari ndipo wanapokimbilia kucheza,’’ walisema.


‘’Tunaamini kwamba Serikali italijenga banda hili lakini hofu yetu kwa sasa ni kuja kuanguka ghafla na watoto muda wote wapo karibu, hivyo hata kama bado kujengwa basi tunaomba livunjwe,’’ walisema.

Mwalimu Mkuu skuli hiyo Ahmada Ali Omar alisema, ubovu wa banda hilo umesababisha wanafunzi 274 kukosa sehemu ya kukaa na badala yake wanawaweka chini ya miti, ili kuhakikisha na wao wanapata elimu kama kawaida.



Alieleza kuwa wameshalifikisha wizarani suala hilo na tayari viongozi wameshakwenda kulikagua, hivyo wanatarajia litajengwa na wataendelea kulitumia baada ya kumalizika.

‘’Chini ya miti ni hatari kwa sababu siku za upepo kuna vumbi na pia tunahofia kukatika kwa matawi na kuwaangukia, vile vile siku za mvua hatuna pakuwaweka, hivyo ni hatari kwa kweli,’’ alieleza mwalimu huyo.

Mwalimu huyo anawashukuru sana viongozi wao wa Serikali, majimbo na shehia kwa ushirikiano wanaouonesha katika kuhakikisha wanapeleka maendeleo ya elimu mbele.

Afisa Mdhamini Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Pemba Mohamed Nassor Salim alisema kuwa, changamoto hiyo wameiona ambapo wana mpango wa kujenga skuli ya ghorofa pamoja na kuyafanyia ukarabati madarasa chakavu, ili kuondosha tatizo hilo.

‘’Kujenga skuli na madarasa ni maelekezo ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi kwamba wanafunzi waende skuli mkondo mmoja tu, ili wapate kwenda madrasa na pia kila darasa liwe na wanafunzi 45 tu ili kupunguza msongomano wa wanafunzi ambao husababisha wanafunzi kutofahamu vizuri,’’ alisema.

Aidha aliipongeza skuli hiyo kwa kutoa ufaulu mzuri kwa wanafunzi wao, ambapo umetokana na ushirikiano mzuri kati ya wazazi, kamati ya skuli, walimu na Serikali kupitia Wizara na kuwataka kuendeleza mashirikiano, ili kuongeza kiwango cha ufaulu.

‘’Hivi karibuni Waziri wetu wa elimu alinipa fedha shilingi laki tatu ili niwapatie zawadi wanafunzi watatu waliofaulu kwa kupata alama ‘A’, hii ni motisha kwa wanafunzi wengine kufanya vizuri,’’ alifafanua.

Skuli ya msingi Minungwini ina wanafunzi 2,277 na walimu 42, ambapo wanakwenda mikondo miwili asubuhi na mchana.

 

                                              MWISHO.                                                              

                                

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch