Skip to main content

BALOZI AMINA AHIMIZA WANANDOA KUSAJILI NDOA ZAO

 


IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@

MWENYEKITI wa Bodi ya Takwimu Zanzibar balozi Amina Salim Ali amewataka viongozi wa dini kuisaidia Serikali katika kuwahamasisha wanandoa kusajili ndoa, zao.

Akizungumza katika mkutano wa usambazaji wa matumizi ya matokeo ya viashiria vya sensa ya watu na makaazi 2022 kwa viongozi wa dini alisema, wanandoa wengi hawana elimu ya kusajili ndoa, hivyo ipo haja kwa viongozi hao kuhakikisha wapofungisha ndoa, kuwahamasisha wanandoa kusajili ndoa zao katika mamlaka husika.

Alisema kuwa, watu wengi katika jamii hawajui kwamba wanatakiwa kupata cheti cha ndoa kwa maslahi yao na Serikali kwa ajili ya kuweka takwimu sawa, hivyo viongozi wa dini wana jukumu la kuisaidia Serikali katika kutoa elimu ili wanandoa wasajili na kupata cheti.

"Kwa kweli hatuna elimu hiyo kwa sababu tukipewa karatasi ya sheha au ya kutoka kwa sheikh tu basi tunatosheka na hilo, lakini kwa elimu tulioipata leo juu ya umuhimu wa cheti cha ndoa, tutakwenda kutengeneza, akinamama wenzangu tujitahidi kulifanya hili," alisema Balozi huyo.

Kwa upande wake Afisa Fat-twa kutoka Ofisi ya Mufti Pemba sheikh Said Ahmad alisema kuwa, kuna migogoro mengi inayotokana kwa kukosa cheti cha ndoa na talaka, hivyo imefika wakati wa kuondosha changamoto hiyo kwa kuwaelimisha wanajamii ili watafute.

"Hivi vyeti ni muhimu sana kwetu kwa sababu ikiwa huna kinaweza kukukosesha fursa kubwa na ukajutia kwa nini hukutafuta hapo mwanzo, ninazo kesi hizo kuna watu wapo nje ya nchi na amepata fursa lakini ili afanikiwe awe na cheti cha ndoa, kwa hiyo wanakosa fursa kwa hasa hapati kuja huku kutia saini," alifahamisha.

Aliishukuru ofisi ya takwimu kwa kuwapelekea mrejesho wa matokeo ya sensa, ambayo yamewasaidia kubaini changamoto kwenye jamii na pia kujua namna ya kupanga mambo yao ya kidini.

Kwa upande wake Mtakwimu Mkuu wa Serikali Salum Kassim Ali alieleza kuwa, kupitia zoezi la sensa lililofanyika mwaka 2022 matokeo yalionesha kuwa takwimu za ndoa, talaka, vizazi na vifo zimekuwa na changamoto kutokana na baadhi ya wananchi kukosa vyeti, hivyo ndoa na talaka zisajiliwe ili takwimu ziende sawa.

Mapema washiriki hao walisema, Serikali iandae mpango wa upatikanaji wa vyeti vya ndoa na talaka kwa haraka, ili wananchi wasione shida kutafuta haki yao hiyo.

"Upatikana wa hivi vyeti ni shida hasa cha talaka na kuwafanya wanajamii wasione umuhimu wa kwenda kutafuta, hivyo Serikali iandae mpango utakasaidia upatikanaji wa vyeti haraka," alisema sheikh Yussuf Khamis Ali.

Nae mwalimu wa madrasa Ahmed Yahya aliishauri Serikali ihamasishe watu watafute vyeti vya talaka, ili ofisi ya takwimu ipate taarifa sahihi zinazoendana na vyeti vya ndoa.

Akifingua mkutano huo Kamisaa wa Sensa Zanzibar Balozi Mohamed Haji Hamza alisema, viongozi wa dini walitoa mchango mkubwa katika kufanikisha zoezi la sensa hivyo ni vyema wakaendelea kuwapatia elimu ili wananchi wapate vyeti vya ndoa, talaka, vizazi na vifo.



Mkutano huo umeandaliwa na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ambao umewashirikisha viongozi wa dini pamoja na walimu wa madrasa ukiwa na lengo la kurudisha shukrani kwao kufuatia zoezi la sensa ambalo walilifanikisha kwa kiasi kikubwa.

                  MWISHO 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...