Skip to main content

AKINA MAMA MADARASA YA KISOMO MJINI KIUYU WAUPONGEZA MRADI WA SWIL

 



HABIBA ZARALI, KU-@@@PEMBA
AKINA mama  wa madarasa ya kisomo cha watu wazima mjini Kiuyu shehia ya Minungwini   wilaya ya Wete Mkoa wa kaskazini Pemba wameushukuru mradi wa kumjenga mwanamke katika nafasi za uongozi (Swil) kwa kuwapatia madarasa ya kisomo cha  elimu ya watu wazima ambayo yamewawezesha kujuwa kusoma na kuandika.
Walisema mradi huo kwa sasa  umekuwa msaada mkubwa kwao  huku wakiwa  tayari wamedhamiria kuingia katika harakati za uongozi na kugombea nafasi yeyote kwa kujiamini muda utakapofika. 
Mmoja kati ya mama hao Ruwaila Ali Haji (26) ambae aliishia darasa la nne katika skuli ya kwake alisema baada ya kujiunga na darasa hilo  Kwa muda wa miaka minne sasa ana uwezo wa kusoma na kuandika.
Alifahamisha kuwa hana sababu ya kutogombania nafasi japo kwa ngazi ya shehia kwa vile moja ya sifa za kuomba uongozi ni kujuwa kusoma na kuandika jambo ambalo Kwa Sasa analimudu.
"Sasa najiamini kugombea nafasi yoyote Kwa sababu sifa nnayo najuwa kusoma na kuandika tena kwa ufasaha"alisema.
Alieleza kwa vile anajuwa kusoma na kuandika yuko mstari wa mbele kuwasomesha watoto wake  wanaporudi skuli jambo ambalo linawafanya watoto hao kuwa na hamu ya kuendelea na masomo yao kila siku.


"Kusema kweli mradi huu wa swil kupitia chama cha waandishi wa habari wanawake TAMWA na PEGAO wametuokowa sisi wanawake baada ya bidii zao za kutuwekea hili darasa na likatuwezesha tukajuwa kusoma na kuandika"alisema.
Nae Viwe Yussuf Makame (70) alisema kabla ya kujiunga na darasa hilo hakujuwa kusoma wala kuandika lakini kwa sasa ana uwezo wa  kumfundisha majukumu wake kusoma masomo ya skuli.
Alisema mradi wa swil umemkomboa na kumuondowa katika hali ya unyonge hasa kwa wakati huu ambapo usipojuwa kusoma na kuandika unaweza kukosa hata haki zako za msingi katika maisha.
"Nawasihi wanawake wenzangu kujiunga na madarasa ya watu wazima hata kama ni wazee kwani mimi kwa umri wangu huu na nimeweza ",alisema.
Asha Omar Issa (35) anajiskia faraja baada ya kujuwa kusoma na kuandika kwani anaweza kusoma ujumbe wa maandishi iwe kwenye karatasi na hata anapotumiwa kupitia simu yake.
"Hata kanga nasoma bila wasi na nikitembea najuwa km hapa pameandikwa hatari au usipite "alisema.
Kwa upande wake mwalimu wa darasa hilo   Maryam Juma Hamad   aliiomba wizara ya elimu na mafunzo ya amali Zanzibar kuwapatia posho la waalimu wa  madarasa ya wanakisomo  hao kwa wakati  ili waweze kujikimu na Maisha.
Alisema tokea kuanzia darasa hilo miaka minne ilopita tayari ameshawanfundisha wanafunzi 50 ambao alianza nao wakiwa hawajui hata kidogo.
Mratibu wa Tamwa Zanzibar ofisi ya Pemba Fat-hiya Mussa Said alisema mradi huo darasa hilo lilianzishwa baada ya mradi kugunduwa changamoto ya akina mama kutojuwa kusoma na kuandika.


Alisema kujuwa kusoma na kuandika Kwa akina mama na ni jambo la kufurahisha na kutoa tama akubwa ya kuthubutu kuona akina mama hao wanajuwa kuandika na kusoma.
"Kwa Sasa hatuwa inaridhisha kwani walianza wakiwa hawajui chochote na sasa wako vizuri"alisema.
Wakitowa michango yao wanafunzi hao wamewaomba wadau na taasisi mbali mbali   kuendelea kuwawezesha   kwa kuwapatia miradi  itakawasaidia kujipatia kipato na kuwaongezea hamasa katika kusoma. 
Hata hivyo Darasa hilo la kisomo  linakabiliwa na ukosefu wa ubao wa kufundishia ,  pamoja na kutokuingizwa kwenye mfumo wa madarasa ya  serikali  ya elimu mbadala licha ya kuwa na mashirikiano mazuri na wizara hiyo. 

 Darasa hilo likiloanzishwa kupitia mradi wa swil kwa sasa lina jumla ya wanafunzi 20 , limefanikiwa kuleta mabadiliko kwa akina mama zaidi ya 50 ambao awali hawakujua kusoma wala kuandika ambapo lotawarahisishia katika shughuli zao  na kutimiza malengo yao ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi.

Mwisho. 


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch