Skip to main content

JUMUIYA ZA WATU WENYE ULEMAVU PEMBA ZATOA NENO UAMUZI WA RAIS

 

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA::

JUMUIYA za watu wenye ulamavu kisiwani Pemba, wamepongeza hatua ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kuvikodisha, visiwa vinane vidogo vidogo, kwa dola za Marekani milioni 271.5 wastani wa shilingi bilioni 600.357.

 

Wakizungumza na mwandishi wa habari kwa nyakati tofauti juu ya hatua ya serikali kuvikodisha visiwa hivyo, walisema bila shaka nia ya serikali ni kuongeza mapato ya nchi.

 

Mjumbe wa kamati tendaji wa Jumuiya ya wanawake wenye ulemavu Zanzibar JUWAUZA Hidaya Mjaka Ali, alisema wazo hilo ni zuri, kwani linaelekea kwenye maslahi bora ya taifa.

 

Alisema, bila shaka katika hatua hiyo, kila mmoja kwa nafasi yake na alipo yatamfikia matunda ya ukodishwaji huo, ambapo ni hatua moja yapo ya kufikia maendeleo ya kweli.

 

‘’Mimi kwa niaba ya JUWAUZA, lazima hili lililoamuliwa na kiongozi wa nchi nilipo ngeze, maana bila shaka linamanufaa kwetu wananchi na taifa kwa ujumla,’’alisema.

 

Hata hivyo, ameziomba mamlaka husika wasiwaache kila hatua wetu wenye ulemavu, kwani wana haki sawa kama yalivyomakundi mengine.

 

Mwakilishi wa vijana wenye ulemavu katika baraza la taifa la Vijana Zanzibar Katija Hamad, alisema hatua hiyo inaonesha, nia ya dhati ya serikali, ya kutaka kuwainua wananchi kiuchumi, jambo ambalo ni vyema nao, wakaangaliwa kunufaika na uwekezaji huo.

 

Alieleza kuwa, hatua hiyo ya serikali inayoongozwa na Dk. Mwinyi, wameifurahia mno, na sasa kilichobakia kwa watendaji sekta ya utalii, kuweka mazingira rafik kwa ajili yao.

 


Mwenyekiti wa Jumuiya ya wasioona Pemba ZANAB Suleiman Mansour, alisema uwekezaji huo ikiwa watashirikishwa kikamilifu, unaweza kuwa na maana pana kwao, ikiwa ni pamoja na ajira za kudumu.

 

“Sisi watu wenye ulemavu, mara zote tumekuwa tukisahauliwa kushirikishwa katika utekelezaji wa sera mbali mbali, na kisha hukumbana na changamoto kama za miundombinu rafiki,’’alieleza.

 

Nae Msaidizi Katibu wa Jumuiya ya Wanawake wenye Ulemavu Zanzibar ‘JUWAUZA’ Bimkubwa Mohamed Ali, alisema watu wenye ulemavu na hasa wanawake, wamekuwa wakiandamwa na changamoto, ambazo zinaweza kuzuilika kabla.

 

“Hatua ya Dk. Mwinyi mpaka kuwashawishi wawekezaji na kuonesha nia ya uwekezaji ni nzuri, lakini lazima sera ziwalazimishe wawekezaji, kutushirikisha na sisi watu wenye ulemavu,’’alishauri.

 

Mkurugenzi wa Baraza la taifa la watu wenye ulemavu Zanzibar mwalimu Ussi Khamis, alisema bado sheria nambari 9 ya mwaka 2006 ya watu wenye ulemavu Zanzibar, haitekelezwi hasa kipengele cha uajira kwa kundi la watu wenye ulemavu.

 ‘’Kuanzia vifungu vya 6 hadi cha 8 vya sheria hii, inafafanua suala la ajira kwa watu wenye ulemavu, sasa kama haki au fursa katika ajira za kitaifa watu wenye ulemavu, wasiaachwe nyuma,’’aliependekeza.

 

Mdhamini Kamisheni ya Utalii Pemba Hamad Amin, amesema watu wenye ulemavu, wana haki sawa na wengine, na niwakati nao kujipanga, ili kunufaika na uwekezaji huo.

 


Mkuu wa Mkoa wa kusini Pemba, Mattar Zahor Massoud, alisema lazima katika ujenzi wa hoteli na nyumba za kulala wageni, zifikiria mazingira kwa watu wenye ulemavu.

 

Awali Mkurugenzi wa Mamlaka ya Kukuza Uwekezaji Zanzibar ‘ZIPA’ Sharif Ali Sharif, alivitaja visiwa hivyo vinane kuwa ni Changuu, kinachoekezwa kwa dola zisizopungua milioni 20 kupitia kampuni ‘Changuu Lodge Ltd’.

 

Kisiwa cha Bawa kitaekezwa na kampuni ‘Bawe Retreat Ltd’ kwa mtaji wa dola milioni 30, ambapo kisiwa cha Chapwani kitaekezwa na kampuni ya ‘Zan Texas Ltd’ kwa dola milioni 20 na kisiwa cha Snake dola milioni 10, kupitia kampuni hiyo.

 

Aidha Mkurugenzi huyo, alikitaja kisiwa cha Kwale kikiwa na uwekezaji kupitia kampuni ‘Group Eight Holding Ltd’ sawa na mtaji wa dola milioni 68.

 

Kisiwa cha Misali Pemba, kitaekezwa na kampuni ‘East African Investment Ltd’ kwa mtaji wa dola za Marekani milioni 83, wakati visiwa Pamunda ‘A’ na ‘B’ vimechukuliwa na kampuni ya ‘Tulia Zanzibar Beach Resort’ kila kimoja kwa dola milioni 15.

“Kisiwa chengine ni Pungume Unguja kilichopewa mwekezaji kupitia kampuni iitwayo ‘Emperial East African Ltd’ kikiwekezwa kwa dola milioni 10.5,’’alieleza Mkurugenzi huyo.

 

Rais wa Zanzbar Dk. Hussein Ali Mwinyi, amenukuliwa na vyombo vya habari akisema, kuwa katika kipindi cha mwezi Novemba mwaka 2020 hadi Disemba 2021, ZIPA imesajili miradi 120 ya uwekezaji, yenye mtaji wa dola za Marekani milioni 877.

 

Miradi hiyo inatarajiwa kutoa ajira zaidi ya 7000, na tayari wawekezaji wameshajitokeza katika visiwa vidogo vidogo 10, vilivyotangaazwa kukodishwa.

  

                  MWISHO

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch