Skip to main content

MLAWITI APACHIKWA MIAKA 19 CHUO CHA MAFUNZO PEMBA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA

MSHTAKIWA Khamis Abdalla Khamis ‘kirere’ wa Kangani wilaya ya Mkoani, aliyetiwa hatiani kwa kosa la utawiti, kabla ya kusomewa hukumu ya miaka 19 ya chuo cha mafunzo, ameiomba mahakama ya mkoa Chake chake, kwanza imchunguze akili zake.

Hayo aliyadai wakati alipopewa nafasi ya kujitetea kabla ya mahakama hiyo ya maalum ya makosa ya udhalilishaji ya mkoa wa kusini Pemba, chini ya Hakimu Muumini Ali Juma, kumsomea hukumu yake.

Mshitakiwa huyo alidai kuwa, anaomba kuchunguuzwa afya yake ya akili, sambamba na kuomba kupunguziwa adhabu, kutokana na umri wake kuwa mdogo.

Aidha alidai kutokana na kuhitajika kwake kwenye nguvu kazi ya taifa, aliomba ahuweni mahakamani hapo, kufungwa kifungo cha nje, na adhabu yake iwe ni kufanya usafi.

‘’Mheshimiwa Hakimu naiomba mahakama yako tukufu, kwanza inichunguuze akili, lakini pia inipunguzie adhabu na kunipa kifungo cha nje, maana umri wangu bado mdogo,’’alidai mshitakiwa huyo.

Hata hivyo Hakimu wa mahakama hiyo Muumini Ali Juma, alizingatia maombi ya mtuhumiwa huyo, na kuamua kumpeleka chuo cha mafunzo kwa miaka mitano ‘5’ kwa kosa la kutorosha na miaka 14 kwa kosa la kulawiti.

Alisema kuwa, adhabu hizo zitumike tofauti, lakini pia pamoja na adhabu hiyo mshitakiwa, ametakiwa kumlipa muathirika fidia ya shilingi milioni 2.

Hakimu huyo alisema, adhabu aliyompa mshitakiwa hiyo ni ya kiwango cha chini, kutokana na aina ya makosa yake, na hasa kwa mujibu wa sheria nambari 7 ya mwaka 2018, sheria ya Mwendo wa makossa ya Jinai ya Zanzibar.

Kabla ya kutolewa hukumu hiyo, Hakimu Muumini alisema ushahidi uliotolewa na mashahidi mahakamani hapo, haukuacha chembe cha shaka, na ulikidhi vigezo vyote.

Alisema upande wa mastaka, ulithibitisha mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na umri wa mtoto, utoroshaji wake pamoja na tendo la kuingiliwa.



‘’Mtu pekee anayeweza kuthibitisha ama kukataa kuingiliwa kwake, ni muhanga, na kwa mujibu mtoto huyo wa miaka 10, alivyotoa ushahidi wakati akiongozwa na wakili wa serikali, alithibitisha,’’alisema Hakimu Muumini.

  Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo, Wakili wa serikali Ali Amour Makame, alisema matendo hayo yamekua yakiathiri ndani ya jamii, hivyo ni vyema ikatolewa kwa adhabu kali.

Alisema, tayari jamii ilishafanya wajibu wake wa kuripoti kwenye vyombo vya sheria na kisha navyo kuchukua hatau za kuifikisha kesi hiyo, mahakamani hapo.

‘’Kazi iliyobakia sasa ni mahakama kutoa hukumu, maana kila pande imeshatekeleza wajibu wake, kama taratibu na sheria zinavyoelekeza,’’alisema Wakili huyo.

 Ilifahamika mahakamani hapo kuwa, mshtakiwa Khamis Abdalla Khamis ‘kirere’ miaka 20 wa Kangani wilaya ya Mkoani Pemba, alimtorosha na kisha kumlawiti mtoto wa miaka 10.

Ambapo alimtorosha kutoka sokoni Kangani na kumpeleka kwenye banda analolala, ambaapo hilo ni kosa kinyume na kifungu cha 113 (1) (b) cha sheria ya Adhabu sheria namba 6 ya mwaka 2018, sheria ya Zanzibar.

Huku kosa la pili alilotiwa hatiani ni la utawiti, wa mtoto huyo ambalo ni kinyume na kifungu cha 115 (1) cha sheria ya Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018, sheria ya Zanzibar.

                                    MWISHO. 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch