Skip to main content

‘NILIPATA ULEMAVU KWA UCHAKAVU WA BARABARA NILIPOKUWA MJAMZITO’

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA:

WANAWAKE wenye ulemavu wa shehia za Michungwani na Wesha wilaya ya Chake Chake Pemba, wamelezea kuchoshwa na vifo vya watoto wao wachanga na sulubu ya kujifungua njiani, wakati wanapopelekwa hospitali, kutokana na uchakavu wa muda mrefu wa barabara yao.

Walisema, imekuwa ni kawaida kwa mwaka kupata vifo vya watoto wachanga kati ya viwili hadi vitatu, au akinamama wajawazito kupata matatizo wakati wanapojifungua kutokana kuchelewa kufika hospitali za Wesha na ya Chake Chake.

Wakizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbali mbali, walisema barabara yao imekua ikichangia kwa asilimia 100 vifo vvya watoto wachanga na wazazi, kutokana na uchakavu wake unaokwamisha gari kupita kwa kasi.

Walisema, matatizo zaidi huwakumba katika kipindi cha mvua, kwa vile barabara hiyo, hujaa mashimo yenye kina kirefu ambayo hairuhusu hata gari ya Ng’ombe kupita kwa utulivu.



Mmoja kati ya wanawake hao mwenye ulemavu wa viungo Raya Salim Khamis, alisema suala la wao na wagonjwa wengine kwenye kijiji chao kupata misuko suko inayotokana na barabara yao, ni  jambo la kawaida hasa kila inapofika kipindi cha mvua.

Alisema yeye mwaka 1990, aliwahi kubebwa kwa gunia kutokana Birikau hadi barabara kuu, na alipofika katikati ya safari, alijifungua.

“Kwa uchakavu wa barabara yetu kwa mwaka huo, nilimpoteza mtoto wangu na mimi mwenye nilipata ulemavu wa mguu uliosababishwa na uchungu mzito, kwa kule kuchelewa kufika hospitali,’’alisema.

Nae Halima Kassim Juma mwenye ulemvu wa uziwi, alisema sasa zaidi ya miaka 40 amekuwa akishuhudia dhiki ya barabara yao, jambo ambalo hata yeye ameshawahi kupoteza mtoto, baada ya kujifungua kwake nyakati za usiku.

“Niliumwa na uchungu wa kujifungua nyakati za usiku mkubwa, na nikajifungua nyumbani na asubuhi nilipelekwa hospiatali na mwangu alifariki, baada ya kupoteza damu nyingi,’’alieleza.

Aidha mama huyo alisema, alianza yeye kubebwa kwa magunia na vitanda kupelekwa hospitali kwa kifungua, na sasa zamu imekuwa ya watoto wake wanapokuwa wajawazito.

Hata hivyo Hussan Yussuf Hamad (39) wa Tondooni shehia ya Wesha, alisema tokea afahamu yeye barabara yao imekuwa na usumbufu, jambo linalowapa dhiki hasa wajawazito na wa wagonjwa.

“Baba yangu alikuwa ni mgonjwa wa pumu na alikuwa akibebwa kwa kitanda kutoka hapa kijijini hadi barabara kuu, na sasa ni muda mrefu hadi leo, kadhia ikiendelea,’’alieleza.

Massoud Seif Massoud na Khamis Ali Said walisema dhiki ya barabara hiyo, imekuwa ni jambo la kawaida kwao, na waathirika ni wanawake hasa wenye ulemavu.

Walisema, kila Mbunge na Mwakilishi anayefika kijijini kwao, huwaahidi kuwatengenezea barabara hiyo kwa kiwango cha kifusi, ingawa baada ya kupata nafasi hizo hushindwa kutekeleza.

Naibu sheha wa shehia ya Michungwani wilaya ya Chake Chake Amina Hamad Fakih, alisema hawajakata tamaa, lakini wameanza kupata wasi wasi na utekelezaji wa ahadi za viongozi juu ya ujenzi wa barabara yao.

Alisema, amekuwa akishirikiana na sheha mwenzake wa shehia ya Wesha kupeleka taarifa kila wakati ofisi ya wilaya na baraza na mji wa Chake Chake juu ya ubovu wa barabara hiyo, ingawa bado wanaendelea kuteseka.

Mkuu wa wilaya ya Chake Chake Rashid Hadid Ali, alisema kwa sasa barabara hiyo pamoja na nyingine zilizomo wilayani humo, zimeshaingizwa kwenye mpango wa kujengwa kwa kiwango cha lami.

Alisema barabara za Birikau- Kijangwani, Wesha Ndagoni na ile ya Gombani- Michungwani zinaangalia kwa karibu na tayari hata kwenye mpango wa wilaya, zimeshawekewa mkakati wa kujengwa kwa kiwango cha lami.



“Kwa mfano kama sisi Mei 22, mwaka huu baada ya kuharibika vibaya barabara hiyo, tulishirikiana na baraza la Mji na wizara husika ya barabara, kuifanyia matengenezo na sasa iko vizuri,’’aleleza.

Hivi karibuni Afisa Mdhamini wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji Pemba Ibrahim Saleh Juma, alisema kwa barabara za ndani wahusika wakuu ni halmashauri au mabaraza ya miji, ingawa wakati mwengine huzijenga hata kwa kiwango cha lami.

Barabara ya Kijangwani- Birikau iliyomo baina ya majimbo ya Chake Chake na Ziwani ambayo ina urefu wa wastani wa kilomita 3.7 imeasisiwa zaidi ya miaka 50 iliyopita, ingawa bado kwa siku za mvua hairuhusu gari kupita.

                                  Mwisho    

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch