Skip to main content

WANAWAKE WENYE ULEMVU PEMBA WAWAPA RAI WAZAZI WENYE WATOTO WALEMAVU

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA

WANAWAKE wenye ulemavu kisiwani Pemba, wamewataka wazazi na walezi wa watoto wenyeulemavu, kutokubali kurubuniwa kwa fedha au kitu chochote cha mali, mara baada ya watoto wao, kufanyiwa vitendo vya ukatili wa kijinsia.

Walisema wadhalilishaji wamekuwa wakitumia mwanya wa umaskini wa wazazi na watoto hao, mara wanapogundulika kuwatendea udhalilishaji watoto wenye ulemvu, kama sehemu ya kuwarubuni, ili kesi hizo zisiendelee.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti, walisema wakati umefika sasa kwa wazazi na walezi kutokubali kuingizwa kwenye mtengo wa kuua kesi, kwa masharti ya kupewa mali.

Mjumbe wa kamati tendaji ya Jumuiya ya wanawake wenye ulemavu Zanzibar ‘JUWAUZA’ Hidaya Mjaka Ali alisema, kutokana na wazazi na walezi wenye watoto wenye ulemavu kuishi katika umaskini wa kipato, ndio maana wadhalilishaji wamekuwa wakitumia, fursa hiyo.

Alieleza kuwa, wadhalilishaji wanapoona kesi imewaelekea, huanza kuwarubuni kwa kuwaomba radhi, na kisha hufuatiwa na kiasi fulani cha fedha, famili ya mtoto, ili kuipoza kesi hiyo.

‘’Kwanza kama hali zetu za kipato ni duni tuzikubali kwa kuishi nazo, lakini tusitafute kupunguza ukali wa maisha kwa fedha za watoto waliodhalilishwa,’’alieleza.

Hata hivyo mjumbe huyo wa ‘JUWAUZA’ aliwakumbusha wazazi na walezi hao kushirikiana kikamilifu na vyombo vya ulinzia na usalama, wakati inpotokezea udhalilishaji kwa watoto wao.

Nae mjumbe wa ‘JUWAUZA’ wilaya ya Micheweni Fatma Ramadhan Shaib alisema, bado wazazi na walezi wanadhani inapotokezea mtoto kudhalilishwa, suluhisho ni kukaa chini ya kuimaliza kienyeji.

‘’Haingii akili kuwa mtoto mwenye ulemavu ameshadhalilishaji, na kisha kwa umaskini wa wazazi au walezi wakubali kuchukua fedha, au kupewa ardhi ili kesi imazike, hili sio sahihi,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Mjumbe huyo wa ‘JUWAUZA’ aliviomba vyombo vya kusimamia sheria, kulisaidia kundi la watu wenye ulemavu, kutokana na mazingira yao.

Nae Mwakilishi wa watu wenye ulemavu kisiwani Pemba kwenye baraza la taifa la vijana Zanzibar, Katija Mbarouk Ali alisema utamduni wa kuyamaliza kienyeji, umekuwa ukijitokeza hasa ikitokezea aliyefanyiwa vitendo ya udhalilishaji, ni mtoto kiziwi.     

‘’Mara nyingi wadhalilishaji wamekuwa wakiwadhalilishaji watoto wenye ulamvu na hasa wenye ulemavu wa uziwi au viungo wakijua hawawezi kufuatilia wala kutoa ushahidi mahakamani,’’alieleza.

Kwa upande wake Afisa Mipango wilaya ya Chake chake, Kassim Ali Omar, amesema watoto wenye ulemavu wamekuwa wakifanywa kama mtaji na baadhi ya wazazi na walezi inapotokezea udhalilishaji.

‘’Wazazi na walezi waelewe kuwa, haki za watoto wao wanazomikononi mwao, hivyo kama wakiamua bora kuchukua fedha au mali nyingine kuua kesi, wanawakosesha haki watoto hao,’’alieleza.

 Afisa Elimu na Mafunzo ya Amali wilaya ya Chake chake, Bur-han Khamis Juma alisema, wapo wanafunzi wenye ulamavu wamekuwa wakikosa mtiririko mzuri wa masomo, hasa baada ya kufanyiwa vitendo vya udhalilishaji.

‘’Ni vyema katika vyombo vya sheria kama vile mahakama, kuwe na adhabu ya zaida kwa wale washtakiwa, watakaotiwa hatiani kwa kuwadhalilisha watoto wenye ulemavu,’’alishauri.

Hata Mratibu wa Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba Fat-hya Mussa Said, alisema pamoja na yote, hayo ni vyema kwa wazazi kuzingatia umuhimu wa kutoa ushahidi mahakamani.

‘’Zipo kesi kadhaa zimekuwa zikifutwa mahakamani, kwa sababu ya wahusika kutofika mahakamani, na hivyo kurejesha nyuma jitahada zinazochukuliwa,’’alifafanua.

Naibu mrajisi wa mahakama kuu Pemba Faraj Shomar Juma, alisema moja ya jukumu la wazazi na walezi, ni kuhakikisha wanawawekea ulinzi watoto wao, kama sheria ilivyotamka.

‘’Ukiangalia sheria ya Mtoto nambari 6 ya Zanzibar ya mwaka 2011, inahimiza ulinzi kwa mzazi au mlezi kwa lengo la kumkinga na majanga likiwemo la udhalilishaji,’’alifafanua.

Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, akizungumza hivi karibu na kamati ya maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili, alisema jambo kubwa ni kuhakikisha jamii inashirikiana.

                              Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch