Skip to main content

WATAALAMU WA ‘TB’ 'WAFUATENI WATU WENYE ULEMAVU WA AKILI VIJIJINI KUWAPA ELIMU'

 



HAJI NASSOR, PEMBA:

JUMUIYA kwa ajili ya watu wenye ulamavu wa akili Zanzibar ‘ZAPPD’ tawi la Pemba, imeziomba mamlaka husika zinazotoa taaluma ya kujikinga na ugonjwa wa kifua kikuu ‘TB’ kuhamia vijijini, ili kundi la watu wa aina hiyo, watambue njia za kujikinga na ugonjwa huo.

Kauli hiyo imetolewa na Mratibu wa Jumuiya hiyo, Khalfan Amour Mohamed, wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, juu ya kundi la watu wa aina hiyo wanavyoweza kufikiwa na taaluma.

Alisema vijana kama hao, ambao wapo mjini wamekuwa wakifaidika kwa kiasi kikubwa na taaluma ya kujikinga na TB, ingawa ukosefu wa taaluma kwa upana, hukosekana kwa wale waliyoko nje ya mji.

Mratibu huyo alieleza kuwa, kwa waliopo maeneo ya mjini, wamekuwa wakipata mabango, vipeperushi, matangaazo mbali mbali na hata ukaribu wa vyombo vya habari, ingawa kwa waliyoko vijijini kuna ufinyu wa taalamu hiyo.

Alieleza kuwa, ni vyema kikosi kazi kinachopambana na kusambaa kwa bekteria wa TB, sasa kupeleka kwa nguvu elimu hiyo vijijini, ambapo watu wenye ulemavu watafikiwa.

“Ni kweli Serikali kupitia wizara ya Afya, imekuwa mstari wa mbele kuhakisha wanatoa elimu ya kujikinga na TB, lakini nguvu sasa ielekezwe vijijini,’’alieleza.

Katika hatua nyingine Mratibu huyo wa Jumuiya kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa akili kisiwani Pemba, Khalfan Amour Mohamed, aliwataka wazazi na walezi wa watoto hao, kuwa karibu mno na vyombo vya habari, ili kusikiliza njia za kujikinga na ugonjwa huo.

Kwa upande wake, Mtaribu wa Idara ya watu wenye ulemavu kisiwani Pemba, Mashavu Juma Mabrouk, alisema kwa vile ni vigumu kuwakusanya makundi ya watu kuwapa elimu, njia pekee ni kusikiliza vyombo vya habari.

Alisema, tayari Idara hiyo, imeshandaa vipindi vya redio na tv kwa ajili ya makundi mbali mbali ya watu wenye ulemavu, ili kujipatia elimu ya kujikinga na TB.



Alifahamisha kuwa, kimsingi kila mazazi na mlezi anawajibu wa kutumia dakika walau 20 kwa siku kumuelimisha mtoto wake, juu ya mambo mbali yakiwemo haya yaliyoikumba dunia kwa sasa.

Katika hatua nyingine Mratibu huyo, aliwataka wale viongozi wa matawi ya taasisi za watu wenye ulemavu wasisite kuwapa taaluma hiyo, pale wanapokutana hata Ofisini mwao.

Nae Mratibu wa Jumuiya ya watu wasioona ‘ZANAB’ Pemba, Suleiman Mansour, alisema bado haja ya wao kukusanywa japo wachache kupewa taaluma hiyo ipo.

 Afisa Mdhamini wizara ya Afya Pemba, Khamis Bilali Ali, aliwataka viongozi wa matawi, kuwakusanya wanachama wao, na kisha wizara itawapelekea wataalamu wa ugonjwa wa TB.

Mkuu wa mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, amesema kundi la watu wenye ulemavu lina, lina haki zote kama ilivyo kundi la watu wengine.

‘’Kama ni kweli kundi la watu wenye ulemavu wa akili linaomba kupewa elimu, hili sio jambo la kucheleweshwa, ni vyema wizara na wataalamu wake wajipange,’’alieleza.

Mkataba wa kimataifa wa haki za watu wenye ulamavu, Ibara ya 27 imezitaka nchi zilizoridhia mkataba huu, Tanzania ikiwemo zitambue haki za kundi hilo kufanya kazi kwa misingi ya usawa kama wengine wasio na ulemavu, ili waweze kumudu maisha yao.

Sheria ya watu wenye ulemavu nambri 9 ya mwaka 2006 kifungu cha 11 (i) kimesiistiza kuwa ‘mtu mwenye ulemavu ana haki ya kupatiwa huduma za afya na kuchukuliwa hatua za kumkinga na jaambo linaloweza kumdhuru’.

Mkataba wa kimataifa wa haki za watu wemue ulemavu Ibara ya 25, umezitaka nchi zilizoridhia mkataba huo, kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapewa huduma bora za matibabu bila ya ubaguzi.

                                   MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch