Skip to main content

USARIFU WA UDONGO ULIVYOKUWA TEGEMEO KWA WANAWAKE PEMBA

 




HANIFA SALIM, PEMBA:::

NI mwendo wa takribani kilomita 2.5 kwa usafiri wa gari binasfi, kutoka mjini Chake chake hadi kijiji cha Pembeni ya Muangaza kilichoko jimbo la Ziwani wilaya ya Chake chake.

Kijiji hicho kiko Magharibi mwa kisiwa cha Pemba, kina wakaazi zaidi ya 800, ambao wanajishughulisha na kazi mbali mbali ikiwemo ujasiriamali, kilimo na uvuvi.

Wengine na hasa wanawake wamjitupa kwenye ubunifu wa kutengeneza vyombo mbali mbali kwa kutumia rasilimali ya udongo maalumu.

Sikuwa na nia ya kwenda kufanya utalii wa ndani katika kijiji hicho, bali nilikuwa na shauku kubwa ya kuangalia ubunifu na usarifu wa udongo unaofanywa na wanawake hao.

Wananawake wa kijiji cha Pembeni ya Mwangaza, wakubwa na wadogo wanajishughulisha na kazi hiyo, hatimae kuzalisha ajira kwao na watu wengine.

Wanawake wa kijiji hicho hutumia muda wao mwingi kwa ajili ya kufanya kazi hiyo, ambayo huwapatia kipato cha kuendeleza maisha yao ya kila siku.

Ikiwemo kuwapatia watoto mahitaji yao muhimu ya kielimu na matibabu, kutokana na ubunifu huo bila ya kumtegemea baba ‘mume’ ambae nae ana majukumu mengine.

Kazi hiyo imeweza kuwapa maslahi makubwa akina mama wa kijiji hicho, na hatimae kupatikana ule msemo unaosema ‘kazi ni kazi alimradi mkono uwende kinywani’.

Licha ya mafanikio ambayo wanaendelea kuyapata wanawake hawa kwa ufinyanzi wa vyomvo vya udongo, lakini waliona ili kufikia ndoto zao ni kuanzisha kikundi cha ushirika.

ZINA MOLA’

Ushirika huo ulioanzishwa mwaka 2020, baada ya kurudi kwenye maonesho yaliofanyika Chamanangwe Pemba, kina wanachama tisa ‘9’ wanawake wakiwa wanane na wanamme mmoja.

“Tulipokwenda katika maonesho ya chakula Chamanangwe wilaya ya Wete, tulipata fursa ya kuonesha bidhaa zetu kama wajasiriamali tukajifunza mambo mengi ndiporudi tulianzisha ushirika huu”, anasema Katibu Mtumwa Amour Juma.

Kwenye ushirika huo, wanajishughulisha na utengenezaji wa vyombo mbali mbali vya matumizi ya nyumbani, kama vile mitungi, vyetezo, mikungu, vijungu, majiko, sahani na vikombe.



“Tunanufaika sana na hichi kikundi, licha ya changamoto tunazozipata, lakini tunazichukuwa kama ni fursa kwetu ya kusonga mbele kimaendeleo, kwani inatusaidia kupunguza nguvu ya ukali wa maisha,” anasema.

Kazi hiyo ndio inayowaendeshea maisha yao ya kila siku kwa kujipatia mahitaji yao ya lazima kama vile chakula, kulipia ada na matibabu pamoja na kuweka hakiba zao benki.

Wanaiona faida ya ufinyanzi, na ndio maana wanaendelea na kazi hiyo inayowapatia kipato, mbali ya matumizi waliyonayo lakini wanahakiba ya zaidi ya shilingi milioni 2.5 benki.

Katika kuhakikisha wanafanya kazi yao vizuri, wanasema wamezalisha zaidi ya vyombo 1000 kwa ajili ya kuuza kwenye masoko mbali mbali, licha ya kuwa hawana soko la uhakika.

Mwanaushirika Hadia Muhidini Haji anasema, anaishukuru Serikali kwa kuwaunga mkono, wajasiriamali kwa kila hatua ambazo wanapitia.

Anasema, ufinyanzi wao ni katika kipindi cha jua kali, tu kwani kipindi cha mvua hawawezi kufanya kazi zao kutokana na kukosa ofisi ambayo wangeweza kuweka bidhaa zao.

Kwa siku huchoma wastani wa vyombo 200 hadi 250, katika hatua za uchomaji wa vyombo huchukuwa muda wa siku mbili hadi tatu.

Bidhaa zao wanauza kwa jumla na reja reja kwa bei tofauti ambapo mikungu na vyungu huuza kwa bei ya shilingi 2,500 hadi 3000 na vietezo shilingi 4000.


“Kutokana na utengenezaji wa kietezo kuwa mgumu zaidi ya mkungu au chengine lazima bei yake iwe tofauti, kwani kietezo kinachukua muda wa wiki moja kukitengeneza hadi kumalizika,” anasema.

Anaiomba serikali kuendelea kuwaangalia wajasiriamali kwa moyo wa huruma, kuwapatia mikopo ili wafanye biashara zao kwa kurejesha na wengine wapatiwe fursa ya kukopa.

Nae Furaha Kheir Juma (76) mlezi wa kikundi hicho anasema, utamaduni huo ambao wanauwendeleza ni urithi kutoka kwa wazee wao ambao wakiufanya.

Anasema, unapotengeneza vyombo hivyo unafinyanga udongo na kuutoa vijiwe vyote, unaweka dizaini unayotaka baadae unavieka juani kwa ajili ya kukauka na kushikana.

“Baadae unapoona kimekauka kuna vifaa vinaitwa Muwale, Kuungo na kisahani hivi kwa kutengenezea kwa kupamba unavotaka baada ya kutulia kuna kuungo unaekea sawa na kiwe kwenye muonekano mzuri,” anasema.



Bidhaa kutokana na utengezaji wake ni kwa kutumia udongo hawawezi kuuza nje ya visiwa vya Zanzibar, kwani katika usafirishaji wanaweza kupata hasara kubwa kinyume na ambavyo wanategemea.

Serikali katika kuwaunga mkono imekuwa ikiwapatia misaada mbali mbali ikiwemo, elimu ya uhifadhi wa fedha, mafunzo ya kibiashara na namna ya kulinda bidhaa zao.

Bidhaa zao wanauza kwa wafanyabiashara, matajiri mbali mbali na zinapotokea fursa za maonesho wanauza zaidi, lakini baada ya Serikali kujenga vituo vya wajasiriamali matumaini yao kupata soko la uhakika.

“Hatuwezi kuajiriwa sote serikalini kutokana na idadi yetu kuwa wengi, lakini kujiongeza kwetu kwa kusarifu udongo kumeweza kutupatia mafanikio makubwa,’’anasema.

“Na hatuna wasi wasi wa matumizi madogo madogo” ni kauli ya mama mmoja ambae nilikutana nae katika kijiji hicho ambacho hadi sasa kimebarikiwa kuwa na rangi ya kijani kibichi.

Anasema, changamoto ambazo zinawakabili ni pamoja na utafutaji wa malighafi za kuchomea vyombo vyao (Magubi-kozi) ambayo inapatikana katika wilaya ya Mkoani, usafiri ambapo hulazimika kukodi magari binafsi, na ofisi.

Ameiomba serikali iwasaidie mashine ya kukandia udongo kutolea vijiwe ambao hulazimika kukanda kwa kutumia vifua jambo ambalo linaweza kupelekea ubovu wa afya zao.

Baada ya hapo huvieka ndani vikauke kwa unyevu unyevu wa joto kwani vinapokiekwa juani vinaweza kukapasuka na kula hasara, kinachoekwa juani kwenye bidhaa za udongo ni mkungu pekee.

Anasema, vijana wengi wa sasa hawajui umuhimu wa kutumia vyungu na vyombo vya udongo wamezoea kutumia masufuria ambayo anasema maradhi mengi ya tumbo hutokana nayo.

Wazee wao wa zamani wakinywa chai katika vikombe vya udongo (Mabunguu), mabakuli ya kukunia nazi wakitengeneza kwa udongo, ya kuvumbikia maziwa na hata wali na muhogo wakipika ndani ya vyungu.

Kuna tofauti kubwa kati ya chakula kinachopikwa ndani ya chungu na sufuria, mchuzi unaopikwa ndani ya chungu huwa na ladha tamu zaidi kuliko sufuria.

Anaishauri jamii irudi katika kutumia utamaduni na asili ya vyombo vya udongo ambavyo havina madhara na kuacha kutumia masufuria ambayo yanatengenezwa kwa kutumia bati.

Mtoto Hamida Juma Amour (17) ni mjasiriamali mtoto ambae amerithi ubunifu wa kusarifu vyombo vya udongo kutoka kwa bibi yake anasema, anajivunia kujua fani hiyo ambayo wengine hawaijui.

Anasema tangu anasoma alikuwa anajifunza ujuzi huo kwa wazazi wake na baada ya kumaliza kusoma kidato cha nne alijiunga na ujuzi huo ambao kwa sasa anajivunia kuupata.

“Ili kuona sisi tunaiendeleza asili ya Kijiji hichi cha Pembeni ambayo tuliirithi kutoka kwa bibi zetu basi tutaiendeleza kuhakikisha vizazi vyetu vinajifunza na kuwarithisha wengine,” anasema.

WATEJA WA VYOMBO VYA UDONGO

Mwanajuma Khamis Hamad wa Chake chake anasema, amekua akivutiwa na vyombo vilivyotengenezwa na rasilimali ya udongo kutokana na kuwa chakula chake ni chenye ladha pekee.

Asha Rajab Mohamed wa Machomane anasema, amekua akinunua vifaa hivyo na kuuza katika duka lake na kujipatia umaarufu mkubwa.

‘’Wazee wetu wa zamani walikua wakitumia vyombo vya udongo wakipika vyakula vyote kwenye masufuria na vyungu lakini sasahivi utamaduni umepotea, nawashauri akina mama turejeshe hii asili yetu,’’ anasema.


TAMWA

Afisa Miradi kutoka Chama cha waandishi wanawake Tanzania TAMWA Zanzibar ofisi ya Pemba Asha Mussa Omar, anasema hawana shida na hilo, ingawa wanategemea zaidi miradi.

Anasema, kama ikitokezea wamepata mradi, watawaingiza kwenye mchakato, ili nao wafikie ndoto zao kama walivyo wanawake wengine.

‘’Kwa sasa hatuna mradi kwa ajili ya kuwanunulia mashine ya kuchakata udongo, lakini kama wanahitajia uwezeshwaji mwengine wafike ofisini,’’anasema.

SERIKALI

Akiwasilisha hotuba ya bajeti ya mwaka 2022/2023 ndani ya baraza la wawakilishi Waziri wa Afisi ya Rais Kazi uchumi na uwekezaji Mudrik Ramadhan Soraga anasema, mfuko wa uwezeshaji wananchi kiuchumi kwa kushirikiana na taasisi za kifedha, umejipangia kutoa mikopo 2,000.

Anasema, mikopo hiyo ina thamani ya shilingi bilioni 3 kwa vikundi vya kiuchumi katika sekta zote za kiuchumi, kuangalia fursa mpya ambazo zinaweza kutekelezwa na wananchi.

Aidha katika bajeti hiyo waziri Soraga ameahidi, kuendelea na juhudi za kutunisha fedha ili mfuko uendelee kuwasaidia wajasiriamali wengi zaidi.

‘’Pia kuimarisha mashirikiano na uratibu wa shughuli za mikopo nafuu hapa nchini pamoja na kuimarisha mashirikiano na taasisi zinazotoa mikopo nafuu,’’ anasema.

Jumla ya vyama vya ushirika 1,848 vimesajiliwa na kati ya hivyo Unguja 709 na Pemba 1,139 pamoja na vyama vya uzalishaji na utoaji wa huduma 910, vinavyojishughulisha na utengenezaji sabuni, SACCOS, ukataji miwa, uvuvi, ufugaji kaa, kilimo pamoja na usafi wa mazingira.

                                    MWISHO.

 

  

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch