Skip to main content

MSIWAPELEKE KWA WAGANGA WA KIENYEJI KUCHUNGUUZA AFYA YA AKILI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA::

WANANCHI kisiwani Pemba, wameshauriwa kuvitumia vituo vya afya vilivyo karibu yao, kwa ajili ya kuwapeleka ndugu na jamaa zao, kufanyiwa uchunguuzi wa afya ya akili, ili wagundulike mapema ikiwa ni watu wenye ulemavu wa akili ama laa.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Chake Chake, Mratibu wa Huduma za Afya ya Akili Pemba Salim Khamis Ali, alisema wapo baadhi ya wananchi, huwapeleka ndugu na jamaa zao kwa waganga wa kienyeji.

Alisema wapo wagonjwa huwapokea wakiwa wameshacheleweshwa mno, kwa kule ndugu na jamaa zao, wanapowagundua kuwa wanaumwa, hukimbilia kwa waganga wa kienyeji, badala ya hospitali na vituo vya afya.

Mratibu huyo alisema, Wizara ya Afya Zanzibar katika kulijali kundi la watu wenye ugonjwa wa akili na wale walemavu wa akili, imeweka huduma zao kwenye vituo vyote vya afya hadi vya vijijini.

Alisema hilo limewekwa, ili sasa kuwapunguzia masafa wananchi, wanaotaka huduma za afya ya akili, ambapo hapo zamani, walilazimika kwenda hospitali za wilaya pekee.

“Ilikuwa huduma hizi za afya ya akili, zinapatikana hospitali za wilaya za Wete, Mkoani na Chake Chake lakini sasa hata kwenye hospitai za coteji na vituo vyote vya afya, huduma hizi zinapatikana,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Mratibu huyo wa Huduma za Afya ya Akili Pemba Salim Khamis Ali, alisema wagonjwa hao wamekuwa wakiongezeka siku hadi siku kisiwani Pemba.

Alisema, hilo husababishwa na mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na masongo wa mawazo, au wakati mwengine mtu kukumbwa na magonjwa mengine kama vile Ukimwi.

“Hata magonjwa kama vile Ukimwi au mtu kuondokewa na mpendwa wake ghafla, haya yote yanaweza kusababisha kukumbwa na ugonjwa wa akili,’’alifafanua.

Baadhi ya wananchi kisiwani Pemba, wamesema bado jitihada za makusudi, zinahitajika ili kulilinda kundi la watu wenye ugonjwa wa akili na hata wale wenye ulemavu wa akili.

Mratibu wa Jumuia kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa akili Zanzibar ZAPPD, tawi la Pemba, Khalfan Amour Mohamed, alisema bado jamii imekuwa ikiwadharau watu wenye ulemvu wa akili.

Alisema, pamoja na mchango mkubwa walionao wananchi wenye ulemavu wa akili, lakini bado jamii haijaona umuhimu wa kuwashirikisha katika shughuli za kila siku.

‘’Wakati mwengine watu wenye ulemavu wa akili huwekwa kundi moja na wale wagonja wa akili, ingawa kitaalamu hao ni makundi mawili tofauti,’’alisema.

Mfanyabiashara wa nguo katika mji wa Chake chake ambae anaulemvu wa akili Maulid Ali Kassim, alisema changamoto kubwa anayoiona kwa jamii ni kutowakubali wao.

‘’Bado jamii haijatuamini kuwa sisi ni sehemu yao, na ndio maana kila tunachokifanya sisi tunabezwa na kuonekana hatuna mchango kwa taifa,’’alisema.

Asha Said Idd ‘dada a’ mwenye ulemavu wa akili mkaazi wa Mkoani Pemba, amesema kama sheria hazijatekelezwa ilivyo, kundi hilo linaweza kuendelea kudai haki zao kila siku.

Waziri katika Ofisi ya Makamu wa Kwanza Zanzibar Harusi Said Suleiman, alisema wamo kwenye mchakato wa kuifanyia marekebisho sheria ya watu wenye ulemavu nambari 9 ya mwaka 2006.

                                     Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...