Skip to main content

''MZEE SODA MIAKA 76 NDIYE ALIYEMBAKA MTOTO WA MIAKA 13'' MPELELEZI ADAI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA::

ASKARI mpelelezi wa kituo cha Polisi wilaya ya Chake chake Lailat Mgindo Nassor, amedai mahakamani kuwa, taulo aliyoitaja mtoto, kuwa alikuwa ameivaa mtuhumiwa, kabla ya kumbaka, ndio aliyoikuta chumbani mwake, wakati wa upekuzi.

 

Alidai kuwa, kielelezo chengine kilichompa uhakika kuwa, mzee huyo wa miaka 76, ndie aliyembaka mtoto huyo wa miaka 13 ni kukimbilia mkoani Tanga, mara baada ya walalamikaji kutoa taarifa kituo cha Polisi.

 

Askari huyo mpelelezi, alidai hayo mbele ya mahakama maalum ya makosa ya udhalilishi ya mkoa wa kusini Pemba, wakati akitoa ushahidi wake, huku akiongozwa na wakili wa serikali, Ali Amour Makame.

 

Alidai kuwa, wakati familia ya mtoto huyo ilipofika kituo cha Polisi kutoa taarifa, walifika nyumbani kwa mtuhumiwa huyo kwa ajili ya kumkamata, ingawa alishatoroka na kwenda mkoani Tanga.

 

‘’Nilijua kuwa alikuwa mkoani Tanga, maana Jeshi la Polisi liliwakamata watoto wake na kuwaweka ndani, ingawa wiki mbili baadae, mtuhumiwa alifika kituo cha Polisi mwenyewe, na watoto wake kuachiwa,’’alidai.

 

Aidha askari huyo mpelelezi alidai kuwa, baada ya kufika kituo cha Polisi Mei 30 mwaka huu, waliambatana na mtoto aliyedai kubakwa hadi nyumbani kwa mtuhumiwa eneo la Mtoni wilaya ya Chake chake, kwa upelelezi zaidi.

 

Aliendelea kudai kuwa, baadhi ya vielelezo kama vile taula, mashuka na seruni ambazo mtoto alizitaja, walizikuta chumbani mwa mtuhumiwa.

 


‘’Mtoto alitupitisha mlango wa nyuma, ambako kuna migomba na ndio mlango aliopitishiwa na mtuhumiwa kabla ya kubakwa siku ambayo alida alimuita kwa ajili ya kumtuma dukani,’’alidai.

 

Kwa upande wake shahidi daktari wa hospitali ya Chake chake Fatma Kassim Ali alidai kuwa, baada ya kumfanyia uchunguuzi mtoto huyo, aligundua kuwa anamichaniko na mipasuko mikongwe kwenye sehemu yake ya siri ya mbele.

 

Alidai kuwa, michaniko hiyo inaweza kusababishwa na mambo kadhaa, ikiwa ni pamoja na kuingiliwa, kuchanika kwa kufanya mazoezi au kuingizwa kitu mithili ya vijiti au kidole.

 

‘’Ni kweli mtoto nilimgundua na michaniko kwenye sehemu zake za siri, lakini inaonesha ni ya zamani kama mwaka mmoja uliopita, maana kama ni mipya damu au unyevu unyevu wengekuwepo unaoashiria maumivu,’’alidai.

 

Awali mara baada ya mtuhumiwa huyo kuwasili mahakamani hapo akitokea rumande, Mwendesha mashataka kutoka Afisi ya Mkurugenzi wa mashataka Ali Amour Makame, alidai kuwa shauri hilo, lipo mahakamani kwa ajili ya kusikiliza mashahidi.

 


Mara baada ya mashahidi hao wawili kumaliza ushahidi wao, na kutimiza idadi ya mashahidi wanne, Hakimu wa mahakama hiyo Muumini Ali Juma, aliupa nafasi upande wa utetezi kuwauliza maswali mashahidi hao.

 

‘’Kwanini Jeshi la Polisi liliwakamata watoto wa mtuhumiwa je, ilikuwa kosa lao ni nini, wakati mtoto aliyedai kubakwa alimtaja baba mzazi wa watoto hao,’’wakili wa utetezi Abeid Mussa Omar alimuuliza askari mpelelezi mahakamani hapo.

 

Aidha wakili huyo wa utetezi, alimuuliza shahidi muuguzi, sababu ya kumchukuguuza mtoto aliyefikishwa hospitali, wakati yeye hana cheo cha udaktari, na kujibu kuwa anayomafanzo juu ya uchunguuzi wa wahanga wa aina hiyo.

 

Mara baada ya kumaliza ushahidi wao, hakimu wa mahakama hiyo Muumini Juma Ali, aliliagharisha shauri hilo Novemba 7, mwaka huu, huku upande wa mashataka ukifunga ushahidi wake, na siku ambayo mahakama itatoa uamuzi juu ya kesi hiyo.

 

 Awali ilidaiwa mahakamani hapo kuwa, mtuhumiwa huyo Khamis Juma Chumu ‘soda’ (76) mkaazi wa Mtoni wilaya ya Chake chake, alidaiwa kumtorosha mtoto wa kike miaka 13, wakati akienda kuchota maji mferejini, na kumpeleka nyumbani kwake.

 

Kufanya hivyo ni kosa, kinyume na kifungu 113 (1) (a) cha sheria ya Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018, sheria ya Zanzibar.

 

Kosa la pili ni la ubakaji, ambalo anadaiwa kulifanya Mei 15, mwaka huu, ambapo anadaiwa kumbaka mtoto huyo majira ya saa 4:15 asubuhi, eneo la Mtoni wilaya ya Chake chake.  

 

Kufanya hivyo ni kinyume, na kifungu 108 (1), (2) (e) na kifungu cha 109 (1) cha sheria ya Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018, sheria ya Zanzibar.

 

                Mwisho     

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch