Skip to main content

LSF: 'CHAPO CHAPENI KAZI'

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA::

MFUKO huru wa msaada wa kisheria ‘LSF’ umeutaka uongozi wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ kufanyakazi zao kwa umakini mkubwa, ili kuendeleza sifa yao ya utendaji kazi.

 

Ushauri huo umetolewa na Afisa Program Mwandamizi kutoka mfuko huo Zanzibar, Alphonce Marandu Gura, wakati akizungumza na watendaji wa ‘CHAPO’ ofisini kwao mjini Chake chake, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kujitambulisha kwa jumuia za wasaidizi wa sheria kisiwani Pemba.

 

Alisema, anayotaarifa ya uchapaji kazi wa watendaji wa CHAPO, hivyo amewakumbusha kuendelea kufanyakazi kwa uweledi na ushirikiano, ili waendelee kujijengezea saifa kwao na jamii kwa ujumla.

 

Alisema, CHAPO ni tegemeo kubwa la wananchi wa wilaya ya Chake chake, hivyo lazima waelewa thamani hiyo, na kuithamini katika kazi zao za kila siku.

 

Alieleza kuwa, kazi ya kuihudumia jamii ni nzito na inakuwa na changamoto kadhaa, na wakati mwengine bila ya kuwepo kwa ufadhili, hivyo ni wajibu wakaendelea kulijua hilo.

 

‘’Mimi kwa mujibu wa maelezo yenu na ripoti zenu, niwapongeze kwa kuendelea kuchapa kazi kubwa na ngumu ya kutoa elimu, msaada na ushauri wa kisheria kwa jamii bila ya malipo,’’alieleza.

 

Hata hivyo Afisa huyo Program Mwandamizi wa ‘LSF’ ofisi ya Zanzibar Alphonce Marandu Gura, aliihimiza ‘CHAPO’ kutuma ripoti zao kwa wakati na zilizokamilika, ili iwe rahisi kuzifanyia uchambuzi.

 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali, alisema ujio wa mtendaji huyo wa ‘LSF’ umewapa ari, nguvu na hamasa ya kufanyakazi zaidi.

 


Mkurugenzi huyo, alimuahidi Afisa huyo kuyafanyia kazi maelekezo na ushauri wake, na hasa eneo la kutuma ripoti kwa wakati na iliyokamilika, kwani wamekuwa wakipata mafunzo juu ya namna ya kuandika ripoti.

 

‘’Sisi kwanza tushukuru kwa ugeni huu kutoka ‘LSF’ kuja kujitambulisha kwetu, baada ya mtendaji aliyekuwepo kumaliza muda wake, na huyu mpya tutashirikiana nae kikamilifu,’’alisema.

 

Mshika mfedha wa ‘CHAPO’ Riziki Hamad Ali, alisema changmoto iliyopo kwa sasa, ni ukosefu wa mafunzo zaidi ya kujengewa uwezo, juu ya mifumo ya matumizi na ulipaji fedha kwa njia ya kisasa.

 

Afisa sheria kutoka Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Pemba Bakar Omar Ali, aliwakumbusha watendaji wa CHAPO, kufanyiakazi kwa vitendo, kila aina ya mafunzo waliopewa.

 


Kwa upande wake Msaidizi mratibu wa ‘CHAPO’ Khadija Said Khalfan, alisema shughuli za kutoa elimu, ushauri na msaada wa kisheria zinakwenda vizuri kwa jamii ya wilaya ya Chake chake.

 

‘’Hapa CHAPO iendelee kujengewa uwezo zaidi, ili ifike pahala iweze kujisimamia wenyewe, badala ya ilivyo sasa kutegemea wafadhili kwa kila kitu,’’alishauri.

 

Afisa Ufuatilia wa zone ya Pemba, Hamisa Bakar Hamad ameutaka uongozi wa ‘CHAPO’ kuendelea kushirikiana na mtendaji huyo wa ‘LSF’ ili kila upande ufanikishe kazi zake.

 

Alieleza kuwa, kila baada ya muda watendaji hubadilika, ingawa tasisi huwa ni ile ile, hivyo kama walivyokuwa wakifanyakazi na mtendaji wa LSF na aliyemaliza muda wake, nI vyema na kwa huyo mpya kushirikiana nae.

 

Hata hivyo ameutahadharisha uongozi wa CHAPO wasijaribu kufanya matumizi ya aina yoyote ambayo hayamo kwenye mpango kazi wao mkuu.

 




Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba, ‘CHAPO’ ambayo shughuli zake kuu ni kutoa elimu, ushauri na msaada wa kisheria bila ya malipo, inawahudumia wananchi wa shehia 32 zilizomo kwenye majimbo ya Chake chake, Wawi, Ole, Chonga na Ziwani.

               Mwisho   

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch