Skip to main content

UCHUMI WA WANAWAKE KASKAZINI PEMBA WAPIGWA MBELEKO NA BARABARA ZA MCC

 

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA:

MYORORO wa thamani katika kuinua kipato cha wajasiriamali, chachu kubwa ni uwepo miundombinu ya uhakika wa barabara.

Ambayo huwaunganisha wajasiriamali hao na wateja wao, iwe walioko kwenye masoko makuu au wale mmoja mmoja katika vitongoji na vijiji, au mitaa.

Aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa rais Zanzibar (marehemu) Maalim Seif Sharif Hamad, aliwahi kusema kuwa, mnyororo wa thamani huanzia kwenye kilimo, uvunaji, soko la uhakika, ubora wa bidhaa na miundombinu ya uhakika ya barabara.

Kilomita 35 za barabara zilijengwa kwa kiwango cha lami kwa ufadhili wa watu wa Marakeni kupitia mradi ‘MCC’ zikijumuisha ile ya Kipangani-Kangagani, Chwale-Kojani, Mzambarau takao-Pandani Finya na ile ya Bahanasa- Mtambwe.

BAADA YA UJENZI WA BARABARA HIZO

Kuanzia mwaka 2014, wanawake walichangamkia kuanzisha vikundi vya ushirika, ili kutanua pato lao, kupitia kazi wanazozifanya.

Wakati aliyekwuwa rais wa Zanzibar wa awamu ya sita Dk. Ali Mohamed Shein, akizifungua barabara hizo, alisema anataka kuona, kuimarika kwa uchumi wa wananchi, kwa kuwepo barabara hizo.

Na hata aliyekuwa Kaimu balozi wa Marekani nchini Tanzania wakati huo Virginia Blaser, alisema uwepo wa barabara hizo, iwe ni daraja la kuwaunganisha kibiashara, wananchi walioko mjini na vijijini.



‘’Leo tunazindua barabara hizi, kwa wananchi pamoja na kuwa na usafiri wa uhakika, lakini ziwe chachu za kukuza na kuendelea ama kuanzisha biashara,’’anasema.

WANAHARAKATI

Siti Habibu Mohamed, anasema wanawake ndio washirika wakuu wa kuleta maendeleo, sambamba na kukuza pato lao, ambapo uwepo wa barabara hizo za ‘MCC’ zimewasaidia.

‘’Wapo wanauchumi kadhaa wanaamini kuwa, uwepo wa barabara kunauhusiano mkubwa na wanawake kukuza pato lake, maana pia ndio wahanga wa changamoto za kutofikia ndoto zao,’’anasema.

Walikuwa wakiwahamasisha wanawake kujikusanya pamoja na kuanzisha vikundi vya ujasiriamali, ikiwemo ufugaji na kilimo, ingawa walikuwa wagumu, lakini baada ya mwaka 2014, sasa wamehamasika.

Afisa Miradi kutoka Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba, Asha Mussa Omar anasema, awali ilikuwa ni changamoto kwao kuwafikia wanawake, ili kuwapa mbinu za kukuza mitaji yao.

‘’Kwa sasa, uwepo barabara hizi za ‘MCC’ kwa kiwango cha lami, zimewapa urahisi wanawake, kutoka vijijini kwenda mjini, iwe ni kwa ajili ya kutafuta soko au kufuatilia rasilimali,’’anasema.

Anaona, ingekuwa sio rahisi kwa wanawake, kutoka kisiwa cha Kojani au Kangagani na Mtambwe, kuwaona kwenye maonyesho ya kitaifa, maana hapo awali, walikuwa wakikabiliwa na changamoto za uchakavu wa barabara.

‘’Leo sisi tunajivunia, kuona hata hali za wajasiriamali tunaowasimamia na hasa kwenye zile barabara tano, wanafursa ya kutoka na kuingia kwa wateja wakati wowote, tofauti kabla barabara hizi kujengwa,’’anasema.

Kwa sasa anaona kuna mpishano mkubwa wa biashara, kati ya wanawake wa kijiji kimoja na chengine, maana usafiri umeimarika, baada ya kuwepo kwa barabara za hakika.

‘’Bidhaa kama Vanila, iliyolimwa na wajasiriamali wanawake Mtambwe sasa imekuwa maarufu, katika masoko ya miji ya Wete na Chake chake na nje ya Pemba, na hata usafirishaji baada ya kuwepo kwa pikipiki ni rahisi,’’anasema.

Kwa kuimarika huko miundombinu ya barabara, sasa TAMWA inavyovikundi 12 vya wajasiriamali wanawake, vinavyojumuisha wanachama 210 kutoka vijiji vilivyopitiwa na barabara za ‘MCC’ mkoa wa kaskazini Pemba.

WAJASIRIAMALI

Hamid Juma Mohamed, wa Uwondwe shehia ya Mtambwe mkoa wa kaskazini Pemba, anaendesha maisha yake kupitia uwekaji na ukopaji wa fedha ‘saccos’ anasema, wamehamasika kuanzisha vikundi vya kilimo cha mboga baada ya kuwa na usafiri wa uhakika.



‘’Sasa tunavuna mboga saa 12:00 asubuhi na saa 12:45 tumeshafika soko la mjini Wete kwa kuuza, ingawa kabla ya ujenzi wa barabara yetu kwa kiwango cha lami, hatukufikiria kuwa na kilimo cha aina hii,’’anasema. 

Meiye Hamad Juma, anasema uwepo wa barabara ya uhakika ni eneo kubwa la kukuza pato lao, na kinyume chake ni kudhoofisha juhudi zao.

‘’Mimi kwa sasa naweza kumtuma mwenye piki piki wakati, siku na muda wowote kunipelekea bidhaa au kunichukulia mali ghafi, maana barabara ni ya uhakika na sio kama zamani,’’anasema.

Salma Hassan Shaame, anaefanyabiashara za nguo kijijini hapo, anasema uwepo wa barabara hiyo, kwa sasa imekuwa chachu ya kukuza pato lake, kutokana na ongezeko la wateja.

‘’Wakati barabara haijajengwa, ilikuwa mauzo yangu kwa siku hayazidi shilingi 60,000 ingawa kwa sasa huuza kati ya shilingi 100,000 hadi shilingi 120,000,’’anasema.

Hata mkulima wa tungule na njugu kijiji cha Kangagani wilaya ya Wete, Aisha Msabaha Himid, anaona sasa wateja wake wanamfuata shambani, hata kipindi cha mvua, kutokana na uwepo wa barabara ya uhakika.

‘’Kabla ya kujengwa kwa barabara hizi na MCC ilikuwa, baada ya kuvuna unaweza kuweka mazao ndani hata mwezi mmoja, ili asubiri mvua zipite na kuyasafirisha mazao kwenda sokoni, lakini kwa sasa wakati wowote unasafirisha,’’anasema.

Kama alivyo Mwajuma Issa Haji wa Pandani, anasema kwa muda mrefu anafuga kuku wa kienyeji, lakini alikuwa akiuza kwa bei ndogo, maana wateja walikuwa wakimfuata.



‘’Sasa hukusanya kuku wangu kati ya 30 hadi 50 na huwaingiza garini hadi soko la Wete, na huuza mmoja kati ya shilingi 15,000 hadi shilingi 20,000 ingawa hutegemeana na ukubwa,’’anafafanua.

Hapa anasema bei hizo hakuwahi kuzipata kwa vile uchakavu wa barabara yao kwa Pandani kwa wakati huo, ulichangia wateja wanaomfuata kumlalia kibei.

Kumbe hata Ashura Makame Mjaka wa Kojani, anasema bidhaa yake ya mafuta ya nazi, unga wa karafuu na mapambo ya akinamama, amepata umaarufu na kuongeza wateja.

‘’Ilikuwa ikfika saa 10:00 jioni popote nilipo nianze safari ya kurudi Kojani, maana uchakavu wa barabara ulikatisha tamaa ya usafiri, ingawa kwa sasa wakati wowote sina wasi wasi,’’anasema.

Anauza kati ya shilingi 75,000 hadi shilingi 85,000 kwa siku katika mitaa ya Mchanga mdogo, Madenjani, Kangagani na Shengejuu jambo linalokuza pato lake.



Mwanzilishi wa usafiri wa chombo aina ya bajaji barabara ya Kipangani- Kangani Omar Abdalla, anasema nae amekuza pato lake, kwa kuwasafirisha abiria kutoka Kangagni hadi njia kuu, ya kwendea miji ya Wete, Chake chake, Micheweni na Mkoani.

‘’Kwa siku hujipatia kati ya shilingi 60,000 hadi 70,000 ingawa hutegemeana  na mwamko wa wasafiri wenyewe, lakini kwa hakika uwepo wa barabara hii iliyojengwa na watu wa Marekani, kwangu ni mkombozi,’’anasema.

Mfanyabiashara wa duka la chakula eneo la Mzambarau takao, Mohamed Omar Habibu, anasema kabla ya ujenzi, wananchi wa Pandani walikuwa wakilaza vyombo vyao vya usafiri, uwanjani kwake.

‘’Wakati mimi nasoma, lazima ilikuwa hadi wanafunzi tujukusanye sita au saba, ili tufuatane kutokana na pori lililokuwepo, ingawa baada ya ujenzi wa kiwango cha lami, sasa nafuu ipo,’’anasema.



Anapotaka kusafirishia bidhaa zake kutoka miji ya Konde, Mapofu na Micheweni kuleta dukani kwake, anaitumia barabara hiyo ya Pandani kutokana na kujengwa kwa kiwango cha lami.

SERIKALI

Afisa Mdhamini wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Uchukuzi Pemba Ibrahim Saleh Juma, anasema tokea kufunguliwa kwa barabara hizo miaka tisa (9) iliyopita hawajawahi kuzifanyia matengenezo, kutokana na uimara wake.

‘’Matengenezo tuliyoyafanya ni barabara ya Bahanasa- Mtambwe kwenye daraja, baada ya kuharibika kutokana na mvua kubwa, iliyonyesha mwaka 2017 na kwa sasa barabara zote tano, ziko madhubuti,’’anasema.

Mhandisi mkaazi mstaafu wa waujenzi wa barabara Pemba wakati wa ujenzi wa barabara za MCC, Khamis Massoud Khamis, anasema uimara wa barabara hizo, ulitokana na aina ya ujenzi.

Anasema ujenzi wa barabara hizo umetofautiana na nyingine, maana tabaka mbili za juu ‘sub base and base’ zilichanganywa kokoto nyembamba na saruji, kwa ujazo wa mita moja na kwa mfuko mmoja wa saruji.

Aina ya ujenzi wa barabara hizo za MCC hazikutumia lami moto ‘asphalt congreate’ bali zilitumia mfumo wa lami ya kuchemsha ‘surface dressing’ na kisha kumwagwa, baada ya muda humiminiwa kokoto zenye ujazo wa milimita 15 hadi 20 na kuzama kwenye lami hiyo.

‘’Baada ya kushindiliwa hadi kuzama kwa kokoto, humwagwa tena lami zikiwa na kokoto ndogo ndogo, zenye ujazo kati ya milimita 8 hadi 10, lengo ni kuziba nafasi ilizoachwa wazi, na kokoto kubwa za awali,’’anafafanua.



Jengine linalotofautiana kwenye ujenzi wa barabara hizo za MCC, ni kutumia shilingi bilioni 1.1 kwa urefu wa kilomita 1, wakati ujenzi wa barabara za kawaida kwa urefu huo, ni hugharimu shilingi bilioni 1.

‘’Ujenzi wa aina hii ya barabara za MCC hutakiwa kufanyiwa matengenezo kila baada ya miaka 10, ingawa kwa kwetu zinaweza kuzidi kutokana na kutokuwepo kwa gari nyingi zenye uzito wa zaidi tani 15, kama uhimili wa barabara zinavyotakiwa,’’anasema.

Hata hivyo Afisa Mdhamini wa sasa wa barabara Ibrahim Saleh Juma anasema, wamekuwa wakiziangalia kila muda barabara hizo, na hawatosita kuzifanyia matengenezo yatakapohitajika.

                                                Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch