Skip to main content

WASAIDIZI WA SHERIA TARAJALI PEMBA WAKUMBUSHWA JAMBO

 

NA HAJI NASSOR, PEMBA 

WASAIDIZI wa sheria tarajali kisiwani Pemba, wameelezwa kuwa, moja ya jambo linalowaondoa kwenye usaidizi wa sheria, ni kujiingiza kwenye siasa za wazi wazi.

 

Hayo yameelezwa na Afisa sheria kutoka Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Zanzibar, Ali Haji kwenye mafunzo yanayoendelea ya siku 15, yanayofanyika Chakechake. 

 

Alisema kila mtu kikatiba yuko huru kuamini dini na hata imani ya chama cha siasa akipendacho, ingawa kwa wasaidizi wa sheria, lazima wajiwekee mipaka.

 

'’Ni haki ya kikatiba kushiriki katika masuala ya siasa na hasa kuchagua na kuchaguliwa, ingawa kwenu wasaidizi wa sheria muwe makini na ushabiki wa kupindukia,’'alieleza.

 


Kwa upande wake Naibu Mkuu wa skuli ya sheria Zanzibar kitengo cha taaluma, Msemo Mavare alisema suala la kuthibitisha jambo mahakamani, lina njia zake kadhaa.

 

Alisema mfano ni kukiri jambo ‘confession’ pasi na kutenzwa nguvu, kuahidiwa jambo, sambamba na njia ya kuwa na mashahidi.

 

Hivyo amewashauri wasaidizi hao wa sheria tarajali, kuisoma kwa kina sheria ya ushahidi, ili kuwasidia wananchi wanaowafikia kutaka msaada na ushauri wa kisheria.

 

"Sheria hii ya ushahidi ni kubwa, lakini hamna budi kuipitia na kuisoma vile vifungu muhimu, kikiwemo cha nani shahidi, aina ya ushahidi pamoja na njia za kutoa ushahidi," alisema.

 

Akiwasilisha mada ya njia za unasihi kwa wahanga wa matukio ya udhalilishaji, Afisa Idara ya ustawi wa jamii Pemba Fatma Abdalla, alisema ni eneo linalohitaji ujuzi wa hali ya juu.

 

Alifahamisha kuwa, shurti moja wapo kwa mtoa ushauri nasihi ni kumjua kwa kina mteja wake, aina ya udhalilishaji aliyofanyiwa na athari.

 

"Huwezi kuwa mshauri nasihi mzuri, ikiwa hawezi kujenga masuali yanayoweza kukupa taarifa, pamoja na ujuzi wa uchaguzi wa lugha,"alifahamisha.

 

Mapema wakili wa serikali Seif Mohamed Khamis, aliwataka washiriki hao, kuhakikisha wanaielewa katiba hasa vile vipengele muhimu zaidi.

 

‘’Kwa mfano Katiba ya Zanzibar yam waka 1984, kuanzia kifungu cha 11 hadi cha 25 kinachoeleezea haki za binadamu, muhakikisha mnavipitia mara kwa mara,’’alishauri.

 

Baadhi wa washiriki, walisema elimu hiyo ni nzuri ingawa changamoto iliyobakia ni jamii kubadili mtazamo kuwa hilo ni jukumu la serikali pekee.

 

Mshiriki Juma Seif kutoka jimbo la Chonga, Wahida Kombo Khamis wa jimbo la Chake chake na Fatma Hamad Faki wa jimbo la Wingwi wameahidi kuifikisha elimu hiyo kwa jamii.

 

                           mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...