Skip to main content

AMINA SHAABAN: MLENGWA WA TASAF PEMBA ANAYEUSHANGAAZA UMMA

 




NA HAJI NASSOR,  PEMBA

“KABLA ya kuja kwa mpango wa kunusuru kaya maskini, hali yangu ya maisha ilikuwa ya kubahatisha hasa kujipatia mlo walau wa siku, ilikua kazi,’’

Ni maneno ya mwanzo ya mlengwa huyo wa TASAF, Amina Shaaban Shamte, alipokuwa akizungumza nami, kwenye eno lake la malisho ya wanyama kijijini kwake Mgogoni wilaya ya Wete Pemba.

Amina kabla ya kutuliwa na TASAF mikononi mwake, ilikuwa jambo la kawaida, kutimiza siku tatu bila ya mlo hata ule wa kumuwezesha kuishi.

 “Kwanza niwashukuru viongozi ambao walileta huu mpango wa kaya maskini, mfumo huu umekuwa ni mkombozi mkubwa   kwetu sisi ambao tuna hali ngumu za maisha”, anasema.

Bi Amina anasema, kabla ya kuja kwa mpango huo wa kunusuru kaya maskini, hakuwa na shughuli yoyote ya kujipatia kipato lakini baada ya kufikiwa na TASAF aliweza kujishuhulisha na biashara ya kuuza nazi na ndio safari yake ya kuona mwanga ilianzia.

Katika kipindi hicho ambacho TASAF haijamfikia, watoto wake kwenye suala la kusoma ilikua ni kwa njia ya kubahatisha, hali iliyopelekea siku moja mtoto wake kusitishwa masomo kwa ukosefu wa ada.

Kumbe sababu ya tukio, hilo ni baada ya mtoto wake kutotoa ada ya shilingi 10,000 ingawa kwa wakati huo nae ilimkwama kooni na kubakia nyumbani

“Kwa kipindi hicho kutokana na hali yangu ya kimaisha, shilingi 10,000 ilikua ni sawa na milioni moja, ingawa alirudi lakini baada ya dhiki na tabu iliyonitoa kijasho,’’anasema.

BAADA YA TASAF

Kwa mara ya kwanza ulipoanza mpango huo wa kaya maskini hakuamini, wakati sheha wake alipomwendea, kwa kuanza kumuandikisha jina kwa ajili ya kufanyiwa usajili.

“Alikuja mwanamke ambae alitumwa na sheha akaniandika na kuniambia, kwa sababu ya ujane na watoto nilionao, kushindwa kujihudumia,’’anaeleza.

Anakumbuka kama leo, kwa mara ya kwanza alipokea shilingi 32,000, na alichukua hatua ya kuwanunulia watoto sare za skuli, mabuku na viatu.



Jengine alichokifanya ni kununua chakula pamoja na samaki mnene, na kwa mara ya kwanza, alikula chakula cha mchana akiwa na furaha na watoto wake.

Kisha kwa miezi menngine mlengwa huyo wa kaya maskini, alifikiria namna ya kuanzisha biashara ambayo ana hakika inaweza kumtoa kimaisha.

‘’Nilianza na ununuzi wa nazi za shilingi 20,000, ambapo kila nazi kwa kipindi hicho nilinunua kwa shilingi 200 na baada ya kuuza kila moja kwa shilingi 500 na kujipatia faida ya shilingi 30,000,’’anasimulia.

Biashara ya nazi, iliendelea kumnogesha na kumuingia moyoni maana, kisha alijikuta na mtaji wa shilingi 150,000 unaotokana na biashara hiyo.

Baadae Amina, alifungua njia nyingine ya kujiongezea kipato, baada ya kuingia kwenye ununuzi wa nguo za mitumba na hasa za kitoto.

“Niliagizia kutoka Unguja roba  bota la nguo hizo kwa shilingi 150,000 na kisha baada ya kuziuza nilijipatia faida ya shilingi 50,000 nilinogewa na kuendelea tena,’’anaeleza.

 Maajabu na hamu ya kufanya biashara hiyo hasa aliyaona kwenye awamu tatu, pale alipochomoa shilingi 300,000 kujitupa tena Unguja, na safari hii akiingiza faida ya shilingi 150,000.

Kumbe Amina, pamoja na biashara yake hiyo, kisha alizaa fikra na hamu ya kununua mifugo, ili maisha yake ayatawale.

 ‘’Nilitumia shilingi 300,000 kununua mtamba wa Ng’ombe ingawa baada ya muda alizaa na kujipatia dume, ingawa nalo halikudumu nilimuuza baadae,’’anaeleza.



Hata mara ya pili, alibahatika Ng’ombe dume ingawa nilimuuza kwa shilingi 500,000 na hapo sasa hatua iliyofuata ni kutaka kuanzisha ujenzi wa nyumba ya kudumu.

Maana wakati huo anaendelea kupokea fedha za mpango wa kunusuru kaya maskini, Amina alikuwa akiishi kwenye nyumba ya tope tena ya kuazimwa.

Kwa sasa akiwa anaishi kwenye nyumba yake ya tofali yenye vyumba vitatu, kwa mchango wake wa hapa na pale, tayari ameshatumia shilingi milioni 5.

‘’TASAF imenitoa kwenye nyumba ya kuazimwa tena ya tope na makuti, na sasa naishi kwenye nyumba ya kifahari iliyoezekwa bati,’’anafafanua.

Sasa anajisifia kuwa ana uhakika wa maisha, achia mbali mlo wa mara tatu kwa siku, jambo ambalo anasema hakuwahi kuliota kwenye mbio zake za maisha.

 MPANGO WAKE WA BAADAE

Moja ni kumalizia kuizeka nyumba, na kutoa mlango maalum wa duka, ili sasa ahamie kwenye biashara ya nguo mpya (special) huku akiendelea pia na nguo za mtumba.



Alifahamisha, mpango wake mkubwa wa baadae ili kuona anaishi katika mazingira bora ni kumaliza kujenga nyumba yake na kueka duka la nguo mpya.

Malengo haya anaweza kuyafikia, maana pamoja na biashara zake hizo pamoja na ufugaji, Amina ni mwanachama wa ushirika unaojishughulisha na ufugaji.

Ushirika huo, uitwao ‘nia njema’ kwake anauona kama dhahabu, maana umekuwa sehemu ya kung’arisha maisha yake ya kila siku.

SHEHA

Sheha wa Shehia ya Mgogoni Said Hamad Khamis, anasema wakaazi wa shehia hiyo ni 4,326 kati ya hao waliomo kwenye kaya maskini ni 143 tokea mwaka 2014 akiwemo Amina.

Anasema, mpango huo wa kunusuru kaya maskini, umeibua miradi kadhaa ya maendeleo ndani ya shehia, ikiwemo ya ufugaji, ujasiriamali na kilimo cha mboga mboga.

 ‘’Kwa mfano pia ipo miradi ya jamii kama ule wa maji safi na salama unaowahudumia wananchi 4000 na uwepo wa kinu cha kusagishia nafaka unaosimamiwa na watu wenye ulemavu,’’anaeleza.

Jambo la kujivunia katika shehia yao ni kuona baadhi ya wananchi waliokuwemo kwenye mpango wa TASAF wamepiga hatua kimaendeleo kwa kujipatia kipato chao wenyewe.

Anasema, changamoto kubwa ambayo imekuwa ikijitokeza wakati wa upokeaji wa fedha za TASAF ni masafa marefu wanayotembea walengwa na ukizingatia wengine ni watu wazima wasiojiweza.

TASAF.

Mratibu wa Mfuko wa maendeleo ya jamii Tanzania ‘TASAF’ Pemba Mussa Said Kisenge anasema, mpango wa kunusuru kaya maskini ni chachu ya kuleta maendeleo kwa wananchi.

Anasema walengwa 14,280 ndio wanaendelea kunufaika kupitia mpango huo wa kunusuru kaya maskini ata hivyo anasema, walengwa ambao wamefikiwa na mpango huo kwa Pemba kuanzia mwaka 2014 hadi 2019 ni 14,280 kupitia shehia 78, hadi sasa fedha zilizofikia mikononi mwa walengwa ni Billioni 14.4, ambapo kwa wastani kila mlengwa amepata shilingi 2,380/=.

                                                    MWISHO.

  

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch