Skip to main content

HIFADHI YA BURUNGE YAGEUKA DHAHABU

 



NA HAJI NASSOR,  PEMBA

TANZANIA imejaaliwa kuwa na vivutio mbali mbali vya utalii.

Vipo vivutio vya Serikali na vivutio vya jamii, vyote vikiwa na jukumu la kutangaza utalii wa Tanzania.

Miongoni mwa vivutio hivyo ni Mlima wa Kilimanjaro, hifadhi ya wanyama Serengeti, Tarangire, Burunge, Ngorongoro, pamoja na maeneo mengine ambayo watalii wanafika.

Hifadhi zote hizo zimekua ni chachu ya maendeleo kwa wananchi waliozunguka hifadhi hiyo, pamoja na taifa kwa ujumla katika kunufaika.

Moja ya hifadhi ambayo wananchi wamekuwa wakinufaika nayo kwa asilimia 100 ni hifadhi ya jamii Burunge ‘WMA’ iliyopo Babati Mkoani Manyara.

Wananchi wananufaika na hifadhii hii, kupitia hifadhi ya wanayama na Ziwa burunge, watalii wengi wamekuwa wakimiminika kutembelea hifadhi hiyo pamoja na kuangalia mafanikio ya ziwa hilo.

Hifadhi ya Burunge imezungukwa na vijiji 10 ikiwemo Sangaiwe, Mwada, Ngolei, Vilima vitatu, Kokoi, Minjingu na baadhi ya vijiji vyengine.

WANANCHI WANASEMAJE JUU YA UHIFADHI

Venust Peter wa Sangaiwe, amesema sekta ya uhifadhi ya wanyama kijiji kwao, imekua ni muhimu kabla ya WMA wanapotaka kufanya kitu kijiji hapo, lazima kuchangishana fedha na kiwango hakipatikani kwani wengine hukimbia kaya zao.

Sasa shuhuli zote za ujenzi hutolewa tenda na watu hupata pesa na mradi kukamilishwa kwa wakati na wananchi hawasumbuliwi tena kuchangia.

“Uhifadhi umetupatia kipato katika kijiji chetu, baada ya elimu tunalima na tunaendelea kuhifadhi wanyamapori, tulikua vijiji vitano sasa vimekua vijiji 10,”amesema.



Stellm Thomas (57) amesema kabla ya uhifadhi ilikuwa ni shida kijijini kwao, kila ujenzi unakaribia lazima kila kaya kuchangishwa shilingi 20,000 sasa imekua ni tafauti na huku vijiji vya jirani vikitamani kunufaika nao.

Kwa sasa hata watoto wanapata chakula skuli na matunda, kutoka katika hifadhi hiyo hii, hali inayowafanya kusoma kwa umakini sasa.

Hifadhi imeweza kujenga shule, vyumba vya kusomea wanafunzi na hata zahanati kijijini Sangaiwe.

Aambapo wajawazito wanajifungulia hapa na wahatembei tena umbali wa kilomita 8 kufuata kituo cha afya.

“Mimi natamani sasa nirudi katika ujana wangu, tulikua tunaenda zaidi ya kilomita 8 kufuata huduma za afya, sasa skuli  ipo, zahanati ipo kijijini kila kitu kipo sawa,”anasema.

Anastazia John Mwanso, anaeleza uhuifadhi umetusaidia kuanzisha vikoba kwa akinamama, ambapo wanakopeshana na baadhi yao wanafanya biashara ndogo ndogo.

UWEPO WA KAMERA WANANCHI WANASEMAJE KATIKA HIFADHI

Wanasema utasaidia wakulima wanaozunguka hifadhi, kupata mazao yao, mbayo walikuwa wakiyakosa kutokana na kuvamiwa na wanyama.

Kamera zitawekwa katika maeneo maamulu, ambayo wanyama wanapita na kuingia katika mashamba ya wakulima, wataweza kuonekana moja kwa moja na walinzi kwenda kumfurusha.

Emelda Patrick Sangu (49), amesema uwepo wa kamera umepelekea kuwapa matumaini makubwa wakulima wengi wanaozunguka hifadhi hiyo ya burunge.

“Uwekaji huo utaambatana na ujengaji wa vibanda pembezoni mwa hifadhi, kwa jili ya walinzi na kuweza kuwafurusha wanyama,’’anasema.



Mwanakijiji Mofulu Sangawa John (33), anasema licha ya mfumo huo kuchelewa kuwafika katika kijiji chao, wakulima wamekuwa na mategemeo makubwa, katika msimu huu kupata mazao mengi.

Kamera hizo zina uwezo wa kumurika umbali wa mita 100, sawa na wanja wa mpira wa miguu, na zitaweza kutoa taarifa mapema, iwapo kuna wanyama wanakaribia kuvuka eneo la hifadhi.

 KAMATI YA JAMII INAZUGUMZIAJE JUU YA UHIFADHI

Mwenyekiti wa kamati ya huduma za jamii Singaiwe Nikodemas Mofulu, amesema wananchi wanajivunia uhifadhi walionao baada ya elimu waliopatiwa.

Ambapo sasa wanapata fedha nyingi kufuatia kutunza eneo la hifadhi ya jamii, kwa ajili ya maendeleo yao.

Kwa sasa wamekua na hoteli za kigeni mbili na wanapata shilingi milioni 48 kwa mwaka, hali inayopelekea kupunguza shida ya masafa marefu ya watoto kufuata huduma za kijamii.

Kwa sasa hakuna kutembea zaidi ya kilo mita nane (8), kufuata zahanati vijiji vya jirani, watoto nao kuacha kuhatarisha maisha yao kwa ajili ya kufuata elimu,’’anasema.

VIONGOZI WA HIFADHI YA BURUNGE WANASEMAJE

Katibu wa ‘WMA’ hifadhi ya Jamii Burunge Benson Mwaise, anasema, wananchi wananufaika na ‘WMA’ kwa kutegemea kupata maji na watalii, hufurahia muonekano wake.

 Alivitaja baadhi ya vijiji zinavyonufaika ni pamoja na Sangaiwe, Mwada, Ngolei na Vilima vitatu, ambapo wamesaidiwa kupata huduma mbali mbali ikiwemo skuli, zahanati hata watoto kupikiwa chakula wanapokuwa masomoni.

Msaada mwengine wanafunzi kupatiwa usafiri wa basi, kutoka katika kijiji chao kwenda na kurudi skuli, pamoja na kuwashajihisha akinamama kujikusanya na kuanzisha ushirika.

“Kweli hifadhi hii imekua nimkombozi mkubwa kwa wananchi wa kijiji cha Sangaiwe na Vijiji jirani, wananchi walikuwa wakiona uhifadhi kama madhila sasa wanajua umuhimu wake,’’anasema.

Mwenyekiti hifadhi ya jamii Burunge WMA Khamis Juma Mgimba, anasema Sangaiwe ni moja ya vijiji ambavyo vinamuingiliano mkubwa na kimepakana na hifadhi ya Tarangire.

Aidha kina wanyama wengi tafauti vijiji vyengine vilivyopakana na hifadhi ya Burunge.

“Kwa sasa tupo na wataalamu kutoka chuo cha Nelson Mandela Arusha, wataweza kuwaweka teknolojia ya kamera itakayo tusaidia katika vijiji, kubaini wanyama wapi wamepita,”anasema.

 JET

Chama cha waandishi wa habari za Mazingira Tanzania (JET), kupitia mradi wa USAID “Tuhifadhi Maliasili” wakizungumza na timu ya wanachama wao, Mkurugenzi mtendaji wake John Chikomo, amesema JET inatekeleza mradi wa miaka mitano.

Ambapo mradi huo wa Tuhufadhi Maliasili, ulianza na mafunzo na baadae ni kutembelea katika shoroba sita zinazofanyiwa kazi.

Anasema kazi kubwa ni kuona waandishi wanazidi kuandika habari za uhifadhi, wanyamapori na shoroba kwa uhakika, likiwemo kundi la wanawake.

MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch