Skip to main content

WANAWAKE WAZIDI KUNGA’ARA KATIKA KAMPENI ZA UCHAGUZI MKUU 2025

 


NA AMRAT KOMBO, ZANZIBAR
Katika harakati za uchaguzi mkuu wa Tanzania unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025, wanawake wamekuwa miongoni mwa vikosi vyenye ushawishi mkubwa katika kampeni. 

Kutoka kuwa mashabiki wa pembeni hadi kuwa viongozi wa kampeni, wagombea, na waratibu wa mikutano, wanawake sasa wanathibitisha nafasi yao katika ujenzi wa demokrasia ya kisasa.

Vyama vya siasa vinatofautiana kwa kiasi kikubwa katika namna vinavyoshirikisha wanawake kwenye kampeni zao, lakini kwa ujumla, taswira ya mwaka huu inaonyesha mwelekeo chanya licha ya vikwazo lukuki.

Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) ilitangaza rasmi kuanza kwa kampeni za uchaguzi mkuu Zanzibar tarehe 11 Septemba 2025 , Kampeni hizo zitaendelea hadi 27 Oktoba 2025 Zanzibar kabla ya siku ya kupiga kura.

Tume hiyo imekamilisha uteuzi wa wagombea kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, ambapo Wagombea wa Urais wa Zanzibar 11, wagombea wa Baraza la wawakilishi 484 ,wagombea wa Udiwani 341.

Katika uzinduzi mkuu wa kampeni, chama Cha Mapinduzi CCM kilianza kufungua rasmi kampeni Zanzibar mnamo 13 Septemba 2025.

Katika harakati hizo mgombea wa urais kwa tiketi hiyo Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema kuwa serikali yake itaendelea kuweka mazingira rafiki kwa wanawake kushiriki kikamilifu katika siasa na uongozi.

“Hatuwezi kuwa na maendeleo endelevu bila ushiriki sawa wa wanawake katika maamuzi ya kitaifa,” Amesema Dkt Hussein

Dk.Mwinyi amesema anatambua watu wengi wanahitaji kuwezeshwa kiuchumi na kwamba awamu ijayo ataweka fungu kubwa zaidi ili kuhakikisha kila kundi linafikiwa.

"Tutawafikia wote katika uwezeshaji ninatoa ahaadi kwenu kuwa tutawafikia makundi yote kipindi kilichopita tulitoa sh.bilioni 96 kwa ajili ya kuwawezesha wananchi kiuchumi tumefanya kwenye sekta ya uchumi wa buluu yaani wavuvi,wakulima wa mwani,wajasiriamali wadogowadogo , ,bodaboda,"Amesema Dk Mwinyi

Kampeni za mwaka huu zimeonyesha picha tofauti, wanawake wakiongoza misafara, wakizungumza majukwaani, na wakitumia mitandao ya kijamii kuwasilisha hoja kwa ufasaha. Ujasiri huu umevutia vijana wengi na kuleta hamasa mpya katika siasa za Zanzibar.

Huku wakiwa wameshika bendera zao, wamejivika ujasiri, na kuingia majukwaani, kwa ajili kuthibitisha kwa vitendo kuwa wakipewa nafasi, wanaweza kung’aa zaidi ya vile jamii ilivyowahi kufikiri hali hii ni tofauti na kampeni za miaka iliyopita.

Mwaka huu wanawake wamekuja na ajenda zenye mguso wa moja kwa moja kwa wananchi, elimu bora, afya kwa wote, usawa wa kiuchumi, uwezeshaji wa vijana, na ulinzi wa mazingira.

Wagombea kama Laila Rajab Khamis ambae anagombea nafasi ya urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha NCCR-Mageuzi , Chumu Juma mgombea makamu mwenyekiti taifa wa Chama Cha Alliance for African Federal Party (AAFP) na mgombea Ubunge wa Jimbo la Makunduchi kwa tiketi ya ya Chama Cha Mapinduzi CCM ,Wanu Hafidhi Ameir wamekuwa mstari wa mbele kutetea sera zinazolenga kujenga jamii yenye fursa sawa kwa wote.

Katika mikutano yao ya kampeni, wamekuwa wakisisitiza kuwa wanawake si wa kutazamwa tu kama wapiga kura, bali kama viongozi wanaoweza kutatua changamoto zinazowakabili wananchi.

Kwa upande wa mgombea urais wa Zanzibar wa tiketi ya chama cha NCCR Mageuzi Laila Rajab Khamis katika kampeni zake amesema akipata ridhaa ya wananchi , ndani ya siku 100 za kwanza viwanda vitakuwa tayari kuanza kujengwa kwa ajili ya kuwapatia ajira vijana.

“Kama tutapata ridhaa ya wananchi , ndani ya siku 100 za kwanza viwanda vitakuwa tayari kuanza kujengwa. Tunataka vijana wa Zanzibar wawe na ajira za uhakika na wachangie maendeleo ya taifa leo”Amesema Laila akiwa kwenye kampeni katika kiwanja cha kibanda maiti.

Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Wanawake katika sheria na maendeleo Afrika (WiLDAF) Zanzibar, zaidi ya wanawake 300 wamepata mafunzo ya kujiandaa kwa uchaguzi wa mwaka huu, na wengi wao wamejipanga kushiriki kikamilifu katika kampeni za ngazi zote , kuanzia udiwani, ubunge hadi uwakilishi.

Kwa upande wa mgombea ubunge wa jimbo la makunduchi wa ticketi ya Chama Cha Mapinduzi CCM Wanu Hafidhi Ameir wakati wa kampeni amesema ,ameanzisha na kusimamia mafunzo kwa viongozi wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) ngazi ya matawi, wadi, jimbo na wilaya ili kuwajengea uwezo viongozi wanawake kwa kujifunza kuongoza kampeni, kujitokeza kwa nafasi za uongozi, na kujua wajibu wao ndani ya chama.

" Kuhakikisha huduma za afya za wanawake kliniki za afya ya uzazi, huduma za mama mjamzito, uchunguzi wa saratani zipo karibu na rahisi kufikiwa jimboni Makunduchi." Amesema Wanu akiwa kwenye kampeni huko Makunduchi Septemba 29 2025

Na kwa upande wa mgombea uwakilishi wa Jimbo la Kikwajuni Asiata Said Abubakar kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA ) wakati akihutubia katika kiwanja cha mjeru kisiwani Unguja amesema ,watahakikisha wanaendeleza miradi ya kiuchumi kwa lengo la kuwafungulia fursa vijana.  

“ Uchumi wa Zanzibar hauwezi kukua kama vijana wetu hawana nafasi ,tumechoka kuona vijana wakiwa watazamaji wa maendeleo”. Amesema Asiata

Wananchi nao hawakuwa nyuma katika kuwaunga mikono wagombea hao kwenye kampeni zao.

“ Tumezielewa ahadi za mgombea urais wa Zanzibar Laila kuhusiana na ujenzi wa viwanda na kuboresha huduma za afya , tumepata matumaini kuwa utekelezaji wa sera hizi utaongeza ajira kwa vijana “.Amesema Juma Mohameed wakati akisikiliza kampeni za mgombea laila huko kibandamaiti. 

“ Wananchi wa jimbo la makunduchi, tumeonesha kuridhika na uteuzi wa Wanu Hafidh kama mgombea ubunge kwani yeye ni kiongozi mzoefu na mwenye ufanisi katika kuleta maendeleo kwenye jimbo letu.” Amesema khamis Ali wakati akisikiliza kampeni za mgombea Ubgunge Wanu huko Makunduchi. 

“ Tunamkubali sana Asiata Said kwani yeye anajali masilahi ya wananchi wa jimbo la kikwajuni na anaweza kuleta mabadiliko katika sekta ya ajira.” Amesema Asha

Mashirika ya wanawake Zanzibar yamepongeza muamko huo ikiwemo Chama Cha Waandishi wa Habari Wanawake TAMWA- ZANZIBAR imetambua mchango wa wanawake 13 wanaotegemewa kugombea nafasi ya urais na umakamu wa rais katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 sawa na asilimia 36 ya wagombea wote 36 walioteuliwa na Tume ya Uchaguzi ya Taifa (INEC) kwa ngazi hizo mbili.

Mashirika hayo yamekuwa kiungo muhimu katika kuongeza mwamko huu. Kupitia miradi kama SWIL ambao mradi wa kuimarisha wanawake katika uongozi na demokrasia (Strengthen Women in Leadership ,wanawake wengi wamepata mafunzo ya kampeni, ujasiri wa kuongea hadharani, matumizi ya mitandao ya kijamii, na uelewa wa sheria za uchaguzi.

“Tunaona huu ni wakati muhimu katika historia ya siasa za Zanzibar na Tanzania kwa ujumla. Idadi ya wanawake 13 kati ya wagombea 36 wa urais na umakamu wa rais ni matokeo ya kazi kubwa ya miaka mingi ya kuwawezesha wanawake kupitia miradi kama SWIL. Hii inaonyesha kwamba wanawake sasa hawako nyuma tena, wanajiamini na wako tayari kuongoza,” amesema Mkurugenzi wa TAMWA–Zanzibar, Dkt. Mzuri Issa

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...