Skip to main content

ZEC YADAI KULAINISHA MAZINGIRA RAFIKI KWA MAKUNDI MAALUM UPIGAJI KURA

 


NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@

TUME ya uchaguzi Zanzibar ‘ZEC’ imesema imeshaandaa mazingira rafiki  kwa watu wa makundi maalumu, wakiwemo  wenye ulemavu, ili kuh’akikisha ushiriki wao, katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29 mwaka huu.

Hayo yameelezwa na Kamishna wa tume hiyo Pemba Ayubu Hamad Bakar, wakati akizungumza na wadau wa uchaguzi, katika mkutano uliofanyika ukumbi wa mikutano Wawi Chake chake Pemba.

Alisema ili kuhakikisha makundi hayo yanashiriki ipasavyo katika uchaguzi huo ‘ZEC" imeweka vituo vya kupigia kura, katika maeneo yanayofikiwa na kila mmoja.

Alisema jingine ZEC, imeandaa vitambulisho maalumu kwa watu wenye ulemavu, imetoa mafunzo maalum kwa maafisa wake, yanayozingatia uhitaji wa watu hao pamoja na kuchapisha vifaa saidizi kwa watu wenye ulemavu wa uoni.



"Ili kuhakikisha ushiriki wa kila mmoja katika mchakato huu wa kidemokrasia, tumeweka mazingira rafiki kwa kila mmoja, ikiwa ni kuwafundisha maafisa wetu, jinsi ya kutoa huduma kwa watu wenye ulemavu na kwa mwaka huu,’’alifamisha.

Alieleza kua, watu wenye ulemavu ni wadau muhimu katika kufanikisha zoezi la upigaji kura, kwani wanaidadi ya kubwa katika daftari la kudumu la wapiga kura.

 Alisisitiza kuwa, upigaji kura ni haki ya kikatiba ya kila mmoja  na kipengele muhimu cha kidemokrasia na utawala bora, ambavyo ni muhimu katika maendeleo ya nchi na watu wake.

Aliongeza kuwa, ushirikishwaji wa makundi hayo ni utekelezwaki wa sera ya jinsia ya 2025, inayolenga ujumuishi, wa kila mtu katika jamii kwenye hatua zote za kimaendeleo  ikiwemo ya kidemokrasia.



Akizungumzia umuhimu wa ushiriki wa makundi maalumu katika mchakato wa uchaguzi mkuu, Kurugenzi ya elimu ya wapiga kura na mawasiliano kwa umma Juma Sanif Shehe alisema, ni  kuwezesha utekelezaji wa haki za binaadamu, pamoja na kuhakikisha ushiriki wao katika demokrasia.

Aliongeza kua, ili kuhakikisha uchaguzi jumuishi tume imetoa mafunzo kwa watu hao,  na kuanzisha madawati katika ngazi za kiutawala, katika tume hiyo ili kuhakikisha mamkundi yote ni jumuishi katika uchaguzi mkuu.



Nao Afisa watu wenye ulemavu wilaya ya Wete  aliipongeza tume ya uchaguzi, kwa kushirikiana na  wakandi maalumu, katika  hatua zake zote za maandalizi ya uchaguzi, kitu ambacho ni chakipekee kwa mwaka huu.

"Tuipongeze ZEC kwa mwaka huu imechukua jitihada za makusudi ili kuhakikisha ujumuishi wa makundi yote katika uchaguzi, kuanzia hatua za awali za uandikishaji, jambo ambalo ni zuri kwetu,’’alifafanua.

                                                     MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...