Skip to main content

SHOTON WA NCCR- MAGEUZI AWAAHIDI MATAMU JIMBO LA MTAMBILE

 

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MGOMBEA Uwakilishi Jimbo la Mtambile kwa tiketi ya chama cha NCCR-Mageuzi Wahid Khamis ‘Shoton’, amesema nia yake ni kuziimarisha huduma za kijamii, ikiwemo maji safi na salama, kama akipata ridhaa.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, alisema anachohitaji ni kupata ridhaa, kutoka kwa wananchi wa jimbo hilo, kwani nia yake ni tbabiti.

Mgombea huyo alieleza kuwa, huduma ya maji safi na salama, anaiona imekuwa ya kudorora kwa baadhi ya vijiji jimboni humo.

Alieleza kuwa, eneo ambalo anataka kuanza nalo ni kijiji cha Kaani Kengeja,  Majenzi, Muwanda Mtambile ili kuona wananchi na hasa wanawake wanakuwa na muda wa kufanya kazi nyingine, badala ya kushughulikia huduma hiyo.



‘’Nimechukua fomu ya kugombea nafasi ya Uwakilishi jimbo la Mtambile, maana mimi ni mwanajamii, ninayeumwa na huduma za wananchi,’’alieleza.

Mgombea huyo alieleza kuwa, jingine ambalo anatamani kuwafanyia wananchi wake, ni kuwawezesha kiuchumi vijana na wanawake, kwa njia ya mikopo, isiyo na riba.

Alieleza kuwa, kwa aina ya mifumo ya wananchi wa Jimbo la Mtambile, ili awasaidie ni kuwapatia mikopo isiyo na riba.

Alifafanua kuwa, baada ya kuapishwa atawakusanya vijana na wanawake wote wa Jimbo hilo, na kisha kuwaorodhesha, ili kuona anawapatia mikopo.

Aidha Mgombea huyo wa Uwakilishi wa Jimbo la Mtambile kwa chama cha NCCR-Mageuzi Wahid Khamis ‘Shoton’ alisema katika Ilani yao, kwanza Tanzania, itikadi ya chama baadae.

‘’NCCR-Mageuzi inaamini kuwa, Tanzania kwanza itikadi ya chama baadae, wakiamini kuwa bila ya Tanzania, vyama visingekuwepo,’’alifafanua.

Hata hivyo, alisema kama akipata tena ridhaa, atashirikiana kwa karibu na wananchi, ili kuona Jimbo hilo linapiga hatua kubwa, ya maendeleo.



Alifafanua kuwa, bado Jimbo hilo linahitaji mtu kama yeye, ili kuyatafuta makundi kama ya watu wenye ulemavu, ili kuyawezesha kiuchumi.

‘’Iwapo wananchi wa Jimbo la Mtambile, wataniona ninafaa kushika nafasi hii, nikifanikiwa pia kundi la watu wenye ulemavu, nitahakikisha, nalisaidia kiuchumi,’’alifafanua.



Hata hivyo, Mgombea huyo aliwataka wananchi wa jimbo hilo, kuendelea kuilinda amani na utulivu uliopo, ili kura ifanyike kwa amani.

Alieleza kuwa, yapo mataifa kwa sababu ya vurugu ya uchaguzi, sasa wananchi wenyewe hawayakai, hivyo kwa Tanzania hilo, aliomba lisitokezee.

‘‘NCCR-Mageuzi inaamini, ili uchaguzi ufanyike kwa amani, kila mwananchi ahakikishe hawi sehemu ya machafuko, kwani ikikosekana hakuna linaloweza kufanyika,’’alifafanua.

Baadhi ya wananchi wa Jimbo la Mtambile, walisema wanaimani naye, na hasa kwa vile ni mgombea wanaeishi nae kila siku.

Mmoja kati ya wananchi hao Ali Mohamed Juma wa Mtambile, alisema ni miongoni mwa wagombea ambao wanaishi ndani ya jimbo hilo.

‘’Mgombea wa NCCR-Mageuzi wa jimbo letu la Mtambile, kwa nafasi ya Uwakilishi, anafahamika kitabia, mwenendo, na yeye bahati nzuri, anaishi hapa hapa,’’alifafanua.

Nae Mwanaisha Haji Kassim wa Kengeja, alisema aina ya mgombea ambae NCCR-Mageuzi wamemsimamisha, anazo sifa zote za kuwa kiongozi.

‘’Amekuwa akishirikiana nasi hata kabla ya kugombea nafasi hii, tena ni mcheshi na tunamuona anafaa kuwa Mwakilishi wetu,’’alisema.

Kwa upande wake Aisha Omar Twaha, alifafanua hata kama chama chao cha NCCR-Mageuzi hakionekani kuwa na wafusia wingi, lakini aliwaomba kura wananchi wote.


Uchaguzi mkuu wa saba wa vyama vingi nchini, unatarajiwa kufanyika Oktoba 29 mwaka huu, ni baada ya kuzinduliwa kwa kampeni Septemba12.

Zanzibar yapo majimbo 50 ya uchaguzi ambapo kwa Pemba, yapo 18, likiwemo la Mtambile, Mkoani, Kiwani, Chambani, Chonga, Ziwani, Wawi, Ole, Pandani, Micheweni, Wete, Mtambwe, Konde, Gando, Kojani, Wingwi na mingine.

              Mwisho    

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...