Skip to main content

ZEC YAJIGAMBA NA UCHAGUZI JUMUISHI 2025, WATU WENYE ULEMAVU WAHAKIKISHIWA MAZIGIRA RAFIKI

 





 NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@

OKTOBA 29 mwaka huu, Tanzania itafanya uchaguzi wake mkuu wa saba wa vyama vingi tokea kuasisiwa mwaka 1995.

Mpaka sasa matayarisho mbali mbali yanaendelea kufanyika, kuanzia kwa wananchi, vyama vya siasa tume ya uchaguzi pamoja na serikali kuu.

Kuelekea siku hiyo, wadau wa haki za watu wenye ulemavu wanaendelea kulilia mazingira rafiki ya uchaguzi kwa watu wenye ulemavu.

Kwani sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 imeweka wazi kuwa, Zanzibar ina takriban asilimia 11.4 ya kundi hilo.

Matokeo hayo ya sensa, yanafafanua kuwa aina ya ulemavu unaoongoza ni wa uoni, ambao unachukuwa asilimia 3.6 ya jumla ya watu wenye ulemavu.

Tume ya uchaguzi Zanzibar (ZEC) imesema jumla ya watu 717,557 wameidhinishwa kupiga kura mwaka huu, na kati yao 8,021 ni watu wenye ulemavu.

Hivyo ni muhimu kwao kuwekewa miundombinu rafiki katika vituo vyote vya kupigia kura, ikijumuisha majengo pamoja na vifaa.

Wenyewe wanasema, lazima mazingira hayo yatiliwe maanani, kwa uhitaji wa aina zote za ulemavu, ili kuhakikisha watu wote wanapata haki yao ya msingi ya kupiga kura.

WATU WENYE ULEMAVU

Said Saleh Sultan wa Mtambile Pemba mwenye ulemavu wa viungo anasema, mazingira rafiki kwao katika uchaguzi ni kuhakikisha vituo vya kupigia kura vinaweza kufikiwa.

Anaeleza ufikiwaji huo ni pamoja na kuweka vituo kwenye sehemu ambazo hazina milima na zenye miundombinu jumuishi, itakayo wawezesha wao kupata ushiriki mpana.

 “Mazingira rafiki kwetu ni kuwekewa vituo vya kupigia kura, katika sehemu zisizo na milima, pamoja na zenye miundombinu jumuishi, tutakazoweza kufika tukiwa na viti mwendo ,anasema.

Rehema Juma Makame wa Kukuu Kangani Pemba mwenye ulemavu wa uoni anasema, miundombinu rafiki ya kupigia kura kwao, ni kuwepo kwa karatasi za nukta nundu vituoni.

Adinan Khamis Juma wa Chake Chake mwenye ulemavu wa uziwi anasema, ujumuishi wao katika uchaguzi  ni kuwepo kwa wakalimani wa lugha ya alama katika vituo vya upigaji kura.

Anaeleza kuwa, wakalimani hao watarahisisha  mawasiliano kwenye maeneo ya kutoa huduma zinazo husu upigaji kura.

Saleh Khamis Khalfan wa Mtambile ambae ana  ulemavu wa ngozi anasema, mazingira jumuishi kwa  wenye ulemavu wa aina yake, ni kuwepo foleni kwa ajili yao.



Anaeleza kuwa, utaratibu huo utasaidia kupunguza muda wa kukaa foleni, ambazo mara nyingi hupangwa katika mazingira hatarishi.

Anasema maumbile ya ngozi zao hayahimili jua kali hasa kwa muda mrefu, ambalo linaathari kubwa kwao.

Sisi wenye ulemavu wa ngozi, mazingira rafiki kwetu katika upigaji kura ni kuwepo foleni maalum kwa ajili yetu, ili kupunguza muda wa kusubiria juani”, anafafanua.

              TUME YA UCHAGUZI ZANZIBAR (ZEC)

Mkuu wa Mkurugenzi wa Elimu ya Wapiga Kura na Mawasiliano kwa Umma wa ‘ZEC’ Juma S. Sheha anasema, wamejipanga kuhakikisha watu wenye ulemavu na mahitaji maalum, wanashiriki ipasavyo katika uchaguzi mkuu.

"ZEC imeandaa vitambulisho maalum kwa ajili ya watu wenye mahitaji maalum, wakiwemo watu wenye ulemavu, ili kuwapa kipaumbele wanapofika katika vituo vya kupigia kura, "anaeleza.




Hatua hizo zilizochukuliwa hazikuja tu kama ajali bali serikali, taasisi binafsi na wadau wingine wa kutetea haki za watu wenye ulemavu, wamekuwa wakilipambania hili kwa namna tofauti.

MIKATABA NA SHERIA INAELEKEZA NINI

Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Watu wenye Ulemavu wa mwaka 2006, Ibara ya 29 inazitaka nchi wanachama, kuweka mazingira rafiki ya watu wenye ulemavu kushiriki katika mchakato wote wa kisiasa.

“Nchi zihakikishe utaratibu wa kupiga kura, vifaa na nyenzo ni sadifu, vinafikika, vinaeleweka na kutumika kwa urahisi, imeeleza sehemu ya ibara hiyo.

 

TUME YA HAKI ZA BINAADAMU

Afisa Mfawidhi wa Tume ya haki za binaadamu na utawala bora Pemba, Suleiman Salim Ahmad anasema, ili kuhakikisha miundombinu rafiki kwa watu wenyeulemavu wa aina zote, tume hufuatilia mwenendo mzima wa uchaguzi.

 Sisi tunafuatilia mwenendo mzima wa uchaguzi kisha tunatoa mapendekezo kwa tume ya uchaguzi nini kifanyike ili watu wenye ulemavu wa aina zote wawe katika mazingira jumuishi,’’ anasema.

JUMUIYA YA WATU WENYE ULEMAVU

Maryam Mohamed Salum Afisa watu wenye ulemavu kutoka Jumuiya ya watu wenye ulemavu Pemba anasema, unapokaribia uchaguzi,  jumuiya hutoa mapendekezo kwa tume ya uchaguzi ili  kuhakikisha unakuwa jumuishi.

Mratibu Baraza la Taifa la watu wenye ulemavu Pemba, Mashavu Juma Mabrouk anasema, baraza hukutana na jumuiya za watu wenye ulemavu na kukusanya maoni yao.

Anasema baada ya kupata maoni hayo, huweka  mapendekezo na ushauri kwa tume ya uchaguzi, juu ya kuimarisha mazingira, vituo vya kupigia kura.

TAMWA ZANZIBAR INAFANYA NINI ?

Meneja programu kutoka Chama cha waandishi wa habari Tanzania TAMWA-Zanzibar Khairat Haji anasema, TAMWA  inatoa mafunzo kwa waandishi wa habari, kuhusu uandishi jumuishi.

Anaeleza kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuhakikisha waandishi wanatambua na kutetea haki za watu wenye ulemavu, katika nyanja zote.

Tumetoa mafunzo ya uandishi jumuishi kwa waandishi wa habari, ili waweze kutetea haki za watu wenye ulemavu, ikiwemo hii ya mazingira rafiki katika vituo vya kupigia kura,’’ anaeleza.

 

                                MWISHO

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...