Skip to main content

VIZIWI WATAMANI KAMPENI JUMUISHI, TAMWA -ZANZIBAR YATOA RAI KWA VYAMA

 

 
NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@

ZANZIBAR ipo ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mashariki mwa Afrika.

Ni miongoni mwa nchi zinazopata viongozi wake kupitia mchakato wa upigaji kura.

Ambapo kila baada ya miaka mitano wananchi wake, wenye sifa zilizotajwa kikatiba, hupiga kura ili kuchagua kiongozi wamtakae.

Mchakato huo humjumuisha kila mtu, ilimradi awe ametimia miaka 18 na asiwe mwenye changamoto ya ufahamu ama akili.

Izingatiwe kwamba, upigaji kura ni haki ya kikatiba ya kila Mzanzibari, kwani katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kifungu cha 7(1) kimetoa haki hiyo.

Kwamba ‘’Mzanzibari alietimiza umri wa miaka 18 anayo haki ya kupiga kura katika uchaguzi unaofanywa Zanzibar,’’kimefafanua.

Kwa kulizingatia hilo, Tume ya uchaguzi Zanzibar ZEC, imeidhinisha jumla ya wazanzibari 717, 557 kushiriki katika uchaguzi mkuu Oktoba 29 mwaka huu.

Huku taarifa kutoka tume hiyo zikieleza kwamba, kati ya hao  watu wenye ulemavu 8,021 wanatarajiwa kushiriki katika zoezi hilo hapa Zanzibar.



Watu wenye ulemavu wa uziwi wakiwa ni miongoni mwa wapiga kura hao, wanahaki ya kupata sera wakati wa kampeni kutoka katika vyama vyao.

WENYEWE WANASEMAJE?

Fatma Kombo Omar wa Kengeja Pemba ni mmoja wa watu wenye ulemavu wa uziwi, akiwa na mkalimani wake anasema, ingawa vyama vyote viko katika mchakato wa kunadi sera, hadi sasa ni sera za chama kimoja tu, ndio zilizomfikia.

Kumbe vyama vyingine vilivyo bakia, hupokea sera zao kutoka kwa watu wanaomzunguka na si kutoka kwa wagombea wenyewe.

“Ingawa kushiriki katika kampeni ni haki ya kila mmoja, lakini mazingira sio rafiki kwetu, na hadi sasa ni sera za chama kimoja tu ndio zilizonifikia,’’anaeleza.

Anaona bado ni vigumu kwao kupata sera za wagombea wote, kama ilivyo kwa watu wingine wasio na ulemavu wa uziwi.

Adinan Khamis Juma wa Chake Chake Pemba ni mtu mwenye ulemavu wa uziwi anasema, pamoja na kuwepo kwa mikataba, sheria na kanuni zinazotaka ujumuishi, ikiwemo siasa, bado hali si shwari kwao.

 Anafafanua kua, amekua akishiriki katika mikutano hayo, ingawa hakuna anachoelewa na hurudi akiwa hana alichofahamu, kwani hakuna mkalimani wa lugha za alama.

Hata Zuhura Haji Mohamed wa Mtambile, anasema wapo wagombea wanao watumia watu wa karibu wawafikishie sera zao, lakini  bado haitoshi.



“Bado ujumuishi wetu katika kampeni ni chanagamoto, na baadhi ya wagombea hutumia watu wetu wa karibu watufikishie sera zao, lakini hatupati ujumbe kamili,”anaeleza.

JAMII INASEMAJE?

Asia Shaib Saleh wa Mjimbini Pemba, anasema ujumuishi   kwa viziwi katika kampeni, bado ni changamoto na wanawachagua wagombea sio kwa kulewa na sera zao.

Anaeleza kua, jamii ndio inayofanya kazi kuwaeleza sera za vyama tofauti,  kazi ambayo ilipaswa kufanywa na wenyewe wanasiasa.

Saleh Bakkar wa Kengeja anasema, mara nyingi watu wenye ulemavu wa uziwi, hukataa kushiriki katika mikutano ya siasa, kwa vile hakuna mazingira rafiki kwao.

“Wenzetu wenye ulemavu wa uziwi, mara nyingi hawashiriki ipasavyo mikutano ya kampeni, kwa kukosekana kwa mazingira rafiki kwao, ikiwemo wakalimani wa lugha ya alama,’’anasema.

 VYAMA VYA SIASA VINASEMAJE?

Katibu wake wa CCM mkoa wa kusini Pemba Kajoro Vyohoroko anasema, katika kampeni za mwaka huu, mikutano yao ya hadhara ya wagombea urais, wameweka wakalimani wa lugha ya alama, ili kuhakikisha ujumuishi.



‘’Kwa miaka iliopita, kundi hili hatukulizingatia ipasavyo, ingawa mwaka huu mikutano yote ya kampeni za wagombea wa urais wa Tanzania na Zanzibar, tumeweka wakalimani wa lugha ya alama,’’anafafanua.

Mohamed Abdallah ni Mwenyekiti wa chama cha ACT –Wazalendo mkoa wa kusini Pemba anasema, hadi sasa chama hicho hutumia watu wa karibu, na watu wenye ulemavu wa uziwi katika kufikisha sera.

 ‘’Kwasasa chama hakina mazingira rafiki kwa watu wenye ulemavu wa uziwi, katika kuhakikisha wanapata sera za chama, na badala yake tunawatumia watu wao wa karibu,’’ anaeleza.



MIKATABA/SHERIA NA SERA

Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa watu wenye uleamu (CRPD,2006) Ibara ya 9, inazitaka  nchi wanachama, zihakikishe zimeweka utaratibu wa watu wenye ulemavu, kufikia huduma zote pamoja na mawasiliano na teknolojia.

Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu ya Dunia ya mwaka 2020/2030 yenye shabaha 169, shabaha 11 inagusia watu wenye ulemavu wa aina zote.

Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kifungu cha 12 (1) kimeweka wazi kua, watu wote ni sawa mbele ya sheria.

Huku mabano (4) na (5) vikieleza kua, hakuna mtu yeyote atakae baguliwa kwa utaifa wake, kabila, jinsia, ulemavu, pahala alipotokea, muelekeo wa kisiasa, rangi au dini.

Ndio maana Sheria ya watu wenye ulemavu nambari 8 ya Zanzibar ya mwaka 2022, kifungu chake cha 29 kinaeleza umuhimu wa watu wenye ulemavu, kufikia miundombinu pamoja na taarifa, mawasiliano na  haki zote za msingi.

NINI ATHARI YAKE?

Zainab Mohamed Ali wa Chake Chake, mwenye ulemavu wa uziwi anasema, moja ya athari zinazojitokeza ni kutowachagua viongozi wawatakao.



Afisa Mfawidhi Tume ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora Pemba Suleiman Salim Ahmad anasema, ni  watu hao kukosa haki yao ya kikatiba ya kupiga kura.

NINI KIFANYIKE?

Yumna Mbarouk Yussuf na Mbarouk Ali Juma wa Pemba wanasema, yvama vyote vya siasa viandae mazingira rafki kwa kuweka wakalimani wa lugha ya alama katika mikutano yote.

Katibu Mkuu wa Chama cha Viziwi Zanzibar ‘CHAVIZA’ Yahya Hamed Seif anasema, ili kuhakikisha ujumuishi wao katika kampeni za vyama vya siasa, vyama vibuni njia za kuwajumuisha.

Kaimu Mratibu wa chama cha waandishi wa habari wanawake TAMWA-Zanzibar Ofisi za Pemba Amina Ahmed Mohamed anasema, ni vyema vyama vyote vya siasa kuweka wakalimani wa lugha ya alama.



Jingine, ni kwa wadau wa haki za watu wenye ulemavu, kuendelea kupaza sauti, ili sheria ya uchaguzi na ile ya vyama vya siasa iwe na kifungu lazimishi juu ya kuwatumia wakalimani.

                                           MWISHO

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...